Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

RTC halikuwa tena shirika la kusaidia wananchi bali lilikuwa ni shirika la kuwatesa wananchi kwani bidhaa zilifichwa kwa makusudi na zikatolewa kwa mlango wa nyuma kwenda mikononi mwa walanguzi.
...Kukiwa na upungufu, bidhaa hufichwa.
 
Kauli za vijana enzi za Nyerere

(1) Sea never Dry - wakimaanisha ipo siku watastowaway wapande meli wakimbie tabu za bongo

(2) One day yes - Wakimaanisha ipo siku watatoka tu


Misamiati ya wanasiasa kabla ya kuja mzee Ruksa

Mtu akiwa na hela au mambo safi ataitwa
Kabaila, Mnyonyaji, Bepari, Bwanyenye
 
Wanaomlaumu Mwinyi kutokusanya Kodi, Ni Tax base gani iliyokuwepo baada ya Mwinyi kuingia Madarakani?, kulikuwa kuna viduka vya Wahindi tu.
...Gamba, kumlaumu, hapana. Ila, ukweli ni kuwa ilibidi kodi ikusanywe kwa kiasi hicho hicho kidogo. Mbona baada ya mambo kuwa magumu kimapato ilibidi ikusanywe.

Alichokifanya Mwinyi ni kuwawezesha wananchi wawe na kipato, ili wenye kuanzisha biashara waanze, Then unatoa Tax Incentive kwa kutowatoza kodi ili Biashara zikomae, then Ukishapata watu wa kutosha wa kuwatoza kodi Unaanza kuwatoza kodi.
...Was this the prevailing policy, then? Are we just assuming?

Mkapa alipoingia Madarakani angalau aliwakuta watu wachache ambao ni Taxable, ambao walipata utajiri wao kipindi cha Mwinyi. Mzee Mwinyi hakuwa na Privilege hii, alikuta nchi hohehahe na wananchi hohehahe Angekusanya kodi kutoka kwa nani?
...Baada ya miaka yake mitano ya mwanzo, nchi ilikuwa imeiva kukusanywa kodi. Mbona hatimae ilianza kukusanywa?
 
Hawa wanajeshi walichoka na hiyo hali kina.

Hatibu Gandi au ‘Hatty Mac Ghee’, Kapteni Mohammed Tamim, Kapteni Mbogoro, Kapteni Christopher Kadege, Luteni Badru Rwechungura Kajaja na Kapteni Mapunda, Kapteni Rodrick Rosham.

Walitaka kumpindua Nyerere hali ilikuwa ngumu ya maisha.
 
mwinyi alifanya economic reforms na kuja na open up policy kwa kufungua milango ya kiuchumi Tanzania. Hili lilifanywa na nchi nyingi kipindi hicho japo Tanzania ilichelewa sana. China kwa mfano Deng Xiaoping miaka ya 1978 alileta sera hii baada ya chairman Mao Zedong kufariki, na hii ndio inasemwa kuwa ndio Turning point ya uchumi wa China ambayo ilijenga misingi ya maendeleo waliyonayo leo.
Hivyo wakati mwinyi akifungua milango hii kwa nia njema, huwenda hakuwa na wasimamizi na watekelezaji wazuri na bobevu lakini hii ilikuwa ni turufu kubwa sana ambayo pengine Leo tungekuwa tunazungumza mengine. Wakati china ikitengeneza uchumi wa kibepari wenye sifa za kisoshalisti Tanzania sisi tuliingia katika uchumi wa kibepari moja kwa moja! Legacy ya mzee ruhusa ni kubwa sana kwa sababu aliichukua nchi ikiwa katika kipindi kigumu mno cha uchumi uliokufa kabisa kuliko raisi yoyote aliyefuatia baada yake. Ni kama vile alipewa "yatima" amlee ambae hana "nguo" wala "chakula" wala "pakulala". Alijitahidi mno. na ni kipindi hiki ndipo biashara zilianza kuibuka na bidhaa zikapatikana hasa zile bidhaa msingi ambazo wakati wa nyuma zilipangiwa foleni asubuhi mpaka jioni,kuanzia sukari ,nguo,dawa ya meno nk. Kila zama na kitabu chake, kulinganishi kipindi chake na sasa kisha eti kumkosoa kuwa hakufanya kitu ni kutokumtendea haki. Alifanya kwa nafasi yake na kutokana na changamoto za wakati wake. Na laiti waliomsaidia wangemuunga mkono na pia waliofuatia kama wangeboresha zaidi pale alipoachia kwa kuweka sera endelevu na miapango ya mda mrefu, Tanzania ingekuwa "China" ya leo! Hongera mzee mwinyi ulifanya yako kwa wakati wako.
...Mchango wako ni wa muhimu.

...Naomba u edit na kuupanga kwa paragraphs ili usomeke vizuri. Sie wengine tunapata tabu kusoma mikeka ilounganishwa.
 
Binafsi japo nilikuwa mdogo nimeshuhudia muuza duka akiuawa kwa ngumi moja tu katika harakati za kumpatia huduma mwananchi ambae alihisi anabaniwa kwa wiki nzima!
pamoja ni habari kuwa na ukweli kwa 100% lakini imenifuhisha sana hakika nimecheka mpaka machozi yamenitoka
 
Wacha kuuponda uongozi wa nyerere, nyerere alijitahidi sana kwa uwezo wake
Jibu swali nimekuuliza vita vya uganda ilikuwa mwaka gani ni ilipiganwa muda gani?
 
Jibu swali nimekuuliza vita vya uganda ilikuwa mwaka gani ni ilipiganwa muda gani?
1978 hadi 1979 mbona hujauliza madhara ya hivyo vita kiuchumi kwa nchi masikini kama tanzania kipindi hicho viliiathiri vipi?
 
Kwa wale waliokuwa tayari wanaelewa nini kinaendelea duniani. Kuna kipindi miaka ya 80 mwanzoni,watoto wa shule walikuwa wanavaa magongo (viatu vya mbao), mwanafunzi akivaa raba za kenya basi darasa zima linajua kwamba yupo mwenzao ambaye Baba yake au Mama yake alikuwa ameenda safari Kenya.

Baadhi yetu ambao wazee walikuwa serikalini, siku Baba akitoka Ulaya, watoto wote hamuendi kucheza mbali, kwani mnajua tu kwamba ndani ya dakika chache baada ya baba kuwa ameshatoka bafuni, mtaitwa ili mpewe zawadi za nguo na viatu.

Hii inaonyesha scarcity kubwa sana ya vitu basic, hali ambayo kwa kweli katika miaka mitano ya mwisho ya JKN ndio ilikuwa hali halisi ya maisha.
 
Ritz, huwa nawatazama hawa watoto wa smart phones nawaona hawana ujanja wowote. Acha tu yaani, tunaongelea enzi hizo za watoto wa Oysterbay kufanya sherehe halafu sisi watoto wa upanga mashariki tunakwenda kwa miguu kwenye nyumba ya mtu fulani. Party ikimalizika kulikuwa hakuna mambo ya boda boda au bajaji, watu wakanyaga kwa miguu taratibu kutoka mitaa ya Obay, wanavuka salender Brigde wanakunja kushoto kuitafuta Aga Khan, wakivuka Gymkhana, yanakuwepo makundi mawili, mmoja linaelekea shaaban robert na jingine linakuwa ni la watoto wa mirambo na ohio kwenye maghorofa ya Railways.
Watu walikuwa wanazifuata party za usiku kwa miguu, lakini walikuwepo wezi wa magari ya baba, wanavizia wazee wamelala, wanaenda gereji wanalisukuma gari taratibu mpaka kwenye kona ya mtaa halafu ndio linawashwa. Mwenye gari mara nyingi hana hela ya mafuta, anafanya kuwaambia marafiki zake wachange ili waweze kwenda na kurudi nyumbani bila ya baba kushtukia mchezo asubuhi ya siku inayofuata.
...Acha kutukumbusha mambo hayo! Unatuhuzunisha!

...Those were the days.
 
Kauli za vijana enzi za Nyerere

(1) Sea never Dry - wakimaanisha ipo siku watastowaway wapande meli wakimbie tabu za bongo

(2) One day yes - Wakimaanisha ipo siku watatoka tu


Misamiati ya wanasiasa kabla ya kuja mzee Ruksa

Mtu akiwa na hela au mambo safi ataitwa
Kabaila, Mnyonyaji, Bepari, Bwanyenye
Vijana wengi waliopanda meli na wale waliotoroka kupitia mipaka ya nchi hii, walifanya hivyo katika miaka ya mwisho ya JKN na ya mwanzo ya AHM. Enzi hizo ndio ulikuwa wakati ambao watoto wa kishua walikuwa wapo tayari kuuza hata masinki, mafriji na magari ili mradi wapate nauli za kuondokea nchini.
 
1978 hadi 1979 mbona hujauliza madhara ya hivyo vita kiuchumi kwa nchi masikini kama tanzania kipindi hicho viliiathiri vipi?
Vita imepiganwa miezi 8 Nyerere katawala miaka 23 kwa faida ya JF tufahamishe athari zake.

Kama una michango na hoja weka watu wakusome siyo kushambulia watu.
 
Vita imepiganwa miezi 8 Nyerere katawala miaka 23 kwa faida ya JF tufahamishe athari zake.
Kumbe ulivyokuwa una shadadia kwa mbwembwe hujui nini na vipi uchumi wetu uliyumba baada ya serikali ya marehemu jk nyerere kugharamia vita ya kumfunza adabu nduli Amini?
 
Kumbe ulivyokuwa una shadadia kwa mbwembwe hujui nini na vipi uchumi wetu uliyumba baada ya serikali ya marehemu jk nyerere kugharamia vita ya kumfunza adabu nduli Amini?
Haya umeshinda ngoja mie nikae pembeni wengine watakujibu.
 
Kumbe ulivyokuwa una shadadia kwa mbwembwe hujui nini na vipi uchumi wetu uliyumba baada ya serikali ya marehemu jk nyerere kugharamia vita ya kumfunza adabu nduli Amini?

Yote hayo aliyataka Nyerere mwenyewe, aliwapa hifadhi waasi wa Uganda Kina Museveni tangu miaka ya Sabini, wakawa wanaleta chokochoko ndani ya Uganda, wewe unafikiri Iddi Amin dadaa kama Raisi wa Uganda angefanyaje?
 
Yote hayo aliyataka Nyerere mwenyewe, aliwapa hifadhi waasi wa Uganda Kina Museveni tangu miaka ya Sabini, wakawa wanaleta chokochoko ndani ya Uganda, wewe unafikiri Iddi Amin dadaa kama Raisi wa Uganda angefanyaje?
Tukuulize wewe
 
Inaposemwa mfumo wa vyama vingi ulirudi tena mwaka 1992, huenda vijana wadogo wanashindwa kuelewa. Ni kwamba Vyama vingi vilikuwepo hadi mwanzoni mwa miaka ya uhuru lakini Serikali ya Nyerere ikavifutilia mbali.
 
Yaani unajiuliza kuhusu legacy ya mzee wa Ruksa? Unajua kwa nini alipachikwa jina hilo ama ulikuwa hujazaliwa?


Luksa maana yake "holela". Kama ndicho hicho unamaanisha tuko wote. Lakini pia kwa nyongeza, wakati wa Mwinyi ndipo:-

1. Vita ya maguruwe ikiongozwa na ustaadhi Rashid sijui nani iliibuka na kuzimwa na ushupavu wa Augustin Mrema.

2. Nicho kipindi shule za Kikristo zilichomwa moto na kupoteza uhai wa watoto wengi wasiokuwa na hatia.

3. Hapo hapo ndipo tuliona urasmishaji wa makundi ya balukta, wenye surualil fupi.

4. Wakati ule ndipo makundi ya mujahidina yalifahamika rasmi.

5. Waraka wa Kigoma Malima ulioasisi ukakasi kwa elimu yetu.

6 Alimpa jina kubwa sana Mheshimiwa Mkapa baada ya yeye kuondoka kwa sababu alichokifaya kilibainisha tofauti ya tawala hizi mbili katika mambo mengi.

Naomba mwenye mazuri mengine tuendee kuchangia.
 
Back
Top Bottom