Lissu anakuwa na nguvu pale panapokuwa na Siasa za mapambano (confrontational politics), zilikuwepo enzi ya Magufuli, Sasa hazipo, kapoteza relevancy

Lissu anakuwa na nguvu pale panapokuwa na Siasa za mapambano (confrontational politics), zilikuwepo enzi ya Magufuli, Sasa hazipo, kapoteza relevancy

Lissu ni mwanasiasa anaye shine/anayeng'aa pale panapokuwa na Siasa za mapambano, Siasa hizo zilikuwepo enzi ya jiwe, yule Mzee wa Chato.

Kwa Sasa ni SSH, hana Siasa hizo za piga nikupige. Ndio maana baada ya ujio wa Lissu, ndani ya muda mfupi "amechuja" na umaarufu wake umechuja kwa asilimia 80.

Aina hii ya Siasa aliwahi kuijadili Mbowe akiwa nje ya nchi, Mbowe alisema anawafahamu watanzania kwa muda mrefu, kwamba Siasa zao ni tofauti na Siasa za Kenya, Kenya Wana Siasa za mapambano, kuandamana, mikutano, hawaogopi. Nadhani Lissu anahitaji kuisoma upya jamii ya watanzania na kucheza ndani ya engo ya saikolojia ya watanzania.

Mbowe alikamatwa ndani ya vuguvugu la katiba mpya, hakuna Cha Mnyika, Heche, Wala nani aliyeandamana. Watu wako bize na mambo yao.

Mbowe alikuwa sahihi alipofanya mabadiliko ya mbinu kwa kuingia katika mjadala na Serikali.

Na ndio watanzania tulivyo, tangu ukoloni, Nyerere alitusoma akajua hawa ni watu wa kwenda nao taratibu, na ni wazi aliona hakuna wa kuandamana Wala kuingia katika vita kupigania Uhuru, kama ilivyokuwa kwa MAU MAU Kenya, Nyerere Kaa mezani, Uhuru ukaja.

Pia Lissu kama kiongozi awe anaangalia muda gani anaongea angalau watu wammisi, watu wamemsikiliza Twitter mpaka wakachoka, kiongozi angalia timing ya kuongea, kaa kimya, ulisema unaongea watu wanashtuka, au kuwa na hamu. Sasa akina maria sarungi wakishavuta Hela za mabeberu, kujustify retirement, wanakimbia kwa Lissu, Lissu anaongea masaa kadhaa, anachuja.

Nadhani Kila nchi Ina set up ya kisaikolojia ambayo wanasiasa wanatakiwa kuisoma na kuifanyia uchambuzi, na pengine hata Kila Jimbo, Tarime na Mkunazini Zanzibar haziwezi kuwa sawa.

Wasalaam.
Tulisema awali, Lissu kitabia ni pacha wa Jiwe.
 
Chadema wamepiga kelele kwenye mikutano yao, kumbe kuna mwenzao ana buyu la asali anasubiri muda ufike aende Ubelgiji
 
..baada ya Lissu kupiga kelele kuhusu bei kubwa za vyakula, serikali imeshtuka na kuamua kuruhusu mchele uagizwe toka nje?
Walijua Lissu anaingia mfungi Ramadhani....!
Kweli serkali sikivu.
 
Pia Lissu kama kiongozi awe anaangalia muda gani anaongea angalau watu wammisi, watu wamemsikiliza Twitter mpaka wakachoka, kiongozi angalia timing ya kuongea, kaa kimya, ulisema unaongea watu wanashtuka, au kuwa na hamu. Sasa akina maria sarungi wakishavuta Hela za mabeberu, kujustify retirement, wanakimbia kwa Lissu, Lissu anaongea masaa kadhaa, anachuja.
Ushauri mzuri, lakini bahati mbaya ni kwamba lisu hana uwezo wa kiakili (intelligence) wa kufanya hivyo. Lisu ni msema ovyo, mbwatukaji, mpayukaji, mtukanaji, nk, bila hoja. Ukichanganya na issue yake ya 'kuwa sawa kutegemeana na majira ya mwezi' ndiyo inakandawija kila kitu sasa.
 
Mpende mabadiliko vijana la sivyo mtakuwa vikongwe kabla ya wakati wenu. Kijana wa 1990s unashabikia CCM ya kina Mzee Kingunge?!
Mbadala wa CCM ni Chadema hii au Lissu huyu?
 
Mkapa aliwaambia mkitaka mabadiliko badilisheni jinsia muolewe…upo tayari kijana Fazili?
Acheni kufikiri ushoga tu fanyeni mabadiliko ya kiuongozi vijana wa siku hizi mmelegea sana.
 
Juzi nilimwambia mtu,huyu ataitwa vituo kadhaa aseme kuhusu risasi baada ya hapo kazi yake imekwisha.
 
Lissu ni mwanasiasa anaye shine/anayeng'aa pale panapokuwa na Siasa za mapambano, Siasa hizo zilikuwepo enzi ya jiwe, yule Mzee wa Chato.

Kwa Sasa ni SSH, hana Siasa hizo za piga nikupige. Ndio maana baada ya ujio wa Lissu, ndani ya muda mfupi "amechuja" na umaarufu wake umechuja kwa asilimia 80.

Aina hii ya Siasa aliwahi kuijadili Mbowe akiwa nje ya nchi, Mbowe alisema anawafahamu watanzania kwa muda mrefu, kwamba Siasa zao ni tofauti na Siasa za Kenya, Kenya Wana Siasa za mapambano, kuandamana, mikutano, hawaogopi. Nadhani Lissu anahitaji kuisoma upya jamii ya watanzania na kucheza ndani ya engo ya saikolojia ya watanzania.

Mbowe alikamatwa ndani ya vuguvugu la katiba mpya, hakuna Cha Mnyika, Heche, Wala nani aliyeandamana. Watu wako bize na mambo yao.

Mbowe alikuwa sahihi alipofanya mabadiliko ya mbinu kwa kuingia katika mjadala na Serikali.

Na ndio watanzania tulivyo, tangu ukoloni, Nyerere alitusoma akajua hawa ni watu wa kwenda nao taratibu, na ni wazi aliona hakuna wa kuandamana Wala kuingia katika vita kupigania Uhuru, kama ilivyokuwa kwa MAU MAU Kenya, Nyerere Kaa mezani, Uhuru ukaja.

Pia Lissu kama kiongozi awe anaangalia muda gani anaongea angalau watu wammisi, watu wamemsikiliza Twitter mpaka wakachoka, kiongozi angalia timing ya kuongea, kaa kimya, ulisema unaongea watu wanashtuka, au kuwa na hamu. Sasa akina maria sarungi wakishavuta Hela za mabeberu, kujustify retirement, wanakimbia kwa Lissu, Lissu anaongea masaa kadhaa, anachuja.

Nadhani Kila nchi Ina set up ya kisaikolojia ambayo wanasiasa wanatakiwa kuisoma na kuifanyia uchambuzi, na pengine hata Kila Jimbo, Tarime na Mkunazini Zanzibar haziwezi kuwa sawa.

Wasalaam.
We kimsingi huna hata faida ya kuwepo hapa duniani maana zaidi ya kupotosha huna msaada kwa binadamu wenzako. Tundu Lissu hakufanya hata mkutano moja wa kisiasa. Yaliyofanyika yalikuwa mapokezi mawili, mapokezi ya kwanza yalifanyika Dar Es Salaam kupokelewa na watanzania wenzake na baada ya pale alichofanya ni kuwasalimia watanzani. Mapokezi ya pili yalikuwa ya ndugu zake yalifanyika kwao wilaya ya Itungi mkoa wa Singida. Tuambie ni lini na wapi alifanya mkutano au shughuli nyingine yoyte ya kisiasa. Hichi ulichokiandika hata mwenyekiti wa CCM anakishangaa achilia mbali watanzania wenzako afterall km we ni mtanzania maana huku kwenye mitandao huwezi jua aliyepost km kweli ni raia wa nchi hii au mzushi fulani tu kutoka nchi jirani.
 
Acheni kufikiri ushoga tu fanyeni mabadiliko ya kiuongozi vijana wa siku hizi mmelegea sana.
Uongozi unaanzia kwenye ngazi ya familia, kama vipi mama awe kichwa cha familia ubaki home kulea watoto kijana, vipi hapo Marioo? Siasa hazikuletei TV, Gari wala mahitaji nyumbani, ni Hussle zako kijana. Jichanganye achana na kina Samia, wao wanafanya yao pia.
 
Back
Top Bottom