Lema na ndoto hizi dhidi ya Rais, sheria ifanye kazi, tumemchoka

Lema na ndoto hizi dhidi ya Rais, sheria ifanye kazi, tumemchoka

Wadau heshima kwenu.
Hivi scorpion akisema nimeota nakutoboa macho utajiskiaje?

Kwanza scorpion anamwamini mungu, inaweza kuwa ni ganja analopata kabla ya kuingia mtaani lakini ndio inaweza kuwa imani yake.

Inapotokea mtuhumiwa wa vitendo viovu, kwamba kihistoria mtu huyu aliwahi kukamata chuma akakuotea kuwa kazi anairudia, utajiskiaje?

Hiyo ni utangulizi, lakini sema kweli ndoto zote tungekuwa tunaziweka hadharani basi dunia hii isingeishika,

Naiomba mamlaka imchukulie hatua kali Ili iwe fundisho, haiwezekani mnaamua tu kumsingizia Mungu tutajuaje kama mnasuka mpango dhidi ya Rais wetu.

Binafsi nasema hapana, enough is enough. This is too much, bado tunamhtaji sana Rais Magufuli, yeye kama miradi yake haiendi basi aiweke ktk mfumo mzuri alipe kodi basi.

Maneno anayoendelea kuyaongea yanatia hofu na lengo lake hasa ni nini,
Unajua lazima utumie akili sana kuandika heading, kinyume cha hapo unaondoa maana yote ya habari, na ujue hata mwanzo uanzaje ili umvutie msomaji. Yaani umefeli kote, ndio maana wanataka iwepo ithibati kwa ajili ya wajinga wachache kama nyie. Kwanza umeanza na ndoto, tayari ni vitu vya kusadikika na havina uhalisia. Ebu jaribu kama ungeanza na Tamko, maana nyuma yake kunautekelezaji. Ukafuatia na Scorpion akiota ndoto, eti nitakutoboa macho, sioni linganishi yako na ndoto ya Mh Lema, kwanza Scorpion anatuhuma za kumtoboa mtu macho, ambazo hazijathibitishwa na mahakama ili ziwe kweli, huenda nazenyewe zikawa uongo. Nakuomba sana, kabla haujanzisha thread uwe na akili ya kushilikisha na jua mko wengi kwenye upande wenu, usiogope kuonekana huna akili, au malipo yako yatapungua ndio uone bora ulete maada dhaifu kiasi hiki. Eti sheria ifuate mkondo, basi ungetupa hata vifungu baadhi ya hiyo sheria ili tuvijue na sisi tusije simulia ndoto zetu, kwa maana biblia inasema siku za mwisho Wazee wataota ndoto, na vijana watafasiri na kutoa maono, angalieni asema Bwana wa Majeshi ambae kwake kila goti litapigwa, nawasilisha.
 
Wadau heshima kwenu.
Hivi scorpion akisema nimeota nakutoboa macho utajiskiaje?

Kwanza scorpion anamwamini mungu, inaweza kuwa ni ganja analopata kabla ya kuingia mtaani lakini ndio inaweza kuwa imani yake.

Inapotokea mtuhumiwa wa vitendo viovu, kwamba kihistoria mtu huyu aliwahi kukamata chuma akakuotea kuwa kazi anairudia, utajiskiaje?

Hiyo ni utangulizi, lakini sema kweli ndoto zote tungekuwa tunaziweka hadharani basi dunia hii isingeishika,

Naiomba mamlaka imchukulie hatua kali Ili iwe fundisho, haiwezekani mnaamua tu kumsingizia Mungu tutajuaje kama mnasuka mpango dhidi ya Rais wetu.

Binafsi nasema hapana, enough is enough. This is too much, bado tunamhtaji sana Rais Magufuli, yeye kama miradi yake haiendi basi aiweke ktk mfumo mzuri alipe kodi basi.

Maneno anayoendelea kuyaongea yanatia hofu na lengo lake hasa ni nini,
Kwani rais hawezi otwa na mtu wa jinsi nyingine?Udogo wa akili na kujipendekeza ndio kunawapa huu ujinga.
 
Lema bila mashaka ataota na kupewa maono ya ni lini atapata dhamana
 
Kwani kufa si ni kufa tu.....

Utabiriwe usitabiriwe kufa ni kufa tu anya time unaeza enda.......

Ata wewe mleta mada unaeza danja kabla ya kusoma komenti za wadau hapa ...........
Embu tabiri na wewe basi tuone..
 
Spencer usipende kuzungumzia nafsi za watu wengine Lema hatujamchoka ila wewe ndiyo umemchoka rais ni wako wewe na sababu za kumpenda ni zako nadhani ulisoma na kiswahili unakielewa unapoandika tumia umoja siyo wingi usilazimishe na wengine kwa mapenzi na faida unayopata wewe.
.
 
Itakuwa hiyo siku kabla hajaenda kulala alikula ganja sana ndizo zilizomfanya aote hiyo ndoto ya kishetani, tumdharau tu, hana lolote analoweza fanya.
 
Unajua lazima utumie akili sana kuandika heading, kinyume cha hapo unaondoa maana yote ya habari, na ujue hata mwanzo uanzaje ili umvutie msomaji. Yaani umefeli kote, ndio maana wanataka iwepo ithibati kwa ajili ya wajinga wachache kama nyie. Kwanza umeanza na ndoto, tayari ni vitu vya kusadikika na havina uhalisia. Ebu jaribu kama ungeanza na Tamko, maana nyuma yake kunautekelezaji. Ukafuatia na Scorpion akiota ndoto, eti nitakutoboa macho, sioni linganishi yako na ndoto ya Mh Lema, kwanza Scorpion anatuhuma za kumtoboa mtu macho, ambazo hazijathibitishwa na mahakama ili ziwe kweli, huenda nazenyewe zikawa uongo. Nakuomba sana, kabla haujanzisha thread uwe na akili ya kushilikisha na jua mko wengi kwenye upande wenu, usiogope kuonekana huna akili, au malipo yako yatapungua ndio uone bora ulete maada dhaifu kiasi hiki. Eti sheria ifuate mkondo, basi ungetupa hata vifungu baadhi ya hiyo sheria ili tuvijue na sisi tusije simulia ndoto zetu, kwa maana biblia inasema siku za mwisho Wazee wataota ndoto, na vijana watafasiri na kutoa maono, angalieni asema Bwana wa Majeshi ambae kwake kila goti litapigwa, nawasilisha.

Kwa utoaji.wake wa taarifa ulizingatia hayo?
 
Spencer usipende kuzungumzia nafsi za watu wengine Lema hatujamchoka ila wewe ndiyo umemchoka rais ni wako wewe na sababu za kumpenda ni zako nadhani ulisoma na kiswahili unakielewa unapoandika tumia umoja siyo wingi usilazimishe na wengine kwa mapenzi na faida unayopata wewe.
.

Umenikata nini na wewe umeandika nini
 
Na siku Kekule naye aliota structure ya molecule ya carbon. Alikuwa anasumbuliwa sana na jambo hili ktk utafiti wake wa kikemia. Alipotoka party usiku alilala akaota nyani 6 wameshikana mikono wanazunguka. Alipoamka tayari alikuwa na hiyo formula inayotumika hadi leo. Ndoto bwana ni ajabu.
 
Na siku Kekule naye aliota structure ya molecule ya carbon. Alikuwa anasumbuliwa sana na jambo hili ktk utafiti wake wa kikemia. Alipotoka party usiku alilala akaota nyani 6 wameshikana mikono wanazunguka. Alipoamka tayari alikuwa na hiyo formula inayotumika hadi leo. Ndoto bwana ni ajabu.

Ndoto nzuri hiyo, ndoto ya kuotea mwenzio mauti inastahili kukemewa.

Ndio maana yeyote anayeintertain anafaaa kuhifadhiwa sero ni mtu hatari huyo
 
Kuna aina 3 za ndoto. Ndoto zitokazo kwa Mungu zenye ujumbe ambao unafunua sehemu ya yaliyomo ktk moyo wa Mungu. Mf Malaika alimtokea Yusufu ktk ndoto akimwonya asimwache Mariamu maana mimba yake ni kwa uweza wa Mungu.
Aina ya 2 ya ndoto ni zile zitokazo kwa shetani adui wa roho ya mwanadamu. Lengo la ndoto hizi ni kuvunja moyo, kunajisi, kuvuruga makusudi mema ya Mungu.
Aina ya 3 ni ndoto za uchovu. Huitwa ndoto za shughuli nyingi.
Hivyo hapo panahitaji kupambanua
 
Kuna aina 3 za ndoto. Ndoto zitokazo kwa Mungu zenye ujumbe ambao unafunua sehemu ya yaliyomo ktk moyo wa Mungu. Mf Malaika alimtokea Yusufu ktk ndoto akimwonya asimwache Mariamu maana mimba yake ni kwa uweza wa Mungu.
Aina ya 2 ya ndoto ni zile zitokazo kwa shetani adui wa roho ya mwanadamu. Lengo la ndoto hizi ni kuvunja moyo, kunajisi, kuvuruga makusudi mema ya Mungu.
Aina ya 3 ni ndoto za uchovu. Huitwa ndoto za shughuli nyingi.
Hivyo hapo panahitaji kupambanua

Ni rahisi sana kujua kama ndoto ile ya kimungu au kishetani.
 
Kuna watanzania wengi wamejaa magerezani as Mahabusu siku na siku,mara upelelez bado haujakamilika,file lipo kwa DPP,sijui mashahidi hawajatimia,hakimu ana dharura,mpelelez ana udhuru,wamejaa hawana wa kuwaskiliza
 
Back
Top Bottom