cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 96,456
- 156,324
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Deo muhimu [emoji23][emoji23][emoji23]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Deo muhimu [emoji23][emoji23][emoji23]
Hapo kwa Katrina, utabiri wangu ni kwamba Analyse hakumtokea huyo binti, ila swaga za binti za mazoezi jumlisha na swaga za Aposto za tizi ndio zitazo mchanganya binti aingie kingi kwa aposto halafu kama kawaida Baba Husna nae golini ni kama yupo na OnanaYaani Analyse Analyse Analyse nimekuita mara 3.
We jamaa mbona unarudia makosa kila siku?
Kwanini hujifunzi?
Why?
Yaani ulivyoandika hivi najua story yako itaisha kwa wewe kumla huyo binti mzee B kujua na kukufutilia mbali na visasi juu.
Mkuu najua episode zitakazofuata utapuyanga tu lakini mbona ni kama deal nzuri zinakujia alafu wewe ndo unaenda kuharishia hapo
Unanikera mkuu japo sijui ilikuwaje na huyo binti lakini.....
😏😏😏
Swahiba ulisahau kunitagAcha tu mkuu 😅
Mithali 6:26
Kushney babhuji.Qwiiiiiiisheeeerrrr
Hapo kwenye kipengele cha kupenda wamama najiona ni mimi mtupu kabisaPortion 02:
.... Kipindi yupo kidato cha nne mwanzoni, kazi zikawa zimepungua sana kule. Maana ilikuwa ni msimu wa mvua. Sikuona haja ya kuendelea kuishi kule ikiwa sitengenezi hela.
Nikamtafuta mdau, nikamuuzia ghetto langu ili niondoke kule. Nikamwambia Ester kwamba nina mpango wa kuondoka pale kijijini. Aliumia tu, ila hakuwa na namna. Siku ambayo kesho yake nilikuwa natarajia kuondoka, Ester alikuja pale ghetto na tulishinda wote siku nzima.
Wakati anataka kuondoka, akaniambia:
Ester: "Nikuambie kitu?"
Mimi: "Niambie"
Ester: "Najua wewe kama mwanaume kuna vitu siwezi kukuzuia usifanye, kama uliweza kuvifanya hapa na Mimi nikiwepo, sidhani kama ukiwa mbali utajizuia. Ila ombi langu kwako ni moja tu"
Mimi: "Ombi gani?"
Ester: "Vyovyote itakavyokuwa, naomba usibadilishe namba ya simu. Na hata ikitokea imeshindikana ukabadilisha basi naomba unitafute kwenye hii namba ya bibi (akanipa note book ndogo ikiwa na namba ya simu)"
Mimi: "Sawa usijali"
Ester: "Unaniahidi?"
Mimi: "Ndio nakuahidi"
Ester alikuwa ananipenda sana,sijui hata alinipendea nini.
Ila nilifurahia kuondoka kule, nikijua sasa hiyo ndio nafasi ya Ester kunisahau. Kwavyovyote vile umbali ungetutenganisha tu. Alafu sio kwamba Ester alikuwa mbaya, hapana. Kiuhalisia kati ya wanawake ambao Nishawahi toka nao, kwenye top 3 yupo. Shida yangu kubwa akili yangu ilikuwa imeshikwa sana na wamama, kiasi kwamba mabinti niliona wananipotezea muda.
Ndio maana siku zote kabla ya kumuomba Mungu anifungulie milango ya neema, nilikuwa namuomba anitoe kwenye huu uraibu wa wamama. Niliamini nikiweza kuwaepuka, basi mengine yote yatakaa kwenye mstari.
***** ***** ***** ****** ****** ******
Nilivyotoka kule, moja kwa moja mpaka Dar. Nikarudisha harakati zangu pale.
Mara chache chache nilikuwa nawasiliana na Ester, japo mara zingine nilikuwa nazipotezea calls zake au text. Hii yote nikumfanya anitoe akilini mwake.
Mwanzoni alilalamika lalamika, mara zote nikawa namwambia kazi nyingi nakuwa busy. Hakuamini utetezi wangu, ila hakuacha kunitafuta.
Ester: "Hivi mbona unanifanyia hivi lakini?. Hunipendi tena?"
Mimi: "Sio kwamba sikupendi, ila naamini Mimi sio mtu sahihi kwako. Natamani upate mtu atakayeweza kukufanya uwe na furaha"
Ester: "Wewe ni mtu sahihi kwangu, na ukiamua niwe na furaha unaweza. Maana kila kitu kipo ndani ya uwezo wako"
Nikaishia kumuitikia tu.
Alimaliza form four, akachaguliwa kwenda advance shule moja ya wasichana inaitwa Igowole ipo kule kule Iringa. Nilimpongeza, nikamtumia hela kama zawadi, maisha yakaendelea.
Kipindi akiwa advance, Mimi nikawa na safari ya kuelekea mkoani Iringa. Maana ni kipindi ambacho nilikuwa nimeanza dili za mkaa na yule Mzee Dingi, hivyo nilimwambia Ester kuwa nitakuwa maeneo ya Usokami. Alivyosikia hivyo alifurahi sana:
Ester: "Kweli unakuja?"
Mimi: "Ndio. Ungekuwa na nafasi tungeonana"
Ester: "Basi tukutane Mafinga, nitaomba ruhusa ya kwenda hospital"
Mimi: "Hivyo inawezekana kupata ruhusa?"
Ester: "Ndio. Wengi wanaendaga sana. Na Mimi nitaomba ruhusa"
Basi tukaweka mipango yetu hivyo. Na kweli alifanikiwa kupewa ruhusa. Mimi nilifika Mafinga usiku, yeye akaja Kesho yake asubuhi. Tulishinda wote mpaka kwenye mida ya saa nane ndio akaondoka.
Wakati tukiwa kituoni anasubiria gari ijae arudi shule, akaniambia:
Ester: "Siku sio nyingi tutakuwa wote huko Dar mpenzi"
Mimi: "Mnahamia Dar?"
Ester: "Hapana, ila chuo nitasomea Dar"
Mimi: "Jitahidi ufaulu vizuri, ndio utaweza kuwa na nafasi ya kuchagua usomee wapi chuo"
Ester: "Najua nitafaulu tu"
Tuliongea ongea pale, mpaka gari ikajaa kisha wakaondoka. Na Mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea kijijini kucheki mkaa.
Nikiwa kule, mashine ikawa inawasha sana. Na wakati wa kukojoa kuna maumivu fulani nayapata. Ile hali ilivyozidi, ikabidi niende hospitali. Pale ndio nikaambiwa nina gono. Hii ndio ilikuwa mara ya kwanza nakutana na huu ugonjwa.
Nikataka kusema Ester kaniambukiza? Ila haraka sana akili yangu ikanikatalia. Maana dalili za kuwashwa nilikuwa nazo tokea nikiwa ndani ya bus naelekea Mafinga. Hii inaonesha ugonjwa nimesafiri nao. Hapo ndio nikamkumbuka Halima, maana ni yeye ndio wiki iliyoisha yote nilikuwa nae. Kivyovyote vile huu mzigo nimeutoa kwake.
Issue ikaja, kama Mimi ninao, basi lazima na Ester nimempa. Kama natumia dawa, basi na yeye inabidi atumie dawa. Ila nitamwambiaje?? Ikabidi zile zile dawa nilizopewa Mimi pale hospital, nimnunulie na Ester. Ila nitampaje dawa wakati haumwi? Na hajaniambia kama anaumwa, nikimtumia dawa lazima aniulize nimejuaje.
Ikabidi nitulie mpaka aniambie. Ila nikawa namjulia hali mara kwa mara ili kujua maendeleo yake. Hazikupita siku nyingi, akaniambia kuwa anatokwa na uchafu mwingi ukeni. Pale pale nikamwambia nitamtumia dawa. Nikaziagiza kwa gari. Alivyozipata akaanza kuzitumia. Hakunihoji chochote, kwamba Mimi sio daktari nawezaje kumuagizia dawa? Alipata nafuu na kupona kabisa.
Siku moja kwenye mazungumzo, nikamuuliza aliwezaje kumeza dawa bila hata kuhoji? Akanijibu "Mimi ni mkeo, naamini huwezi kunidhuru."
Nikabaki kimya kwa muda. Mara zote amekuwa akiniita Mimi mume wake, ila kwa upande wangu sikuwahi kumchukulia hivyo. Sikutaka kuendelea na hiyo mada.
********** * **
Hatimae akamaliza kidato cha sita na katika waliochaguliwa kwenda jeshini jina lake lilikuwepo. Akaniuliza kama nipo tayari endapo ataamua kuja kuishi na mimi kwa ile miezi mitatu badala ya kwenda jeshini. Nikamkatalia na kumpa sababu nyingi za yeye kwenda jeshini. Mwisho wa siku akakubaliana na mtazamo wangu.
Ila ukweli ni kwamba sababu zote nilizompa hazikuwa ndio dhumuni halisi la kumtaka aende jeshini. Ambacho sikutaka ni yeye kuja ninapoishi, maana kipindi naishi Dar ghetto palikuwa na jam kama la kwenye ATM ifikapo mwisho wa mwezi. Sikupenda Ester anione vile.
Kabla hajaenda aliomba anitumie documents zake za shule ambazo angekuja kuzihitaji kwenye kuapply chuo na mkopo. Nikamwambia azitume kwenye email yangu, akafanya hivyo.
Wakati wa kwenda jeshini ulipowadia aliomba sana apitie Dar ninapoishi alafu ndio aende huko jeshini. Nikamkataa kwa mara nyingine, maana kama angekuja ungekuwa msala mwingine. Hakuwa na namna akaenda jeshini bila sisi kuonana. Niliamini akiwa jeshini lazima atakutana na mtu ambae atamfanya aachane na Mimi, hivyo yeye kwenda jeshini kwangu niliona ni ahueni.
Matokeo yalipotoka alifaulu vizuri tu, na kipindi cha kuapply vyuo kilipoanza akaniomba nimuombee maana taarifa zake nilikuwa nazo:
Mimi: "Nitajie kozi unazopenda kusoma pamoja na vyuo ili nikufanyie hiyo application"
Ester: "Chagua vyuo vyovyote vya hapo Dar. Kozi weka zinazoendana na tulivyoongeaga Kipindi kile"
Kuna chuo kimoja pale Dar wao kwa mwaka wanaweza wakawa na mabash hata 10. Yani hata wakiambiwa wameletewa mkuu wa chuo mpya, basi wataandaa bash. Niliona kile chuo ndio kitamfaa Ester, maana kivyovyote vijana wa pale hawawezi kumuacha salama. Niliamini atakuwa na furaha sana endapo atakuwa na mtu mwingine tofauti na Mimi. Sikujiona kama namfaa kabisa.
***** ***** ***** ***** ****** ****** *****
Akiwa jeshini, tuliendelea na mawasiliano kama kawaida. Wakati wanakaribia kuhitimu, akaniambia kuwa kabla ya kwenda kwao atapitia Dar kwangu akae siku kadhaa maana amenimiss.
Kipindi ananiambia hivyo, tayari nilikuwa ninaplan ya kwenda Bagamoyo na madam Nuru. Kama Ester anakuja, basi natakiwa kuhairisha hiyo safari. Na endapo nikihairisha basi nijiandae na msala toka kwa huyu shangazi.
Sikuwa na namna, ikabidi nimkatae tena Ester kwamba kuna kazi naifanya ambayo inanifanya niwe mbali na ghetto kwa muda mrefu sasa.
Ester: "Sasa nina zawadi zako ambazo sitaki kwenda nazo nyumbani. Inabidi nikupe, itakuwaje?"
Mimi: "Hapo sijui inakuwaje. Ni zawadi gani?"
Ester: "Wewe jua ni zawadi tu. Kuna rafiki zangu huku ni wakazi wa Dar, nitaongea nao nione kama kuna ninayeweza kumpa akuletee"
Mimi: "Okay sawa"
Siku ya wao kurudi ilipofika, akaniambia kuna mtu amempa. Hivyo akifika Dar atanipigia.
Na kweli, kuna muda namba ngeni ikanicheki. Kuongea nae nakuta ni mdada ambae ni rafiki wa Ester. Akaniambia yeye anakaa maeneo magomeni, hivyo akifika tukutane pale River side anikabidhi mzigo wangu kisha aendelee na safari yake. Tukakubaliana akikaribia anijulishe ili nianze kusogea.
Kweli alifanya hivyo. Nikasogea mdogo mdogo mpaka River side. Nafika pale, nakutana na Ester akiwa na rafiki yake.
Ester: "Mimi ndio zawadi yenyewe baby, najua umechukia ila ndio nishafika tayari"
Sio siri nilimind kuliko alivyofikiria. Ila sikuwa na namna, Nikaondoka nae mpaka maskani. Ujio wake ulifanya safari ya Bagamoyo ifie hewani, maana siku tatu mbele ndio nilikuwa natarajia kusafiri.
Niliplan siku ikifika kumuongopea Ester kuwa naondoka kikazi, lakini kumbe alipekuwa simu yangu na kuona Chatting zetu alafu akakausha. Siku moja kabla ya siku ya safari, ilikuwa mida ya usiku baada ya kumaliza kula akaniambia kwamba anajua sababu ya Mimi kukataa asije kwangu wakati anatoka jeshini. Kiufupi alinieleza vyote alivyosoma kwenye simu.
Akaniambia kama nitaondoka na kwenda na yule mwanamke, basi sitokaa nimuone tena kwenye maisha yangu. Maana Ile nidharau ya kiwango cha juu sana, kumuacha yeye ndani na kwenda kwa mwanamke mwingine.
Japo sikuwa na mipango yoyote ya future na Ester, ila iliniwia vigumu kuondoka na kumuacha pale ghetto, hasa baada ya kuwa ameshaujua ukweli. Kiufupi hii ilikuwa ni nafasi nzuri ya Mimi kuvunja mahusiano yetu, maana kama ningeondoka ni wazi pasingebaki chochote kati yetu. Ila sijui kwanini, nikajikuta moyo wangu unakuwa mzito.
Nikamuomba msamaha na kuahidi siondoki tena, nitabaki na yeye. Akachukua simu yangu na kumblock Madam Nuru. Hakujua kama ameblock mtaji wangu.
Kati ya mashangazi yote ambayo nishawahi kuwa nayo, hakuna aliyenifanya nikala bata kama huyu Madam. Sometime akiwa na ziara za kiofisi, alikuwa ananitanguliza Mimi huko anakoenda. Hakuwa mgumu kwenye kutoa hela. Kitendo cha Ester kuamua kumblock, ni sawa na kumblock boss wangu. Nikajua pale kibarua kimeshaota nyasi, ila sikuwa na namna.
Maana kama nisingekubali ablockiwe, Ester alikuwa tayari kuondoka usiku ule ule. Hakuwa mwenyeji Dar, hakuwa na ndugu wa karibu pia. Sikuwa na uhakika angeenda wapi.
Ila ningejua timbwili ambalo lingefatia, basi ningefikiria mara mbili kuhusu kumblock Madam Nuru.
Some next portion hapa: Life style yangu ilinipotezea mwanamke mzuri
Tyr naona umeenda kuvurunda tena.Portion 16:
...... Safari haikuboa. Mpaka tunafika, Mimi na yule Mzee aliyekuwa pembeni yangu tulikuwa tunapiga story kana kwamba tulifahamiana siku nyingi. Nilikuja kufahamu jina lake, anaitwa Mr. B. Alikuwa ni mtu mwenye ufahamu na mambo mengi sana. Japo taaluma yake ilikuwa ni tofauti kabisa na ya kwangu, ila wote tulifanya kazi kwenye taasisi zilizopo chini ya wizara moja. Mtu wa kariba yake ni kama dhahabu endapo ukiwa karibu yake. Nadhani ndio maana hata Mzee wa Kongowe alitaka niwe nae karibu.
Mr. B alikuwa nimpenda kusoma vitabu, na hicho ndio kilisaidia Mimi na yeye kuelewana. Katika vitabu vyote ambavyo nimeshasoma, kila nilichomtajia, alikuwa nae ameshakisoma. Alifurahishwa na tabia yangu ya kupenda kusoma vitabu. Akaniandikia list ya vitabu 10 ambavyo alisema angependa niwe nimevisoma ndani ya mwaka mmoja. Na tokea siku ile, amekuwa na utaratibu wa kunipa list ya vitabu vya kusoma kila tunapouanza mwaka. Tokea nimefahamiana nae, nimejikuta nasoma vitabu vingi sana tofauti na kipindi cha nyuma.
Kwa kiasi kikubwa amenisaidia sana kuibadilisha akili yangu.
Siku moja tukiwa short break wakati wa training, ulikuwa muda wa chakula. Kuna picha moja nilimpiga Mr. B wakati anakula. Ilikuwa ni picha nzuri, hivyo akahitaji nimtumie.
Baada ya kuipata picha, akaamua kusave namba yangu. Whatsap wanamtindo ukitaka kusave namba ya mtu, basi sehemu ya kuandika jina wataweka jina ambalo huyo mtu ndio ameliweka Whatsapp. Mimi Kwa upande wangu niliandika "Amphibian" hivyo Mr. B alivyokuwa anasave namba yangu, likakaa ilo jina.
Mr. B: "Amphibian? Seriously?"
Nilijisikia noma sana, sikuwahi zingatia ile sehemu na sikuona kama ni kitu kikubwa. Ila Kwa mtu wa heshima kama yule, niliona kama ameniona miyeyusho.
Ila na yeye kwenye kuisave namba yangu, akaamua kuisave hivyo hivyo Amphibian. Na ndio jina ambalo amekuwa akiniita tokea siku hiyo. Mpaka kuna muda huwa nahisi akitajiwa jina langu halisi anaweza asinitambue kwa haraka.
Training ilikuwa ni ya siku 30 kisha tukarudi nchini na kutawanyika, maana tulienda watu wa taaluma tofauti tofauti, japo karibia wote tulikuwa chini ya wizara moja.
Ile siku ambayo ndio tulirudi, mida ya usiku Mzee wa Kongowe akanipigia simu:
Mzee: "Vipi mambo yameendaje huko?"
Mimi: "Vizuri tu, hata Mr. B tunaelewana vizuri sasa hivi"
Mzee: "Nimefarijika kuona unaenda vizuri nae"
Analyse: "Ndio Mzee, tunaelewana kwa kiasi fulani"
Mzee: "Ukielewana nae vizuri, ni mtu mzuri sana huyu. Anaweza kukusaidia pakubwa"
Analyse: "Nitajitahidi kuendana nae"
Mzee: "Unajua kwenye maisha kila kitu huwa kina zeeka. Kitu pekee ambacho hakizeeki ni connection na watu. Na hicho ndio kila mtu anapambania. Kwa Mr. B upo sehemu sahihi. Anaweza kukusaidia zile sehemu zote ambazo Mimi sikuweza".
Analyse: "Mzee ni mkarimu na muelewa sana, nina imani nitaenda nae vizuri"
Mzee: "Pamoja na kumuona muelewa, ila hanaga uvumilivu kwenye mambo mawili, mali zake na binti yake wa mwisho. Kuwa mwangalifu na hivyo vitu"
Analyse: "Ilo lisikupe shaka Mzee"
Mzee: "Unajua sisi ambao familia zetu sio popular kwenye siasa, tunatumia nguvu kubwa ili kuweza kukaa level za juu. Na ndio maana tukistaafu ni rahisi kusahaulika. Kesho yako inategemea na mambo utakayofanya leo, jitahidi kila nafasi unayoipata unaitumia vizuri, huwezi jua siku moja itakuweka kwenye level gani"
Analyse: "Nitajitahidi sana kwenye ilo Mzee"
Mzee: "Nakukumbusha tena huyo sio ndugu yako, hivyo jitahidi kumfanya awe karibu nawe. Jitahidi usivuke mipaka"
Baada ya hapo tukaagana, akakata simu.
***** ***** ***** ******
Tokea niondoke Dar kwa kiasi fulani nimekuwa na amani, japo imekuwa ngumu kuzoea life la huku nilipo. Ofisi anayofanyia kazi Mr. B ipo mkoa huu huu niliopo hivyo imekuwa rahisi sana Mimi na yeye kuinteract. Amekuwa ni mtu wa kunishauri na kunipa facts za hapa na pale ambazo zimekuwa msaada kwangu.
Kwa muda mrefu nimekuwa nikijaribu kubadilisha vitu kwenye maisha yangu , ila nimekuwa nafeli mara zote. Hii inatokana na kwamba nilikuwa najaribu kubadilisha kila kitu, ila nasahau kubadilisha fikra zangu. Tokea nimefahamiana na Mr. B, nimekuwa napigania sana kubadili fikra zangu, na Kwa kiasi fulani nauona mwanga.
Siku zote amekuwa akijaribu kunipa mwongozo kwenye vitu kadha wa kadha. Kawaida huwa nikishatoka kazini kuna sehemu napendaga kwenda kukimbia kimbia na kucheza mpira kidogo. Jioni moja nikiwa natoka mazoezini, nikakuta missed calls za Mr. B, ikabidi nimpigie:
Mr. B: "Amphibian hujambo?"
Analyse: "Sijambo Mzee. Shikamoo"
Mr. B: "Marahaba. Mbona hupokei simu zangu?"
Analyse: "Nilikuwa mazoezini kidogo Mzee, hivyo simu sikuwa nayo"
Mr. B: "Mazoezi gani ya muda huu, mbona unaleta ujanja ujanja kijana?"
Analyse: "Muda huu ndio narudi, ila nilienda mapema tu"
Mr. B: "Wik end ratiba yako ipoje?"
Analyse: "Usafi tu mida ya asubuhi, na jioni ndio kama hivi nakuja kupunguza mafuta ambayo sina"
Mzee akacheka:
Mr. B: "Basi kama utaweza, ukitoka kwenye hayo mazoezi yako, uje nyumbani kwangu"
Analyse: "Siku gani haswa ambayo utahitaji nije?"
Mr. B: "Jumapili itakuwa vizuri zaidi"
Analyse: "Sawa Mzee"
Baada ya kukata simu, nikabaki najiuliza "Huyu Mzee ananiitia nini?". Sikupata jibu, na sikuona haja ya kuendelea kujiuliza maswali mengi wakati nikienda nitajua.
Hiyo siku tuliyokuwa tunaongea ilikuwa ni alhamisi. Ilipofika jumapili, mida ya saa moja nikawa njiani kuelekea kwake. Nilikaribishwa vizuri, nikakuta msosi umeshaandaliwa nikajumuika nao mezani. Nikiangalia mezani, naona mboga ni nyingi kuliko vyakula vingine. Kibaya zaidi nikaambiwa Mimi ndio nianze kupakua. Nikapakua aste aste, lakini nilivyoanza kula nashangaa wali umeisha, nimebaki na mboga tu kwenye sahani. Nilikuwa naona aibua wakati hakuna hata aliyekuwa na muda na Mimi.
Baada ya kula, tukawa tunapiga story na Mr. B pale sebuleni:
Mr. B: "Vipi mambo yako yanaendaje sasa hivi?"
Analyse: "Mungu ni mwema Mzee, yanaenda"
Mr. B: "Nafurahia sana kuona jinsi ulivyosharp. Usipoteteleka, utafika mbali sana"
Analyse: "Mungu anisimamie"
Mr. B: "Hivi ukiachana na hii kazi yako, unajishughurisha na kitu gani kingine?"
Nikataka nimwambie namiliki bodaboda kuna mtu nimempa mkataba, ila nikasita. Maana Mshua wangu mwenyewe nilivyomwambiaga nimenunua bodaboda, aliniambia nitafute kitu kingine maana hiyo sio biashara, muda wowote naweza kupigiwa simu niambiwe chombo kipo chini ya fuso, mtaji na faida vinapotea ndani ya sekunde chache. Hivyo kama Mshua alinikataa, huyu Mzee itakuwaje?
Analyse: "Sina chochote zaidi ya kazi yangu Mzee"
Mr. B: "Seriously?. Una nguvu, una muda, inakuwaje unakubali vyote vipotee hivyo?"
Analyse: "Kitu cha kufanya ndio sikioni"
Mr. B: "Mbona vya kufanya vipo vingi sana?. Anzisha hata kampuni, kuna watu wanakampuni za (....) au (....) mambo yao yanaenda vizuri tu. Commitment na dedication ndio kila kitu"
Analyse: "Ni kweli unachosema, ila mtaji wa kuanzisha hiyo kampuni ndio ugumu ulipo"
Mr. B: "Ugumu? Kwani kampuni ni nini mpaka iwe ngumu kuanzisha?"
Nikamulezea uelewa wangu juu ya kampuni. Akacheka:
Mr. B: "Kuna tofauti kati ya kampuni na ofisi Amphibian. Hapo wewe umeelezea ofisi za kampuni, na sio kampuni yenyewe. Kuna watu wanamiliki kampuni na hawana hata physical office, wana laptop na briefcase tu na mambo yao yanaenda. Acha kuniangusha kijana"
Analyse: "Sikuwahi fikiria hivyo, nitajaribu kuyafanyia kazi mawazo yako"
Mr. B: "Unajua kwa umri ulionao sasa hivi, hiki ndio kipindi cha kujaribu sana uwekezaji. Kuna wakati utafika hela yako itakuwa inaisha kabla hata haijakufikia mkononi. Ukishafika kipindi hicho kama hujawekeza popote, basi sahau kabisa kuhusu uwekezaji wowote wa maana"
Analyse: "Ni kweli Mzee"
Mr. B: "Kwa sisi Watanzania, mpaka kufika hapa tulipo tunakuwa tumepitia kwenye mikono ya watu wengi. Hivyo na sisi tunamadeni ya watu wengi hata kama hawatokuja kutudai. Hivyo ukiona kipato chako kinakutosha wewe tu, basi jua haupo salama. Maana pia kuna dharura ambazo zikija, zinahitaji uwe na uwezo wa kuhudumia hata familia kumi ndio huweze kuzitatua".
Akakaa kimya kidogo, kisha akaniuliza:
"Hivi unawekaga akiba?"
Analyse: "Mara chache chache"
Mr. B: "Ukiwa mwanaume kati ya vitu unavyotakiwa kuviogopa sana, ni kutokuwa na akiba. Otherwise, you're not safe"
Nikabaki kimya kwa muda, maana kulikuwa na uzito mkubwa kwenye vitu alivyoongea. Nilihitaji kufanya maamuzi kutoka kwenye jambo aliloniambia. Nilikaa kimya kwa muda mrefu mpaka pale aliponishtua:
Mr. B: "Naona akili yako ipo mbali sana kwasasa. Take your time, plan kitu kizuri. Alafu nisije nikawa nimekubana hapa, ukitaka kwenda kupumzika niambie tu. Maana najua kesho unahitajika kazini mapema"
Analyse: "Sikuwa nimeangalia saa kabisa, kumbe muda ndio umeenda hivi. Basi acha niwakimbie Mzee"
Mr. B: "Uwe unakuja tunapiga story kama hivi, hapo ni nyumbani pia"
Analyse: "Sawa Mzee, nitajitahidi niwe nakuja. Maana ninavingi sana vya kuchukua toka kwako"
Mr. B: "Anytime Amphibian"
Analyse: "Basi utaniagia kwa Mama ndani"
Mr. B: "Huyo atakuwa ameshaenda kulala, nitakuagia usijali"
Tukatoka nje, akawa ananisindikiza. Wakati tunataka kutoka getini, kuna mdada amevaa tight, raba na vesta akawa ameingia:
Mr. B: "Amphibian, huyu ni Binti yangu anaitwa Katrina, sidhani kama ushawahi kumuona"
Analyse: "Hapana, ndio mara ya kwanza hii"
Mr. B: "Huyu bwana ndio last born wangu, tena na yeye ni mpenda mazoezi kama wewe, hapo alipo anatoka evening walk"
Tukasalimiana na Katrina. Manzi mwenyewe ni ananata kuliko hata gundi, yani super glue ikasome. Maana tulisalimiana lakini alikuwa kama vile hana time na mimi. Kwa muda mchache niliomuona, ni kama aliishika akili yangu. Lakini kwa ule unataji wake, nikayafuta akilini mawazo yoyote juu yake maana sikuwa tayari kurudia makosa yaliyonifanya niondoke Jiji la Chalamila.
Lakini kumbe haikuwa rahisi kama nilivyodhani. Sijui ni Mimi ndio niliingia kwenye kumi na nane zake, au ni yeye ndio aliingia kwenye zangu, maana nilijikuta kwenye mazingira ambayo sikupenda kabisa niingie. Katrina alikuja kuwa kikwazo kwangu. Na hii ni baada ya kushindwa kufuata ushauri wa Mzee wa Kongowe kuhusiana na vitu vya Mr. B ambavyo ni untouchable.
Niliteleza padogo sana.....