Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Ajabu ni kuwa serikari inamjengea hekaru lenye thamani ya zaidi sh billion Sita at 91!
 
Du ulikuwa unaenda ymca vp rungwe wakati wa disco toto dj jhone p pantalaki na cris fabi?
 
Du ulikuwa unaenda ymca vp rungwe wakati wa disco toto dj jhone p pantalaki na cris fabi?
Ndugu yangu acha tu, enzi zile za rungwe oceanic, iliyokuwa mali ya Marehemu Mzee Mwakitange. Petty Ray Kasambula na volkswagen yake, nikiisikia tu usiku wa manane najua jamaa anatoka mbowe kupiga muziki. Alikuwepo Marehemu Choggy Sly, alikuwepo mtu anakwenda disco pale YMCA na mwamvuli mkononi akiigiza mbwembwe za wamarekani.
Alikuwepo kaka yake Jack Pemba anaitwa Chuche (nadhani ni marehemu), alikuwa fundi wa kucheza robot na baadae break dance.
Hizo zilikuwa enzi za maisha ya utotoni, marehemu Mama anatoa fedha ya disco toto jumapili mchana, halafu wakati naondoka kuelekea disco namsikia akiniambia usipite "gizani wakati wa kurudi usiku, tembea kwenye mwanga wa taa". Yaani anasema nisipite gymkhana kwenye ule mtaa wa ghana avenue kwa sababu kulikuwa na giza sana usiku. Siku zimekwenda na haziwezi tena kurudi.
 
Hahahahahaha!! Mkuu umekumbusha mbali sana unakumbuka hii.



Cc: Kimbunga
 
Mzee Mwinyi alikuwa akimsikiliza Nyerere wala habishani naye wala hagombani naye lakini inapokuja kwenye kufanya maamuzi anafanya maamuzi kwa jinsi yeye anavyoona inafaa!


Uko sahihi Kabisa!!! Nyerere anapiga kelelee Mzee Mwinyi alikuwa na adabu sana hakuwahi kumjibu ila pia hakuwahi kuyumbishwa nae!
Maigizo ya Ujamaa na Azimio la Arusha alitupa kuleee!

Tofauti kubwa ya Mzee Mwny na Marais wengine ni kutokuwa kwake na wapambe na wapishi wake wa Propaganda.

Mwinyi pekee ndio Rais ambae hakuwahi kujikweza na kujifaragua kwa majivuno.

Mwinyi kaibadilisha sana hii nchi kutoka Maisha ya ki primitive ya kuamini hata kumiliki friji ya kupoza maji ya kunywa ni kuhujumu uchumi
 
Hahahahahaha!! Mkuu umekumbusha mbali sana unakumbuka hii.

View attachment 345781

Cc: Kimbunga
Ritz, huwa nawatazama hawa watoto wa smart phones nawaona hawana ujanja wowote. Acha tu yaani, tunaongelea enzi hizo za watoto wa Oysterbay kufanya sherehe halafu sisi watoto wa upanga mashariki tunakwenda kwa miguu kwenye nyumba ya mtu fulani. Party ikimalizika kulikuwa hakuna mambo ya boda boda au bajaji, watu wakanyaga kwa miguu taratibu kutoka mitaa ya Obay, wanavuka salender Brigde wanakunja kushoto kuitafuta Aga Khan, wakivuka Gymkhana, yanakuwepo makundi mawili, mmoja linaelekea shaaban robert na jingine linakuwa ni la watoto wa mirambo na ohio kwenye maghorofa ya Railways.
Watu walikuwa wanazifuata party za usiku kwa miguu, lakini walikuwepo wezi wa magari ya baba, wanavizia wazee wamelala, wanaenda gereji wanalisukuma gari taratibu mpaka kwenye kona ya mtaa halafu ndio linawashwa. Mwenye gari mara nyingi hana hela ya mafuta, anafanya kuwaambia marafiki zake wachange ili waweze kwenda na kurudi nyumbani bila ya baba kushtukia mchezo asubuhi ya siku inayofuata.
 
Du ulikuwa unaenda ymca vp rungwe wakati wa disco toto dj jhone p pantalaki na cris fabi?
Ma-DJ wakali kabisa wa enzi hizo walikua pamoja katika show Club Africana. DJ Meb, Neagre Jay, DJ Choggy Sly (RiP) , DJ John Peter Pantalakis, mratibu wao Nassoro Born City (RiP), DJ Kalikali (RiP) na DJ Eddy Sally (RiP) ... Masiku yamepita.
 
Mwinyi aliiporomosha nchi yeye alikuwa yupo bize kusafir kwenda arabuni kuoa huku nchi ikididimia kiuchumi
Hovyooooooooo sana uyu mzee wa ruksa kama sio mkapa kufunga mkanda Leo hi tungekuwa Sawa na Zimbabwe

Mkapa alitengeneza uchumi baada ya kuharibiwa na Mwinyi baadae mkwere akaja na kuanza kutumbua mpaka Sasa nch imeoza
 
Ma-DJ wakali kabisa wa enzi hizo walikua pamoja katika show Club Africana. DJ Meb, Neagre Jay, DJ Choggy Sly (RiP) , DJ John Peter Pantalakis, mratibu wao Nassoro Born City (RiP), DJ Kalikali (RiP) na DJ Eddy Sally (RiP) ... Masiku yamepita.
Rits umenikumbusha hao watu hasa marehem Nassor boncity na usimsahau seyduu.
 


Ally Hassan Mwinyi alikabidhiwa nchi ya Ujamaa na kujitegemea ikiwa haijawahi kujitegemea hata kwa dakika mbili tangu uhuru.

Kila bidhaa muhimu iliadimika mpaka meno tukashauriwa tusafishie Mikaa eti inafaa ki Afya.

Personally 1982 nikiwa uwanja wa Karume niliwahi kukamatwa na Mgambo kwa kuvaa Suruali iliyodhaniwa iliingizwa nchini kwa Magendo.

Mwny ID ya JPM mum tag aelewe kuwa tulishateseka in advance kwa niaba ya watoto na wajukuu zetu asirudishe Taifa tukaishi kijima mpaka hati ya kusafiria kuna nchi zimepigwa muhuri wa No entry.

Hati yangu ya kusafiria ilinizuia kwenda South Africa, West German, South korea na Israel.
 
Phillipo,

Utaniliza daah! Nakumbuka Kulikuwa na dala dala likiitwa Scaba Scuba la watoto wa mjini lilikuwa la mwisho kuondoka lakini la kwanza kufika mjini.

Toto disco Msasani na kukimbilia basi la mwisho pale kawe, Mbowe Club, YMCA, Chezimba, Mawingu club.

Mzee wapi hiyo Olimpio au Bunge hahahaha.
 


Wewe unapaswa kuelewa hakuna Nchi ya Ujamaa na kujitegemea iliyoshindwa hata kusambaza Unga wa ugali kwa raia wake (tena sio bure) isipokuwa Tanzania ya Nyerere tukawa tukihoji tunadanganywa Oscar Kambona kakimbia na hela zote za Serikali kakimbilia kwa Makabaila na Mabeberu Uingereza
 
Mwinyi alipoingia madarakani kwa kweli nchi ilibadilika kwa kasi, ukosefu wa bidhaa muhimu ulikwisha, foleni kwa bidhaa za kawaida ilikiwsha , mafuta diesel na petrol zilipatikana bila tatizo mambo ya 'kuruka' ili upate kununua kitu yalikwisha , wakulima walizalisha mazao na hata mvua zilifunguka na watu wakapumua. hata usafiri uliboreka sana
 
Unapo sema mzee mwinyi kaharibu nchi labda ungetupa takwimu za nchi alipo ikuta.
Lakini ukumbuke mzee mwinyi alisema hadharani pale Daimond kuwa kaachiwa haina akiba ya chochote kile akafafanua zaidi kuwa kapewa nchi haina akiba ya chakula, haina akiba ya mafuta ya petroli na disel nk.
Na wakati akisema hayo JKN Alikuwa hai na hakukanusha.
Na kwa jinsi alivyo kuwa JkN asingeweza kukaa kimya kama mzee mwinyi amemsingizia .
Ww labda umezaliwa miaka ya 1990 haya unayoyaandika umehadisiwa tu hukuyaona.
Mkuu nyuma ya 1985 nchi ilikuwa na shida ya kila kitu hapo ilala kulikuwa na mtu anaitwa Mpangala ndio alikuwa kwenye kitengo kinaitwa ugawaji.
Huyu mtu kalikuwa kamungu kadogo ulizia habari zake utazipata nenda hata pale club ya yanga watakupa taarifa zake.
Amini kabisa kama mzee mwinyi kaisongeza pakubwa sana nchi hii.
Hata DSM watu wameongezeka sana ktk utawala wa mzee mwinyi.
Wakati wa JKN watu walikuwa wanakamatwa kwa uzembe na uzururaji ikisalimika kufungwa unapelekwa geza au mwanamilapo.je unakujua?
 
Duh hii rohombaya yako imezidi sasa
 
Forodhani primary school. Enzi za kwenda kutazama basketball pale gymkhana ambapo sasa hivi pamejengwa hotel ya serena.

Pale kulikuwa na viwanja viwili, kimoja cha soka ambacho kilikuwa kikitumiwa na timu ya bima na hata pamba football club wakija dar walikitumia kwa ajili ya mazoezi, halafu kulikuwa na uwanja wa mpira wa kikapu wa timu ya pazi, ikimilikiwa na marehemu Malai, mzee wa Malai freight forwaders.

Msasani beach ndio ulikuwa ukumbi wa wajanja kufanyia sherehe za harusi zao. Enzi za disco pale Motel Agip, baadae likahamia New African ghorofa ya saba. Yaani acha tu ndugu yangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…