Lengai Ole Sabaya aachiwa Huru kwa sharti la kutofanya kosa la Jinai kwa kipindi cha mwaka mmoja
The Resident Magistrate Court in Moshi, Kilimanjaro has found former Hai District Commissioner, Lengai Ole Sabaya, guilty of the criminal charges, and sentenced him to one-year in community service with the condition that - #TheGuardian
20230405_194051.jpg
 
Hii nchi Wenyenchi ndiyo wanaoijua,siyo Wananchi! Tusishangae akiteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa.
 
Amekomeshwa hatarudia tena mpumbavu huyo na namshauri awe anasikiliza ushauri wa lema akiendelea na kibri chake atafia gerezani.
 
Hongera sana Sabaya Mungu ni mkubwa sana sasa upo mtaani waliokufitini wataona aibu kubwa sana


USSR
Karma iz bitch
Kijana sabaya alikua anajimwambafy sana
For sure sabaya alikua anajitapa na kuumiza sana watu ...
 
Ilibid atolewe muda mrefu tu, kesi imepigwa sana tar ili kusubiri report ya CAG, Moto bungeni na mtaani umeanza kuwaka ndo wameona wamtoe ili tusahau report, kesho vyombo vyote vya habari ni kuhusu jamaa

Ametolewa leo ili kuficha madudu report ya CAG
 
Aliyewahi Kuwa mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amehukumiwa Kifungo cha Nje cha Mwaka mmoja baada ya kukiri makosa na kuomba mahakama imwangalie kwa jicho la huruma.

=======
1680719426702.png
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, imemtia hatiani aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya mara baada ya kukiri kosa na kumfunga kifungo cha mwaka mmoja nje bila kufanya kosa lolote la jinai.

Sabaya amekiri kosa hilo kwa njia ya ‘Plea Bargaining, ambao ni mchakato wa makubaliano / maridhiano maalumu katika kesi ya jinai kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka kupitia Mwendesha mashtaka na mshtakiwa ambapo mshatikiwa anaweza kukiri kosa moja au zaidi ili aweze kupata nafuu katika kesi inayomkabili.

Sabaya ambaye alisalia kwenye kesi namba 2 ya mwaka 2022 baada ya wenzake Sylvester Nyegu, Nathan Msuya, John Aweyo na Antero Asey ambao septemba 7, 2022 waliachiwa baada ya kufanya makubaliano mahakama na mwendesha mashtaka Mkuu wa serikali.

Msingi wa kesi hiyo kwa Mujibu ya hati ya mashtaka inadaiwa Mnamo Februari 21. 2021 Sabaya na waliokuwa wenzake hao walijipatia kitita cha Tsh Milioni 50 Kutoka kwa mfanyabiashara Alex Swai wakimtisha kutoa taarifa zake za ukwepaji kodi.

Ikumbukwe pia tangu kesi hiyo kuanza kwake Juni Mosi, 2022 haikuwai kusikilizwa kutokana na sababu mbalimbali za kisheria.

Kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Salome Mshasha leo Aprili 05, 2023 ilifika Mahakamani kwa ajili ya kutajwa lakini upande wa mashtaka kupitia kwa Wakili Mwandamizi wa Serikali Verediana Mlenza akadai mshtakiwa ameomba makubaliano nje ya Mahakama na Mwendesha mashtaka Mkuu wa serikali.

Maombi ambayo Mahakama iliyaridhia na kumuachia huru Mshtakiwa huyo Lengai ole Sabaya kwa shart la kifungo cha nje kwa muda wa mwaka Mmoja, na kumtaka amlipe fidia ya Tsh Milioni Tano mfanyabiashara Elbariki Swai ambaye ni Muathirika wa tukio hilo.


Source: ITV Habari

Pia soma: Lengai Ole Sabaya aachiwa Huru
 
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, ambaye amekuwa akikabiliwa mashtaka saba ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu leo Aprili 05, 2023 ameachiliwa huru.


Taarifa zaidi zitakujia hapa hapa baadae.

Chanzo: Jambo TV

===

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, leo April 5, 2023 ameachiliwa huru na mahakama baada ya kufutiwa mashtaka saba yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu.

Mahakama imetoa uamuzi wa Lengai Ole Sabaya kulipa kiasi cha shilingi milioni 5 kama fidia kwa mwathirika na hapaswi kufanya kosa lolote la jinai kwa muda wa mwaka mmoja.

Sabaya ambaye mapema asubuhi ya leo alifika kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Moshi, kabla uamuzi wa kuachiwa haujatangazwa, kupitia Kifungu cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai namba 91 kifungu cha 1A, kesi yake ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2022 ilifanyiwa marejeo kama upande wa mshtakiwa ulivyoomba.

Mawakili upande wa Jamhuri waliiomba mahakama kubadilisha mashtaka ya Lengai Ole Sabaya kutoka kuwa ya kesi ya Uhujumu Uchumi na kufungua kesi yenye Mashtaka ya Makosa ya Jinai baada ya Lengai Ole Sabaya kuomba kufanya mazungumzo nje ya mahakama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Ombi hilo la Sabaya lilikubaliwa na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Salome Mshasha baada ya Mawakili wa Lengai Ole Sabaya kuridhia na kufutwa kwa kesi yake namba 2 ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2022.

Baada ya kuridhia hilo, kesi mpya aliyofunguliwa Sabaya ni kesi kesi ya Jinai Namba 31/2023 ambayo ndani yake kulikuwa na mashtaka mawili mapya dhidi yake, kosa la kwanza likiwa ni kuchukua madaraka ambayo siyo yake.

Imeelezwa kuwa Lengai Ole Sabaya na wenzake, Januari 19, 2021 katika eneo la Masama Mbosho wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, bila kibali walivamia duka la Alex Evarest SwaI na kuchukua mali na kuzizuia na kujipatia kaisi cha fedha shilingi milioni 50.

Kosa la pili ni kuzuia upatikanaji wa haki ambapo Januari 19, 2021 katika maeneo tofautitofauti katika Wilaya ya Hai na Tulia jijini Arusha na maeneo tofauti ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, walikula njama za kumfanya Alex Swai kuwa ametenda kosa la kukwepa kodi.

Baada ya kusomewa mashtaka, Sabaya alikiri kufanya makosa yote hayo mawili mbele ya hakimu Salome Mshasha.
Daah
Kama binadamu tunatakiwa kuwa tunajifunza sana kwa Mambo kama haya tunapokuwa tunayasikia, tunayaona na kuyapitia.
Linganisha nguvu kubwa sana iliyotumika/rasilimali zetu zilivyotumika kwa ajili ya jambo lenye kutia watu aidha upofu au kwa namna ya pekee kuwafundisha watanzania jinsi mamlaka husika zilivyo aidha imara au dhaifu,
Mambo haya yote ni elimu kubwa kwetu kuendelea kutambua umuhimu /uhitaji wa katiba na sheria zenye kukidhi matakwa ya wananchi kwa wakati mahsusi wa sasa.
 
Kwa Kweli mama ameutendea haki mwezi mtukufu wa ramadhani kwa kumuachia sabaya.
 
Mambo mengine tusiwe tuna ingiza kichwa kichwa.
Sabaya amekiri makosa yake yote aliyo kuwa ameshtakiwa nayo, hata lile la uhujumu uchumi na kuhoji genge la uhalifu. Maana yake Sabaya ni jambazi.
Hastahili kugombea nafasi yoyote ya kisiasa wala ya serikali.
Ana makosa ya kijinai. Huyo wakili ni mihemko tuu ..
Kama amekili makosa na amepewa hako kaadhabu kadogo itakuwa kuwa kiongozi?
 
Back
Top Bottom