Ahead
JF-Expert Member
- Jan 11, 2013
- 2,292
- 2,566
Ndugu acha kumfananisha Lissu na lowassa huyu bwana ni mpinzani kweli,tena haogopi mtu,hatafuni maneno ni mkweli ni mwadilifu tofauti na lowassa aliyekuwa mwoga na mwenye doa kubwa la ufisadi,hoja tu ya ufisadi ilikuwa pigo kwa upinzani lakini watu kwa kuichoka ccm walimpa kura zaidi ya mil 6.Mrema mwenyewe alikuwa nayo kuliko hata lowasa
Ndugu huu mwaka ni tofauti lisu anauzika lisu anajiamini, ccm imechokwa na wakulima mf wa korosho,vijana hasa wahitimu vyuo, watumishi wa umma walionyanyasika miaka 5 bilakuongezwa mishahara na kudharirishwa ovyo, wafanyabiashara mpaka wengine wamejinyonga mf yule wa viroba Dodoma, ndugu ccm ijipange uchaguzi huu sio kama miaka mingine watu wanajitambua mtampinga lissu kwa hoja gani mtu makini na mwadilifu na pia yeye ni alama ya uonevu kwa kupigwa risasi za kutosha.
Pia tofauti na lowassa, lissu anakwambia hakuna kuibiwa kura.Ushauri wangu kwa chadema mwaka huu nendeni vijijini mjini tunajielewa tutawapa kura tu nendeni vijijini hata kwenye makao makuu ya kata mkaongezee tu kura ili waibe mpaka washindwe msijifurahishe na mafuriko ya mjini au gaweni timu vizuri,wengine wajikite mjini wengine vijijini.N.b mimi sina chama ila kura yangu kwa upinzani wa kweli.
Sent using Jamii Forums mobile app