Leo nimegundua kwanini watu wakifumaniana wanafanya ukatili

Kama ulimkuta bikra sawa. Ila kama sio unapomnyandua anakuchora tu kudadek ......
 
Chief! Ahsante kwa muda wako na mawazo yako, Lakini naomba utambue kuwa mambo ya mapenzi ni mazito kwa maana kila mmoja ana kipaumbele chake, kuna wanaume wengine wanapenda watoto, sasa kumfumania mkeo halafu aondoke na watoto ni ngumu, kuna wengine akifumania anasamehe (wana moyo wa ajabu hawa). Lakini pia kuna wengine akifumania anashindwa kutoa talaka maana kwa dhati ya moyo wake bado anampenda mkewe (jamii husema wamelishwa limbwata japo wakati mwingie huwa siyo kweli). Walio wengi wanapofumania hupenda kujichukulia sheria mkononi.

Binafsi haya yote nimeyasikia na mengine kuona sasa juzi kati wakati nasikiliza hukumu ya kisheria kupitia redioni ndo nikagundua kwa nini watu hufanya ukatili wanapofumania, ni kwa kuwa aina ya adhabu kwa kosa hilo haikujali hisia za waathirika wa hayo mapenzi (mkuu kuna mtu anaweza kukupenda 100% , sasa fikiria mtu huyo akufumanie hiyo faini itatuliza hisia zake kweli?)

Naomba uniambie kama hiyo adhabu ya faini inafaa/kutosha!!
 
Kama ulimkuta bikra sawa. Ila kama sio unapomnyandua anakuchora tu kudadek ......
Mke anauma haijalishi ulimkuta bikra au siyo bikra, vinginevyo iwe humpendi!!
 
Una heri enenda na ukatende kama ulivyosema
 
Mke anauma haijalishi ulimkuta bikra au siyo bikra, vinginevyo iwe humpendi!!
Nakubaliana nawe ila ni vizuri kuzuia hasira na kujiweka salama zaidi kuliko kuhamaki kisa limtu lisilojielewa.
 
Nakubaliana nawe ila ni vizuri kuzuia hasira na kujiweka salama zaidi kuliko kuhamaki kisa limtu lisilojielewa.
Hili nalo neno kwa upande wa kuzuia madhara zaidi. Je, Adhabu ya faini inatosha kulingana na uzito na uthamani wa kosa?
 
Utawaacha wangapi?
 
Halafu wakware wakisha kusoma wanakugeuza mnyonge wao, hivyo inakuwa kila siku wewe ni wa kuanza upya tu.
Si kweli kuwa wanawake wakicheat hawaachi. Wengine yalitutokea ingawa tulioa bikra, unajiuliza faida ya ndoa yako ni K au ni investment kwa huyo mwenza. Yaani watoto etc. Na kama akijutia mnaendelea kuishi wote ila kidonda huwa hakiponi hadi ufe. Ila lazima wote wawili waone kuwa umechukizwa na wawe wanakumbuka maumivu ya kitendo chao cha kucheat. Nawe unakuwa mwangalifu si kubweteka
 
Ndiyo maana kuna mdau nilimjibu kuwa kuacha mwanamke siyo sawa na kuacha takamwili chooni, kwa mujibu wa hoja yako ni kweli kuwa kuna wanaosamehewa na kuacha pamoja na kujutia lakini kuna wengine ukimsamehe yeye anahisi dawa zake (ushirikina) ndio zimefanya kazi, hivyo atakudharau na kuendelea, pia kuna mwingine atakwambia ameacha kumbe wamebadilisha mbinu na mazingira ya kukusaliti.

Kuhusu kuwekeza kwenye "K" au watoto ni jambo zuri lakini una uhakika gani kama hao watoto waliokuja kupitia hiyo "K" ni damu yako (wanaume inatudhuru sana) Unaweza kuhangaika na watoto wakishafika ngazi ya chuo Baba yao mzazi anajitokeza halafu hana mbele wala nyuma na mke anakuambia ukweli kuwa huyo ndiyo Baba yao mzazi (maana wakati huo hana cha kupoteza) na hatimaye unagundua kuwa ulifanywa mjinga kipindi kirefu cha maisha yako.

Kuhusu kusamehe ni jambo zuri lakini unaposema "umesamehe ila kidonda hakiponi" jua wazi kuwa hujasamehe na hivyo unajidanganya na kujiumiza mwenyewe maana Msamaha wa kweli unaambatana na kuachilia pia. Unaposamehe halafu ukashindwa kuachilia matokeo yake ni kufa kwa sonona (hivyo ndiyo mke mzinzi anapenda ili apate mali kiurahisi)

Sasa naomba unijibu. Kwa usumbufu na madhila yanayopatikana katika sakata la fumanizi je, adhabu ya faini inatosha?
 
Ndiyo maana kuna mdau nilimjibu kuwa kuacha mwanamke siyo sawa na kuacha takamwili chooni, kwa mujibu wa hoja yako ni kweli kuwa kuna wanaosamehewa na kuacha pamoja na kujutia lakini kuna wengine ukimsamehe yeye anahisi dawa zake (ushirikina) ndio zimefanya kazi hivyo atakudharau na kuendelea pia kuna mwingine atakwambia ameacha kumbe wamebadilisha mbinu na mazingira
unajua mkeo alikua demu wangu
..........Sijui kama mke wangu alikuwa demu wako, lakini hata kama alikuwa (wakati uliopita) sasa ni mke wangu wa ndoa hivyo nina haki ya kumlinda. Sasa basi hata wewe yawezekana mke uliyenaye (kama umeoa) alikuwa demu wa mtu, Je, ukiwafumania na kuwapeleka mahakamani adhabu ya faini utaridhika nayo?
 
Ukimfumania mkeo, lazima watoto waende kwa Mkemia mkuu kwa DNA. Hilo halina mjadala. Hivi nikuulize, unaweza kumpeleka mgoni wako mahakamani au polisi? Jibu ni hapana ila unayamaliza mwenyewe. Lakini la maana ni kuhakikisha mwanaume hana marinda. Hapo heshima itakuwepo
 
Halafu wakware wakisha kusoma wanakugeuza mnyonge wao, hivyo inakuwa kila siku wewe ni wa kuanza upya tu.
Ndoa wakuu sio za kuingia kichwa kichwa kuna ethics zake
Wajanja huwa wanajitathmini kuona kama wanaweza kuwa na ndoa na kuna baadhi wanahitimisha kuwa hawawezi kuwa kwenye ndoa ,
Kuna wanawake wanastahili kuolewa , na kuna wengine hawastahili kuolewa , ninaposema hawastahili kuolewa sina maana mbaya , bali ni kutokana na mambo kadhaa mwanamke anaweza kuwa proved beyond kuwa ndoa kwao ni changamoto , big booty , guu la bia ,macho ya kula kungu halafu kidume unajitwisha zigo unaweka ndani !!!,. Utatafuta lawama na wagoni.
 
Marinda tu
How is your life worth it ? , Yaani nihangaike na mwanaume mwenzangu wakati wanawake wanatushinda?
Umeshawahi kupiga gharama za kufumania? Unazimudu vzr? , Hiyo mission nzima una uhakika haitakuja kugeuka criminal ikakupeleka jela huku ukimuacha mgoni free na wanaokutegemea katika shida ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…