Leo msafara una magari 25 hadi 30 kwa Kiongozi mmoja!

Kibunango

Platinum Member
Joined
Aug 29, 2006
Posts
8,468
Reaction score
2,349
Ulinz wa Viongozi kwa kweli unatia kinyaa!

Ni kuanzia kwa rais wa Jamhuri ya Muungano hadi kwa rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Huu ulinzi wao umezidi mipaka, unatisha na wala haupo sambamba na hali halisi ya nchi yetu! Kumbuka tu tunasema kuwa nchi yetu ni ya amani na utulivu!

Tukiwa tuaendelea kuzindua hiyo Royal Tour huku viongozi wakiwa kwenye ulinzi mkubwa namna hiyo kushinda hata wa yule wa Ukraine, dunia hii itatuelewa vipi?

Kuna kipindi cha awamu ya kwanza kadhia hii ilipigwa marufuku. Awamu ile msafara ulifikia magari kumi... na ukakemewa hadi kurudi kwa magari matano

Leo msafara una magari 25 hadi 30 kwa Kiongozi mmoja! Tunajenga nchi au tunabomoa? Huu ni ufahari au ni ulimbukeni au ni dalili ya ukosefu wa ajira?

Hili limepigiwa kelele na wengi hapa kijiweni na ni vema tukapata ufafanuzi kwa nini hali hii ipo na inaendelea kukua! Mbona wakiwa nje ya nchi, ulinzi wao ni wakawaida tu!

Tukiwa katika hali ya sasa ya mfumko wa bei ni vema hao viongozi kuonyesha kweli nchi yetu ipo katika hali ngumu na sio hizo anasa wanazotuonyesha!
 
Huwa ninashangaa sana kiongozi anasema yuko madarakani kwa ushindi wa kishindo, lakini ana ulinzi Mkali kuliko aliyeingia kwa kupindua nchi. Ukitaka ucheke ufe, akiwa nje ya nchi ambako hana hata kura moja ana ulinzi wa kawaida mno. Hapo ndio ninawaelewa wazungu wanapotufananisha na nyani.
 
Kwani maadui wa rais wako nje ya nchi au ndani tena wanauwa kwa sindano!
 
Hiyo misafara ya viongozi wa hii nchi kwa kiasi kikubwa ndio kichocheo cha umasikini wa hili taifa, pesa inayotumika kugharamia mafuta ya hayo magari kwa mwaka ni nyingi sana.

Haiwezekani kila siku wanasema wanapiga vita umasikini huku wao wanaendeshwa kwenye msafara wa v8 unaozidi magari ishirini, hawa watu hawako serious.

Hiki ni kielelezo kwamba viongozi wa nchi masikini hutumia madaraka yao for publicity, wala sio kuhudumia wananchi wanaowaongoza, madaraka kwao ni sawa na kushinda bahati nasibu, ndio maana hupongezwa from different angles wanapoteuliwa.
 
Rais akiwa na ulinzi mdogo akapigwa mshale bado wabongo mtaleta maneno..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…