Lengai Ole Sabaya aachiwa Huru kwa sharti la kutofanya kosa la Jinai kwa kipindi cha mwaka mmoja
Mamlaka imeamua kunsamehe tu.....ashukuru Sana connection zake za kifamilia huko Ccm.
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, ambaye amekuwa akikabiliwa mashtaka saba ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu leo Aprili 05, 2023 ameachiliwa huru.

View attachment 2577142

Taarifa zaidi zitakujia hapa hapa baadae.

Chanzo: Jambo TV
 
Lilikuwa n swala la muda tu Sabaya kuachiwa, ukiachana na kelele za wasiojua namna siasa za Tz zinakwenda.


Huyu jamaa, Bashiru na mwenzao Makonda ni watu waliojilimbikizia pesa nyingi wakati wa JPM, nadhani sasa ataenda kutulia ale mema ya nchi kutokana na pesa alizochuma.
 
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, ambaye amekuwa akikabiliwa mashtaka saba ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu leo Aprili 05, 2023 ameachiliwa huru.

View attachment 2577142

Taarifa zaidi zitakujia hapa hapa baadae.

Chanzo: Jambo TV
Jamani kiswahili chetu mara nyengine kinaleta matatizo kwa sababu hatuna maneno sahihi ya kutumia katika situation fulani fulani. Sasa kama hapa penye taarifa hii. Neno kuachiliwa huru hapa linatatiza maana hakuna mahali inaposema kuwa amefutiwa mashitaka yake, kwa maana hiyo huwezi kusema kuwa yuko huru ikiwa ametolewa jela kwa dhamana na anangoja kesi yake itajwe tena. Mtu kuwa huru ni kuwa unaweza kufany autakalo na kwenda utakako bila ya kuviarifu vyombo vya dola na kuruhusiwa.

Labda wanaotuma hizi taarifa watueleze kuwa huyu mtu yuko huru wakimaanisha hana kesi tena na yuko huru kufanya yake kama watanzania wenzake au yuko nje kwa dhamana na masharti?
 
AHIMIDIWE YESU ALIKUFA NA KUFUFUKA ILI WATU WAKE WAPONE. KARIBU SAANA KAKA YETU NA MCHAPAKAZI NDUGU YANGU SABAYAA. KARIBU TUSHEREHEKEE SIKUKUU YA KUFUFUKA KWA BWANA YESU MWOKOZI WA ULIMWENGU. HAKIKA YESU WETU NI HAKIII. YAAANI NIKO NATIRIRIKWA NA MACHOZI YA FURAHA KWA KUACHIWA HURUU KAKA YANGU HUYU. MUNGU IBARIKI MAHAKA ZETU NA WANASHERIA WOTE WA SERIKALI.
 
Hapa ndipo panapo hitajika mabadiliko makubwa ya kikatiba, haiwezekani huyu anatoka ingawawa anatuhuma nzito ila kwa sababu ni mbowe au sabaya anatolewa na yule anafungwa kwa kwa vituhuma vile vya kijinga tuu ila kwa vile ni mtoto wa muuza vitumbua anaozea jela , maana ya kuwa na sheria ninini?
 
Back
Top Bottom