Pre GE2025 Lissu: Mbowe ni muongo, tulifanya kikao cha siri kwa siku 3. Alikataa nisigombee Urais na Uenyekiti huku yeye akisema hajaamua

Pre GE2025 Lissu: Mbowe ni muongo, tulifanya kikao cha siri kwa siku 3. Alikataa nisigombee Urais na Uenyekiti huku yeye akisema hajaamua

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Tundu Lissu ametangaza nia kuwania nafasi ya urais mwakani na kwamba chama chake kinajiandaa kupata ushindi wa kutosha dhidi ya Rais Samia Suluhu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye anatarajiwa kugombea kupitia chama hicho.

Akiongea na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo baada ya kurejea kutoka nje ya nchi alipokuwa kwa mapumziko mafupi baada ya ziara ya chama chake Kanda ya Kaskazini aliyoifanya sambamba na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Lissu alisema kwa sasa chama chake kinaandaa wagombea katika nafasi mbalimbali kwa ajili ya kushinda uchaguzi ujao.

“Nia yangu ya kugombea mwaka 2025 iko palepale nitaitikia wito Watanzania na nitaitikia wito wa chama changu” amesema Lissu.

Alipoulizwa kuhusu kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama chake amesema hana mpango huo na kukanusha uvumi wakuwepo mgogoro kati yake na Mwenyekiti wake Freeman Mbowe kuhusu kuwania nafasi hiyo.

“Nimesema mara mia kwamba sigombei uenyekiti wa chama sasa huo mvutano unatoka wapi ni wa kutengenezwa tu na vyombo vya habari” amesema Lissu.

Source: nipashe Jue 2024
Mbona unaleta habari za mwaka jana? Acha kuchanganya mada wee mgonjwa wa malaria!
 
Wakuu

Kimeumana CHADEMA, Tundu Lissu amvaa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe baada ya kurejea Tanzania kutoka nchini Ubeligiji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuulizwa kuhusu alichokisema Mbowe kuwa walishauriana asigombee Uenyekiti CHADEMA, pengine baadae angegombea Urais

Soma, Pia: Mbowe: Ilikuwa ghafla sana Lissu kutangaza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa

"Kwanza hili niliseme kwa masikitiko, kwasababu si jambo nzuri kusema Mwenyekiti (Freeman Mbowe) amesema uongo, kwenye hili amesema uongo. Tulikutana kwa siku tatu hapa Msimbazi, Kanisani tukipatanishwa, tukizungumza juu ya hiki kinyang’anyiro na kwa siku tatu zote Mwenyekiti alisema yeye hajaamua kugombea nafasi yoyote [kwa siku tatu], Katibu Mkuu John Mnyika ni shahidi."
View attachment 3194110
Sidhani kama Mbowe anataka kugombea urais. Na inawezekana kuwa ni kweli alikuwa hajaamua kugombea uenyekiti. Mimi nahisi alifanya uamuzi wa kugombea baada ya lugha za kebehi dhidi yake kusheheni mitandaoni. Naamini alikuwa chini ya presha kubwa kutoka kwa ndugu na jamaa za kumtaka asigombee. Ni zile alizoita character assassinations ndio zilimsukuma afanye huo uamuzi.

Kazi sasa ni kwa wapiga kura. Ukweli haya mambo ya vijembe yanasikitisha na yanachosha.

Amandla...
 
Wakuu

Kimeumana CHADEMA, Tundu Lissu amvaa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe baada ya kurejea Tanzania kutoka nchini Ubeligiji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuulizwa kuhusu alichokisema Mbowe kuwa walishauriana asigombee Uenyekiti CHADEMA, pengine baadae angegombea Urais

Soma, Pia: Mbowe: Ilikuwa ghafla sana Lissu kutangaza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa

"Kwanza hili niliseme kwa masikitiko, kwasababu si jambo nzuri kusema Mwenyekiti (Freeman Mbowe) amesema uongo, kwenye hili amesema uongo. Tulikutana kwa siku tatu hapa Msimbazi, Kanisani tukipatanishwa, tukizungumza juu ya hiki kinyang’anyiro na kwa siku tatu zote Mwenyekiti alisema yeye hajaamua kugombea nafasi yoyote [kwa siku tatu], Katibu Mkuu John Mnyika ni shahidi…."
View attachment 3194110
😂😂😂😂😂😂😂
Ila Lissu jamani huwa ananifurahisha anavyoongea


No wonder hata zile risasi alipigwa na chadema wenzake
Ila wakamtupia zigo baba wa watu.
 
Sidhani kama Mbowe anataka kugombea urais. Na inawezekana kuwa ni kweli alikuwa hajaamua kugombea uenyekiti. Mimi nahisi alifanya uamuzi wa kugombea baada ya lugha za kebehi dhidi yake kusheheni mitandaoni. Naamini alikuwa chini ya presha kubwa kutoka kwa ndugu na jamaa za kumtaka asigombee. Ni zile alizoita character assassinations ndio zilimsukuma afanye huo uamuzi.

Kazi sasa ni kwa wapiga kura. Ukweli haya mambo ya vijembe yanasikitisha na yanachosha.

Amandla...
Nafasi ya mgombea uRais pale Chadema ni biashara

Kwa Sasa wanawavizia February na Dr Naniliu PhD 😂😂😂
 
Wakuu

Kimeumana CHADEMA, Tundu Lissu amvaa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe baada ya kurejea Tanzania kutoka nchini Ubeligiji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuulizwa kuhusu alichokisema Mbowe kuwa walishauriana asigombee Uenyekiti CHADEMA, pengine baadae angegombea Urais

Soma, Pia: Mbowe: Ilikuwa ghafla sana Lissu kutangaza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa

"Kwanza hili niliseme kwa masikitiko, kwasababu si jambo nzuri kusema Mwenyekiti (Freeman Mbowe) amesema uongo, kwenye hili amesema uongo. Tulikutana kwa siku tatu hapa Msimbazi, Kanisani tukipatanishwa, tukizungumza juu ya hiki kinyang’anyiro na kwa siku tatu zote Mwenyekiti alisema yeye hajaamua kugombea nafasi yoyote [kwa siku tatu], Katibu Mkuu John Mnyika ni shahidi…."
View attachment 3194110
Aisee...

Ndo uzuri wa huyu mwamba. Huwa hazunguki mbuyu, hamung'unyi maneno, hafichi ukweli, ukienda solemba, anakulipua hapohapo..

Ni nadra sana kuwa na viongozi wa namna ktk karne hii...

Na kwa hili, hata mimi, nilivyomtazama na kumsikiliza Mwenyekiti Freeman Mbowe kwenye interview yake na Salim Kikeke nilimwona kabisa kuna kitu hakiko sawa kwake, kuna mambo anaficha, hasemi ukweli...

Kauli yake siku ile kuwa "Makamu Mwenyekiti wangu Tundu Lissu ametushitukiza wengi kugombea uenyekiti" inasema mengi sana..

It's very sad kuwa kwa yeye Freeman Mbowe (kiongozi wa chama, Mwenyekiti) kusema uongo kama hiyo inaweza kuwa busara kama tunavyoambiwa "ANA BUSARA..."
 
Wakuu

Kimeumana CHADEMA, Tundu Lissu amvaa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe baada ya kurejea Tanzania kutoka nchini Ubeligiji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuulizwa kuhusu alichokisema Mbowe kuwa walishauriana asigombee Uenyekiti CHADEMA, pengine baadae angegombea Urais

Soma, Pia: Mbowe: Ilikuwa ghafla sana Lissu kutangaza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa

"Kwanza hili niliseme kwa masikitiko, kwasababu si jambo nzuri kusema Mwenyekiti (Freeman Mbowe) amesema uongo, kwenye hili amesema uongo. Tulikutana kwa siku tatu hapa Msimbazi, Kanisani tukipatanishwa, tukizungumza juu ya hiki kinyang’anyiro na kwa siku tatu zote Mwenyekiti alisema yeye hajaamua kugombea nafasi yoyote [kwa siku tatu], Katibu Mkuu John Mnyika ni shahidi…."
View attachment 3194110
Mbowe kakutana na kisu cha ngariba😅
 
Huyu Mzee anapenda vita sana vya maneno.
Anasema ana mdomo mpana,

Wanaomshabikia kuna siku atawarudia..

Kama hata vikao vya sir anaropoka mpaka eneo walilofanyia.. imagine ni top boss wa CDM.....

Siasa za upinzani kuendesha chama sio kazi rahisi .

Kuendesha chama kwa kusema tu?

Tupo
 
kama ccm mwenyekiti ndo raisi why not CDM ? Sina mahaba na mwana , ila kwa hali ya chadema natamani ashinde
 
Back
Top Bottom