Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Kwani huyo lisu anajiona nani hasa hadi ampangie vya kufanyiwa ndo arudi? kwani kuna mtu kamuita au alivokaa huko miaka yote jua halikuwaka TZ au mvua haikunyesha?

Ikiwezekana kae huko na afie huko hakuna amtakae. Waswahili wanakwambia ukitaka kudeka hakikisha yupo wa kukudekeza, sasa asilazimishe kudekezwa. Akitaka arudi apambane na hali yake kama hatak abaki huko, mxiuuuu
 
Mimi namshauri Lisu arejee tu, sioni hayo madai yake yakitekelezwa. Ila nina uhakika hawezi kufanyiwa madhila yoyote, kwakuwa aliyekuwa anaagiza afanyiwe ule udhalimu alikuwa ni Magufuli kutokana na kiburi cha madaraka, na kutokutaka kukosolewa. Hayo madai yake mengine aje atayafuatilia akiwa hapa kwa yale yanayowezekana.
 
Kwani huyo lisu anajiona nani hasa hadi ampangie vya kufanyiwa ndo arudi? kwani kuna mtu kamuita au alivokaa huko miaka yote jua halikuwaka TZ au mvua haikunyesha? Ikiwezekana kae huko na afie huko hakuna amtakae. Waswahili wanakwambia ukitaka kudeka hakikisha yupo wa kukudekeza, sasa asilazimishe kudekezwa. Akitaka arudi apambane na hali yake kama hatak abaki huko, mxiuuuu
Kinachokuuma ni nini?

Meko na ndungai waliwa brain wash sanaaa
 
Mimi namshauri Lisu arejee tu, sioni hayo madai yake yakitekelezwa. Ila nina uhakika hawezi kufanyiwa madhila yoyote, kwakuwa aliyekuwa anaagiza afanyiwe ule udhalimu alikuwa ni Magufuli kutokana na kiburi cha madaraka, na kutokutaka kukosolewa. Hayo madai yake mengine aje atayafuatilia akiwa hapa kwa yale yanayowezekana.
Bado hali sio shwari.
Kumbuka watu wa meko bado wana ile mentality ya unyama na uuaji.
Itachukua muda kidogo hawa wauaji kubadiki misimamo yao.
Bado wanatembea kwenye kivuli cha meko na ukatili wake.
Angalia tu a hata baadhi ya wana JF kwenye hii thread.
Bado wana ukatili na roho mbaya ambayo walimezeshwa na meko na kina heri wa uvccm.
Kwa hio bafo haki si shwari
 
Umri huu nilionao niludi shule nikafanye nini changamoto nilionayo ya kuwasomesha wadogo zako kwangu ni shule tosha kama umenielewa na ujumbe wangu umefika hizo tofauti za r na l si kitu kwangu
Na kweli, "asiludie" tena kukuuliza uliza maswali[emoji23][emoji23]
 
  • Kicheko
Reactions: Pep
huyu bwana alikuwa mwanasiasa kuanzia lini? tangu jiwe achukue urais? kwa kuwa kamdindia jiwe ndio anajiita mwanasiasa leo? uwanasiasa wa kibongo unachekesha sana. ukiwa tu tofauti na chama tawala ama kiongozi wa nchi basi nawe mwanasiasa!

sijui labda mtu atanijuze hapa JF!

maana mimi namjua Lissu kama wakili mmoja hodari sana na isingekuwa hali ya hewa ya nchi iliyopita, angefaa sana kuwa mwanasheria mkuu wa serikali. nampa asilimia 1000%. ila kujua sheria huwa unakua adui katika uongozi wa nchi maana wapigaji ni wengi kuliko watii kwenye utendaji wa serikali maana huwa wana watu wao pembeni ambao wanaweka mambo yao sawa na mtu asistukie maovu yao. asingeweza kuwa rais wa kudumu maana wengi wangelizwa sana maana Lissu anatazama sheria zaidi, haijalishi nani ataguswa.

hivi, anajua ukweli wa ushambulizi wake? ana uhakika kweli kuwa jiwe ndio ali ochestrate sakata lote?

kuna watu wanapumua kwenye hii nchi leo hii ambao hawastahili kuwepo maana ni vinyonga hatari sana. na hivi bado wanapumua, hii nchi haitokuwa na utulivu wala amani mpaka walale salama!

arudi tu huku akiamini 'adui' yake 'hayupo' tena ila atambue siasi mbaya sana na saa zingine unaweza ukawa chambo!
 
Bado hali sio shwari.
Kumbuka watu wa meko bado wana ile mentality ya unyama na uuaji.
Itachukua muda kidogo hawa wauaji kubadiki misimamo yao.
Bado wanatembea kwenye kivuli cha meko na ukatili wake.
Angalia tu a hata baadhi ya wana JF kwenye hii thread.
Bado wana ukatili na roho mbaya ambayo walimezeshwa na meko na kina heri wa uvccm.
Kwa hio bafo haki si shwari

Mkuu ule unyama wote ulikuwa unaagizwa na Magufuli. Hao wanyama ni kweli bado wapo, ila nani wa kuwapa maagizo? Hata hivyo sipingi angalizo lako.
 
Kuhusu malipo ya Tundu Lissu kama posho na stahiki zake mbalimbali kwa mujibu wa Spika Ndugai, kuna maswali yanahitaji majibu;

1. Ndugai anasema Tundu keshalipwa

- Tshs. 200,000,000 (za nini?Haijulikani...!!)

  • Tshs. 360,000,000 (za mini? Haijulikani...!!)
  • Tshs. 500,000,000 (za mini? Haijulikani...!!
...............................................................
JUMLA Tshs. 1,060,000,000 (billion moja na sitini milioni..!!!)
................................................................

2. Je, Spika Ndugai anaweza kutoa uthibitisho Wa malipo haya kutoka Bunge kwenda kwa Tundu Lissu ili kukata mzizi Wa fitina..??

3. Kama Tundu Lissu amelipwa pesa zote hizi na serikali kupitia Bunge, iweje bado analalamika kudhulumiwa mafao na haki yake ya kulipiwa gharama za matibabu..??

4. Je Spika Ndugai anaweza kutoa mchanganuo wa pesa zote alizolipwa Tundu Lissu ni kwa ajili ya nini?

NB:
Mimi naamini mambo mawili juu ya sakata hili;

MOSI: fedha za mafao, gharama za matibabu, posho na mishahara ya Tundu Lissu kuanzia Septemba, 2017 hadi ukomo wa bunge la 11 zimelipwa lakini hazijaenda kwa muhusika..!

PILI; Spika Ndugai anaweza kuwa sahihi kwa sababu yeye (inawezekana) anapokea taarifa tu za utekelezaji na kisha kuzitetea tu bila kujiridhisha kuwa zina ukweli. Hapa tunaweza kusema (labda) anacheza ngoma ya watu wengine...!

TATU; Tundu Lissu, binafsi, naamini hawezi kudai pesa mara mbili huku akitambua kuwa ameshalipwa..!

NNE; Kama Spika anadai Lissu alishalipwa Tshs. bilini 1.06 halafu wakati huohuo muhusika anasema hajapokea hata senti, hapa inakuwa na maana gani hasa..?

Je, kuna uwezekano kuna ufisadi wa fedha bungeni kwa kutumia kivuli cha ugonjwa na kuvuliwa kwa ubunge wa Tundu Lissu...?

Uchunguzi ufanyike tu...
Usipoteze muda wako kumuamini ndungai.
Ana
Mkuu ule unyama wote ulikuwa unaagizwa na Magufuli. Hao wanyama ni kweli bado wapo, ila nani wa kuwapa maagizo? Hata hivyo sipingi angalizo lako.
Mkuu; angekuwa hajawaagiza wale wote waliofanya ule unyama wangekamatwa fasta.
Polisi wa TZ wapo vizuri sanaaa
 
Mh Lisu, endelea kula maisha uko Ughaibuni, siku ukichoka, Rudi Ikungi upumzike.
 
Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.
Sijaelewa hi; kwamba Lissu akiwa hospitalini alikua anawekewa pesa za mafuta za kwenda jimboni kwake? Hapa wa kulaumiwa ni nani? Bunge au Lissu??? Somebody to help me please
 
TATU; Tundu Lissu, binafsi, naamini hawezi kudai pesa mara mbili huku akitambua kuwa ameshalipwa..!
Wewe unamwamini lissu kwa asilimia ngapi? mimi ni kwa 50% namndugai 50% sasa ilikutoa utata ARUDI TZ WAKAE PAMOJA KILA MTU ASIBITISHE ALIVYOTOA ALIMPA NANI NA LISSU AONYESHE KAMA HAJAPOKEA KWELI mhuniyule haaminiki
 
Back
Top Bottom