Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Hasa yale mabulungutu ya madafu hata wobongoflava wanagawaga.
 
Kama wana guts wapeleke kesi mahakamani😅😅
 
Magufuli kusachiwa siyo ajabu hakuwa mtanzania wa kawaida kama unavosema alikuwa Rais wa nchi hivyo serikali inaamini alikuwa ana mambo mengi anayajua hivyo kusachiwa nyumbani kwake siyo ajabu. Na je tunajuaje labda mama janeth ndio alisema huko serikalini kwamba njoeni kuna hela nyingi zipo chumba fulani na marehemu hakuwa mfanyabiashara You never know. LISSU ASIPUUZWE ANA HOJA NA ASIKILIZWE.
 
Lissu haaminiki anatangaza Rais samia kauza bandari kwa DP-WORLD kumbe uwongo mtupu. Lissu anawapeleka watanzania mputamputa.
 
Ina maana baada ya magu kufariki,kuna walioenda nyumbani kwake kupekua?
Kwa mbaali naanza kuona dalili za wanaosema TL amehongwa na kundi fulani ili kuvuruga hoja ya bandari.
Na mpaka hapa hoja ya bandari inaweza kupotea tuanze kujadili upuuzi huu.

Kama tokea uhuru tungepata rais fisadi kama magufuli,tanzania ingekuwa mbali sana.
Ila kwa sababu tulipata waadilifu,ndo maana tunaanza kugawa hata urithi wetu.
 
Mwandishi Luqman Maloto alishawahi kuandika kuhusu hii ishu ila hakutaja kiasi.
Hata wengine walisema china, wengine canada, wengine malaysia..na huyu kasema nyumbani..kwa hiyo yeyote anaweza sema awazavyo.
 
Nadhani wengi walimwamini sana Jpm kumbe naye alikua mlaji mbinafsi
Waliomuamini JPM hawawezi kumuamini Lissu..na waliomuamini Lissu hawawezi kumuamini JPM..ndio maana kila mtu alipata kura zake.

Mmoja ni kiongozi aliyetenda kwa vitendo, mwingine ni kiongozi wa maneno..pia usisahau hata watangazaji wana mashabiki na wachezaji wana mashabiki..ila utajua yupi ana mashabiki zaidi.
 
..binafsi najiuliza mabulungutu ya pesa aliyokuwa akitembea nayo Magufuli yalikwenda wapi baada ya kufa? Nani aliyachukua? Alikuwa anayaweka wapi?
Kwani hizi anazotoa samia kwenye magoli ya simba na yanga mpaka tunaambiwa na msigwa mama kasema pesa zipo nyingi tu anazitoa wapi??
 
Kwahiyo tukubaliane hoja ya Lissu kusema Rais samia kagawa bandari bure kwa waarabu ni ya uwongo?
 
Sio wavuvi tu..kama eneo serikali imezuua kuingia na wewe ukaingia basi unachukuliwa kama jangili..nenda kawinde kwenye hifadhi za taifa uone kama utachekewa na askari wa game.

Enzi za Magufuli hata ukikutwa unaharibu maeneo ya hifadhi za maji ilikuwa ni shida..vyanzo vya maji vilikuwa vinalindwa na askari.
 
Somo ninalolipata kutokana na makala hii ni kwamba Tanzania haijawahi kuwa na chama cha upinzani,
bali kuna vyama vya upinzani pandikizi. Kwa kusema hivyo
nijitetee kwa kusema,Kitendo cha dokta sulaa alichotufanyia 2015 akisaidiana na porofesa wa buguruni
mimi kama mfuasi wa upinzani miaka hiyo kilinipa fundisho kwamba
viongozi wa upinzani ni mapandikizi wa chama kijani wanapoona dalili za upinzani kuingia ikulu,wanapiga hatua moja nyuma kwa kuanzisha mtafaruku baina yao ili wasishike dola.

Sasa hii hoja aliyoiibua TL kwangu naona ni mwendelezo huo huo,wa kutufanya wajinga.
Tujifanye anachokisema ni kweli,niulize swali,je huu ni wakati sahihi kuingiza hoja hiyo
kipindi hiki cha kukomboa bandari zetu na kupigania katiba mpya?

Ninachoshukuru,binafsi baada ya kuona ubabaishaji huu mkubwa
nimeamua kuisaka kadi ya chama tawala,ili mdogo mdogo
hata nigombee ujumbe wa shina,kwa kufanya hivyo nitawatendea haki
wanashina langu nitakalokuwa naongoza.
 
Tundu Lissu haaminiki anatangaza kuwa Rais Samia anagawa bandari bure kwa waarabu kumbe uwongo mtupu. Lissu anawapeleka watanzania mputamputa.
 
Ukiwa Rais unakua Mali ya state, ndio maana mjane wake anaendelea kulipwa 80% ya salary ya sitting president, anapewa magari, wapishi, wasaidizi na atajengewa nyumba. Hata kaburi lake linalindwa na askari wetu. Baada ya kifo lazima vijana wapite kukusanya documents za office zikahifadhiwe.
 
Kumbe pesa haiwezi kukupa furaha wala kuzuia kifo, nimegundua leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…