Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Nyumba yoyote anayokwenda raisi iwe yake binafsi au ya serikali; walinzi wake lazima waikague kila chumba kuhakikisha ipo secure.

Sasa hizo hela alikuwa anazificha wapi, anapokuwa akienda huko. Tena wanaenda kabla yeye mwenyewe ajafika, $42m sio hela unazoweza zificha zisionekane.

Porojo tu, raisi ata anapoenda ata nje ya nchi kuna watu wanatangulia kukagua anapofikia siku kadhaa kabla ya yeye kufika.
Umeambiwa alijenga HANDAKI na kuficha pesa huko, unashindwaje kuelewa? Shule za kata zimeathiri sana vijana
 
Kabisa ndugu, anayepingana na hoja ya Lissu na atangulie Mahakamani ili akapatiwe ushahidi huko. Kwa bahati nzuri Mahakama zimewekwa mfukoni na maccm, kwahivi hakuna kitakachofichwa
watu wanafunguliwa mashitaka kwa kesi za kijinga tu, haya madai ni makubwa sana kuachwa hivihivi, Lissu afunguliwe mashtaka tujue ukweli uko wapi.
 
Kwamba Tundu Antipas Lisu anatuambia baada ya kufa Nyumba ya Shujaa Magufuli ikasachiwa na fedha hizo zikakutwa?

Kwanini alisachiwa kama ndivyo?

Tundu Antipas Lisu ana habari gani kwa Watanzania ambazo hawazijui? Tamaduni za misiba ya kitanzania zinajulikana mambo ya kusachiana hayapo

Niishie hapo

Mlale Unono 😀
Jikono Jandama alikuwa Fisadi/Mwizi ,tusipepese macho Bwashee.
 
Nilisema hili humu nikatukanwa tena zilikua zimewekwa kwenye majaba na viroba mwendazake bhana[emoji23][emoji23][emoji23]
Halafu kuna watu wanajidai eti Magufuli anasingiziwa wakati tuu katika ziara zake mabarabarani alikuwa anagawa fedha akitembea nazo kukutwa nazo nyumbani kwake ndio wanasema anasingiziwa.
 
UPDATES.........
Lissu ameprove nilichosema mimi[emoji1314][emoji1314]Lissu: USD 42Milioni (takribani Sh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Na niliyasema hayo mwezi march kupitia uzi huu hapa nikaishia kutukanwa na kuambiwa eti namsingizia na kuitwa mzushi kupitia post hii[emoji1314][emoji1314]Leo ni miaka 2 tokea kifo cha Hayati Magufuli
Screenshot_20230806-001754.jpg
 
Mbona hii taarifa wala sio ngeni ?
Nafikiri kuna waandishi Kati ya Maloto au Ansbert Ngurumo walishawahi kuripoti...hii taarifa....

Nashangaa wanaostuka kama mpya
Na nashangaa na wanachadema nao wanamuona Lissu kama kapotoshwa. ...
Kuna waziri yoyote wa awamu ya nne ambaye hakuwahi kunufaika binafsi na uwaziri wake?

Je ndani ya ccm yupo asiyechukua chochote kupitia nafasi yake ?
 
Kwamba Tundu Antipas Lisu anatuambia baada ya kufa Nyumba ya Shujaa Magufuli ikasachiwa na fedha hizo zikakutwa?

Kwanini alisachiwa kama ndivyo?

Tundu Antipas Lisu ana habari gani kwa Watanzania ambazo hawazijui? Tamaduni za misiba ya kitanzania zinajulikana mambo ya kusachiana hayapo

Niishie hapo

Mlale Unono [emoji3]
UPDATES.........
Lissu ameprove nilichosema mimi[emoji1314][emoji1314]Lissu: USD 42Milioni (takribani Sh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Na niliyasema hayo mwezi march kupitia uzi huu hapa nikaishia kutukanwa na kuambiwa eti namsingizia na kuitwa mzushi kupitia post hii[emoji1314][emoji1314]Leo ni miaka 2 tokea kifo cha Hayati Magufuli
 
That’s only because I have time to waste today. Otherwise I wouldn’t even bother.
Dah,

Kumbe siku nyingine unajisemea "Mmang'ati hayo yanafukuzana kaa nyumbu saa hizi!!" 😀 😀

The elitist black privilege is so thick, I could cut it with a knife.
 
Kuna waziri yoyote wa awamu ya nne ambaye hakuwahi kunufaika binafsi na uwaziri wake?

Je ndani ya ccm yupo asiyechukua chochote kupitia nafasi yake ?
Inahusiana vipi na suala hili la kukutwa na hela nyumbani kwake?
 
View attachment 2709505


Akiongea na wananchi wa Bugarama Halmashauri ya Geita Vijijini Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Antipas Lissu leo Jumamosi ya Agosti 5, 2023 amesema kuwa aliyekuwa Rais wa Tanzania The Late, John Magufuli baada ya Kufariki kiasi Cha Dolla za Kimarekani milioni 42 (zaidi ya Sh. Bilioni 100), zilikutwa nyumbani kwake Chato.

Kiasi hicho cha fedha ni nyingi hasa ukilinganisha na mshahara wa Rais, Lissu aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara, wakati akiwasilisha mada ya uuzwaji na uwekezaji wa bandari.

Lengo la kuweka habari hii hapa ni mstuko nilioupata.
Hata mimi nilimuona na kumsikia "live" kupitia YouTube online TVs..

Mimi sikuwa shocked kivile kwa sababu hizi "rumours" za mwendazake kukutwa na mabilioni ya shilingi na mamilioni ya dollar nyumbani kwake zilianza kusikika na kuusambaa immediately siku chache baada ya kifo chake..

Sasa taarifa hizi ndo tu zinaanza kuvujishwa rasmi na kutoka nje ya corridors za Lumumba. Na ujue tu sasa kuwa, huko CCM mambo ni moto. Ni kusalitiana juu ya kusalitiana kati ya Team CCM ya Hayati JPM vs Team CCM ya Rais Samia Suluhu Hassan na sababu ni ishu moja tu, Mkataba wa bandari za Tanganyika uliosainiwa na Wazanzibari hawa wawili Samia & Mbarawa..!!

Naona Team SSH wamechochwa na Team Hayati JPM na wao sasa wanaanza kuachilia waliyokuwa wameyasitiri kwa muda mrefu. Hawawezi kuyasema wao. Wanapenyezewa watu dizaini ya kina Tundu Lissu na kuyaachilia hewani..

Na sina shaka yoyote na Tundu Lissu kwa sababu jamaa huwa yuko makini kuachilia mambo kama haya waziwazi pasipo kuyaweka katika mizani ya ukweli kwanza na kuya - strategize kisheria iwapo kina Ramadan Kingai watataka kuandika wito mwingine tena..

I am pretty sure that, he got that from very reliable sources within the government...!

Tunasema na tunaendelea kusema tena, wasipotumia akili kulimaliza la bandari kwa kuzingatia matakwa ya wenye nchi, basi wataparurana wenyewe kwa wenyewe huko CCM na serikalini mpaka wauane tena..!!
 
Hiyo bilion 100 Hata Diamond wa Wasafi anayo ndio ushangae kwa kidume Shujaa Magufuli Waziri miaka 20 Rais miaka 6?

Bavicha mnawaza kimaskini Sana😂😂
Diamond ni kwa jasho lake, lakini Magufuli ameipataje hela nyote hiyo ...ndio swali?
 
watu wanafunguliwa mashitaka kwa kesi za kijinga tu, haya madai ni makubwa sana kuachwa hivihivi, Lissu afunguliwe mashtaka tujue ukweli uko wapi.
Kinana mbona huwa wanasema ana manini huko lakini sijawahi kumsikia kamshitaki mtu.

Tanzania hatuna litigious culture
 
Aliyeua wavuvi zaidi ya 60 kwenye kisiwa cha Rubondo aliuwa chama gani ?
Raia wengi (wavuvi) walipoteza maisha yao huko, JPM alikua MHALIFU sana

 

Akiongea na wananchi wa Bugarama Halmashauri ya Geita Vijijini Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Antipas Lissu leo Jumamosi ya Agosti 5, 2023 amesema kuwa aliyekuwa Rais wa Tanzania The Late, John Magufuli baada ya Kufariki kiasi Cha Dolla za Kimarekani milioni 42 (zaidi ya Sh. Bilioni 100), zilikutwa nyumbani kwake Chato.

Kiasi hicho cha fedha ni nyingi hasa ukilinganisha na mshahara wa Rais, Lissu aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara, wakati akiwasilisha mada ya uuzwaji na uwekezaji wa bandari.

Lengo la kuweka habari hii hapa ni mstuko nilioupata.
Lissu kazeeka, muonekano wake sasa kawa mzee kabisa.
 
Back
Top Bottom