Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, hivyo kumchinjia rasmi baharini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco
wewe pasco sasa ndio tunaanza kukuelewa,nani anamkubali Lowasa ndani ya ccm zaidi ya wachumia tumbo?,hata baada ya ukweli kudhihihirika kuwa ile ripoti ya kumbeba Lowasa ilikuwa ya kupikwa na Team lowasa,na ina ofisi jengo moja na team lowasa na floor moja na milango inatazamana bado wachumia tumbo mnahangaika kumbeba mtu ambae hata kupanda mwenyewe lift ya lori hawezi.

kama utafiti ule umesema adui namba moja wa nchi hii ni ufisadi na rushwa inakuwaje kinara wa ufisadi awe rais?

mtueleze mnataka kumfanya nini mzee kasori mpaka amekimbia mji wake hapo arusha?:flame::couch2:shame on you
 
Safi sana. Endeleeni kunyukana ivo ivo. Team zote 6 kazeni buti, msikubali.
 
Hii thread naona kama vile imelenga kujihami zaidi kuliko kutoa taarifa!

Hata hivyo,binafsi niliwahi kupost uzi hapa mwaka jana nikionya kuwa Lowassa hawezi pitishwa kwani hakubaliki na safu ya juu niliyoitaata "top layer ya viongozi wa CCM" na nikasema kabisa hii issue inaweza kukisambaratisha kama sio kukigawa chama hiki.

Hivyo, mimi sishangai na mpaka leo bado naamini jina la Lowassa halitapita na hicho ndio kitakachokuja kutokea.

Time will tell

Fahamu kuwa hakuna fisadi yeyote mwenye uthubutu wa kuondoka CCM kwani kufanya hivyo ni kuvuruga maslahi yake. Je Lowasa akiondoka CCM ufisadi wake utalindwa na nani? Nakuhakikishia kuwa mafisadi wote watakufa na CCM yao. Hayo unayosema wewe ni vitisho tu
 
Acheni kila mtu anayetaka urais jina lake lifike pote pale. Safari hii MDAHALO usiwe hiari. Kazi ifanyike usiku na mchana kuhakikisha kila mgombea anapata ulazima wa kushiriki kwa hiari. kwa mfano kupangwe hivi (hapa nachokoza tu ruksa mawazo ya kuboresha):-
1. Midahalo wa siku 3 Sera ya mgombea kuhusu (a) Uchumi wa nchi; kilimo, uzalishaji na biashara (b) Elimu (c) Mambo ya nje.
2. Wagombea wote watashiriki Mdahalo ambao utaratibiwa na neutral body kutoka tanzania au ikibidi kutoka nje,
3. Mshiriki aruhusiwe kuleta muwakilishi au ushiriki utakaosomwa katika maandishi na pointi zake zitazingatia mapungufu haya kutokushiriki mwenyewe
4. Pointi za kushiriki zitapangwa kwamba hata yule atakayeamua kutokushiriki atapata pointi za kushiriki, ya kwanza ni pointi ya kushinda hatua aliyofikia katika kinyang'anyiro cha kutafuta urais.
 
Mpaka sasa bango chafu la Lowassa ni ufisadi, ambalo limeshindwa kuthibitishwa uhalisia wake. Hiyo inawafanya makada na wananchi kuamua kumkumbatia baada ya kugundua mchezo mchafu unaoendelea. Wananchi wanafurahishwa na maamuzi magumu na sahihi aliyo nayo Lowassa kwa Taifa.
 
mbona hutaji wagombea kuelza mikakati dhidi ya ufisadi?


Acheni kila mtu anayetaka urais jina lake lifike pote pale. Safari hii MDAHALO usiwe hiari. Kazi ifanyike usiku na mchana kuhakikisha kila mgombea anapata ulazima wa kushiriki kwa hiari. kwa mfano kupangwe hivi (hapa nachokoza tu ruksa mawazo ya kuboresha):-
1. Midahalo wa siku 3 Sera ya mgombea kuhusu (a) Uchumi wa nchi; kilimo, uzalishaji na biashara (b) Elimu (c) Mambo ya nje.
2. Wagombea wote watashiriki Mdahalo ambao utaratibiwa na neutral body kutoka tanzania au ikibidi kutoka nje,
3. Mshiriki aruhusiwe kuleta muwakilishi au ushiriki utakaosomwa katika maandishi na pointi zake zitazingatia mapungufu haya kutokushiriki mwenyewe
4. Pointi za kushiriki zitapangwa kwamba hata yule atakayeamua kutokushiriki atapata pointi za kushiriki, ya kwanza ni pointi ya kushinda hatua aliyofikia katika kinyang'anyiro cha kutafuta urais.
 

Attachments

  • IMG_7349687624889.jpeg
    IMG_7349687624889.jpeg
    38.6 KB · Views: 198
Wanataka watuletee jina gani lingine sasa,.? HAIWEZEKANI. EL RAISI.
 
taja maamuzi matatu magumu aliyowahi kuchukua lowasa kitaifa?

na utuambie kwa nini mzee kasori katibu wa nyerere ametishiwa maisha" baada ya kuanika ukweli kuhusu lowasa kukataliwa na nyerere baba wa taifa



Mpaka sasa bango chafu la Lowassa ni ufisadi, ambalo limeshindwa kuthibitishwa uhalisia wake. Hiyo inawafanya makada na wananchi kuamua kumkumbatia baada ya kugundua mchezo mchafu unaoendelea. Wananchi wanafurahishwa na maamuzi magumu na sahihi aliyo nayo Lowassa kwa Taifa.
 
Alivunja mkataba wa kinyonyaji wa mwaka 1929 na mwaka 1959 wa Misri uliozuia matumizi ya maji ya ziwa victoria na leo hii kanda ya ziwa wanakunywa maji safi na salama; aliamuru ujenzi wa chuo cha UDOM kwa kutumia pesa zetu za ndani na si kutegemea za Billy Gates; uamuzi mgumu wa kuvunja mkataba wa city water na kupelekea uanzishwaji wa kampuni za wazawa za usimamizi wa maji
 
Kazi ni kazi tu mkuu PASCO aijali mlipaji ni nani so long taaluma inatumika, mmoja ya watanzania wakweli kwenye kauli na mtendo ni wewe.

Lowassa amekuwa akijionyesha kukubalika mtaani kwa kushinda ngumi zisizo professional na kweli hizo anaziweza maana kichwa, teke, mahala pakupiga upangiwi we piga tu waanguke. Hila unapopambana ngumi zinazo amuliwa na referee kuna sheria zake za sehemu za kupiga ukifanya foul kuna consequences.

Amuulize David Milliband kilicho muangusha akiwa kama kipenzi cha viongozi wa labour waliokuwa na nafasi za juu na wapiga kura wao bila ya kutumia pesa tena; siasa za vyama zina rules zake na lazima uzieshimu particularly kabla ujavuka mto wa chama vinginevyo ni kutwanga maji kwenye kinu ata ukiletewa form na kila mtu ndani ya jamii kwanza ni kile chama chako je unacheza na rules za ushindi wa ndani kwanza.
 
Back
Top Bottom