Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Eeeh Mungu muweza, epushia mbali tusirudi kwenye zama zile za foleni. Ingawa kwa wakati ule mimi nilikua na umri kati ya miaka 7-10 hivi nakumbuka vema maduka ya Kaya na hilo shirika la Biashara la Mkoa RTC. Kwa kweli lazima tumshukuru Mzee Mwinyi, hali ilijua mbaya sana. Hata kama aliteleza lakini ukipima mizania, huyu Mzee anabaki na Legacy kubwa sana kwa Uchumi huu wa Tanzania. Utawala wa sera za Kijamaa ulishindwa kabisa kutatua matatizo yetu!
Atakayekosa kumshukuru Mzee Mwinyi, hana shukrani
 
Sahimtz,

Tuendelee na habari za Mzee Mwinyi tukiendelea zaidi utaniliza.
Ritz mzee mwinyi hana mfano mema yake kwa nchi hii hayatasahaulika kwakila mpenda nchi hii.
Ni rais pekee alie pata kuwa rais wa nchi mbili kwa nyakati tofauti.
Ni kiongozi alie wafundisha raiya wake kujua kutafuta pesa na kujikwamua.
Wimbi lote hili la wafanya biashara za kila aina ni zao la mzee mwinyi kabla ya hapo wafanya biashara walikuwa ni jamii yakihindi na kiarabu.
Kila kizuri cha nchi hii kilikuwa cha wahindi na waarabu leo wazawa wanakila kitu kizuri kuanzi majumba magari nk.
 
Jamani tuwe wakweli, enzi za Nyerere kuna kipindi tulikula ugali wa Yanga. Tasteless kabisa yaani, ukiula wala hauhisi kwamba unakula chakula. Tulivaa nguo za kupika. Salim Ahmed Salim akafanya mpango zikapatikana raba fulani za vitambaa ndio zikawa zinauzwa nchi nzima, zilikuwa zinaitwa Asante Salim. Miaka ya mwisho ya JKN ilikuwa migumu sana, enzi za maduka ya kaya, kila nyumba ilikuwa na daftari la kuandikia bidhaa zilizonunuliwa kutoka katika duka la kaya.
 
Nani amekusimulia hizi habari kuwa nchi ilididimia kiuchumi wakati wa wa Mzee Mwinyi. Amekudanganya sana.

Kwa kifupi, hiyo ndiyo hali aliyoikuta Mzee Ali Hassan Mwinyi. Ilikuwa ni nchi ngumu mno ambayo, alimanusura, ingesababisha serikali ya Mwalimu Nyerere ipinduliwe lakini jaribio la Maafisa wa Jeshi lilizimwa.
 
Yaani unajiuliza kuhusu legacy ya mzee wa Ruksa? Unajua kwa nini alipachikwa jina hilo ama ulikuwa hujazaliwa?
Mimi ngoja nimsaidie mleta uzi , mzee Mwinyi ni Muungwana na mvumilivu wa kutupwa ! Ameacha alama ya kutukuka baada ya KUZABWA KIBAO na raia lakini wala hakutumia mabavu ya urais kulipa kisasi , badala yake akasamehe .
 
Naon wafuatao wamekataa kuja kuchangia na kutusaidia undanizaidi wa mzee Mwinyi:

1. PHILEMON MICHAEL
2. MOHAMMED SAID (mwanahistoria)
3. MZEE MWANAKIJIJI
4. PASCO WA JAMIIFORUMS
5. MKANDARA
6. KANDA MBILI
7. PASCAL MAYALLA ( wa zamani Masai studio/DTV na mwandishi wa habari maaruf)
8. WILLIAM MALECELLA
9. TAFITI KISHA JADILI
10. MZITO KABWELA
 
Legacy?!? ni IPI?! Labda ya kuiporomosha nchi na Mkapa kuja kuiinua. Ni kama JK alivyoiangusha na sasa JPM anavyohaha kuiinua.

Natamani sana kutokee mtu humu kwenye huu uzi ambae anaweza kutupatia audio za hotuba mbili za awali za Ali Hassan Mwinyi alipozungumza na wazee wa Dar., pale Diamond Jubilee. Hususan ile iliyoitwa mikuki miwili". Hotuba hizo za Mwinyi zimepotezwa kabisa kwenye historia. Hazionekani, hazisikiki.

Hotuba hizo zingekupa picha kamili ya umasikini alioachiwa Mwinyi na Nyerere.

Kwa kifupi, Mwinyi alikuta nchi haina kabisa pesa za kigeni, haina kabisa akiba yoyote. Haina kabisa hata mafuta ya kuendesha viwanda (vilivyo baki hai) au magari (makorokocho).

Mwinyi alipokea nchi ikiwa hohehahe, haina mbele wala nyuma.
 
Binafsi japo nilikuwa mdogo nimeshuhudia muuza duka akiuawa kwa ngumi moja tu katika harakati za kumpatia huduma mwananchi ambae alihisi anabaniwa kwa wiki nzima!
 

Wamesahauliwa kwa makusudi kabisa walioanza kudai uhuru Tanganyika seuse Mwinyi na mazuri yake yote.

Yakiwekwa wazi makorokocho aliyoyakuta Mwinyi na mabadiliko makubwa aliyoyafanya ya kuwatoa Watanzania kizani na kuwaweka kwenye nuru basi tutawaona wa kabla yake kuwa ni nuksi kubwa iliyowahi kuikumba hii nchi. Kabla ya Mwinyi hata kula ilikuwa dhiki kubwa. Mategemeo ya kuishi Mtanzania aliyakuta ni miaka 38 tu kwa kukosa lishe bora na kukosa huduma muhimu za kiafya na kijamii.

Mwinyi akabadili yote hayo na Watanzania wakaanza kuiona ahueni ya maisha.
 
Vijana wengi wamedanganywa kuhusu mambo mengi ya nchi hii. Lakini napenda kuongeza kidogo kuhusu Mzee mwinyi kisecta.

1. Miundo mbinu ...hapa Dar es salaam mwaka 1980-85 hakukua na bara bara ilokua haina mashimo, hata ile ya ikulu . Samora pale mahandaki utafikiri tuko vitani. Bara bara za mikoani zote mbovu mashimo matupu. Safari ya Tanga ilichukua masaa 12 kufika.

Alianza kujenga bara bara ile chalinze Tanga na ni moja ya roads imara zimedumu zaidi ya miaka 25 sasa.. Sio hizi za sasa za lami ya uji.
Akaendelea na roads nyengine kuanganisha nchi na Dar es salam angalau ikatwndikws road mpya kabisa sehemu kubwa ikaws afadhali.

Kwenye elimu aliruhusi private school zisaidie serikali na makanisa na taasisi nyengine zikaingia kusaidia elimu na kuondoa ukiritimba..

Afya nako ulikua mtihani mtupu madaktari bingwa wengi wamekimbia angalau wakaanza kubaki baada ya maslahi yao kuanza kuangaliwa na hospitali kujengwa mpya na kuimarishwa.

Kilimo. Hichi alikuta yu maandishi yasomekayo kilimo ndio msingi wa uchumi wetu lakini hakuna anae lima kwa uchumi...akafugua kilimo na kuanza kujitoshelza kwa chakula kwa mara ya kwanza tangu 1970.

Alikuta wafanyakazi hoi na raia waloamrishwa kufunga mikanda...sijui kama mnajua hili la kufunga mikanda...ila aliifungua akasema tafuteni muishi kama watu.

..Vyombo vya habari tukaachana na katuni za chakubanga za propaganda.
Sinema nazo tukaachana movie ya ujamaa ya .. Yombayomba...maana ni uongo vijiji vilishakufa kwa njaa..sijui kama vijana wanajua movie hii maarufu ..tukilazimishwa kwenda kuiangalia..juu ya uzuri wa ujamaa.

Hakika mwinyi tumshukuru kama sio yeye tusingekua watu free mind. Alitufungua matongo tongo akaleta mfumo wa vyama vingi , ni Baba wa mabadiliko ya kweli ya Tanzaniaa...walokuja baada yake walifunguliwa njia vizuri kuendeleza nchi na sio kurudi tena kwenye foleni ya sukari..
 

Wamesahauliwa kwa makusudi kabisa walioanza kudai uhuru Tanganyika seuse Mwinyi na mazuri yake yote.

Yakiwekwa wazi makorokocho aliyoyakuta Mwinyi na mabadiliko makubwa aliyoyafanya ya kuwatoa Watanzania kizani na kuwaweka kwenye nuru basi tutawaona wa kabla yake kuwa ni nuksi kubwa iliyowahi kuikumba hii nchi. Kabla ya Mwinyi hata kula ilikuwa dhiki kubwa. Mategemeo ya kuishi Mtanzania aliyakuta ni miaka 38 tu kwa kukosa lishe bora na kukosa huduma muhimu za kiafya na kijamii.

Mwinyi akabadili yote hayo na Watanzania wakaanza kuiona ahueni ya maisha.
 
Mwinyi hakuwa mdini kama wewe
 
Ritz kwa kusoma michango yako kwenye huu Uzi umri wako uko above 45yrs.Sijawahi kuona ukichangia kiungwana na kistaarabu kwa kiwango huko.Jukwaa la siasa limeharibu sana akili za watu.
 
Alkua anaambiwa na WB na IMF Nate anatimiza so hapakuwa na ujuzi wala ubunifu kupigia mfano!! Ruhusu demokrasia- sawa! ruhusu soko huria-sawa! nk. nk. Kuhusu legacy may be that but for me there was nothing best in particular!

Uliwahi kuisikia hotuba yake ya "mikuki miwili"?
 
Mwinyi hakuwa mdini kama wewe

Usitake kubadili mada.

Mwinyi miaka miwili tu ya mwanzo alimfunika kabisa Nyerere mpaka Nyerere akawa anaita waandishi na kuongea nao kujaribu kuuponda utawala wa Mwinyi. Lakini wapi, watu wakawa wanamuona kama comedian tu.
 
Mwinyi aliichukua nchi kutoka kwa Julius K Nyerere, nchi ambayo ilikuwa inayumba kiuchumi kutokana na kutoka kupigana vita ya kumng'oa Iddi Amin dadaa, unategemea hizo huduma mzuri na wananchi kupata chakula bora vingetoka wapi?
 
Sasa naanza kuelewa kwa nini kina Hans Pope walitaka kumpindua Nyerere. Mzee alimess up mazima na uchumi wa nchi, na maisha yakawa magumu mno. Kwa hali ilivyokuwa alikuwa hana jinsi zaidi ya kung'atuka tu.
Majalada ya kesi ya uhaini ya Mwaka 1984 yanabaki kama kumbukumbu ya jaribio la mapinduzi walilotaka kulifanya wanajeshi baada ya kuona Nyerere hakushaurika wala hakuwa na namna ya kukosolewa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…