Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy?!? ni IPI?! Labda ya kuiporomosha nchi na Mkapa kuja kuiinua. Ni kama JK alivyoiangusha na sasa JPM anavyohaha kuiinua.

Aliiporomosha kutoka wp mpaka wp?
Mzee mwinyi aliwahi kuhutubia wazee wa DSM pale daimond akasema kaachiwa nchi ikiwa hoi haina akiba ya mafuta ya prtroli,disel,chakula, madawa na hata pesa ktk benki kuu hakuna.

Sasa kama kiongozi kaikuta nchi haina akiba ya vitu muhimu kama hivyo atakuwa kaiporomosha au kaipandisha?
Nahayo maneno kayasema wakati JKN yuhai na hayakukanushwa.

Mm nataka nikuambie mzee mwinyi kawasaidia sana wtz wazawa leo tuna matajiri wengi sana watz wazawa tofauti nahuko nyuma matajiri wengi kama sio wote walikuwa jamii ya kihindi na kiarabu.

Leo wtz wazawa wengi sana wanajiweza vizuri tu.
Hili ni chimbuko la sera na mikakati ya mzee mwinyi.

Yapo mengi mema mazuri ya utawala wa mzee mwinyi chimbua utayajua tu.
Leo hakuna mtu anakaa foleni kisa mkate au mchele au sembe....ngoja niishie hapo kwanza.
 
Moja kubwa kwa mara ya kwanza tangu azimio la ujamaa nchi ilijitoshekeza kwa chakula. Uzalishaji ndani ulikua na ruhusa ya kuagiza ilikutolewa.

Umiliki wa magari ukawa bila ya vikwazo ..kila mbongo akawa ana hamu ya kuwa na magari...zamani lazima uombe kibali na huchukua mpaka miaka 5 kupata hicho kibali

Pamoja na kuondoa njaa alifuta log book za kuchukulia chakula RTC na Petrol na Diesel vibali vikafutwa. Kabla yake gari unaendesha kwa lita 10 kwa wiki.
Pia akaruhusu nasi tuwe na TV , akivunja falsafa ya alomtangulia kuwa TV ni anasa. Vituo vya watu binafsi na hatimae TVT ikaanzishwa..ndio hii TBC
Pia akaruhusu Radio ninafsi
Akaruhusu magazeti binafsi
Tunashukuru hatukupiga tena foleni ya Mchele, Sembe na Sukari.....
In fact kiume alipindua upside down siasa muflis za kijamaa. Alikua jasiri kufanya maamuzi yale . Bila ya uamuzi ule Mkapa asingeweza kwenda kinyume na baba ake ..bado tungekua kama Korea ya Kaskazini



Mengine Ritz ameya eleza

In fact alofanya Mzee Mwinyi hakuna anayemfikia hata mmoja ..ila kuyaendeleza na kuyaboredha yale yale
 
Alkua anaambiwa na WB na IMF Nate anatimiza so hapakuwa na ujuzi wala ubunifu kupigia mfano!! Ruhusu demokrasia- sawa! ruhusu soko huria-sawa! nk. nk. Kuhusu legacy may be that but for me there was nothing best in particular!
Nina hakika hukiwepo kipindi chake usingeliandika hivi. waulize wazee wako waliopitia enzi za mwl na za mzee ruksa halafu ndio uje hapa. Hakuna raisi aliepita kipindi kigumu cha kuongoza nchi kama yeye. Wanaolalamika kiwa alishusha uchumi.watuambie aliushusha kutokea wapi?kwa sababu uchumi tayari ulikuwa taabani!
 
Mungu akupe maisha marefu na afya tele mzee wetu mzee ruksa iliikuta nchi iliyokuwa hohe hae inchi imejichokea na sera na siasa muflis za ujamaa kila kitu foleni na hata ukiunga foleni huna hakika ya kupata bidhaa lakini ukaja ukaufungua mlango wa ruksa hakika ruksa ikaifaa sana nchi yetu.
Kipindi kile nchi ilihitaji kiongozi mwenye haiba yako ukaamua kwenda kinyume na asili ya ujamaa ili inchi ipone hakika baadhi ya mazuri ambayo tunayashuhudia hadi leo yalitokana na jasho lako.
Uliyafanya haya kwa ujasiri japo haiba yako yaonekana ya upole ila ulifanikiwa kuivusha nchi katika kipindi kigumu kweli kweli.

Nakumbuka ukituaga kwenye hutuba yako mwaka 1995 ukatuambia"MABAYA YANGU NIACHIENI LAKINI MAZURI YANGU TUGAWANE".hakika ni kweli leo mazuri yako tunagawana hatuungi tena foleni kupata mafuta,mkate unga wala sukari.
Hongera sana mzee ruksa mola aendelee kukupa afya njema na miaka mingi zaidi.
 
Mimi ninayokumbuka wakati wa Mwinyi ni haya;
  1. Rukhsa, nchi kugeuzwa kokoro
  2. Kaburi la Azimio la Arusha
  3. Kupotea kwa tausi viwanja vya Ikulu na Karimjee
  4. Kushuka kwa hadhi ya Ikulu
  5. First Lady kuitwa shemeji
  6. Kuzuka kwa mihadhara ya kidini
  7. Mgogoro wa Loliondo na Waarabu
  8. Mwanzo wa biashara ya Wanyama
  9. Ukwepaji wa kodi kushika kasi
  10. Mwanzo wa kuingia mikataba mibovu
  11. Kuzaliwa kwa IPTL, hadi leo inatutafuna.
  12. Kutothaminiwa kwa wasomi na wataalamu
  13. CCM kutekwa na wafanyabiashara na walanguzi.
  14. Kampuni za mfukoni na utapeli kushika kasi
  15. Nchi kuendeshwa kwa mtindo wa yupo yupo
Mengine nawaachia...
 
Kisiasa, Uongozi wa Mwinyi ulifanikiwa katika mambo makuu mawili; kufunguliwa kwa milango ya demokrasia na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Dhana ya demokrasia, japo haikutumika katika chaguzi za kipindi chake, lakini angalau miaka miwili kabla ya kuondoka madarakani nchi ilifungua mlango wa demokrasia ambapo siasa za vyama vingi zilianza wakati yeye akiwa madarakani.Kwa pamoja na Uhuru wa Vyombo vya habari, nchi ikajenga mazingira mapya kutoka yale ya utawala usiokosolewa kuja utawala uliokosolewa hadharani. Kwa mara ya kwanza ikashuhudiwa demokrasia ya Rais kuchorwa na kusemwa vibaya.

Vijana wa Chuo Kukuu cha Dar es Salaam wao walifikia hatua mbaya zaidi pale walipoifuja demokrasia hiyo kwa kuchora picha za matusi dhidi ya Rais Ali Hassan. Kama tutakavyoona katika kipengele cha elimu, Mwinyi alileta nafuu kubwa ya maisha ya Wanataaluma Chuoni hapo.

Japo wanataaluma walianza kuonesha mfano mbaya wa matumizi ya uhuru wa kujieleza ambao haukuwepo enzi za Nyerere lakini bado Mwinyi hakufunga mlango wa demokrasia.

Kwa mara kwanza tangu miaka ya 1960, Watanzania wakaanza kushuhudia majukwaa ya upinzani dhidi ya Chama tawala na serikali. Ukizungumzia mwanzo wa mageuzi ya kisiasa basi lazima utayakuta ndani ya kipindi cha Mwinyi.

Kama kuna eneo lililoung’arisha mapema utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi basi lilikuwa ni lile la Uchumi. Mwinyi aliaswa na wataalamu wa uchumi kuwa aachane kabisa na fikra zilizoshindwa na Mwalimu Nyerere kama alitaka kufanikiwa katika eneo hili.
You have tried to your best to answer the question Bila KUJITOA ufahamu. That is maturity [emoji106] [emoji817] [emoji818]
 
Kipindi cha mzee ruksa vijana wakaanza kupanda ndege kwenda dubai kuchukua mzigo na kuleta mjini kufanya biashara.

Akina mama wakafurika Zanzibar kuchukua mali.

Mwaka 1994 Watanzania tukaangalia world cup kwenye TV zetu wenyewe!, acheni bhana Mzee Ruksa jembe
 
Mimi ninayokumbuka wakati wa Mwinyi ni haya;
  1. Rukhsa, nchi kugeuzwa kokoro
  2. Kaburi la Azimio la Arusha
  3. Kupotea kwa tausi viwanja vya Ikulu na Karimjee
  4. Kushuka kwa hadhi ya Ikulu
  5. First Lady kuitwa shemeji
  6. Kuzuka kwa mihadhara ya kidini
  7. Mgogoro wa Loliondo na Waarabu
  8. Mwanzo wa biashara ya Wanyama
  9. Ukwepaji wa kodi kushika kasi
  10. Mwanzo wa kuingia mikataba mibovu
  11. Kuzaliwa kwa IPTL, hadi leo inatutafuna.
  12. Kutothaminiwa kwa wasomi na wataalamu
  13. CCM kutekwa na wafanyabiashara na walanguzi.
  14. Kampuni za mfukoni na utapeli kushika kasi
  15. Nchi kuendeshwa kwa mtindo wa yupo yupo
Mengine nawaachia...
Hakuwa na zuri?
 
Awamu yake Pesa ilikua nje nje yaani maisha yalikuwa mazuri sana kwa Mtanzania miaka hiyo nilikiwa mdogo Marehemu dada yangu(Allah amrehem na ampunguzie azabu za kaburi) kila siku alikua anaokota ela maana tulikua tunaishi karibu na baa moja ivi yaani asubuh akiamka anaenda hapo basi anaokota pesa nyingi sana. Mbali na neema zote ila wenye roho mbaya walisema anaongozwa na mkewe wakati aliyetoka alikua haongozwi na mkewe lakini hali ya maisha ilikuwa ngumu kuliko Sudan kusini.
 
Alipokea kijiti cha uongozi wakati nchi ikiwa katika hali ngumu mno kiuchumi.

Sijui kama ulikuwepo kipindi hicho mkuu.

Kama ungekuwepo sijui kama ungeandika hayo uliandika labda kama unaleta ubishi na ushabiki sawa.
Mkuu Ritz naomba legacy ya aliempa kijiti Mzee ruksa nakusudia legacy ya Nyerere.
 
Mimi ninayokumbuka wakati wa Mwinyi ni haya;
  1. Rukhsa, nchi kugeuzwa kokoro
  2. Kaburi la Azimio la Arusha
  3. Kupotea kwa tausi viwanja vya Ikulu na Karimjee
  4. Kushuka kwa hadhi ya Ikulu
  5. First Lady kuitwa shemeji
  6. Kuzuka kwa mihadhara ya kidini
  7. Mgogoro wa Loliondo na Waarabu
  8. Mwanzo wa biashara ya Wanyama
  9. Ukwepaji wa kodi kushika kasi
  10. Mwanzo wa kuingia mikataba mibovu
  11. Kuzaliwa kwa IPTL, hadi leo inatutafuna.
  12. Kutothaminiwa kwa wasomi na wataalamu
  13. CCM kutekwa na wafanyabiashara na walanguzi.
  14. Kampuni za mfukoni na utapeli kushika kasi
  15. Nchi kuendeshwa kwa mtindo wa yupo yupo
Mengine nawaachia...
Nilitaka kushangaa usingejitokeza kwenye huu uzi haya mbona umeyasahu.

16. foleni za unga wa njano na magendo ya bidhaa. Hata ‘sigara kali’ achilia mbali ‘sports’ na SM, ziliuzwa kwa bei ya kuruka

17. Kabla ya mikokoteni kufikisha magunia mawili-matatu ya unga wa njano, au mchele mdundiko, au kitumbo uliotoka Japan, watu kwanza walipanga mawe au makorokoro yoyote yale kwa sababu ya jua kali la saa nane mchana.

18.Foleni zilikuwa za kusukumana kwani watu walikuwa wengi kuliko bidhaa. Ndiyo kusema, wengine walirudi nyumbani mikono mitupu baada ya jitihada za kusukumana ili kulifikia dirisha la duka kushindikana. Wengine walizirai kwenye foleni! Ugumu hasa ulikuwa katika kupata sukari au mchele uliokuja kwa nadra

19.Mara nyingi, mchele na sukari vilipatikana kwa magendo majumbani mwa watu. Walanguzi walikuwa wakitazama au kuangalia huku na kule kabla ya kukupimia kibaba cha sukari, na wakati mwingine vibaba vyenyewe vilikuwa “mkude”

20.Vibaba-mkude” ni vibaba vya kupunjia. Kwanza unalanguliwa lakini pili unapunjwa. Ilikuwa ukienda sokoni unatazamwa usoni. Kisha unaulizwa unataka nini. Kama ulitaka mchele, basi mtu alibonyea bonye uvunguni mwa kikazi chake cha biashara na kubenjua gunia lililofichwa vizuri.

21.Unapimiwa kibaba mkude bila wewe mwenyewe kuona. Kwa kuwa ulihitaji mchele, na umeupata baada ya kuhangaika sana, basi huulizi tena. Tangu hapo, unatakiwa uondoke haraka sana baada ya kupimiwa, usiweke kiwingu cha kuleta “manjagu” bure

22.Mteja alitakiwa awe ‘shapu’, hakuna kuzubaa-zubaa! Na mtu alipokwenda kwenye nyumba yenye mchele au sukari ya magendo, hakutakiwa kupitia mlango wa mbele, bali azunguuke uchochoroni na kupitia mlango wa nyuma. Ukitoa sauti kali kuuliza sukari au mchele, hupati! Hawakuuzii ng’o, unaambiwa hakuna

23.Mameneja wa RTC ndio walioshamirisha magendo kwani walikuwa wakiwatumia “watoto wa mjini” kutoa bidhaa kwa mlango wa nyuma kutoka kwenye magodaoni ya Shirika la Ugawaji

24Nyerere aliamini kuwa, kwa kutumia sekta ya Umma kuhodhi bidhaa labda alikuwa anashinda vita dhidi ya ubepari kumbe alijenga mazingira ya kuwatesa wananchi wake na kuwanufaisha Maafisa wabadhirifu

25. Kiwango cha ubadhirifu wa mali ya Umma kilikuwa ni kikubwa kinyume na madai ya baadhi ya watu kuwa wakati wa Nyerere hakukuwa na ufisadi na ubadhirifu!

Wengine wataongezea....
 
Ni katika miaka kumi ya Mwinyi ndipo watu wakaanza kuvaa mitumba inayotazamika. Kabla ya hapo nadiriki kabisa kusema kwamba tulikuwa tunavaa marapurapu. Lakini katika miaka michache ya uongozi wa Mwinyi kinadada wakaanza kupendeza, mafuta ya nywele kwa ajili ya vichwa vya kinamama yakaanza kupatikana madukani.

Nakumbuka kabla Mwinyi hajaingia kwenye uongozi, mimi na watoto wenzangu tuliokuwa tunaenda disco toto pale YMCA tulikuwa tunapenda kusimama karibu na meza ya DJ marehemu Kalikali, lengo haswa lilikuwa ni kuzishangaa nywele zake, alikuwa ameweka madawa kichwani (kama Didier Drogba).

Sasa sisi kwa sababu hatukuwa tumezoa kuona nywele zimepakwa mafuta, tukawa tunacheza muziki karibu yake ili tutazame kichwa chake kwa karibu. Na jamaa alikuwa anawapata sana warembo kwa sababu ya nywele zake kuwa zimepakwa madawa.

Tulizoea enzi zile kutumia mafuta ya nazi vichwani, kunyolewa kwa viwembe chini ya miembe. Kwa kweli Mzee Mwinyi alileta rukhsa ya kufanya biashara, na watu wakaanza kupendeza. Saloon za kinamama zilianza miaka ya mzee Mwinyi. Mitumba ilishamiri enzi zile. Magari aina ya corolla yakawa mengi haswa yakimilikiwa na wahindi.

Mungu amempa umri mkubwa mzee Mwinyi naamini ni kwa sababu ya ubinadamu wake.
 
Mzee Mwinyi alipokea nchi katika hali ngumu sana kiuchumi. Alifanya aliyoweza na kwa mtazamo wangu mengi yalikuwa positive.
Lakini tunajua hakuwa malaika mzee wa watu kwani kuna sehemu angeweza kufanya vizuri zaidi. Ni kipindi chake rushwa ilianza kuota mizizi miongoni mwa watumishi wa umma na wanasiasa. Hakuwa mkali kusimamia hali hiyo. Ndiyo kipindi mission Town waliibuka kwa wingi.
Kwa ujumla kipindi chake kilikuwa ni cha mpito toka ujamaa wa Mwl kuingia uchumi huria wa sasa.
 
Kipindi cha mzee ruksa vijana wakaanza kupanda ndege kwenda dubai kuchukua mzigo na kuleta mjini kufanya biashara.

Akina mama wakafurika Zanzibar kuchukua mali.

Mwaka 1994 Watanzania tukaangalia world cup kwenye TV zetu wenyewe!, acheni bhana Mzee Ruksa jembe
Kula like[emoji106] [emoji106] mia
 
Back
Top Bottom