Uchaguzi 2020 Lissu anaongelea tu Serikali za Majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji zitatoka wapi

Uchaguzi 2020 Lissu anaongelea tu Serikali za Majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji zitatoka wapi

Nigeria inabebwa na wingi wa watu wa ndani na wa nje, lakini utaifa wake upo hoi, sababu ni hiyo ya kujitambulisha kimajimbo.

Nchi nyingi zenye sera hii zinakuwa na vuguvugu jingi sana la ubaguzi wa ndani haswa masuala ya ukabila.
US, UK, German, Kenya, South Africa, Nigeria zina majimbo tunazizidi nini.
 
Hivi mnadhani kwa kuwa chama tawala nyie mna hatimiliki ya akili za Watanzania? Kwamba sisi hatuelewi tunachoambiwa kuhusu majimbo yanayosemwa na kwamba tutapelekwa tu halutakuwa na vikao vya kuamua namna gani hayo majimbo yaendeshwe? Faida mojawapo ya majimbo tumeelezwa ni kuongozwa na Magavana wa kuchaguliwa, sasa hivi Wakuu wa mikoa na wilaya hawana tofauti na viongozi wa Kikoloni (Area commissioners) waliokuwa wanqogopwa kwa kukamata wananchi na kuwaweka ndani hata kwa makosa yasiyotajwa kwenye sheria.

Mmemsilkia Magufuli mwenyewe akisema wazi hata vitambulisho vya Machinga watu hawakupaswa kulazimishwa, lakini uliza mikoani Wakuu wa Wilaya ambao ni wateule wa Rais na Makada wa CCM wamewatendea nini Wananchi?

Ni watumishi wangapi wamekamatwa kwa amri ya maDc kwa kosa la kuchelewa kikao cha mkubwa, huku sheria ikimtaka DC kukamata na kuweka ndani masaa 24 kwa makosa ya jinai na uvunjifu wa amani pekee na si makosa ya Nidhamu? Tumechoshwa na umyanyasaji wa "Wakoloni" wenu weusi.
Suluhisho la hasira zako haliwezi kuwa sera ya majimbo ya kukopi na kupesti kutoka nchi nyingine.

Nchi huwa haifanyiwi majaribio kwa sera zisizokuwa na msingi wa asili, watu wataumia.
 
Uwezo wako ni mdogo sana kuelewa. Hilo suala la gharama limeelezwa vizuri sana humu jf na sina sababu ya kulirudia. Ni kupoteza muda. Soma Uzi za wenzako kabla ya kukurupuka kuandika yako.
 
Kweli wewe ni kilambimkwidu.

Alokuambia singida Wanategemea alizeti tu ni nani?
Au ndo ushabiki mkuu
 
Upinzani wetu ni ule wa kutoka bungeni wakati wa mijadala muhimu ya kitaifa.

Ni upinzani mzigo kwa walipa kodi.

Mfano jimbo la kawe lina hazina ya rasilimali watu ya kutosha lakini mbunge wetu Halima kwa miaka kumi hata mara moja hajawahi kuonekana bunju A wala B yeye muda wote ni kuzozana na watu Twitter.

Hajawahi kushughulika na shida za Kawe, na huo ni mfano mmoja tu.
Hujajibu swali langu!!

Nimesema kama sera ya majimbo ni ya kichoyo na kibaguzi Sasa kwa nini na Sera yetu ya sasa ya mikoa Magufuli amesema mchana kweupe hawezi peleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani?

Alisema jimboni kwa Bwege kabla hata ya kampeni na amesema maeneo mengi akiwa kwenye kampeni?

Huu ubaguzi na uchoyo nayo ni sera ya majimbo?
 
Suluhisho la hasira zako haliwezi kuwa sera ya majimbo ya kukopi na kupesti kutoka nchi nyingine.

Nchi huwa haifanyiwi majaribio kwa sera zisizokuwa na msingi wa asili, watu wataumia.
Unanilazimisha niendelee kuamini uwezo wako wa kufikiri ulivyo wa chini siku zote. Nimekupa mfano mmoja tu wa ubovu wa madc wa sasa na jinsi wanacyoumiza wananchi. Na nikuongeze la pili, Tanzania hakuna mkoa unaokaliwa na Kabila moja pekee, Tabora kuna Wanyamwezi, Waha, Wanyakyusa, Wangoni, Wakara, Wahaya nk! Ukabila utatoka wapi kwenye mkoa kama huo?
 
Hujajibu swali langu!!

Nimesema kama sera ya majimbo ni ya kichoyo na kibaguzi Sasa kwa nini na Sera yetu ya sasa ya mikoa Magufuli amesema mchana kweupe hawezi peleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani???
Alisema jimboni kwa Bwege kabla hata ya kampeni na amesema maeneo mengi akiwa kwenye kampeni????

Huu ubaguzi na uchoyo nayo ni sera ya majimbo???
Nimekujibu kwa kukwambia kuwa upinzani umejikita kupinga kila kitu hata mambo ambayo ni progressive.

Upinzani unafanya siasa hata katika masuala yasiyohitaji siasa.

Huko kwa bwege kiusalama kuna masuala mabaya sana yalifanyika na yakataka kuivunja kabisa Tanzania, siwezi kuyaandika humu jukwaani.
 
Upinzani wetu ni ule wa kutoka bungeni wakati wa mijadala muhimu ya kitaifa.

Ni upinzani mzigo kwa walipa kodi.

Mfano jimbo la kawe lina hazina ya rasilimali watu ya kutosha lakini mbunge wetu Halima kwa miaka kumi hata mara moja hajawahi kuonekana bunju A wala B yeye muda wote ni kuzozana na watu Twitter.

Hajawahi kushughulika na shida za Kawe, na huo ni mfano mmoja tu.
Mwambie Gwajima atakuja kuwatembelea ila tambua matatizo ya bunju a na b yapo na Marais ni wa ccm Toka Uhuru unamlahum mdehe unachekesha kweli.
 
Nigeria inabebwa na wingi wa watu wa ndani na wa nje, lakini utaifa wake upo hoi, sababu ni hiyo ya kujitambulisha kimajimbo.

Nchi nyingi zenye sera hii zinakuwa na vuguvugu jingi sana la ubaguzi wa ndani haswa masuala ya ukabila.
Unapo sema utaifa wa nigeria upo hoi unamaanisha nini ? Nimeishi nigeria 2002 hadi 2011 sijaona hicho unacho kisema wewe kabisa au ni stori za vijiweni?
 
Sera ya majimbo msingi wake ni ubinafsi, ukabila na roho ya uchoyo.

Ni sera ambayo imechukuliwa kutoka nje pasipo kuangalia msingi wa utaifa wetu.

Msingi wa utaifa wa Marekani ni tofauti na ule wa Russia ni tofauti na ule wa Zambia ni tofauti na ule ww Afrika ya Kusini.

Ni sera ambayo ukiitazama kwa juu juu unaweza kudanganyika.
Hapana, hujaielewa. Hata mimi bado naitafakari kama inafaa, lakini nimejibidisha kuielewa.
Maana yake halisi ni kuwa watu wenyewe kwenye maeneo yao, yawe mikoa au wilaya, ndio wawe wanachagua au kuwateua viongozi wao, kama wakuu wa mikoa, wilaya na halmashauri.

Pia maeneo hayo, pamoja na Bunge, viongezewe madaraka ya kuamua badala ya Rais pekee.
 
2015 upinzani ndyo ulikuja na hoja ya elimu bure. Ccm walianza na kupinga sana uwezekano wa elimu bure ila mwisho ww siku wakaona isiwe shida na wao wakadandia hoja et elimu bure had 4m 4.

Sasa kabla ya uchaguzi kuisha utaona ccm itakavyodandia hii hoja.
 
Jibu swali tunazizidi nini??? Hivi huko CCM nako wanasema wana mjengaji hoja kwa ulivyo kilaza hivi???😂😂😂

Suala ni Tanzania yetu na kesho yetu itakuwa vipi tukiruhusu sera ya majimbo.

Punguza unyonge wa kiakili ridhika na cha kwako ulichopewa na Mungu.
 
Sera ya majimbo msingi wake ni ubinafsi, ukabila na roho ya uchoyo.

Ni sera ambayo imechukuliwa kutoka nje pasipo kuangalia msingi wa utaifa wetu.

Msingi wa utaifa wa Marekani ni tofauti na ule wa Russia ni tofauti na ule wa Zambia ni tofauti na ule ww Afrika ya Kusini.

Ni sera ambayo ukiitazama kwa juu juu unaweza kudanganyika.
Unaizungumziaje USA?

Sent from my OPPO R11s using JamiiForums mobile app
 
Unajua gharama za kuendesha Wilaya?

- Mkuu wa wilaya
-Mbunge tena wilaya zingine wabunge ni wawili
- Mkurugenzi
-DAS
-Mwenyekiti wa Halimashauri

Hawa wote wanasimamia wilaya 1, mfumo wa kijima sana huu
Nilitaka nimwambie hivi thanks.
Huyu Yehodaya ukweli anaujua lkn alishaamua kujitoa ufahamu.
 
Lisu anaongelea tu majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji jimbo litatoa wapi

Anaeleza kijanja janja huku akificha kuwa uendeshaji jimbo unatakiwa uendeshwe kwa pesa za ndani ya jimbo ikiwemo miradi ya maendeleo

Chukulia Singida tegemeo lake kuu la uchuimi ni kuuza vidumu vya mafuta ya alizeti.hivyo vyaweza jenga barabara za lami? Kilomita moja tu ya lami inasoma Gharama ya bilioni moja .Hivyo vidumu vya alizeti vyaweza jenga barabara na kulipa mishahara ya wafayakazi wa jimbo?

Afafanue pia kuhusu gharama za kuendesha jimbo asilaghai tu ohh mujiamulie wenyewe!!!

Ukimsikiliza uaona kabisa mlaghai kwenye gharama Za uendeshaji na za miradi ya maendeleo zitakako toka hagusi anahamia hoja nyingine mbio
Mbona unafoka sana?
Kumbuka kuwa magavana wa majimbo ni viongozi wa kuchaguliwa na wananchi wa eneo husika.Are we togather?
 
Unapo sema utaifa wa nigeria upo hoi unamaanisha nini ? Nimeishi nigeria 2002 hadi 2011 sijaona hicho unacho kisema wewe kabisa au ni stori za vijiweni?
Nigeria kuna ukabila uliojengwa kwa msingi wa majimbo yao. Wanajitambulisha kwa ukabila wao.

Sera ya majimbo itaigawa nchi.
 
Back
Top Bottom