Leo nimepika Ndizi nyama msela mimi ni tamu mnoo

Leo nimepika Ndizi nyama msela mimi ni tamu mnoo

Nilikua na hamu ya ndizi nyama hivyo kwa kua nalijua jiko nikapita zangu sokoni nikachukua mazaga kadhaa nikaingia jikoni😆 na nitawaelezea jinsi nilivyopika hatua kwa hatua

MAHITAJI;

Carry powder, paprika powder, black pepper, soya souce, tui la nazi (tui la 1 na tui la 2), ndizi mshale 8, nyama nusu, carrot na pilipili hoho (paprika)
View attachment 3193027
Nikachemsha nyama hadi zikaiva na kulainika kabisa mimi huwa sipendi nyama ngumu
View attachment 3193032
Baada nyama kuiva nikabadilisha sufuria maana ilikua ndogo nikaweka ndizi zilizokatwa vipande vidogo kisha nikachanganya paprika powder, black pepper, carry powder, soya souce na chunvi
View attachment 3193033View attachment 3193034

Baada ya kukoroga na kuhakikisha viungo vimekolea vizuri nikaweka nyama na tui la nazi la pili
View attachment 3193035

Kisha nikaweka mchuzi wa nyama
View attachment 3193037
Baada ya hapo nikafunika ili mchanganyiko wangu uive kwa muda fulani
View attachment 3193039
Baada ya mchanganyiko kuiva nikaongeza hoho, carrot na tui la kwanza (tui zito)
View attachment 3193040
View attachment 3193041
Kisha nikafunika tena kwa dakika kadhaa ili mchanganyiko uive vizuri baada ya dk kama nane chakula chetu kilikua tayari kwa kuliwa
View attachment 3193048
Chkula kilikua chamoto sana na kitamu chenye radha nzuri na kinanukia
View attachment 3193052

Natamani niwaonjeshe utamu wa hiki chakula ila ndo hivyo tena haiwezekani😜 na pia wengi watajiuliza ulikunaje nazi? Jibu nilitumia blender kisha nikaichuja

Wale tulio single bila wapenzi tuwe na mazoea ya kupika tukipata muda vyakula vya mama ntilie vipo kibiashara zaidi na pia vina kasoro nyingi mno

Mimi ni mtu wa pwani napenda sana chakula kilichopikwa kwa mchanganyiko wa nazi juzi nilitoka mafia nikambebea mama nazi za kutosha chache nikabaki nazo
View attachment 3193106
Umejitahidi ila tu
1. Ndizi nyama haziwekwi viungo zaidi ya karoti, kitunguu, pilipili (kwa wanaopendelea) hoho na nyanya kidogo sana (ni vyema zaidi kuacha kuweka nyanya)

2. Maji ya kwanza kupikia ndizi yanawekwa kidogo, hayatakiwi kuonekana juu ya ndizi.

Kuhusu nazi tayari umeshauriwa huko juu kwa usahihi, otherwise ulipata nyama nzuri sana ndio maana ndizi zimekuwa nzuri.

Ushauri huu wa mapishi ya ndizi ni kutokea kwa wenye ndizi nyama zetu, uchagani.
 
Wanasema kupika ni Sanaa ila kwangu hii Sanaa imenikataa, labda wali wa kwenye rice cooker na wenyewe huwa hadi Leo nabahatisha kwenye swala la kukadiria maji.

Kuna siku yanakua mengi so nakunywa uji, kuna siku yanakua kidogo so natafuna mchele na kuna siku yanakua poa nakula zangu wali😂😂😂😂... Anyway, hongera sana mkuu.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣lol
 
Aaliyyah njoo mwaya chef wangu..!!
Mtoa mada, wakati mwingine jaribu kutia njegere ama mchicha, uta enjoy zaidi..!!

Hongera kwa chakula kizuri, wenzio hawajui hata kuchemsha maji ya kuoga huko duniani..!😂
 
Mwanangu unajua kupika? Basi mkwe wangu atafaidi sana...sio kwenye mapishi peke yake na kwenye mambo mengine pia. Hongera sana.
najulia wapi mama?🤣

kumenya ndizi tu siwezi

ntajifunza lakini kama ndo njia ya kupata vimwali
 
Sasa hapo umemaliza kula piga Lita 1 ya maji baridi kiasi then Twenzetu Sehemu tulivu tukapige Nyagi or K vant uku tukisubili game ya Simba uko ugaibuni na Liverpool v Maniyuu pale Anfield
 
Mbona ghafla Sana mmeamia lini huku kwenye mapishi kama kigezo😃😃
Umenichekesha wakati uzi umenipa majonzi
Mkuu,raha sana kuwa na mwanaume anayejua kupika sana....nakumbuka nilikuwa naenda kwake niko zangu naangalia movie yeye ananipikia chakula kitamuuu 😭😭

Au labda kwasababu mimi sijuagi kupika
 
Umejitahidi ila tu
1. Ndizi nyama haziwekwi viungo zaidi ya karoti, kitunguu, pilipili (kwa wanaopendelea) hoho na nyanya kidogo sana (ni vyema zaidi kuacha kuweka nyanya)

2. Maji ya kwanza kupikia ndizi yanawekwa kidogo, hayatakiwi kuonekana juu ya ndizi.

Kuhusu nazi tayari umeshauriwa huko juu kwa usahihi, otherwise ulipata nyama nzuri sana ndio maana ndizi zimekuwa nzuri.

Ushauri huu wa mapishi ya ndizi ni kutokea kwa wenye ndizi nyama zetu, uchagani.
Najifunza madam🙏
 
Umenichekesha wakati uzi umenipa majonzi
Mkuu,raha sana kuwa na mwanaume anayejua kupika sana....nakumbuka nilikuwa naenda kwake niko zangu naangalia movie yeye ananipikia chakula kitamuuu 😭😭

Au labda kwasababu mimi sijuagi kupika
Ilikua GG hiyo (both Team to score) unakula kisha baadae unaliwa
 
Back
Top Bottom