Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Wala nisiende mbali, chuki sio kupigana makonde tuu, chuki ipo hata kwenye matamshi ya mtu. Lema aliposema utapata baraka kwa Mungu ukimzomea Lowassa. Wewe kwa mtazamoa wako yale maneno yalikuwa ni chuki, kejeli, utovu wa nidhamu au labda kwa mtazamo wa upinzani ule ulikuwa ni ujasiri? kauli nyingi za upinzani zimejazwa chuki ambazo ukiwauliza ni za nini, wanakosa majibu. Hivi, mtu mwenye akili timamu anaweza kusimama hadharani ukasema nimeota mtu fulani atakufa?, unaweza kutumia kauli hiyo kwa mtoto aliye mzaa? au unaweza kuwaambia wanafamilia nimeota baba yetu atakufa? kama sio chuki ni nini?

Sina hakika na kile unachowaza kama kina uhalisia, pia sina hakika kama unajua maana ya chuki? Labda nikuelezee kilichomtokea Lema, LEMA HAKUOTA NDOTONI WALA HAKUTUMIWA SMS BALI ALIPATA "MAONO" YENYE MAAGIZO FULANI NA HAKUA NA BUDI KUYAFIKISHA KWA MHUSIKA. RAIS WAKO ANAJUA MAONO NI KITU GANI NA ANAMJUA MUNGU KAMA UNAVYOMSIKIA KILA MARA AKISEMA YEYE NI MPENZI WA MUNGU PALE ANAPO SEMA KWELI HIVYO ANAJUA NJIA ZA MUNGU KUWASILIANA NASI NA MOJA WAPO NI HIYO YA MAONO. ENDAPO ANGESEMA HATA MIMI NILIONGEA NA MUNGU AJANIAMBIA JUU YA MAONO YAKO TUNGEAMINI KWELI LEMA KATUCHANGANYA LAKINI YEYE KAMFUNGA KWA SABABU ZAKE BINAFSI HATA WEWE HUZIJUI,.

MWISHO WA SIKU TUSEME MJUMBE KAFUNGWA, HUKU KWETU TUNASEMAGA MJUMBE HAUWAWI LAKINI HUYU ALMANUSURAH AUWAWE.

NIMALIZIE TU KUSEMA HAINA HAJA YA NGUVU KUBWA SANA KUJUA NANI MWENYE CHUKI, KAMA HATA KUJULIANA HALI KAMA WATU WA TAIFA MOJA NI USALITI BASI HIYO NDIYO CHUKI NA SIO KINGINE.
 
Sina hakika na kile unachowaza kama kina uhalisia, pia sina hakika kama unajua maana ya chuki? Labda nikuelezee kilichomtokea Lema, LEMA HAKUOTA NDOTONI WALA HAKUTUMIWA SMS BALI ALIPATA "MAONO" YENYE MAAGIZO FULANI NA HAKUA NA BUDI KUYAFIKISHA KWA MHUSIKA. RAIS WAKO ANAJUA MAONO NI KITU GANI NA ANAMJUA MUNGU KAMA UNAVYOMSIKIA KILA MARA AKISEMA YEYE NI MPENZI WA MUNGU PALE ANAPO SEMA KWELI HIVYO ANAJUA NJIA ZA MUNGU KUWASILIANA NASI NA MOJA WAPO NI HIYO YA MAONO. ENDAPO ANGESEMA HATA MIMI NILIONGEA NA MUNGU AJANIAMBIA JUU YA MAONO YAKO TUNGEAMINI KWELI LEMA KATUCHANGANYA LAKINI YEYE KAMFUNGA KWA SABABU ZAKE BINAFSI HATA WEWE HUZIJUI,.

MWISHO WA SIKU TUSEME MJUMBE KAFUNGWA, HUKU KWETU TUNASEMAGA MJUMBE HAUWAWI LAKINI HUYU ALMANUSURAH AUWAWE.

NIMALIZIE TU KUSEMA HAINA HAJA YA NGUVU KUBWA SANA KUJUA NANI MWENYE CHUKI, KAMA HATA KUJULIANA HALI KAMA WATU WA TAIFA MOJA NI USALITI BASI HIYO NDIYO CHUKI NA SIO KINGINE.

Hivi umesha pitia nyuzi za wana chadeama kwenye mitandao ya kijamii, na kujionea kauli zinazo toka huko ikiwa zingine ni vitisho na kebehi kwa wana CCM? Ni dhahiri unajarubi kumtetea Lema, mimi hilo sina pingamizi nalo ni haki yako. Lakini uliona wapi mtu anamtabiria kifo rafiki yake? mara nyingi watu humtabiria kifo adui yake ili wapate nafasi ya kufanye yale wanayo yataka pindi adui yao anapo toweka. Sasa kama wewe unaona Lema ni mtu msafi kiasi cha kuwa karibu na Mungu na Mungu huyo huyo akaamuwa kutowa ujumbe kupitia Lema, hapo napata picha nina ongea na mtu wa aina gani.
 
duh yaani kusalimiwa ndo watu mnalalamika hivi...
acheni basi wakuu...
 
Hivi umesha pitia nyuzi za wana chadeama kwenye mitandao ya kijamii, na kujionea kauli zinazo toka huko ikiwa zingine ni vitisho na kebehi kwa wana CCM? Ni dhahiri unajarubi kumtetea Lema, mimi hilo sina pingamizi nalo ni haki yako. Lakini uliona wapi mtu anamtabiria kifo rafiki yake? mara nyingi watu humtabiria kifo adui yake ili wapate nafasi ya kufanye yale wanayo yataka pindi adui yao anapo toweka. Sasa kama wewe unaona Lema ni mtu msafi kiasi cha kuwa karibu na Mungu na Mungu huyo huyo akaamuwa kutowa ujumbe kupitia Lema, hapo napata picha nina ongea na mtu wa aina gani.

Lema hajawai kuwa mtabiri, lema alipata maono na ndio maana hajajiItaja kuwa yeye ni nabii. Kumbuka maono anaweza kupata mtu yeyote yule kulingana na Mungu anavyotaka.. Tangu lini dola ikatishiwa na upinzani? haiwezekani labda waasi ndio wanaweza kuitisha dola.
 
It does not help you can still make an application for the Court of appeal to make a review of the same!
Aiseee!!! nawashauri wanasheria wa Lema wafanye hiyo kitu haraka ili tupate hiyo hukumu! Ahsante sana kwa kunihabarisha!!
 
Hawa ni yule mnyama asiye na kumbukumbu husahau baada ya sekunde tu. Kwani yeye Lema mwenyewe anahubiri upendo na amani? Akwende zake amuache Rais wetu kipenzi afanye kazi. Hamna jipya nyie.
 
Kwani wewe unahubiri upendo toka lini hata utake Rais ahubiri upendo? Kazi ni moja tu hadi muwe na adabu na heshima kwa Mkuu wa nchi. Mlizoea kumtukana Kikwete sasa mmekutana na mwamba. Sifa zote mlizotaka kwa Rais ajae zipo kwa Mr. President JPM
 
Kama ungekuwa unatumia lugha za kistaarabu kiasi hiki tangu awali basi unge epuka kadhia iliyokukuta. Mwanzo mzuri Kamanda na ujumbe utafika. Bila shaka hautakamatwa there is nothing wrong in it, hakuna kuombeana vifo humu. Kweli Jela yastahili kuitwa chuo cha mafunzo a.k.a The Correction Centre.
 
Nyerere alitoa mfano mfupi tu akasema.. Kwa nchi changa kama hii tukikumbatia ukabila tutaangamia, alikuwa na maana ya vitu kama ukabila (wakati huo wa chama kimoja ) usitutenganishe... Mzaramo aende kuoa kule chato. Mtukufu Tafadhali njoo urekebishe kauli yako...
 
Ukabila haufai!..aache upendeleo na chuki kwa wasio wa upande wake
 
Huwezi ukamtukana, kumvunjia Heshima, Au kumdharau Rais,Mwenyekiti wa chama cha hao wabunge, Halafu
hao wabunge waje kukupongeza au kukusalimia kwa mbwembwe!!
Hii inaonyesha na wao wapo kundi moja la kumdharau Rais na Mwenyekiti wao wa chama.

Yote na yote Pongezi kwa kujua huyu ni Mh Rais
safi sana
naona sasa umeanza kujitambua.
Lema Magufuli ndiye Rais wa Tanzania kwa sasa
umpende usimpende ndiye Rais wako,
Jaribu kuwa Na Heshima kwa Mamlaka
nadhani sasa ataelewa nini mana ya upendo. kudharau mamlaka hata kama zinamapungufu. si upendo huo.
 
Mh Rais Magufuli nakusalimu.

Nimetoka Magereza hivi karibuni ambako nilikuwa huko kwa zaidi ya miezi minne kwa kunyimwa masharti ya dhamana kwa dhamana iliyokuwa wazi.

Mh Rais, nimeona kwenye vyombo vya habari leo kuwa kwamba wale Wabunge waliokuwa wanataka kunisalimia nilipokuwa Magereza kuwa ni wasaliti wa chama cha CCM, Mh Rais wengi walinisalimia, Wachungaji, Masheikh, Wabunge na Viongozi mbali mbali, sidhani kama hatua hii ilikuwa ni usaliti isipokuwa upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yoyote haswa wakati wa matatizo.

Mh Rais, nimeogopa sana kwa kauli hii yako, je Taifa linakwenda wapi, hivi kweli sisi Wabunge ni maadui? Kama viongozi tutafikiri utengano ni moja ya njia ya kuimarisha vyama vyetu, basi bila shaka tutakuwa tunalitendea Taifa ubaya .

Dhambi hii ikikomaa basi ni hakika kwamba lugha za udini, ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa, ni muhimu sasa tukajenga utamaduni wa kuhimiza mshikamano wa Kitaifa bila kujali itikadi kama kweli tunawapenda masikini na wanyonge wa nchi hii.

Nawaomba Wabunge wenzangu walionijali wakati niko magereza wasijisikie vibaya kwani walifanya jambo jema na muhimu kwa wakati muhimu sana katika maisha yangu, ninatarajia kuwa Spika wa Bunge atatoa kauli juu ya kauli yako.

Mh Rais wakati wa Msiba wa Christina Lissu dada yake na Mh Tundu Lissu nilikuona katika msiba ule wewe na Mama yetu Mke wako, je Mh Rais na wewe ulikuwa unasaliti Chama chako?

Mh Rais neno la Mungu linasema, Wapendeni maadui zenu, waombeni wanaowauzi , wabarikini wanaowaonea kwani kufanya hivi ni kuishi kwa thawabu za Mwenyezi Mungu.

Mungu akubariki sana, natumaini Mh Rais sitakamatwa leo kwa ujumbe huu mfupi.


Godbless J Lema (MB)
Wabunge wa UKAWA walipozuiliwa kuwa na mahusiano na wa CCM ulikuwa umezaliwa?
 
Jameni pa moja na kujadili mambo ya siasa,mkumbuke Yesu yu karibu kurudi.Msipoteze muda mwingi kwenye mambo ya kupita,wengine pressure ziko juu.Yesu ndiyo kimbilio pekee,wanadamu wanaweza kubadilika lakini Yesu habadiliki.Wanadamu wanaweza wakakuahidi wasitende lakini ahadi za Mungu ni hakika na kweli.
Je leo umemshukuru Mungu walau umeamka mzima?
 
Siasa kweli si uadui ila kwa Watanzania ni uadui maana ukiona jinsi mifumo ya nchi inavyofanya kazi katika utekelezaji wa majukumu yao ni dhahiri 'SIASA TANZANIA NI UADUI' Mfano; Mkuu kusema waliokwenda kumpa Lema hi! akiwa lupango eti ni usaliti. Jamani kivipi inakuwa usaliti kisa vyama tofauti.
 
Mh Rais Magufuli nakusalimu.

Nimetoka Magereza hivi karibuni ambako nilikuwa huko kwa zaidi ya miezi minne kwa kunyimwa masharti ya dhamana kwa dhamana iliyokuwa wazi.

Mh Rais, nimeona kwenye vyombo vya habari leo kuwa kwamba wale Wabunge waliokuwa wanataka kunisalimia nilipokuwa Magereza kuwa ni wasaliti wa chama cha CCM, Mh Rais wengi walinisalimia, Wachungaji, Masheikh, Wabunge na Viongozi mbali mbali, sidhani kama hatua hii ilikuwa ni usaliti isipokuwa upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yoyote haswa wakati wa matatizo.

Mh Rais, nimeogopa sana kwa kauli hii yako, je Taifa linakwenda wapi, hivi kweli sisi Wabunge ni maadui? Kama viongozi tutafikiri utengano ni moja ya njia ya kuimarisha vyama vyetu, basi bila shaka tutakuwa tunalitendea Taifa ubaya .

Dhambi hii ikikomaa basi ni hakika kwamba lugha za udini, ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa, ni muhimu sasa tukajenga utamaduni wa kuhimiza mshikamano wa Kitaifa bila kujali itikadi kama kweli tunawapenda masikini na wanyonge wa nchi hii.

Nawaomba Wabunge wenzangu walionijali wakati niko magereza wasijisikie vibaya kwani walifanya jambo jema na muhimu kwa wakati muhimu sana katika maisha yangu, ninatarajia kuwa Spika wa Bunge atatoa kauli juu ya kauli yako.

Mh Rais wakati wa Msiba wa Christina Lissu dada yake na Mh Tundu Lissu nilikuona katika msiba ule wewe na Mama yetu Mke wako, je Mh Rais na wewe ulikuwa unasaliti Chama chako?

Mh Rais neno la Mungu linasema, Wapendeni maadui zenu, waombeni wanaowauzi , wabarikini wanaowaonea kwani kufanya hivi ni kuishi kwa thawabu za Mwenyezi Mungu.

Mungu akubariki sana, natumaini Mh Rais sitakamatwa leo kwa ujumbe huu mfupi.


Godbless J Lema (MB)

Mkuu Karibu uwatumikie wapiga kura wako kwa kasi sasa.

Ujumbe wako umefika.

My Take;

Twende mbele turudi nyuma me bado na mashaka na viongozi walio chini yake na wanao mletea hizo Informations zote kwa imani yangu wanampoteza Rais kabisa nahisi kunawatu bado wanamakundi makubwa ndani ya CCM na wanachomeana sana kwa JPM uhasama ndani ya serikali mpaka kupakaziana nyie ni viongozi wa nchi hii mjitambueni Jamani hii ni Tanzania yetu sote. Mmekuja na slogan KAZI KWANZA matokeo yake mnatuvuruga ni are?

Mkianza zambi ya kubaguana ati wao ni CCM sie ni CUF,CDM, ACT itawakula mpaka mjute na hizo ndimi zenu za kuchonganisha nyie kwa wenyewe. Kumbukeni wabunge nyie ni Taasisi na mhimili mwingine sasa vuruganeni mtashangaaa
 
Vyama vya upinzani havina budi kuungana na kuwa na tamko moja juu ya haya yanayofanywa na mzee
 
Lema fanya yako..Jimboni hakuna maji ya uhakika wala umeme!Miundo mbinu ya shida na vijana wengi hawana ajira!Ila kila siku una deal unarukia yasiyokuhusu..Fanya yako na shughulikia kero za wananchi wako!Period

Ukisha kuwa kiongozi wa mahali na umechaguliwa na wananchi wako iwe ni CCM CUF ACT NCCR we ni kiongozi wa wote sasa Kama kiongozi wa nchi ananza kuwavuruga hao viongozi itakuwaje so me ni CCM we ni CUF huyu kiongozi atatuongoza vipi,hili nalo ni tatizo pia

POLITICS IS BATTLE OF IDEAS
 
Back
Top Bottom