Uchaguzi 2020 Lissu anaongelea tu Serikali za Majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji zitatoka wapi

Uchaguzi 2020 Lissu anaongelea tu Serikali za Majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji zitatoka wapi

Zipo nchi nyingi tu maskini zenye sera ya majimbo.
Kwani sera ya majimbo ndio utajiri?Nchi kuendelea Kuna factor nyingi kuwa tu na mfumo mzuri wa utawala haitoshi lakini kwa mazingira ya Tzn ,tukiweka mfumo huu nchi itapaa Sana kiuchumi.Leo hii Zanzibar iko hoi kiuchumi kuliko awali kwa sababu iko treated Kama mkoa
 
Mie naona wewe ndiye hujaelewa mantiki ya kile kinachoongelewa na Lissu! Hebu jiulize kidogo hivi mwaka 2015 ccm ilipokuwa inaahidi kutoa elimu bure, walikuwa wanabainisha fedha zitatoka wapi? Zipo mpaka pesa za kuendeshea kijiji na kata zikosekane vipi pesa za kuendeshea jimbo? Pia tunapojadili jambo hili tuelewe kwamba Lissu hamaanishi kwamba atajengelea ukuta kuziba kila jimbo kama ule mgodi wa Mererani, hapana ! Na wala hamaanishi kuwa kuyagawa majimbo manake hakuna kupeleka au kupokea fedha toka mfuko mkuu, hapana bali kuna baadhi ya vitega uchumi vitawekewa muongozo ili vinufaishe watanzania wote! Tuache upotoshaji ilimradi tu kutafta hoja ya kupinga mawazo mapya!
 
Hata utawala wa majimbo unazo changamoto zake nyingi tu, nenda kazitembelee nchi zenye majimbo utazifahamu kwa ukaribu.
Hakuna 100% solution of anything,kuna trade-offs..

Utawala wa mikoa ni most pathetic system ever happen..

Majimbo na mikoa,majimbo system ni afadhali kuliko huo uchafu wa kikoloni..

Pick your poison!
 
Lisu anaongelea tu majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji jimbo litatoa wapi.

Anaeleza kijanja janja huku akificha kuwa uendeshaji jimbo unatakiwa uendeshwe kwa pesa za ndani ya jimbo ikiwemo miradi ya maendeleo.

Chukulia Singida tegemeo lake kuu la uchumi ni kuuza vidumu vya mafuta ya alizeti. Hivyo vyaweza jenga barabara za lami? Kilomita moja tu ya lami inasoma Gharama ya bilioni moja. Hivyo vidumu vya alizeti vyaweza jenga barabara na kulipa mishahara ya wafayakazi wa jimbo?

Afafanue pia kuhusu gharama za kuendesha jimbo asilaghai tu ohh mujiamulie wenyewe.

Ukimsikiliza uaona kabisa mlaghai kwenye gharama za uendeshaji na za miradi ya maendeleo zitakako toka hagusi anahamia hoja nyingine mbio.
Lissu hajasema kuwa mkoa kama Singida ndio uwe jimbo. Wala hajasema kuwa kanda kama ya Kati ndiyo iwe jimbo. Kwa maelezo yake (msikilize vizuri kwenye video za Kagera), mikoa, wilaya na halmashauri zaweza kubaki zilivyo. Muhimu ni mambo matatu. 1. Mikoa, wilaya na halmashauri zipate madaraka zaidi ya maamuzi ya kiutawala na ya maendeleo kutoka hodhi ya Rais, ambaye anapoamua peke yake anaweza kuwa mbaguzi. 2. Watoa maamuzi muhimu kama Mkuu wa Mkoa, Wilaya na DED wapigiwe kura na wananchi ili wawajibike kwao. 3. Wabunge warudishiwe madaraka yao ya kikatiba ya kufanya maamuzi ya matumizi ya fedha na kupanga maendeleo ya nchi nzima, siyo ku rubber-stamp kila matakwa ya Rais. Ukiielewa hii dhana ya majimbo ya Lissu, hutakuwa na wasiwasi wa gharama tena kwa kuwa haziongezwi na mabadiliko haya ya uwajibikaji kwa wananchi.
 
Wabunge watabaki kuwa wawakilishi wa mhimili wa bunge kubwa katika serikali kuu,madiwani watakuwa wawakilishi katika mabunge ya majimbo,wakuu wa majimbo na watendaji wake watakuwa wawakilishi wa dola waliochaguliwa na wananchi katika majimbo yao.
Wabunge na madiwani wanachaguliwa na wananchi kumbuka kuhusu hilo jambo.

Cha muhimu ni hao wanaochaguliwa kuwa karibu na hao wanaowapigia kura.
 
Acha uongo,Vurugu za kikanda na za kikabila zilikuwepo kabla ya mfumo wa Kaunti,mfumo wa kaunti umemaliza tatizo hilo
Na ww uwezo wako wa kufikiria umeishia hapo siyoo? Chukua Mfano kenya wanaotumia mfumo wa Kaunti zinazoongozwa na Ma senator, unasikia kila siku vurugu za kikanda na kikabila na Baadhi ya Kaunti kama Nairobi na Mombasa kuwa na Uwezo Mkubwa kulinganisha na nyingine.

Hii inaleta mgawanyiko ndani ya taifa na Mwisho kukosa Muungano wa kitaifa kama Kenya wanavolia kila siku.
 
SERIKALI YA MAJIMBO
Wakati naandaa somo kuhusu umuhimu wa serikali za majimbo kiuchumi; tuanze kutafakari jambo hili;
Nchi ya Rwanda ina ardhi yenye ukubwa karibu sawa na mkoa wa Tanga. Rwanda ina kilometa za mraba 26,338 wakati Tanga ina 26,677 (Tanga ni kubwa kidogo)

Rwanda ina idadi ya watu karibu milioni 13 wakati Tanga ina idadi ya watu milioni 2.

Tanga ina fursa zaidi za kiuchumi; kuna fursa ya kuingiza fedha za kigeni kama misitu mikubwa, na hifadhi za wanyama (Saadan, Mkomanzi) sambamba na vivutio vingi vya utalii kuliko Rwanda. Kuna bahari, kuna madini, kuna ardhi kubwa kwa ajili ya kilimo.

Lakini kwenye maeneo ya Uchumi, Elimu, Miundombinu, Michezo, Kilimo, Biashara... Utaona Tanga ni kama kitenisi kwenye uwanja wa Rwanda.

Nini sababu kubwa ya tofauti hizi?

Je! Vipi kama Rwanda ingekuwa ni mkoa mmojawapo wa Tanzania, na mfumo wa utawala ukawa kama ilivyo sasa kwa mikoa mingine ya Tanzania? Rwanda ingekuwa kama ilivyo Sasa?

Kumbuka Tanga ambayo ni kubwa kuliko Rwanda bado kuna mikoa 13 ya Tanzania ambayo ni mikubwa zaidi.

Tutafakari kwanza maswali haya.
R = Rwanda
T = Tanga
Dr. Christopher Cyrilo
Umeweka kwa mfano rahisi sana hata Meko ataelewa
 
Lissu hajasema kuwa mkoa kama Singida ndio uwe jimbo. Wala hajasema kuwa kanda kama ya Kati ndiyo iwe jimbo. Kwa maelezo yake (msikilize vizuri kwenye video za Kagera), mikoa, wilaya na halmashauri zaweza kubaki zilivyo. Muhimu ni mambo matatu. 1. Mikoa, wilaya na halmashauri zipate madaraka zaidi ya maamuzi ya kiutawala na ya maendeleo kutoka hodhi ya Rais, ambaye anapoamua peke yake anaweza kuwa mbaguzi. 2. Watoa maamuzi muhimu kama Mkuu wa Mkoa, Wilaya na DED wapigiwe kura na wananchi ili wawajibike kwao. 3. Wabunge warudishiwe madaraka yao ya kikatiba ya kufanya maamuzi ya matumizi ya fedha na kupanga maendeleo ya nchi nzima, siyo ku rubber-stamp kila matakwa ya Rais. Ukiielewa hii dhana ya majimbo ya Lissu, hutakuwa na wasiwasi wa gharama tena kwa kuwa haziongezwi na mabadiliko haya ya uwajibikaji kwa wananchi.
mumeshabadilika baada ya kuwabana na hoja Za nguvu humu mwambieni afute aliyotamka Kwenye kampeni yahusuyo matumizi ya mapato

Sera lenu hata nyie wenyewe hamulielewi mnajikanyaga Kanyaga tu
 
Hakuna jimbo linalojitosheleza kwa kila kitu,majimbo lazima yatategemeana na yatashirikiana vizuri,yenye madini mengi yatahitaji chakula,barabara,na bandari kusafirisha madini yake n.k n.k
Maisha hayaishii kwenye utawala pekee, tanashuka kwenye mahusiano ya wananchi.

Yanashuka kwenye matumizi ya rasilimali za nchi.

Ubaya ya mfumo wa majimbo ni ule uchoyo kwamba rasilimali hii isiguswe na majimbo mengine.

Kinachopatikana Mtwara kinatumika kwa faida ya nchi nzima.

Kinachopatikana Kagera kinatumiwa kwa faida ya nchi nzima na hiyo ndio maana ya umoja.
 
Bila ya matusi kichwa chako ni kama hakiwezi kufanya kazi.

Sera ya majimbo msingi wake ni ubinafsi na uchoyo haina upendo wa kitaifa ndani yake.

Wale wenye rasilimali chache wafe na umaskini wao na wale wenye utajiri waishi vizuri kivyao!!.

Nchi itasambaratika mapema sana kwani serikali kuu haitaweza kuyashinda malalamiko ya majimbo yatakayoachwa nyuma.
eti nchi itasambaratika ndio yule kichaa wenu kawaambia halafu mlivyo hamnazo you run with that nonsense!

Kama ni hivyo basi USA,South Africa,Kenya,Canada,India...na even your beloved stupid totalitarian China ungekuta washa sambaratika,lakini wapo na wanazidi prosper..

Hamna hoja kwenye hili,Lissu katoa msumari na wananchi seem to accept hapo ndio matako yanawauma sana..

Eti tutasambaratika,jibu la hovyo sana...halafu wananchi hawajawaelewa na majibu yenu kabisa mnabaki kuchanganyikiwa even more

Natukana yes,kashitaki kwa mawe!
 
Eti vidumu vya mafuta?

Unajua singida inazalisha mafuta kiasi gani?

Unajua singida inazalisha alizeti kiasi gani?

Unajua singida inazalisha mahindi na mtama kiasi gani?

Unajua singida inazalisha ng'ombe kiasi gani?

Sera ya majimbo ni suluhisho la wezi wa rasilimali za nchi.

Hofu yenu kuu ni kunyang'anywa tonge mdomoni maana mmezoea kumiliki mapesa yote mnayachezea mnavyotaka.

Majimbo yatakata huo mrija wa ufisadi.

Mkatafute namna nyingine ya kuishi, msitegemee kuishi kwa kupora fedha za wananchi.
Hakutakuwa tena na mambo nitampa kazi nyingine.
 
Lisu anaongelea tu majimbo kujiamulia mambo ila haelezi gharama za uendeshaji jimbo litatoa wapi.

Anaeleza kijanja janja huku akificha kuwa uendeshaji jimbo unatakiwa uendeshwe kwa pesa za ndani ya jimbo ikiwemo miradi ya maendeleo.

Chukulia Singida tegemeo lake kuu la uchumi ni kuuza vidumu vya mafuta ya alizeti. Hivyo vyaweza jenga barabara za lami? Kilomita moja tu ya lami inasoma Gharama ya bilioni moja. Hivyo vidumu vya alizeti vyaweza jenga barabara na kulipa mishahara ya wafayakazi wa jimbo?

Afafanue pia kuhusu gharama za kuendesha jimbo asilaghai tu ohh mujiamulie wenyewe.

Ukimsikiliza uaona kabisa mlaghai kwenye gharama za uendeshaji na za miradi ya maendeleo zitakako toka hagusi anahamia hoja nyingine mbio.
Wewe na mwenyekiti wako ni vichwa vya panzi hamna akili! Ukweli usemwe, CCM ina uhaba mkubwa sana wa vijana wenye akili!!
 
Hujajibu swali langu!!

Nimesema kama sera ya majimbo ni ya kichoyo na kibaguzi Sasa kwa nini na Sera yetu ya sasa ya mikoa Magufuli amesema mchana kweupe hawezi peleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani?

Alisema jimboni kwa Bwege kabla hata ya kampeni na amesema maeneo mengi akiwa kwenye kampeni?

Huu ubaguzi na uchoyo nayo ni sera ya majimbo?
Kwamba tunaanzisha majimbo kwaajili ya mtu mmoja amesema hatapeleka maendelea sehemu Fulani?

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Ya
eti nchi itasambaratika ndio yule kichaa wenu kawaambia halafu mlivyo hamnazo you run with that nonsense!

Kama ni hivyo basi USA,South Africa,Kenya,Canada,India...na even your beloved stupid totalitarian China ungekuta washa sambaratika,lakini wapo na wanazidi prosper..

Hamna hoja kwenye hili,Lissu katoa msumari na wananchi seem to accept hapo ndio matako yanawauma sana..

Eti tutasambaratika,jibu la hovyo sana...halafu wananchi hawajawaelewa na majibu yenu kabisa mnabaki kuchanganyikiwa even more

Natukana yes,kashitaki kwa mawe!
Yani ni ajabu wananchi wamekubali lakini ni viongozi pekee wa ccm ndiyo hawataki, tule tuvyeo twakupeana tunaenda kuisha
 
Ya

Yani ni ajabu wananchi wamekubali lakini ni viongozi pekee wa ccm ndiyo hawataki, tule tuvyeo twakupeana tunaenda kuisha
Wananchi walikubali wapi hiyo Kura walipiga wapi?
 
Hata mjifariji vipi ndio maana tuko kwenye uchaguzi watu ndio wataamua na sio wewe na wenzako mnaohofia njaa kwenye matumbo yenu.
Waende wakajiajiri maana hakutakuwa na vyeo vya kupeana bali itakuwa mwenye uwezo ndiyo anakuwa kiongozi
 
Back
Top Bottom