Lindi hadi Mbeya kwa barabara kuna umbali gani?

Lindi hadi Mbeya kwa barabara kuna umbali gani?

Naomba kuuliza kwa mwenye kujua. Ukitoka Lindi Hadi Mbeya Kwa barabara. Umbali ukoje kulinganisha na Dar Hadi Mbeya.

Hali ya barabara pia ikoje?
Niliwahi pita hiyo ruti ni mkeka na hakuna gari nyingi zaidi unakutana lori za Dangote hakikisha mafuta unajaza ya kutosha hakuna vituo vingi vya mafuta
 
Hiyo njia ya kusini si ya makorongo matupu?
Ni barabara poa tu na ni salama kuliko Dar-Mbeya.

Haina pot holes nyingi zipo za kawaida tena chache.

Ila ni ndefu sana ni kama km 1100 hivi.
 
Sijapita ila sina imani na barabara za kusini. Maana nilienda Lindi kuna sehemu nyingi sana kuna vipande vya maintenance.

Ila naamini kwakua ni barabara kuu inaweza kua mkeka mwanzo mwenga.
Ni mkeka safi tu kuliko barabara nyingi za nchi hii.
 
Ni barabara poa tu na ni salama kuliko Dar-Mbeya.

Haina pot holes nyingi zipo za kawaida tena chache.

Ila ni ndefu sana ni kama km 1100 hivi.
pia usisahau kipande cha kutoka songea to njombe kina kona kali na miinuko/mabonde ya kutosha sana inabidi awe na utulivu katika uendeshaji.
 
Hivi we ni wa nchi hii kweli? We kusini unakuchukuliaje, kwanini unafikiri barabara ya kusini iwe ya makorongo kwa hiyo kwa hiyo akili yako ndogo. Hiyo lami huko ulipo ilijengwa na wananchi? Acheni upumbavu kusini ni Tanzania serikali inapeleka maendeleo maeneo yote.. Kwanza ujue barabara ya kwanza ya lami ilijengwa kusini, yaani Trunk Road number one, T001 imeanzia Dar mpaka Tunduma. Barabara ya lami kutoka Makambako kupitia Njome mpaka Songea iljengwa enzi za Nyerere kabla hata lami haijafika hata Dodoma (T006). sasa hivi kuna lami tena nzuri ya kisasa. Kutoka Lindi-Masasi-Mtwara tangia kipindi cha Mkapa. Lindi-Masasi-Tunduru-Songea iko muda mrefu. Songea-Njombe-Makambako-Mbeya tangia kipindi cha baba wa Taifa.Kuna lami kutoka Songea-Mbinga-Mbamba Bay(ziwa Nyasa). Njombe-Makete

Huwezi amini kusini hata stand zao za wilaya ni za kisasa hazipo hata huko kwenu, kwa mfano wilaya ya Nanyumbu iliyoko mkoa wa Mtwara ina stand ya Kisasa eneo linaitwa Mangaka. Stand ya wilaya ya Tunduru ni ya kisasa ni wilaya chache sana ktk nchi hii inazo. Lami imefika mpaka wilaya ya Newala ambayo iko mkoa wa Mtwara, lami imefika Ruangwa ambayo iko mkoa wa Lindi.
Nyie endeleeni tu kukenua meno kama Ngedere na ujinga wenu wa kutojua nchi yenu. Katembee uijue nchi siyo unakaa nyuma ya keyboard unaandika kwa hisia tena kuwawazia wenzako mambo mabaya. Kusini mbona kuchele. Sema watu wa kusini wastaarabu sana hawana tabia za kujisifu km watu wa kanda za kaskazini(hasa wachaga) na kanda ya ziwa (hasa wasukuma). Watu wengine kweli mna upungufu wa akili, anayejenga barabara ni serikali halafu mtu anakuja hapa eti kwetu kuna lami, kuna sehemu nchi hii wanakijiji wameshawahi kuchangia kujenga lami? Serikali yetu inajenga miundo mbinu kwa uwiano mzuri.
Kusini gani hiyo unayoisifia hivi?

Sent from my SM-G950F using JamiiForums mobile app
 
Unataka kusema kama unaendesha tanker ni hatari hiko kipande??
hatari kwa kweli ila ukiwa makini unatoboa vizuri tu na kingine jiandae kukutana na new force maana madereva wake wengi wako rough sana njia hiyo.
 
Mwezi wa pili nataka kwenda songea. Ila lazima nipite mbeya kwa issu fulani ninatoka mwanza. Ni route ipi kwa gari kufika mbeya kutoka mwanza, gharama zake kutoka mwanza to mbeya na mbeya to songea.
 
Mwezi wa pili nataka kwenda songea. Ila lazima nipite mbeya kwa issu fulani ninatoka mwanza. Ni route ipi kwa gari kufika mbeya kutoka mwanza, gharama zake kutoka mwanza to mbeya na mbeya to songea.
Utapita via dodoma then iringa unaipata mbeya gharama sijajua ingia kwenye website za mabasi
 
Back
Top Bottom