Lifahamu kiundani zao la Nyanya chungu (Ngogwe) na jinsi ya kulilima

Lifahamu kiundani zao la Nyanya chungu (Ngogwe) na jinsi ya kulilima

Uvunaji wa ngogwe (Nyanya chungu) hufanyika kila wiki baada ya miezi miwili toka kupandikiza, na uvunaji huendelea kwa miezi 6 hadi 7. Mimea ikianza kukauka kwa kuzeeka hukatwa kwenye shina chini na kuachwa lichipue tena na uzaaji huanza upya tena baada ya miezi 2 hadi 3. Matunda yaliyovunwa huwekwa kwenye viroba na kusafirishwa kwenda sokoni.
Kubota Leo nimesia mbegu za nyanya chungu na biringanya.nimeona nikisubiri mpaka niende shambani kwangu nitazidi kuchelewa hivyo busts ni za maya hapa home ndo nimeamua kupanda mboga mboga kwani nimeona nitafaidika zaidi ya huo urembo wa maua.jiandae kupokea usumbufu kutaka kwangu
 
Kubota Leo nimesia mbegu za nyanya chungu na biringanya.nimeona nikisubiri mpaka niende shambani kwangu nitazidi kuchelewa hivyo busts ni za maya hapa home ndo nimeamua kupanda mboga mboga kwani nimeona nitafaidika zaidi ya huo urembo wa maua.jiandae kupokea usumbufu kutaka kwangu

Nakushukuru kwa kuhamasika, Nyanya chungu na Bilinganya ni mazao ndugu! Mahitaji yao yanafanana, huduma yake inafanana na maadui na magonjwa yao yanafanana! Karibu tuongee Mama Timmy!
 
Nakushukuru kwa kuhamasika, Nyanya chungu na Bilinganya ni mazao ndugu! Mahitaji yao yanafanana, huduma yake inafanana na maadui na magonjwa yao yanafanana! Karibu tuongee Mama Timmy!
Nashukuru sana.endelea na moyo huo huo.nakupa Mia ya Mia kwani umenitoa kwenye urembo wa maua mpaka kupanda mboga mboga.
 
Nashukuru sana.endelea na moyo huo huo.nakupa Mia ya Mia kwani umenitoa kwenye urembo wa maua mpaka kupanda mboga mboga.

ningependa kupata mbegu na mie nilime kwa style hiyo ya kupandia nyumbani badala ya maua,napata wapi mbegu nzuri za nyanya chungu na bilinganya,na maelekezo ya kuztunza hadizkue,na znachukua mda gani kukua hadi mavuno
 
ningependa kupata mbegu na mie nilime kwa style hiyo ya kupandia nyumbani badala ya maua,napata wapi mbegu nzuri za nyanya chungu na bilinganya,na maelekezo ya kuztunza hadizkue,na znachukua mda gani kukua hadi mavuno

Kama unaweza ku-download kwenye hii thread kuna attachment mbili nimeweka zenye maelezo japo kwa kifupi juu ya kutunza zao hili! Pia kuhusu mbegu, zinapatikana kwenye maduka ya pembejeo kwa wingi kabisa! Jitahidi sana mkuu usome huu uzi wote kuanzia mwanzo wadau wamechangia sana kuhusu wapi kwa kupata mbegu na mizengwe yake.

Angalizo: Kama ukinunua mbegu ukasia ukaimwagilia vizuri kabisa ni rahisi sana kuota, ukiona pamoja na juhudi ya umwagiliaji bado zisiote ujue mbegu hiyo ilikuwa si nzima. Nimewahi kukutana na tatizo hilo la mbegu kutoota. Kama utapenda kununua mbegu kwa mkulima lazima uhakikishe unaenda kuthibitisha mwenyewe shambani kwake kama ni aina ya nyanya chungu unayotaka! Usipofanya hivyo ukaenda kununua mbegu sokoni tu utakuja shangaa mimea mingine haizai, mimea mingine inamatunda madogo madogo kama njugu na matunda ya ajabu ajabu. Zingatia kununua mbegu bora kutoka kwenye vyanzo vya uhakika!
 
Nami nilikwenda Ruaha kwa nia ya kulima kitunguu lakini mwenyeji wangu akanipa wazo la kuanza na nyanyachungu. MUNGU akijalia kuanzia wiki ya mwisho ya January nitaanza kuokota moja moja. Nitawajuza.

Mkuu Omugurusi, nadhani hivi sasa uko bize kuhesabu noti, sijui kama unapata fursa ya kufika hapa jukwaani. Naomba utujuze iwapo mwenyeji wako alikuwa sahihi kwa wazo lake uanze na nyanya chungu! Funguka mkuu Watanzania wengi wanasubiri ahadi yako!
 
Kubota Leo nimesia mbegu za nyanya chungu na biringanya.nimeona nikisubiri mpaka niende shambani kwangu nitazidi kuchelewa hivyo busts ni za maya hapa home ndo nimeamua kupanda mboga mboga kwani nimeona nitafaidika zaidi ya huo urembo wa maua.jiandae kupokea usumbufu kutaka kwangu

Mama Timmy mbona kimya? Ziliota? Kitalu kinaendeleaje! Nisumbue mweee!!!
 
Kama unaweza ku-download kwenye hii thread kuna attachment mbili nimeweka zenye maelezo japo kwa kifupi juu ya kutunza zao hili! Pia kuhusu mbegu, zinapatikana kwenye maduka ya pembejeo kwa wingi kabisa! Jitahidi sana mkuu usome huu uzi wote kuanzia mwanzo wadau wamechangia sana kuhusu wapi kwa kupata mbegu na mizengwe yake.

Angalizo: Kama ukinunua mbegu ukasia ukaimwagilia vizuri kabisa ni rahisi sana kuota, ukiona pamoja na juhudi ya umwagiliaji bado zisiote ujue mbegu hiyo ilikuwa si nzima. Nimewahi kukutana na tatizo hilo la mbegu kutoota. Kama utapenda kununua mbegu kwa mkulima lazima uhakikishe unaenda kuthibitisha mwenyewe shambani kwake kama ni aina ya nyanya chungu unayotaka! Usipofanya hivyo ukaenda kununua mbegu sokoni tu utakuja shangaa mimea mingine haizai, mimea mingine inamatunda madogo madogo kama njugu na matunda ya ajabu ajabu. Zingatia kununua mbegu bora kutoka kwenye vyanzo vya uhakika!
nashukuru Mungu akubariki
 
Linapokuja suala la ujasiliamali ni mazao yenye majina makubwa tu kama matikiti, vitunguu na Tomato hutajwa! Nyanya chungu ni zao lisilovuma sana japo linawatoa sana wakulima na linawalaji wengi sana. Nyanya chungu mfano aina maarufu kama YEBOYEBO ni zao linalonivutia sana kwa sifa zifuatazo:

1. Afrika ni nyumbani kwao linazaa sana hata wakati wa joto kali ambapo kwa tomato na hoho hubabuka sana kwa jua
2. Tomato na Hoho hupunguza sana kutoa maua na matunda kwenye joto kali YEBO YEBO hupeta tu
3. Mazao mengi ya bustani huhitaji madawa ya ukungu kupita kiasi majira ya mvua, nyanya chungu hazideki ki hivyo
4.Tomato na hoho usafirishaji wake ni kama mayai, nyanya chungu zisafirishwapo mara nyingi watu hukaa juu yake
5. Kipindi cha kuanza kuchuma hadi mmea kuchakaa kwa aina nyingi za tomato ni mwezi mmoja, hoho zenye ubora ni miezi 2, lakini nyanya chungu huchumwa kwa zaidi ya miezi 8 ili mradi zinamwagiliwa maji na mbolea.
6. Wakati bei ya Tomato ikianguka mkulima nae hugalagala chini asisimame tena lakini nyanya chungu haimtupi mkulima kivile

Kwa wenye mitaji midogo wanaotaka kuikuza ili waweze kupata nguvu kubwa ya kilimo bila kuwa na presha inayopanda na kushuka Nyanya chungu ni zao lenye uhakika mkubwa!

Swali ni kwa nini zao hili halitajwi sana yaani halivumi ?

je naeza lima nyanyachungu morogoro eneo ambalo wazawa wanalima mahindi tena bila mbolea?kwa msimu huu wanapoanza wao kulima mahindi?
 
je naeza lima nyanyachungu morogoro eneo ambalo wazawa wanalima mahindi tena bila mbolea?kwa msimu huu wanapoanza wao kulima mahindi?

Unaweza kulima na utavuna tu! Ila ukae ukijua kuwa zao litakoma kuzaa pale unyevunyevu wa shambani utakapoisha, na pia mavuno yatategemea na kiasi cha rutuba ya asili ya eneo. Kama kuna rutuba tosha zao litasitawi tu.
 
Unaweza kulima na utavuna tu! Ila ukae ukijua kuwa zao litakoma kuzaa pale unyevunyevu wa shambani utakapoisha, na pia mavuno yatategemea na kiasi cha rutuba ya asili ya eneo. Kama kuna rutuba tosha zao litasitawi tu.
asante naendelea kutafakari,nimeambiwa na mtu aliye lima mwaka jana alitumia laki nne hadi kuvuna,kwa heka 4,so mi ndo natafakari ni zao lipi likalo nipa faida zaidi kwenye ardhi hii ndo nimemaliza chuo najipanga kimaisha naitaji zao ambalo atleast litanipa mazao mengi,na kwasababu ndo naanza ningependa low risk crop,naomba ushauri wako
 
Ni kweli anza na zao ambalo ni low risk na lenye faida. Anza eneo dogo. Awamu hizi za kwanza zitakuwa ni darasa lako la vitendo ambapo utajifunza kwa vitendo utunzaji wa zao husika na changamoto zake na matokeo yake utayaona kwa macho. Pia itakuwa ni darasa lako la kujifunza mambo ya masoko na mbinu za uuzaji. Kuna mazao low risk ya shamba na kuna mazao low risk ya Bustani. Ni budi uwe wazi unataka kufanya uzalishaji wako eneo gani na iwapo kilimo ndiyo itakuwa full time employment kwako. Wakati ukiendelea kutafakari pitia kusoma ushauri niliowahi kumpa ALF kwenye thread yake ya "Msaada wa ushauri" huenda kukawa na kipengele kitakachokufaa.

Ninakusisitiza sana mtumie huyo jamaa yako ambaye tayari alishaingia kwenye gemu ili utumie uzoefu wake. Kama alilima kwa gharama ndogo namna hiyo akapata faida mtumie na ulime zao hilo hilo japo kwa eneo dogo. Huyo jamaa atakuwa tayari anajua wapi kwa kuuza, anajua wateja na anajua changamoto za zao hilo, huyo jamaa mchukulie kuwa ni sehemu ya mtaji wako pia. Usianze kulima zao ambalo huna taarifa zake zozote, hujui mbinu za kulilima, hujui soko lake na hujui changamoto zake usifanye hivyo katu!
 
Mh! nimeitoa hii thread kwenye archive nimeikunguta vumbi naileta tena sebuleni wenye kusoma wasome mtaokota kitu tu!
 
Mh! nimeitoa hii thread kwenye archive nimeikunguta vumbi naileta tena sebuleni wenye kusoma wasome mtaokota kitu tu!

Mkuu huu uzi ulikua mtamu halafu ukafa ghafla I hope waliolima watakuja kutoa mrejesho
 
Mkuu huu uzi ulikua mtamu halafu ukafa ghafla I hope waliolima watakuja kutoa mrejesho

Mkuu Sabayi ndiyo maana niliuliza kwenye thread, hivi vizao vingine kwa nini havina mvuto wa kuvijadili? Ila acha watu wazinyanyapae tu ili ushindani uwe mdogo kwa sisi tulioujua uzuri wa ngoma. Ngoja hapa niwaite wakubwa hawa huenda wakatuchangamsha japo kuvunja mbavu tu:

  • Mkuu Malila ulishamtembelea yule DR........ pale Buguruni? Alikubali kuingiza hii kitu kwenye prescription zake!?
  • Mkuu Omugurusi bado unaendelea kukamua hiyo mimea huko Ruaha?
  • Mkuu Mama Timmy lile zoezi la kupanda mseto wa maua na Nyanya chungu lilifanyika?
  • Husniyo vipi Mkuu uliingia na wewe kwenye hili game?

Wakuu tunaomba feedback!!!
 
Mkuu Sabayi ndiyo maana niliuliza kwenye thread, hivi vizao vingine kwa nini havina mvuto wa kuvijadili? Ila acha watu wazinyanyapae tu ili ushindani uwe mdogo kwa sisi tulioujua uzuri wa ngoma. Ngoja hapa niwaite wakubwa hawa huenda wakatuchangamsha japo kuvunja mbavu tu:

  • Mkuu Malila ulishamtembelea yule DR........ pale Buguruni? Alikubali kuingiza hii kitu kwenye prescription zake!?
  • Mkuu Omugurusi bado unaendelea kukamua hiyo mimea huko Ruaha?
  • Mkuu Mama Timmy lile zoezi la kupanda mseto wa maua na Nyanya chungu lilifanyika?
  • Husniyo vipi Mkuu uliingia na wewe kwenye hili game?

Wakuu tunaomba feedback!!!

Sijamtembelea yule wa Buguruni, ila nilimtembelea yule wa Farm Base tawi la Mkuranga, nimeingia ktk hili game kwa mikakati mathubuti, kwanza nataka liwe game organic, nilikosea nikaanza bila tahadhari, mbuzi wamefanya vitu vyao na kuku nao wamemaliza. Baada ya vurugu hii, sasa nimeanza na kutenganisha, yaani wapi ale kuku na wapi niweke mboga. Namhitaji kuku kwa sababu ya mbolea yake, kadharika mwisho niwe na zero grazing ili niweze kuotesha miembe, mbuzi anakula majani aina nyingi mno hadi mchongoma !!!!! Muda si mrefu nami nitaanza kuingiza vitu sokoni.
 
Back
Top Bottom