Limekaaje suala la madalali kulipwa kodi ya mwezi mmoja?

Limekaaje suala la madalali kulipwa kodi ya mwezi mmoja?

Sio kila mchangiaji kwenye uzi fulani basi anakua anakubaliana, najua ugumu wakutafuta nyumba bila dalali, mimi kipindi natafuta nyumba huwa natembea nao tunawekeana malengo anipitishe kwenye nyumba kama tano kwa siku na nachagua ni eneo gani na siku ya mwisho namtoa hela vocha elfu 5,ndani ya week lazima upate nyumba then kwenye kulipana inategemeana sasa na nyumba inapngishwa kiasi gani yani hili swala ni maongezi tu sio lazama mfuate kanuni,
Mimi...wakati naishi DSM...nikitafuta nyumba na dalali Nampa hela Yake bika hiyana...

Au nampa nusu nusu kila nikipata mshahara ndani ya miezi miwili namaliza deni
 
Habari za muda huu wakuu? Heri ya mwaka mpya pia.

Leo nimekuja kuuliza na kutafuta majibu ya juu ya suala la madalali wa nyumba kulipwa kodi ya nyumba ya mwezi.

Hili suala limekaaje hii ni baada ya kuona mijadala kadha wa kadha kupitia mitandao ya kijamii tofauti.

Je, kwanini kodi ya mwezi?

Inasimamia kitu gani?

Wataalamu wa computer fursa hiyo, changamkieni fursa hiyo.

Njooni ni kitu kama Airbnb app, ambayo itwakutanisha wenye nyumba na watafuta nyumba kisha ninyi mtafaidika na waweka matangazo ya biashara.

Changamkieni fursa tuwaondoe hawa wapuuzi kama ilivyo kwa mabasi.
 
Mimi...wakati naishi DSM...nikitafuta nyumba na dalali Nampa hela Yake bika hiyana...

Au nampa nusu nusu kila nikipata mshahara ndani ya miezi miwili namaliza deni

Ni mpangilio tu cha msingi apate chochote kitu,
 
Ni matapeli tu hawa wanaohusika sana katika kuongeza gharama za kupanga nyumba/chumba. Hawataki kufanya kazi za maana bali kusubiri mteremko.,
- Na wenye nyumba wanavyopendana na madali sasa.

- Kuna nyumba ukienda hupewi chumba/nyumba mpaka uje na dalali.

- Mwenye nyumba unakuta kashaset anapangisha chumba 70000 dalali anakuja anamwambia mzee usitoe chumba hichi nakuletea kichwa cha laki moja, mwenye nyumba hapo ni full shangwe na kumwona dalali ndio mtu.
 
Nashukuru Mungu nimepata kibanda changu na nimehamia sa hivi mambo ya Madalali wa nyumba nitayasikia kwenye Bomba tu.
Kupata kibanda chako siyo sababu ya kutoona tatizo linalowakabali wale wasio na nyumba. Nadhani hata serikali haifuatilii hili tatizo kwa sababu viongozi wengi hawakumbani na hili tatizo.
 
Dalali anakwambia ana nyumba ukimfuata anakwambia tumpitie mwenzangu,mkifika huko nako mnaambiwa mkampitie mwingine....nyumba ina msururu wa madalali wanne! Hapo lazima wapandishe Kodi ili ile hela ya mwezi iwakimu wote wanne.
Kimsingi udalali wa kwenye kupangisha nyumba siyo mbaya ila Bongo unafanyika kienyeji na kitapeli sana sana. Tatizo ni serikali hasa serikali za mitaa. Wangeweza kuweka mfumo maalum kwa kukutanisha wenye nyumba na wapangaji kwa njia rahisi, inayoeleweka na ya kistaarabu na kwa ada nzuri.
 
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Yes unakuta dalali huyu uliekutana nae hana nyumba, ila mwenzake anayo so anakuunganisha nae,m kwahiyo chain ni lazima ikuumize, upo sahihi wengi wanaumizwa kwa mtindo huo
Unakuta mpaka kiatu kimeisha upande lakini kwenye nyumba za watu utazani yeye ndiye mwenye nyumba, bei anapandisha yeye wezi wakubwa wale watu
 
- Na wenye nyumba wanavyopendana na madali sasa.

- Kuna nyumba ukienda hupewi chumba/nyumba mpaka uje na dalali.

- Mwenye nyumba unakuta kashaset anapangisha chumba 70000 dalali anakuja anamwambia mzee usitoe chumba hichi nakuletea kichwa cha laki moja, mwenye nyumba hapo ni full shangwe na kumwona dalali ndio mtu.
Dodoma Ndiyo Bhalaa!!
Chumba Kipo Eti Hupewi Mpaka Dalali
 
Dodoma Ndiyo Bhalaa!!
Chumba Kipo Eti Hupewi Mpaka Dalali
Siyo Dodoma ni maeneo mengi. Ndio ujue kuwa kazi yao ni muhimu maana wao ndio wanakuwa kama wadhamini wako kwa mwenye nyumba. Ukienda ukavurunda alipokupangisha dalali ndiye atapewa lawama kwanza
 
Hao jamaa siwakubali wapuuzi sana, wanataka hela kubwa kwa blah blah let say room kwa mwezi 100 eti nayeye anataka 100K ukimpa hata 50K anakomaa kama vile kuna kazi ya maana kafanya. Nishajua dawa yao
 
Unakuta mpaka kiatu kimeisha upande lakini kwenye nyumba za watu utazani yeye ndiye mwenye nyumba, bei anapandisha yeye wezi wakubwa wale watu
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Mkuu nimecheka
 
Swala linaniuma hili jamani khaaa, yaani dalali nilimpa sh 50 elfu yangu mpaka leo inaniuma jamani khaaaaa
 
Habari za muda huu wakuu? Heri ya mwaka mpya pia.

Leo nimekuja kuuliza na kutafuta majibu ya juu ya suala la madalali wa nyumba kulipwa kodi ya nyumba ya mwezi.

Hili suala limekaaje hii ni baada ya kuona mijadala kadha wa kadha kupitia mitandao ya kijamii tofauti.

Je, kwanini kodi ya mwezi?

Inasimamia kitu gani?
Kuna magroup ya facebook CHAMA CHA WAPANGAJI TZ jiunge humo unasahau dalali
 
Achana na udalali, kuna suala ya wenye nyumba kuchukua kodi kuanzia miezi mitatu, sita hadi mwaka. Wakati unakuta mshahara mtu analipwa on monthly basis, sasa unajiuliza kama nalipwa kwa mwezi mwezi ninapata wapi hela ya kulipa miezi sita?

Na serikali iko kimya kabisa
Kwa swala hili nadhani tulalamike pia ada za shule kulipwa kwa Mwaka au kwa terms badala ya kwa mwezi.
 
Madalali Wana umuhimu mkubwa pia katika haya maisha! Wanasaidia na kurahisisha maisha Sana tu ila tatizo ni hiyo Kodi ya mwezi mmoja Basi!!! Kwani lazma iwe Kodi ya mwezi?
 
Ni upuuzi mtupu ambao katika Nchi nyingine haufanyiki wa kumpotezea mpangaji muda na kumuongezea gharama. Nchi nyingine nyumba zinatangazwa kwenye magazeti au online na kodi, location ya nyumba na phone number ya mwenye nyumba huwekwa hadharani.
Wewe ni nani hadi uropoke kwamba hili halinihusu? 😳😳😳
Acha ujinga wako wa kuwaamulia watu nini kinawahusu au hakiwahusu
Jombaa yaonekana una Hasira balaa.

Chukua Kidonge cha utulivu;
Kwanza, hii ni Tanzania sio ze-ugaibuniz😅
Pili, mimi ni dalalitz, ninayo mamlaka ya kukuambia kuwa yapo yakukuhusu na yapo yasiyokuhusu pia kwa muktadha wa iwapo umemtafuta Dalali, -Sawasawa?

Tatu: Wazazi wangu walikuwa wastaarabu sana,Hawakunifunza kutusi watu.
Lakini haya Maisha sheeeeenzy sana,
Yamenikutanisha na Mahayawani mithili yako, yanayonilazimisha nitoe matusi.
FYI ninao ufaulu mzuri tu katika matusi sasa wewe jichanganye Nyau wewe.
 
Back
Top Bottom