Licha ya Mapungufu, Sheria Mpya ya Uchaguzi Pia ina Mazuri Yake!, Imerejesha Mamlaka ya Uchaguzi kwa Wananchi, Hakuna Kupita Bila Kupingwa!.

Licha ya Mapungufu, Sheria Mpya ya Uchaguzi Pia ina Mazuri Yake!, Imerejesha Mamlaka ya Uchaguzi kwa Wananchi, Hakuna Kupita Bila Kupingwa!.

Wanabodi,
Hili ni bandiko mwendelezo wa three series za uchambuzi wangu wa sheria mpya ya Uchaguzi, 2023. Kama hukuona 1st series, anzia hapa Asante Rais Samia kwa Muswada huu. Umuhimu wa mabadiliko ya Katiba kabla ya Sheria hii bado ni muhimu sana. Huu ni uchambuzi Wangu - Part 1 kisha uje hapa
Asante Rais Samia kwa Muswada huu. Umuhimu wa mabadiliko ya Katiba kabla ya Sheria hii bado ni muhimu sana. Huu ni uchambuzi Wangu - Part 1
Kisha Je Wajua Muswada Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2023 ni Batili?. Ni Mvinyo wa Zamani, Kwenye Chupa Mpya?. Why Ubatili Huu?!.
Pia unaweza kupita hapa Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi, Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!. na hapa Tujifunze kuwa na Shukrani kwa Madogo ili Tupatiwe Makubwa!. Japo Tulitaka Kikubwa, Tumepewa Kiduchu!, Tukipokee Tushukuru, au Tususe Kudai Kikubwa?.

Binadamu tuna mtindo wa kuangazia mapungufu zaidi na kujikuta tunakuwa blinded na mapungufu hivyo kutoona mazuri, hata kwenye Biblia ukitaja tuu jina la Yuda, mind za wengi zinakwenda kwa usaliti wa Yuda Iskariote, kumbe kwenye watumishi wa Yesu, kulikuwa na Yuda wawili, Yuda Iskariote msaliti na Yuda Tadei mtu mwema. Jina la Yuda limeghubikwa na usaliti hadi wema wa Yuda Tadei kufunikwa na usaliti wa Yuda Iskariote.

Ndivyo ilivyo hii sheria mpya ya uchaguzi, kufuatia sheria hii kuletwa na ubatili ule ule tunaoupigia kelele kila uchao, tunajikuta tunakuwa too blind to see mema na mazuri ya muswada huu
Hivyo leo naendelea na uchambuzi wangu wa kifungu hadi kifungu huku nikiainisha the good, the bad and the ugly.
Karibu.
View attachment 2831115
Leo naendelea na uchambuzi wangu wa muswada huu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2023, kwa mukhtaasari wa sura zote 10 za sheria hii, kuwaelimisha elimu ya uraia na elimu ya sheria na haki ili Watanzania tuitumie kikamilifu hii miezi 3 ya kutoa maoni na mapendekezo ya maboresho ya sheria hii.
Muswada huu unatunga Sheria ya Uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani ya mwaka, 2023. Kwa ujumla, Sheria hii inaunganisha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292. Hivyo sasa masharti ya uchaguzi wa Rais na Wabunge na Madiwani ni sheria moja na kutekelezwa na mamlaka moja ambayo ni Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hapa ninapendekeza chaguzi zote nchini, uchaguzi wa Rais na Wabunge, Madiwani na Serikali za Mitaa, ufanyike siku moja na kusimamiwa na Tume moja Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hili ni jambo jema!.
Wiki iliyopita nilichambua sura ya kwanza mpaka ya tatu, leo naendelea

Sura ya Nne ya Muswada inaweka masharti yanayosimamia uchaguzi wa Wabunge na imegawanyika katika sehemu mbili, sehemu ya kwanza inahusu sifa za wagombea katika uchaguzi wa Ubunge. Sehemu ya Pili inahusu uteuzi wa wagombea Ubunge ambapo inaainisha siku ya uteuzi, uteuzi wa wagombea, utaratibu wa namna ya kuweka dhamana kwa mgombea wa nafasi ya ubunge, masharti ya mgombea kuteuliwa kwa jimbo moja tu, pingamizi na uamuzi juu ya uhalali wa fomu ya uteuzi

Sura hii pia inaainisha utaratibu wa kufuatwa endapo kuna mgombea mmoja tu halali wa nafasi ya ubunge au endapo hakuna mgombea. Kwa mujibu wa Sehemu hii endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa nafasi ya Ubunge ameteuliwa, mgombea huyo atapaswa kupigiwa kura na atatangazwa kuwa amechaguliwa endapo atapata kura nyingi za ndiyo kati ya kura zote halali zilizopigwa

Maoni: Hili ni jambo jema, zuri na lenye maslahi kwa taifa kwa kurejesha mamlaka kwa wananchi, sasa hakuna tena ushindi wa mtu kupita bila kupingwa!. Kupita bila kupingwa kulifanya chama kuwachagulia wananchi kiongozi. Hii itaondoa zile figusu za kuzuia watu wasigombee, kuwanunua wapinzani na kuzuia fomu zisirejeshwe na mtu kutangazwa mshindi wa kupita bila kupingwa!. CCM ina wabunge 18 ambao wamepita bila kupingwa!.

Sura ya Tano ya Muswada inahusu masharti ya uchaguzi wa Madiwani. Sura hii imegawanyika katika Sehemu Tatu, ambapo Sehemu ya Kwanza inabainisha masharti ya uendeshaji wa uchaguzi wa madiwani, muda wa kuwa madarakani kwa Madiwani, namna na wakati wa kuitisha uchaguzi mdogo na uwakilishi katika Kata. Sehemu ya Pili inaweka masharti kuhusu sifa za mgombea na mazingira ya mtu kukosa sifa ya kuteuliwa katika uchaguzi. Sehemu ya Tatu inajumuisha masharti kuhusu siku ya uteuzi, uteuzi wa mgombea, dhamana za wagombea, utaratibu wa kuweka pingamizi na utaratibu unaopaswa kufuatwa ikiwa kuna mgombea mmoja tu wa nafasi ya udiwani au ikiwa hakuna mgombea.

Sura ya Sita ya Muswada inaweka masharti kuhusu uchaguzi, utaratibu wakupiga kura na uteuzi wa wabunge na madiwani wanawake viti maalum. Sura hii imegawanyika katika Sehemu Sita, ambapo Sehemu ya Kwanza inaweka masharti mbalimbali kuhusu siku ya uchaguzi na tangazo la uchaguzi. Kwa mujibu wa masharti hayo, taarifa ambazo zitakuwa katika tangazo la uchaguzi ni pamoja na siku na muda wa kuanza na kufunga upigaji kura, anwani ya vituo vya kupigia kura, wapiga kura waliopangwa kwa kila kituo cha kupigia kura na taarifa za wagombea walio teuliwa kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi. Sehemu ya Pili inaweka masharti kuhusu mgombea kujitoa na utaratibu unaopaswa kufuatwa endapo mgombea atafariki au hakuna mgombea. Sehemu ya Tatu inaweka masharti kuhusu kampeni za uchaguzi na namna kampeni zinavyopaswa kuendeshwa, ikiwa ni pamoja na masharti kuhusu kuwasilisha ratiba ya mikutano kwa msimamizi wa uchaguzi kwa lengo la kuepuka migongano ya mikutano. Sehemu hii inaweka pia masharti kuhusu upatikanaji na wajibu wa vyombo vya habari vya umma na matakwa ya kutokuwa naupendeleo na kuepuka ubaguzi kwa mgombea yeyote katika utoaji wa matangazo.
Maoni: Hapa bado kuna tatizo, mgombea mmoja ana ving’ora, ana media team ya serikali, ana PA ya serikali, ana magari ya serikali na watendakazi wa serikali!. Nchi za wenzetu, rais aliye madarakani anapongombea tena, anakuwa scrapped off all presidential privileges isipokuwa ulinzi na wale wagombea wengine wote wa urais wanapatiwa ulinzi na basic logistical support kama ni ving'ora, wote ni ving'ora na sio utaratibu wetu wa mgombea mmoja mwenye dola ameshika mpini kugombea kisu cha makali kuwili na wagombea makapuku!, unategemea ushindani wa haki?.

Sehemu ya Nne ya Sura hii inaainisha utaratibu wa uchaguzi unaojumuisha masharti kuhusu siku na muda wa kupiga kura, mawakala wa upigaji kura, masanduku ya kura, muundo wa karatasi za kura na katazo la kuweka wazi kura.

Sehemu ya Tano inaweka masharti kuhusu utaratibu wa kupiga na kuhesabu kura. Masharti hayo yanajumuisha watu wanaostahili kupiga kura, mazingira yanayoweza kumfanya mtu kupotezasifa za kupiga kura, utaratibu wa kupiga kura, watu wanao ruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura, mazingira yanayoweza kusababisha kuahirishwa kwa upigaji kura inapotokea vurugu, kufungwa kwa zoezi la upigaji kura na utaratibu wa kuhesabu kura. Kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii, mawakala wa upigaji kura wanatambuliwa kuwa mawakala wa kuhesabu kura. Vilevile Sehemu hii inaainisha wajibu wa msimamiziwa kituo baada ya kuhesabu kura, utaratibu wa kujumuisha kura katika uchaguzi wa wabunge na madiwani na utaratibu wa kutangaza matokeo ya ubunge na udiwani. Sehemu ya Sita ya Sura hii inaweka masharti kuhusu uteuzi wa wabunge na madiwani wanawake viti maalum na unatambua utaratibu ulioainishwa katika Katiba na Sheria za Serikali za Mitaa kuhusu wabunge na madiwani wanawake viti maalum.
Itaendelea wiki ijayo.
Wasalaam
Paskali
Gari ina misingi yake injini na chases na hii Sheria Ina msingi wake nao ni wasimamizi kutokuwa na mashaka pande zote
 
Pascal sijui kichwa chako kikoje? bado unatafuta wapi wakuone wakupe uteuzi? This is one aspect among a million! How come you praise such a silly single rubbish!
Mkuu The Retired, this is all about being appreciative, kushukuru kwa kidogo ili upatiwe kikubwa!. Kama unanihesabu na mimi ni praise team, nafukuzia teuzi, endelea kuniona hivyo, wenye jicho la tatu who can read in between the lines, wananijua sifukuzii teuzi na Maza mwenyewe niliisha mweleza Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

Kama mamlaka ya uteuzi ni Rais Samia, mtu mwenye guts kupandisha bandiko kama
HII kweli huyu ni msaka teuzi?!.

Acheni kazi iendelee!
P
 
Hata mm suara la mgombea mmoja Bado Nina mashaka nalo.
Yaan kura zipigwe za ndio au hapana wakati hakuna mawakala wa vyama vingine vya siasa unafikili Kuna uhalali hapo?
Kura ya ndiyo au hapana hairutubishi demokrasi bora chama husika kipewe muda wa kuleta jina jingine ndani ya siku 14 wakishindwa ndipo kura ya ndiyo/hapana ipigwe na mawakala na Tume wahusike kuhesabu kura hizo. matokeo yake yawe na kifungu cha kupingwa mahakamani na mwananchi yeyote
 
Tatizo kubwa la sheria hii ni uchaguzi kendelea kusimamiwa na Wakurugenzi wa majiji na manispaa hapa ni shida kubwa hakuna mabadiliko lakini pia uandikishaji wa wapiga kura kwa vipindi viwili tu, hili zoezi linapaswa lifanywe kuwa endelevu chini ya maofisa wa Tume.
 
Mimi bado sijafurahishwa, kura za ndio na hapana, bado ni kizungumkuti. Watu watapiga ndio tu hata kama hawataki.

Hivi haiwezekani kabisa kama hajatokea mtu kuahirishwa uchaguzi wa sehemu husika mpaka mtu apatikane.
Watu kupiga ndio na hapana kwa mgombea mmoja ni usanii tu kama wa Nyerere na kivuli.

Kwanini kwenye uchaguzi wa vyama vingi wenye demokrasia mtu agombee peke yake ? Eti kisa unakuta mshindani wake kaenguliwa na tume.....hii sio demokrasia.

Hizo hapana zitapuuwa tu, Kuna chama hakitegemei hata kura kushinda.
 
Hapa umenena vyema na hiki ndio kichaka Cha akina Tulia Ackson kujidai kuwa CCM wanamiliki Dola
Swala langu kwa chama changu tawala, hivi tunaogopa nini kuunda tume huru kukawa na uchaguzi huru. Jinsi mtandao wetu ulivyo mkubwa, jinsi wananchi wanavyotuamini tunashindwaje kwenye uchaguzi. Kwa vyovyote vile hawa wapinzani wana kelele tuu. Hawawezi hata kwa miaka 100 kufanikiwa kushika dola. Ushauri wangu ni kuwa tume iwe huru ili tupunguze kelele. Mwisho wa siku tutawauliza kwa mbwembwe sana kuwa, haya tume huru hiyo.na bado mmeshindwa sasa semeni jingine
Wakatabahu
 
Hata kama tumeamua kupaka rangi tu, mbona hakuna tofauti na rangi ya nyuma... Upotevu wa pesa tu.
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko mwendelezo wa three series za uchambuzi wangu wa sheria mpya ya Uchaguzi, 2023. Kama hukuona 1st series, anzia hapa Asante Rais Samia kwa Muswada huu. Umuhimu wa mabadiliko ya Katiba kabla ya Sheria hii bado ni muhimu sana. Huu ni uchambuzi Wangu - Part 1 kisha uje hapa
Asante Rais Samia kwa Muswada huu. Umuhimu wa mabadiliko ya Katiba kabla ya Sheria hii bado ni muhimu sana. Huu ni uchambuzi Wangu - Part 1
Kisha Je Wajua Muswada Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2023 ni Batili?. Ni Mvinyo wa Zamani, Kwenye Chupa Mpya?. Why Ubatili Huu?!.
Pia unaweza kupita hapa Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi, Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!. na hapa Tujifunze kuwa na Shukrani kwa Madogo ili Tupatiwe Makubwa!. Japo Tulitaka Kikubwa, Tumepewa Kiduchu!, Tukipokee Tushukuru, au Tususe Kudai Kikubwa?.

Binadamu tuna mtindo wa kuangazia mapungufu zaidi na kujikuta tunakuwa blinded na mapungufu hivyo kutoona mazuri, hata kwenye Biblia ukitaja tuu jina la Yuda, mind za wengi zinakwenda kwa usaliti wa Yuda Iskariote, kumbe kwenye watumishi wa Yesu, kulikuwa na Yuda wawili, Yuda Iskariote msaliti na Yuda Tadei mtu mwema. Jina la Yuda limeghubikwa na usaliti hadi wema wa Yuda Tadei kufunikwa na usaliti wa Yuda Iskariote.

Ndivyo ilivyo hii sheria mpya ya uchaguzi, kufuatia sheria hii kuletwa na ubatili ule ule tunaoupigia kelele kila uchao, tunajikuta tunakuwa too blind to see mema na mazuri ya muswada huu
Hivyo leo naendelea na uchambuzi wangu wa kifungu hadi kifungu huku nikiainisha the good, the bad and the ugly.
Karibu.
View attachment 2831115
Leo naendelea na uchambuzi wangu wa muswada huu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2023, kwa mukhtaasari wa sura zote 10 za sheria hii, kuwaelimisha elimu ya uraia na elimu ya sheria na haki ili Watanzania tuitumie kikamilifu hii miezi 3 ya kutoa maoni na mapendekezo ya maboresho ya sheria hii.
Muswada huu unatunga Sheria ya Uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani ya mwaka, 2023. Kwa ujumla, Sheria hii inaunganisha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292. Hivyo sasa masharti ya uchaguzi wa Rais na Wabunge na Madiwani ni sheria moja na kutekelezwa na mamlaka moja ambayo ni Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hapa ninapendekeza chaguzi zote nchini, uchaguzi wa Rais na Wabunge, Madiwani na Serikali za Mitaa, ufanyike siku moja na kusimamiwa na Tume moja Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hili ni jambo jema!.
Wiki iliyopita nilichambua sura ya kwanza mpaka ya tatu, leo naendelea

Sura ya Nne ya Muswada inaweka masharti yanayosimamia uchaguzi wa Wabunge na imegawanyika katika sehemu mbili, sehemu ya kwanza inahusu sifa za wagombea katika uchaguzi wa Ubunge. Sehemu ya Pili inahusu uteuzi wa wagombea Ubunge ambapo inaainisha siku ya uteuzi, uteuzi wa wagombea, utaratibu wa namna ya kuweka dhamana kwa mgombea wa nafasi ya ubunge, masharti ya mgombea kuteuliwa kwa jimbo moja tu, pingamizi na uamuzi juu ya uhalali wa fomu ya uteuzi

Sura hii pia inaainisha utaratibu wa kufuatwa endapo kuna mgombea mmoja tu halali wa nafasi ya ubunge au endapo hakuna mgombea. Kwa mujibu wa Sehemu hii endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa nafasi ya Ubunge ameteuliwa, mgombea huyo atapaswa kupigiwa kura na atatangazwa kuwa amechaguliwa endapo atapata kura nyingi za ndiyo kati ya kura zote halali zilizopigwa

Maoni: Hili ni jambo jema, zuri na lenye maslahi kwa taifa kwa kurejesha mamlaka kwa wananchi, sasa hakuna tena ushindi wa mtu kupita bila kupingwa!. Kupita bila kupingwa kulifanya chama kuwachagulia wananchi kiongozi. Hii itaondoa zile figusu za kuzuia watu wasigombee, kuwanunua wapinzani na kuzuia fomu zisirejeshwe na mtu kutangazwa mshindi wa kupita bila kupingwa!. CCM ina wabunge 18 ambao wamepita bila kupingwa!.

Sura ya Tano ya Muswada inahusu masharti ya uchaguzi wa Madiwani. Sura hii imegawanyika katika Sehemu Tatu, ambapo Sehemu ya Kwanza inabainisha masharti ya uendeshaji wa uchaguzi wa madiwani, muda wa kuwa madarakani kwa Madiwani, namna na wakati wa kuitisha uchaguzi mdogo na uwakilishi katika Kata. Sehemu ya Pili inaweka masharti kuhusu sifa za mgombea na mazingira ya mtu kukosa sifa ya kuteuliwa katika uchaguzi. Sehemu ya Tatu inajumuisha masharti kuhusu siku ya uteuzi, uteuzi wa mgombea, dhamana za wagombea, utaratibu wa kuweka pingamizi na utaratibu unaopaswa kufuatwa ikiwa kuna mgombea mmoja tu wa nafasi ya udiwani au ikiwa hakuna mgombea.

Sura ya Sita ya Muswada inaweka masharti kuhusu uchaguzi, utaratibu wakupiga kura na uteuzi wa wabunge na madiwani wanawake viti maalum. Sura hii imegawanyika katika Sehemu Sita, ambapo Sehemu ya Kwanza inaweka masharti mbalimbali kuhusu siku ya uchaguzi na tangazo la uchaguzi. Kwa mujibu wa masharti hayo, taarifa ambazo zitakuwa katika tangazo la uchaguzi ni pamoja na siku na muda wa kuanza na kufunga upigaji kura, anwani ya vituo vya kupigia kura, wapiga kura waliopangwa kwa kila kituo cha kupigia kura na taarifa za wagombea walio teuliwa kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi. Sehemu ya Pili inaweka masharti kuhusu mgombea kujitoa na utaratibu unaopaswa kufuatwa endapo mgombea atafariki au hakuna mgombea. Sehemu ya Tatu inaweka masharti kuhusu kampeni za uchaguzi na namna kampeni zinavyopaswa kuendeshwa, ikiwa ni pamoja na masharti kuhusu kuwasilisha ratiba ya mikutano kwa msimamizi wa uchaguzi kwa lengo la kuepuka migongano ya mikutano. Sehemu hii inaweka pia masharti kuhusu upatikanaji na wajibu wa vyombo vya habari vya umma na matakwa ya kutokuwa naupendeleo na kuepuka ubaguzi kwa mgombea yeyote katika utoaji wa matangazo.
Maoni: Hapa bado kuna tatizo, mgombea mmoja ana ving’ora, ana media team ya serikali, ana PA ya serikali, ana magari ya serikali na watendakazi wa serikali!. Nchi za wenzetu, rais aliye madarakani anapongombea tena, anakuwa scrapped off all presidential privileges isipokuwa ulinzi na wale wagombea wengine wote wa urais wanapatiwa ulinzi na basic logistical support kama ni ving'ora, wote ni ving'ora na sio utaratibu wetu wa mgombea mmoja mwenye dola ameshika mpini kugombea kisu cha makali kuwili na wagombea makapuku!, unategemea ushindani wa haki?.

Sehemu ya Nne ya Sura hii inaainisha utaratibu wa uchaguzi unaojumuisha masharti kuhusu siku na muda wa kupiga kura, mawakala wa upigaji kura, masanduku ya kura, muundo wa karatasi za kura na katazo la kuweka wazi kura.

Sehemu ya Tano inaweka masharti kuhusu utaratibu wa kupiga na kuhesabu kura. Masharti hayo yanajumuisha watu wanaostahili kupiga kura, mazingira yanayoweza kumfanya mtu kupotezasifa za kupiga kura, utaratibu wa kupiga kura, watu wanao ruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura, mazingira yanayoweza kusababisha kuahirishwa kwa upigaji kura inapotokea vurugu, kufungwa kwa zoezi la upigaji kura na utaratibu wa kuhesabu kura. Kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii, mawakala wa upigaji kura wanatambuliwa kuwa mawakala wa kuhesabu kura. Vilevile Sehemu hii inaainisha wajibu wa msimamiziwa kituo baada ya kuhesabu kura, utaratibu wa kujumuisha kura katika uchaguzi wa wabunge na madiwani na utaratibu wa kutangaza matokeo ya ubunge na udiwani. Sehemu ya Sita ya Sura hii inaweka masharti kuhusu uteuzi wa wabunge na madiwani wanawake viti maalum na unatambua utaratibu ulioainishwa katika Katiba na Sheria za Serikali za Mitaa kuhusu wabunge na madiwani wanawake viti maalum.
Itaendelea wiki ijayo.
Wasalaam
Paskali
Unafurahia kupewa haki robo au siyo? Wewe ni mwaandishi mnafiki kama unaona jema kwenye sheria zenye mapungufu makubwa yatakayosababisha jamii zetu zikose haki zao za kuchagua viongozi wanaofaa na kutuletea wapuuzi wanaharibu maendeleo yetu na kuingia mikataba mibovu yenye gharama huko mbele siyo tu kwetu bali hadi vizazi vyetu.
 
Mkuu Paskali ni mwanamahakama!! Anavigezo vya kutuelimisha!
NI msomi wa sheria na hajapewa certification ya kutafsiri sheria kama inavyotakiwa.

Tafsiri anayotupa inajikita kwenye tasnia yake aliyosomea na haijikiti kwenye uhalisia na hitaji la wakati.

Sijambeza bali nime-m-challenge
 
NI msomi wa sheria na hajapewa certification ya kutafsiri sheria kama inavyotakiwa.

Tafsiri anayotupa inajikita kwenye tasnia yake aliyosomea na haijikiti kwenye uhalisia na hitaji la wakati.

Sijambeza bali nime-m-challenge
Mkuu Msanii , an advocate is an official of the court, hivyo ni certification tosha kutoa legal opinion, kwa mujibu wa katiba yetu, hakuna certification yoyote ya kutafsiri sheria kwa yeyote zaidi ya Mahakama Kuu!.

Tuna tatizo kubwa sana la legal interpretation, toka kwenye sheria zetu hadi kwa majaji wetu!. Mfano mzuri ni huu- Katiba ndio sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni batili!.

Mtunga katiba alidhamiria katiba ndio inayobatilisha sheria batili na sio Mahakama Kuu!, kazi ya Mahakama Kuu ni kuthibitisha tuu huo ubatili na kutamka sheria fulani ni batili, tangu baada ya tamko hilo la Mahakama Kuu kuwa sheria fulani ni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, anayeibatilisha sheria batili hiyo ni katiba ya JMT na sio Mahakama!. The role of the court is kutamka tuu kuhusu huo ubatili na katiba ndio inaubatilisha!.

Bunge la Tanzania limetunga sheria batili, Mahakama Kuu ikatangaza ubatili huo na kuubatilisha, serikali yetu ikakata rufaa kupinga uamuzi wa huo!, kama katiba ndio sheria Mama, katiba imetamka sheria yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni batili, serikali imetunga muswada wa sheria batili, ikaupeleka huo muswada Bungeni kutungwa sheria, Bunge likatunga sheria batili, Mahakama ikaitangaza ni sheria batili, baada tuu ya Mahakama kutangaza ubatili wa sheria batili, ni katiba ndio inaibatilisha!, hivyo baada tuu ya uamuzi ule wa Mahakama, sheria batili hiyo inakuwa imebatilika there and then!, sasa serikali inapata wapi mamlaka ya kuikatia rufaa katiba?.

Nimejitolea kuendesha elimu ya katiba, sheria na haki ili kuwaelimisha Watanzania waijue katiba yao, sheria zao na haki zao, ili waweze kutimiza wajibu wao!.

Somo la kwanza ni kuijua katiba ni nini, katiba ni ya nani, na mamlaka ya katiba ni yapi na yametoka kwa nani!. Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio kila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?

Somo la pili nikaendesha kuhusu katiba ni sheria Mama, maana yake ni nini?. Ijue Katiba kwa Jicho la Mtunga Katiba: Mtunga Katiba alimaanisha nini aliposema "Katiba ni Sheria Mama"? Ni kweli Katiba ni Sheria Mama?

Na baada ya ubatili huo kutangazwa na Mahakama Kuu, serikali yetu ikakata rufaa, ikashindwa!. Ikauchukua ubatili huo na kuuchomekea kiubatili ndani ya katiba yetu!.

Mahakama Kuu ikakata na kutoa uamuzi kuwa sheria hiyo ni batili na uchomekea huo wa batili ndani ya katiba yetu pia ni batili!. Serikali ikakata rufaa ikashindwa tena!.

Kwa vile Jaji Mkuu anateuliwa na rais, serikali ikaomba review ya Mahakama ya rufaa, na Mahakama ya Rufani ikiongozwa na CJ mwenyewe akisaidiwa na majaji 7, Full Bench, wakatoa uamuzi wa ajabu kabisa kuwahi kutokea!, eti Mahakama haina uwezo wa kuliingilia Bunge kwenye jukumu lake la utungaji wa sheria, kama Bunge limetunga sheria batili na kufanikiwa kuipenyeza mpaka kwenye katiba ya JMT, then, Mahakama haina mamlaka ya kuingilia hilo ni Bunge lenyewe ndio lirekebishe!.

Yaani katiba ivunjwe na Bunge kwa kutunga sheria batili kinyume cha katiba, halafu kikauchomekea ubatili huo kiubatili ndani ya katiba yetu!, Mahakama yenye uwezo wa kutamka ubatili huo, inaligwaya Bunge!, sasa ndio serikali inaleta sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule!, unategemea nini?!.

P.
 
Bila kupingwa

Ule utaratibu ulikuwa ni wa kishetani sana

Hata Nyerere hakuwahi Kupita bila kupingwa [emoji23]

2025 tutaona wagombea wa CCM wakipitishwa wao tu kisha siku ya uchaguzi ajapigiwa kura yy tu,sasa hii ina tofauti gani ya kupita bila kupingwa?
Akipigiwa kura yy tu DED atamnyima kutangazwa?
Mnajidanganya sana watz,CCM ingekua na nia njema ingeondoa mchskato mzima wa uchaguzi mikononi mwa DED ambao siku hizi wanateuliwa hadi Wenyeviti wa CCM kiwa DEDs
 
2025 tutaona wagombea wa CCM wakipitishwa wao tu kisha siku ya uchaguzi ajapigiwa kura yy tu,sasa hii ina tofauti gani ya kupita bila kupingwa?
Akipigiwa kura yy tu DED atamnyima kutangazwa?
Mnajidanganya sana watz,CCM ingekua na nia njema ingeondoa mchskato mzima wa uchaguzi mikononi mwa DED ambao siku hizi wanateuliwa hadi Wenyeviti wa CCM kiwa DEDs
Wenzako wanaangalia Maokoto

Awe na mshindani au Peke yake lazima amwage mpunga 😂
 
Kwa nchi ya Tanzania, ambayo imejaa mambo ya hovyo kwenye maadili ya uchaguzi na utawala, ni vema tusiwe na wagombea wa kupita bila kupingwa wala mgombea mmoja wa kupigiwa kura ya ndiyo au hapana.

Mahali popote ambapo kutakuwa na mgombea mmoja tu aliyepitishwa na tume, chama/vyama ambavyo mgombea/wagombea wake wameondolewa na tume kwa kutokukidhi vigezo wapewe siku 7 za ama kuleta wagombea wapya, au wagombea walioenguliwa kurekebisha makosa yaliyotajwa, kama sababu zilizotajwa zinarekebishika.

Lazima tuondokane na ule upumbavu wa kumwondoa mtu kwa sababu za kijinga kuwa eti amekosea kujaza fomu. Kama amekosea kujaza fomu (ingawa huwa ni uwongo) apewe siku moja kurekebisha hayo makosa ya ujazaji wa fomu.

Sheria ile inayosema kuwa eti tume ya uchaguzi isishtakiwe ifutwe. Badala yake kuwepo sheria ya kifungo hadi cha miaka mitano kwa wasimamizi wa uchaguzi ambao matendo yao yalilenga kuharibu mfumo wa demokrasia kufanya kazi, kama vile msimamizi wa uchaguzi kukataa kupokea fomu ya mgombea, msimamizi wa uchaguzi kufunga na kuikimbia ofisi yake muda aliostahili kuwepo ofisini, kumtangaza mgombea ambaye hakuna uthibitisho wa kupata kura nyingi kuwazidi wagombea wengine, na mengine yanayofanana na hayo. Makosa yote ya wasimamizi wa uchaguzi yaliyolenga kuzuia demomrasia kufanya kazi, wahusika adhabu yao iwe kifungo jela, bila option ya kulipa faini.
Uko Right Kwa nchi yenye mfumo wa vya vyingi,swala la mgombea 1 kupita na kubigiwa kura ya Ndio or Hapana ni uhuni tu, si kweli vyama vyote eti Mgombea apite awe mmoja ni dalali za rushwa na njia yakupata ushindi wa mezani.
 
Wananchi wa Bukombe,
Tunaitumia serikali na CCM Salaàm za Mwaka Mpya wa 2024.

Lkn pia tunasema 2025 hapa Bukombe ndani ya CCM na ikiwezekana uchaguzi Mkuu iwapo atakuwa tayari kuendelea kuwa mbunge basi asipaswe kuwa na mpinzani. Kazi alizofanya ni nyingi sana lkn kubwa zaidi amewekeza kwa wananchi (Sisi).

Pamoja na kuwa uchaguzi ni jambo la kikatiba lkn si lzm kumsumbua kiongozi huyu - CCM Bukombe imeungana, madhehebu ya dini yameungana, taasisi za umma zimeungana" mambo yako safiiiii".

Tutasikika!
 
Wananchi wa Bukombe,
Tunaitumia serikali na CCM Salaàm za Mwaka Mpya wa 2024.

Lkn pia tunasema 2025 hapa Bukombe ndani ya CCM na ikiwezekana uchaguzi Mkuu iwapo atakuwa tayari kuendelea kuwa mbunge basi asipaswe kuwa na mpinzani. Kazi alizofanya ni nyingi sana lkn kubwa zaidi amewekeza kwa wananchi (Sisi).

Pamoja na kuwa uchaguzi ni jambo la kikatiba lkn si lzm kumsumbua kiongozi huyu - CCM Bukombe imeungana, madhehebu ya dini yameungana, taasisi za umma zimeungana" mambo yako safiiiii".

Tutasikika!
Amefanya nini Bukombe?
 
Mmeanza so ndio!!?
Majaliwa ndio mgombea 2025 Hilo lipo wazi!

Biteko no waziri mkuu!!

TEC wakizingua tunamweka Gwajima,wakileta udini!!

Tuna plan A na Plan B!

Mkileta wenge hasa mkojani akikomalia Bas wale jamaa watachukua tulale saa 12:00 jioni!

Mbingu,mawe na vitu vyote vimekubali haya!!
Tunasubiri kwa uvumilivu!!
 
Back
Top Bottom