Lengai Ole Sabaya aachiwa Huru kwa sharti la kutofanya kosa la Jinai kwa kipindi cha mwaka mmoja
Ila kajifunza
Sio kwamba waliamua kumtunza kwa muda huko ili kukidhi shauku ya raia wengi waliotaka kuona Sabaya akiwajibishwa kwa makosa yake baada ya MZEE kufariki?

Hasa ukiangalia namna walivyolimaliza hili swala.
 
Wadau nawasabahi.HATIMAYE DC MSTAAFU wa Hai GEN.SABAYA yupo HURU pamoja na Kesi zote 3 kumkabili na AMEZIMALIZA kwa KUKIRI MAKOSA kwa DPP na KUACHIWA HURU kwa STAILI ya PLEA BARGAINING.
Sasa nimeamini UKIFUNGWA TANZANIA ni UZEMBE wako.Moja ya Makosa ya GEN SABAYA ni KUONGOZA GENGE la UHALIFU kwa kutumia SILAHA kosa ambalo ni KUBWA lakini AMEKIRI na kuachiwa HURU.Watanzania Tutarajie MAJAMBAZI Mafisadi Wahujumu Uchumi Wauza Madawa hakuna ATAKAYEFUNGEA kwa Mtindo huu wa "PLEA BARGAINING"
Narudia tena UKIFUNGWA TANZANIA ni UZEMBE WAKO kwani PLEA BARGAINING ni OFFER kwa WAHALIFU
20230405_152145.jpg
 

Hatimae haki imetendeka,njia zote haramu za kukukomoa zimeshindikana!
"Kweka" na Baba mkwe Gang wa Hai,leo ni siku mbaya kwenu!
Walamba Asali mjifunze kwamba kuna siku moja pia itatokea!

Tunaomba ripoti ya CAG ijadiliwe kwa Uhuru kabisaa!

Mungu ni ni Mwema...
Karibu Uraiani Jemedari Sabaya!
Future yako bado ipo kubwa kabisa kwenye siasa,Achana na CCM ya asali Boyz kwa sasa!

Utumishi na uhusika wa kweka kwenye hili unapaswa kuchunguzwa,hata kama si leo,jinai huwa haiozi.
 
Sheria ni za watu masikini?

Ukate watu masikio na miguu, upige watu, upore mali za watu na bado unaambiwa upo huru....
Hapo hata mm sijaridhika. Lkn nadhani kesi bado inaendelea kaachiwa kwa maana ya kupewa dhamana baada ya makosa ya uhujumu uchumi kufutwa ambayo kisheria hayana dhamana. Kinyume na hapo itakuwa ni dhuluma kwa waathirika.
 
aise hii Nchi mbona tamu sana ?

unakula milioni 50 unalipa faini ya milioni 5 ?

Wazee tuingie mzigoni mambo iko huku
 
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, ambaye amekuwa akikabiliwa mashtaka saba ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu leo Aprili 05, 2023 ameachiliwa huru.


Taarifa zaidi zitakujia hapa hapa baadae.

Chanzo: Jambo TV

===

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, leo April 5, 2023 ameachiliwa huru na mahakama baada ya kufutiwa mashtaka saba yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu.

Mahakama imetoa uamuzi wa Lengai Ole Sabaya kulipa kiasi cha shilingi milioni 5 kama fidia kwa mwathirika na hapaswi kufanya kosa lolote la jinai kwa muda wa mwaka mmoja.

Sabaya ambaye mapema asubuhi ya leo alifika kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Moshi, kabla uamuzi wa kuachiwa haujatangazwa, kupitia Kifungu cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai namba 91 kifungu cha 1A, kesi yake ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2022 ilifanyiwa marejeo kama upande wa mshtakiwa ulivyoomba.

Mawakili upande wa Jamhuri waliiomba mahakama kubadilisha mashtaka ya Lengai Ole Sabaya kutoka kuwa ya kesi ya Uhujumu Uchumi na kufungua kesi yenye Mashtaka ya Makosa ya Jinai baada ya Lengai Ole Sabaya kuomba kufanya mazungumzo nje ya mahakama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Ombi hilo la Sabaya lilikubaliwa na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Salome Mshasha baada ya Mawakili wa Lengai Ole Sabaya kuridhia na kufutwa kwa kesi yake namba 2 ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2022.

Baada ya kuridhia hilo, kesi mpya aliyofunguliwa Sabaya ni kesi kesi ya Jinai Namba 31/2023 ambayo ndani yake kulikuwa na mashtaka mawili mapya dhidi yake, kosa la kwanza likiwa ni kuchukua madaraka ambayo siyo yake.

Imeelezwa kuwa Lengai Ole Sabaya na wenzake, Januari 19, 2021 katika eneo la Masama Mbosho wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, bila kibali walivamia duka la Alex Evarest SwaI na kuchukua mali na kuzizuia na kujipatia kaisi cha fedha shilingi milioni 50.

Kosa la pili ni kuzuia upatikanaji wa haki ambapo Januari 19, 2021 katika maeneo tofautitofauti katika Wilaya ya Hai na Tulia jijini Arusha na maeneo tofauti ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, walikula njama za kumfanya Alex Swai kuwa ametenda kosa la kukwepa kodi.

Baada ya kusomewa mashtaka, Sabaya alikiri kufanya makosa yote hayo mawili mbele ya hakimu Salome Mshasha.


God is good all the time
 
Jamani kiswahili chetu mara nyengine kinaleta matatizo kwa sababu hatuna maneno sahihi ya kutumia katika situation fulani fulani. Sasa kama hapa penye taarifa hii. Neno kuachiliwa huru hapa linatatiza maana hakuna mahali inaposema kuwa amefutiwa mashitaka yake, kwa maana hiyo huwezi kusema kuwa yuko huru ikiwa ametolewa jela kwa dhamana na anangoja kesi yake itajwe tena. Mtu kuwa huru ni kuwa unaweza kufany autakalo na kwenda utakako bila ya kuviarifu vyombo vya dola na kuruhusiwa.

Labda wanaotuma hizi taarifa watueleze kuwa huyu mtu yuko huru wakimaanisha hana kesi tena na yuko huru kufanya yake kama watanzania wenzake au yuko nje kwa dhamana na masharti?
Uko sahihi mkuu. Kesi bado inaendelea kaachiwa kwa maana ya kupewa dhamana baada ya makosa ya uhujumu uchumi kufutwa ambayo kisheria hayana dhamana.

Sasa wasioujua kusoma na wakrupukaji wanapotosha.
 
MAANA PANA YA HUKUMU YA LEO
Nini maana ya hukumu hii ya kihistoria dhidi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya Lengai Ole Sabaya baada ya kukiri kosa, kutiwa hatiani na kupewa adhabu ya kulipa faini na kuachiwa toka magereza kwa masharti.

Sasa mkuu huyu wa wilaya wa zamani hataweza kuteuliwa kushika nafasi ktk ofisi ya umma wala kugombea nafasi ya kisiasa kutokana na kupatikana na hatia kesi yake ilipokuwa inasikilizwa.

5 Apr2023
#BREAKING: SABAYA AACHIWA HURU BAADA ya KUSOTA MAHABUSU MIAKA 2...


Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, leo April 5, 2023 ameachiliwa huru na mahakama baada ya kufutiwa mashtaka saba yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu. Mahakama imetoa uamuzi wa Lengai Ole Sabaya kulipa kiasi cha shilingi milioni 5 kama fidia kwa mwathirika na hapaswi kufanya kosa lolote la jinai kwa muda wa mwaka mmoja
 
MAANA PANA YA HUKUMU YA LEO
Nini maana ya hukumu hii ya kihistoria dhidi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya Lengai Ole Sabaya baada ya kukiri kosa, kutiwa hatiani na kupewa adhabu ya kulipa faini na kuachiwa toka magereza kwa masharti.

Sasa mkuu huyu wa wilaya wa zamani hataweza kuteuliwa kushika nafasi ktk ofisi ya umma wala kugombea nafasi ya kisiasa kutokana na kupatikana na hatia kesi yake ilipokuwa inasikilizwa.

5 Apr2023
#BREAKING: SABAYA AACHIWA HURU BAADA ya KUSOTA MAHABUSU MIAKA 2...


Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, leo April 5, 2023 ameachiliwa huru na mahakama baada ya kufutiwa mashtaka saba yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu. Mahakama imetoa uamuzi wa Lengai Ole Sabaya kulipa kiasi cha shilingi milioni 5 kama fidia kwa mwathirika na hapaswi kufanya kosa lolote la jinai kwa muda wa mwaka mmoja
Una maanisha mbowe nae hataweza kugombea nafasi yoyote? Maana alikutwa na hatia
 
Inamaana gani kupigwa faini ya 5mn Tano kama hakukutwa na hatia alafu achiwe Tena kwa masharti
SABAYA hajapatikana na hatia wala hajaombewa msamaha na walamba asali akina ZITTO au Askofu Shoo. Mwana ume ni kushina kesi sio kulamaba asali ikulu. Ok
 
Back
Top Bottom