Ms R
JF-Expert Member
- Jan 19, 2023
- 8,853
- 19,587
ExactlyAnataka haraka kuna wanawake wengine hatuendi hivyo binafsi sipendi kutongozwa hadharani labda uwe utani kama wa bibi na mjukuu, ndo maana kuna pm
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ExactlyAnataka haraka kuna wanawake wengine hatuendi hivyo binafsi sipendi kutongozwa hadharani labda uwe utani kama wa bibi na mjukuu, ndo maana kuna pm
Tumsamehe bureYani page 5 kajaa yeye tu na hii tabia wanayo wanaume wengi tu humu mara mia anaefungua uzi wa kutongozea kuliko kutongozea kwenye mada serious za watu wengine
Jamaniiiii 🤣🤣😂😂😂watu mko macho balaai
Ngoja ngoja huumiza matumbo halafu nishafeli tayari 😭😭😭Anataka haraka kuna wanawake wengine hatuendi hivyo binafsi sipendi kutongozwa hadharani labda uwe utani kama wa bibi na mjukuu, ndo maana kuna pm
Mimi ni a funny person japo utani wangu mostly ni wa kukera, ila huwa i just mean jokes, shida sasa ni mtu akiwa anachukulia issues personal😂😂😂😂Toka kuniita malaya hadi leo kufurahi iviiii daaah 😂😂
mi inategemea umenigusa wapi kwenye huo utaniMimi ni a funny person japo utani wangu mostly ni wa kukera, ila huwa i just mean jokes, shida sasa ni mtu akiwa anachukulia issues personal
Hapo kwenye kuwafikiria watoto wakiwa mbali nimekuelewa sana.Miaka 5 nyuma nilipatwa na hiki kisa, sijui huwa kuna nini kinatokea kwa wenzetu naweza kusema alikuwa mke kabisa maana kwao walinifahamu posa na mahari nilishamaliza na watoto wawili nimemzalisha sasa kipindi chote hicho alikuwa anafanya shughuli ndogondogo tu.
Sasa ikatokea fursa sehemu nikamwambia mama kwa haya maisha tunayoishi itachukua muda kutoboa hapa ebu kamatia iyo fursa ya kazi tusaidizane bwana bwana bwana kumbe ndio nilikuwa namaliza familia yangu wakuu kitendo cha yeye kupata ile kazi tu na vile nilimtumia mtu ninayemjua ilikuwa rahisi sana kwake kutoboa.
Picha linaanza kwanza amepangiwa mkoani akili ikacheza mmh nikiwa nipo kwenye dilema ya maamuzi kwao wakawa wapo karibu nae zaidi na wakamwambia aende huko kwa kuwa watoto bado wadogo waende kwa bibi yao yaani mama yake hadi mambo yatakapokuwa sawa kule then awachukue.
Basi mwezi ukaisha mwezi wa pili mara miezi sita nikaanza kuona mapicha picha kwanza sikuwahi kuona hela yake ingawa alikuwa analipwa mara 4 ya mshahara wangu bado nilitakiwa kutuma pesa ya matumizi kwangu hakuwa shida maana naelewa mwanaume ndio mtunza familia kifedha.
Alifanikiwa kurudi kipindi cha mwanzo mwanzo tu tena akaniletea nyodo hatari stori zake sasa ooh mwaka huu nanunua gari sijui wewe umeshindwa hiki na kile nikitaka tunda anajivutaa nikajisemea hii ngoma ndio imeshavuja hapa. Kwakweli haikufika hata mwaka tukabwagana.
Hakuna kipindi nilikonda kama kipindi kile full mawazo alafu ndugu zake wananichora tu kenge wale!
ilibaki kidogo nidondoke nifeee!
Kuna mama mmoja mtu wa makamo akanifuata na kuniweka chini kisha akanipa ushauri mmoja wa nguvu sana akaniambia kijana wangu usiwe mnyonge hivyo tafuta mwanamke mdogo na mzuri kuliko mkeo then furahia maisha haya maisha ni mafupi sana na utamsahau.
Kwa kweli namshukuru sana yule mama maana from there maisha yalibadilika taratibu nilianza kumsahau yule mwanamke na mambo yake ingawa bado muda mwingine naumia ila ndio maisha isee
tuishi nao kwa akili!
Kwanini nimeleta huu uzi?
Nataka vijana wenzangu hasa hawa wadogo ambao wanajianda kuingia kwenye maisha ya familia wawe makini na kujitaidi wajipende na wao wasijitoe sana kwa ajili ya familia zao things change na maumivu utayopitia sio ya kawaida mm nilikuwa najiona mgumu nilikuwa nashangaa wanaume wanaolalamikia wake zao ila yalivyonikuta nilijishangaa najikaza ila uso na mwili vilijionyesha kuwa nipo kwenye maumivu jamani maumivu ya mahusiano hayaelezeki tena kwa sisi ambao tulishakuwa na familia utashangaa chakula hakipiti wala maji hayashuki.
Kuna bond inayojitengeneza ukishazoea kuwaona watu wako wa karibu kila siku kuitoa hiyo ni ngumu sana yaani kuna muda nilikuwa nikikaa hivi fikra za watoto wangu wapo mbali muda niliopoteza kuwa na mwanamke yule nilikuwa nafamilia ghafla naishi mwenyewe machozi yanatoka yenyewe tu.
Nashukuru sana gospel music inafariji sana.
Xavi Hernandez (The Pass Master)Mimi ni a funny person japo utani wangu mostly ni wa kukera, ila huwa i just mean jokes, shida sasa ni mtu akiwa anachukulia issues personal
Hakuna namna maisha lazima yaende mbele.Pole sana brother.
Sad story!!! No commentExperience yangu hata umfanyie wema gani atakuacha tu..
Arusha 2014 jirani yangu alikuwa anafanya kazi taasisi fulani, financially alikuwa yuko poa sana. Kulikuwa kuna binti alikuwa anakuja kwake mostly on weekends... Siku ndo akani tambulisha hii ni pisi yake ila inasoma mkoa x chuo kikuu mwaka wa pili... Miaka ikaenda ile pisi ikawa haionekani kumbe ilikuwa chuo.
Mambo yakaenda vibaya kwa yule dada alifeli chuo so hakuweza kumaliza chuo. familia ikamtema mazima kwamba atajua na maisha yake. Familia ilienda mbali na kumuambia pesa walizo nazo niza kusomesha wadogo wa yule binti. So binti akamshirikisha boyfriend wake ambaye ni jirani yangu. Jamaa akamuambia aje tu maana hata kwenda nyumbani aliogopa.
Basi jamaa kwa kujua one day in this life atakuwa mke wake, akalibeba lile jambo na kuamua kumpeleka chuo kikuu kimoja kiko Arusha, alim somesha, chakula, mavazi yaani kwa kifupi alikuwa mzazi na boyfriend at once. akawa anaenda chuo for all the three years tumekaa nae pale, ila this time alitoboa graduation kila kitu fresh. Walikuwa poa sana kiukweli, ilikuwa ni couple moja strong sana ile unajua demu aki graduate wanafunga ndoa.
Demu aliendelea kukaa pale hadi akapata nafasi katika kampuni flani hivi alianza kwa kujitolea baadae akapata ajira ya kudumu, ila kupatikana hii kazi ni kwa juhudi za huyu mwamba. sijui salary yake but alikuwa ana safiri sana. Matatizo ndo yakaanza kule ndani. Demu alikuja kubadilika ndugu zangu siyo poa, kama mara tatu wameshikiana visu mule ndani, alikuja kumuacha mwamba kama hamjui and familia ikamuambia arudi nyumbani huyo jamaa siyo mume wake.
Jamaa alifanya attempt kama mbili za kutaka kujiua, alikuja kuwa mtu wa pombe sana, sigara nyingi sana (wakati hakuwa mnywaji kivile, wala mvutaji wa sigara) alikuja kukonda, kwenda job late, ananukia na pombe, kwa kifupi aliyumba sana ile kampuni ilijaribu kumbeba sana because bosi pia alijua what he was going through. Alivyoachishwa kazi akaja kuniaga akarudi kwao. That brother he was torn apart because of love. he couldn't take it anymore... Dada yake alikuja kunipigia March 2023 the brother died. Yule dada yupo tu huwa namuona mjini na life lake tu.
Kwa kifupi after that scenario nimeona unaweza ukaigiziwa maisha vizuri tu, riziki ikapatikana zaidi kwa mke au mpenzi wako hamuwezi toboa tena...! Dharau zitaanza tu kama hiyo pisi ilishamrudia jamaa na lovebite. . . !
💩Sisi ndio wake zenu dada zenu na mama zenu
Hamuwezi kutuchukia sisi ni maua mazuri ya kupendeza😅
Poleni sana wakuu .
Yako!
Mtu siku zote anakuwa sahihi hadi pale ambapo anakuwa sio sahihi,ni ngumu kutabiri tabia ya mtu watu huabadilika.Bahati mbaya sana ni kuwa wale wote wanaofurahia ndoa zao kwa amani huwa wapo kimya na kamwe hutowasikia.. Ila ndugu zangu waliitendwa utawasikia Kila sehemu wakilalamika..
Sitaki kuamini kuwa kila mahusiano ni mabaya.. Vijana oeni na mabinti oleweni.. Jipe muda, hakikisha huyo unayeingia naye kwenye ndoa ni mtu sahihi.. Mtangulize Mungu naye atakuongoza..
NB; NDOA NI JELA.. NDOA NI KIFUNGO.. CHAGUA VYEMA UTAKAYEISHI NAYE NDANI YA KIFUNGO/JELA HIYO..
Swali lako linahitaji ufafanuzi mrefu sana.. Kifupi niseme tu hao ambao ndoa zimewashinda walibahatisha..Mtu siku zote anakuwa sahihi hadi pale ambapo anakuwa sio sahihi,ni ngumu kutabiri tabia ya mtu watu huabadilika.
Kwa hiyo wote ambao ndio zimewashinda hawakumtanguliza Mungu au sio???
Naweza kumpata huyo mtaalam wa kutia gundu nina kazi nae mhm sanaPole sana Mkuu, kuna kisa kilimkuta jamaa fulani mwaka 2006 alimchukua Mwanamke tena alikuwa Barmaid akawa anaishi naye jamaa alikuwa analipwa 150,000 tu, sasa akamtafutia kazi za Kuuza duka mjini yule Mwanamke akawa anapata hela maana na dili zilikuwa zinatokea kwenye ishu za kuuza duka. Yule demu alijichanga akanunua mabati na akayasafirisha kwao Singida. Taarifa zilisema kwao kajenga nyumba ya bati, lakini kwa jamaa alikuwa analeta mapicha picha sana mpaka alikuwa anampeleka jamaa yake Polisi na kule Polisi alikuwa anahonga hela yaani jamaa alikuwa ananyanyasika sana na Kipesa alikuwa kazidiwa na yule Mwanamke. Watu wenye roho mbaya wakamtia gundu yule Mwanamke maana alikuwa na dharau sana. Akafukuzwa kazi na Jamaa waliachana. Mara ya mwisho mwaka 2010 yule demu nilimuona Tandale kwa Mtogole anachoma Mahindi.