Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Sasa Lissu hat asiporudi kwani tunakosa Nini
HiviI anajionaje hasa
Mbona anajiona yeye NI Bora Sana kuliko watanzania wengine
 
Sioni ni kivipi hayo yote aliyoyataja kama yanatekelezeka!

..nadhani tatizo ni UZITO wa wahusika waliotaka kumuua TL.

..angekuwa ameshambuliwa na wahuni au vibaka zingefanyika juhudi kubwa kuwakamata ili " kung'arisha " legacy za watu fulani.

..key FACT ktk shambulizi lile ni kuondolewa kwa walinzi ktk eneo aliloshambuliwa TL.

..Wachunguzi wafuatilie mtiririko wa amri ya kuondolewa walinzi wa area D siku ya tukio. Naamini watafika mahali watampata mhusika aliyepanga tukio lile la kinyama.
 
Dar es Salaam. Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameomba kuhakikishiwa mambo sita ili aweze kuanza safari ya kurejea nchini akitokea Ubelgiji anakoishi tangu Januari mwaka 2018.

Lissu, aliyepelekwa kwa matibabu nchini Ubelgiji Januari 2018 baada ya kushambuliwa kwa risasi akitokea bungeni Dodoma Septemba 7, 2017, amelieleza Mwananchi kuwa mambo hayo yakifanyika, akirejea nchini ataishi kwa amani na hatakuwa na wasiwasi.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake, kusamehewa kwa wafungwa wote wa kisiasa, kupewa gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi, kulipwa gharama za matibabu, kupewa mafao yake ya ubunge na kesi zinazomkabili kuangaliwa kwa jicho la pili, akisema amebambikiwa.

Wakati Lissu akieleza hayo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema, “mara ya mwisho ilitolewa taarifa anasubiriwa Lissu aje achukuliwe maelezo yake ila alikataa, kwa maana hiyo uchunguzi haujakamilika. Mtu aliyetendewa kosa akikataa kuja polisi kuandika maelezo hawezi kukamatwa..., anatakiwa aje atoe maelezo yake.”

Mwananchi lilimtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai kuzungumzia suala hilo jana bila mafanikio, lakini mara kadhaa gazeti hili limewahi kumnukuu akisema Lissu alilipwa stahiki zake zote.

Lissu, aliyegombea urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka jana alisema aliporejea nchini na kushiriki uchaguzi huo alikuwa na walinzi, lakini baada ya uchaguzi waliondolewa, hali aliyodai ilitishia usalama wake.

“Nadhani mnakumbuka nilikamatwa nikapelekwa polisi baadaye nikaachiwa na jinsi nilivyoondoka huko, hili jambo na mengine nikihakikishiwa basi nitarejea,” alisema.

Lissu alimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa anaweza kumsaidia katika mambo hayo sita kwa sababu kiongozi huyo alipokuwa makamu wa Rais alikwenda kumjulia hali wakati amelazwa hospitali jijini Nairobi.

Baada ya kushambuliwa Dodoma, Lissu alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu kuanzia Septemba 8 mwaka 2017 hadi Januari 2018 na kati ya waliomtembelea ni Rais Samia wakati huo akiwa makamu wa rais, na kwenye mahojiano na gazeti hili makamu mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kwa kitendo hicho ni wazi kuwa Samia anaweza kumsaidia.

“Nataka nielezwe waliotaka kuniua ni kina nani na nikirudi Tanzania nitakuwa salama kiasi gani.

“Je, nikirudi nitaendelea na kesi na nitakuwa huru kufanya siasa? Vipi kuhusu haki zangu walizokalia, hivi unajua sijalipwa na Bunge, hawakunilipa gratuity (kiinua mgongo),” alisema Lissu.

Akifafanua zaidi kuhusu haki zake bungeni, Lissu alisema alikuwa mbunge kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015 kabla ya kuelezwa kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi Juni mwaka 2019, akisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka hiyo minne hakupata kiinua mgongo.

“Pia wakati naugua sikulipwa gharama za matibabu na katika hili Rais Samia anajua nilikuwa wapi na alikuja kunijulia hali. Kimsingi hili nalo napaswa kupewa majibu ni kwa nini sikulipwa,” alisisitiza.

Mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki mkoani Singida alihoji kuhusu lilipo gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi.

“Kwa nini wameshikilia gari langu wakati hakuna kesi wala uchunguzi wowote uliofanyika tangu niliposhambuliwa.

“Pia kama watawafungulia wafungwa wa kisiasa na kufuta kesi za kisiasa zinazowakabili wengi, nikiwemo mimi, kwa kweli nikipewa majibu ya haya ninarudi nyumbani,” alisema.
Kauli ya polisi

Akieleza zaidi kuhusu suala hilo, Misime alisema: “Kazi ya Jeshi la Polisi Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi ni kulinda maisha ya watu na mali zao. Kubaini, kuzuia kusimamia sheria na kudumisha amani na utengamano. Kulingana na mikakati iliyowekwa hali ya ulinzi na usalama ni amani na utulivu kwa wananchi, wakiwepo na wageni kutoka nchi mbalimbali.

“Hivyo kama kuna mtu anataka kuja

Tanzania, awe raia halali au mgeni anakaribishwa kwa sababu hali ya ulinzi na usalama ni shwari na ya amani kubwa,” alisema.

Misime alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Jeshi la Polisi hutoa ulinzi kwa wananchi wote bila ubaguzi na kama kuna mwenye changamoto za kiusalama ni jukumu lake kutoa taarifa kwa njia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Msimamo wa Ndugai

Aprili mwaka jana, Spika Ndugai alisema Lissu amelipwa mishahara yake yote, ukiwamo wa Juni 2019 ambao anadai hajalipwa.

Alisisitiza kuwa amelipwa zaidi ya Sh200 milioni, posho mbalimbali zaidi ya Sh360 milioni na kwamba amelipwa zaidi ya Sh500 milioni kwa kipindi alichokuwa Ubelgiji. Alieleza hayo mara baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2020/2021.

Mbali na madai hayo, Spika alilitangazia Bunge kuwa Lissu alikuwa na madeni ya Sh70 milioni aliyokopa maeneo mbalimbali kupitia Bunge na kumtaka arejeshe fedha hizo.

Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.


CHANZO: MWANANCHI

GJ Malisa, BAK n MAg3 wanasemaje?😂😂😂

Mungu anamuumbua Lissu, alisema JPM anamuwinda kaondoka

kwani anaogopa kuuliwa na nani??
 
GJ Malisa, BAK n MAg3 wanasemaje?😂😂😂

Mungu anamuumbua Lissu, alisema JPM anamuwinda kaondoka

kwani anaogopa kuuliwa na nani??

..Nani anaweza kutoa amri walinzi waondolewe area D ili kupisha walenga shabaha wamuue TL?

..Na kwanini mtu huyo anakingiwa kifua mpaka leo?
 
..Nani anaweza kutoa amri walinzi waondolewe area D ili kupisha walenga shabaha wamuue TL?

..Na kwanini mtu huyo anakingiwa kifua mpaka leo?

Uko tayari kuambiwa mshaambiwa mwaka wa tatu sasa tatizo hamuelewi

Hata Lissu anajua ukweli wote kabisa na bado watamtafuta tu

Katika dunia ya forces duniani kuna clean cops na dirty cops

waliotaka kumuu Lissu ni wahuni waku kodiwa tu na baadhi ya viongozi wachafu ambao may be walitaka kujikomba kwa JPM na wakashindwa.JPM angetoa amri ya kuuawa yule asingepona...unless haujui capability ya polisi, TISS na jeshi letu...dont think too low kwa emotion

mbona samia nae ashawahi kusema hapa??




JPM anaweza kulaumiwa kukilea hiki kikundi na kutotaka kuchukua hatua, ila hakuna presidential order Lissu auawe, it was bad timing, na nani anaua vile? hakuna snipper?

Kuwa eti cctv ziliondolewa ni utoto sana kwa TZ ambako bado unaweza kwenda kagera ukajifanya daktari na ukapokelewa!!!

wewe unaona Tanzania tuna ulinzi wa maaba kwenye facilities zetu?

why JPM hakuchukua hatua??? hii iko kwa Lossu sasa na tabia zake za ajabu,alipopigwa tu risasi mkasema JPM hapo hapi sio? sasa mlitaka afanye nini tena na mtu alikuwa mbishi vile!!!!?

Tuache hii maada
lissu arudi tu sasa aache mashart

Na kama assumption ya dirty copy haiko sahihi, basi kuna third part, wanamsubiri...yeye anajua hilo, kuwa Lissu hana kabisa maadui wengine wa kutaka kumuua? mwanasheria? think

Mimi naishia hapa mkuu

Revisit your fact taratibu sio kwa muono wa wengi, watu wanakufa kwa risasi moja na sio 16....there was so many technique za kumuua mtu na sio mchana risasi 16..wauaji walitaka sifa kwa nani??? serikali inataka sifa?

Lissu akaenda hospitali, kisha ikulu ikaruhusu aende nairobi sio??😂😂😂😂
 
Kama unaona mazingira sasa ni bora kwako kuishi tz, basi urudi tu, hamna wa kumpa masharti, na siamini kama kunamtu unawasiliana nae hatimize hayo masharti. Kama hali imerejea kuwa shwari njoo, kama haujiamini basi endelea kukaa huko!
 
Uko tayari kuambiwa mshaambiwa mwaka wa tatu sasa tatizo hamuelewi

Hata Lissu anajua ukweli wote kabisa na bado watamtafuta tu

Katika dunia ya forces duniani kuna clean cops na dirty cops

waliotaka kumuu Lissu ni wahuni waku kodiwa tu na baadhi ya viongozi wachafu ambao may be walitaka kujikomba kwa JPM na wakashindwa.JPM angetoa amri ya kuuawa yule asingepona...unless haujui capability ya polisi, TISS na jeshi letu...dont think too low kwa emotion

mbona samia nae ashawahi kusema hapa??




JPM anaweza kulaumiwa kukilea hiki kikundi na kutotaka kuchukua hatua, ila hakuna presidential order Lissu auawe, it was bad timing, na nani anaua vile? hakuna snipper?

Kuwa eti cctv ziliondolewa ni utoto sana kwa TZ ambako bado unaweza kwenda kagera ukajifanya daktari na ukapokelewa!!!

wewe unaona Tanzania tuna ulinzi wa maaba kwenye facilities zetu?

why JPM hakuchukua hatua??? hii iko kwa Lossu sasa na tabia zake za ajabu,alipopigwa tu risasi mkasema JPM hapo hapi sio? sasa mlitaka afanye nini tena na mtu alikuwa mbishi vile!!!!?

Tuache hii maada
lissu arudi tu sasa aache mashart

Na kama assumption ya dirty copy haiko sahihi, basi kuna third part, wanamsubiri...yeye anajua hilo, kuwa Lissu hana kabisa maadui wengine wa kutaka kumuua? mwanasheria? think

Mimi naishia hapa mkuu

Revisit your fact taratibu sio kwa muono wa wengi, watu wanakufa kwa risasi moja na sio 16....there was so many technique za kumuua mtu na sio mchana risasi 16..wauaji walitaka sifa kwa nani??? serikali inataka sifa?

Lissu akaenda hospitali, kisha ikulu ikaruhusu aende nairobi sio??😂😂😂😂


..maelezo yako ni very thoughful.

..tukio lolote linalofanywa na wanadamu lina chances fulani za ku-fail.

..huwezi kuchukulia kufeli kwa tukio lile kama kigezo cha ku-rule out au kuwahusisha watu fulani fulani.

..hujawahi kusikia daktari mahiri bingwa anayesifika aliyeokoa magonjwa wa kila aina akafanya kosa lisilotarajiwa ktk kazi yake?

..hujawahi kusikia taasisi kubwa mahiri duniani kwa ufanisi zimefanya makosa ktk shughuli zake?

..maelezo ya Mama Samia yalilenga hadhira aliyokuwa akizungumza nayo. Mimi na wewe tuna uwezo wa kufikiria na kuchambua kwa mapana na marefu zaidi.

..waliohusika na tukio lile wanasutwa na FACT moja ndogo, lakini muhimu sana.

..Ni nani aliondoa walinzi wa area D? Alitumwa na nani? Kwanini anakingiwa kifua?

NB.

..kuhusu ndege kuruhusiwa kwenda Nairobi, walijua ule ni mzoga utawafia njiani, lakini MUNGU aliamua vingine.

Cc Mmawia
 
Dar es Salaam. Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameomba kuhakikishiwa mambo sita ili aweze kuanza safari ya kurejea nchini akitokea Ubelgiji anakoishi tangu Januari mwaka 2018.

Lissu, aliyepelekwa kwa matibabu nchini Ubelgiji Januari 2018 baada ya kushambuliwa kwa risasi akitokea bungeni Dodoma Septemba 7, 2017, amelieleza Mwananchi kuwa mambo hayo yakifanyika, akirejea nchini ataishi kwa amani na hatakuwa na wasiwasi.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake, kusamehewa kwa wafungwa wote wa kisiasa, kupewa gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi, kulipwa gharama za matibabu, kupewa mafao yake ya ubunge na kesi zinazomkabili kuangaliwa kwa jicho la pili, akisema amebambikiwa.

Wakati Lissu akieleza hayo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema, “mara ya mwisho ilitolewa taarifa anasubiriwa Lissu aje achukuliwe maelezo yake ila alikataa, kwa maana hiyo uchunguzi haujakamilika. Mtu aliyetendewa kosa akikataa kuja polisi kuandika maelezo hawezi kukamatwa..., anatakiwa aje atoe maelezo yake.”

Mwananchi lilimtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai kuzungumzia suala hilo jana bila mafanikio, lakini mara kadhaa gazeti hili limewahi kumnukuu akisema Lissu alilipwa stahiki zake zote.

Lissu, aliyegombea urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka jana alisema aliporejea nchini na kushiriki uchaguzi huo alikuwa na walinzi, lakini baada ya uchaguzi waliondolewa, hali aliyodai ilitishia usalama wake.

“Nadhani mnakumbuka nilikamatwa nikapelekwa polisi baadaye nikaachiwa na jinsi nilivyoondoka huko, hili jambo na mengine nikihakikishiwa basi nitarejea,” alisema.

Lissu alimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa anaweza kumsaidia katika mambo hayo sita kwa sababu kiongozi huyo alipokuwa makamu wa Rais alikwenda kumjulia hali wakati amelazwa hospitali jijini Nairobi.

Baada ya kushambuliwa Dodoma, Lissu alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu kuanzia Septemba 8 mwaka 2017 hadi Januari 2018 na kati ya waliomtembelea ni Rais Samia wakati huo akiwa makamu wa rais, na kwenye mahojiano na gazeti hili makamu mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kwa kitendo hicho ni wazi kuwa Samia anaweza kumsaidia.

“Nataka nielezwe waliotaka kuniua ni kina nani na nikirudi Tanzania nitakuwa salama kiasi gani.

“Je, nikirudi nitaendelea na kesi na nitakuwa huru kufanya siasa? Vipi kuhusu haki zangu walizokalia, hivi unajua sijalipwa na Bunge, hawakunilipa gratuity (kiinua mgongo),” alisema Lissu.

Akifafanua zaidi kuhusu haki zake bungeni, Lissu alisema alikuwa mbunge kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015 kabla ya kuelezwa kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi Juni mwaka 2019, akisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka hiyo minne hakupata kiinua mgongo.

“Pia wakati naugua sikulipwa gharama za matibabu na katika hili Rais Samia anajua nilikuwa wapi na alikuja kunijulia hali. Kimsingi hili nalo napaswa kupewa majibu ni kwa nini sikulipwa,” alisisitiza.

Mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki mkoani Singida alihoji kuhusu lilipo gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi.

“Kwa nini wameshikilia gari langu wakati hakuna kesi wala uchunguzi wowote uliofanyika tangu niliposhambuliwa.

“Pia kama watawafungulia wafungwa wa kisiasa na kufuta kesi za kisiasa zinazowakabili wengi, nikiwemo mimi, kwa kweli nikipewa majibu ya haya ninarudi nyumbani,” alisema.
Kauli ya polisi

Akieleza zaidi kuhusu suala hilo, Misime alisema: “Kazi ya Jeshi la Polisi Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi ni kulinda maisha ya watu na mali zao. Kubaini, kuzuia kusimamia sheria na kudumisha amani na utengamano. Kulingana na mikakati iliyowekwa hali ya ulinzi na usalama ni amani na utulivu kwa wananchi, wakiwepo na wageni kutoka nchi mbalimbali.

“Hivyo kama kuna mtu anataka kuja

Tanzania, awe raia halali au mgeni anakaribishwa kwa sababu hali ya ulinzi na usalama ni shwari na ya amani kubwa,” alisema.

Misime alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Jeshi la Polisi hutoa ulinzi kwa wananchi wote bila ubaguzi na kama kuna mwenye changamoto za kiusalama ni jukumu lake kutoa taarifa kwa njia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Msimamo wa Ndugai

Aprili mwaka jana, Spika Ndugai alisema Lissu amelipwa mishahara yake yote, ukiwamo wa Juni 2019 ambao anadai hajalipwa.

Alisisitiza kuwa amelipwa zaidi ya Sh200 milioni, posho mbalimbali zaidi ya Sh360 milioni na kwamba amelipwa zaidi ya Sh500 milioni kwa kipindi alichokuwa Ubelgiji. Alieleza hayo mara baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2020/2021.

Mbali na madai hayo, Spika alilitangazia Bunge kuwa Lissu alikuwa na madeni ya Sh70 milioni aliyokopa maeneo mbalimbali kupitia Bunge na kumtaka arejeshe fedha hizo.

Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.


CHANZO: MWANANCHI
We baki huko huko,maana nchi kama nchi haikuitajii kiivyo
 
yaani unatoa na masharti unadhani Samia ni mkeo?

kwa hio yasipotimia unazira kurudi Tanzania tukome kabisa?
 
Kwani huyo lisu anajiona nani hasa hadi ampangie vya kufanyiwa ndo arudi? kwani kuna mtu kamuita au alivokaa huko miaka yote jua halikuwaka TZ au mvua haikunyesha?

Ikiwezekana kae huko na afie huko hakuna amtakae. Waswahili wanakwambia ukitaka kudeka hakikisha yupo wa kukudekeza, sasa asilazimishe kudekezwa. Akitaka arudi apambane na hali yake kama hatak abaki huko, mxiuuuu
Acha upumbavu wako. Huyo ni mtu anatejijua na siyo mjinga kama wewe ambaye unaweza kugeuzwa upande wowote kwa sababu unadhani wewe siyo chochote.
 
Lissu anaongea kama mtu aliyeshika switch ya tanesco, kwamba akishindwa kurudi anazima umeme nchi nzima
Kuna watu wajinga sana. Na wewe ni mmoja wapo. Unadhani mpaka uwe na uwezo wa kumfanyia mtu jambo fulani ndiyo utadai haki zako? Ndiyo maana mnagezwa kama nyumbu kwa sababu mnadhani hamna cha kuwafanya wanaowageuza.
 
Dar es Salaam. Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameomba kuhakikishiwa mambo sita ili aweze kuanza safari ya kurejea nchini akitokea Ubelgiji anakoishi tangu Januari mwaka 2018.

Lissu, aliyepelekwa kwa matibabu nchini Ubelgiji Januari 2018 baada ya kushambuliwa kwa risasi akitokea bungeni Dodoma Septemba 7, 2017, amelieleza Mwananchi kuwa mambo hayo yakifanyika, akirejea nchini ataishi kwa amani na hatakuwa na wasiwasi.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake, kusamehewa kwa wafungwa wote wa kisiasa, kupewa gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi, kulipwa gharama za matibabu, kupewa mafao yake ya ubunge na kesi zinazomkabili kuangaliwa kwa jicho la pili, akisema amebambikiwa.

Wakati Lissu akieleza hayo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema, “mara ya mwisho ilitolewa taarifa anasubiriwa Lissu aje achukuliwe maelezo yake ila alikataa, kwa maana hiyo uchunguzi haujakamilika. Mtu aliyetendewa kosa akikataa kuja polisi kuandika maelezo hawezi kukamatwa..., anatakiwa aje atoe maelezo yake.”

Mwananchi lilimtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai kuzungumzia suala hilo jana bila mafanikio, lakini mara kadhaa gazeti hili limewahi kumnukuu akisema Lissu alilipwa stahiki zake zote.

Lissu, aliyegombea urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka jana alisema aliporejea nchini na kushiriki uchaguzi huo alikuwa na walinzi, lakini baada ya uchaguzi waliondolewa, hali aliyodai ilitishia usalama wake.

“Nadhani mnakumbuka nilikamatwa nikapelekwa polisi baadaye nikaachiwa na jinsi nilivyoondoka huko, hili jambo na mengine nikihakikishiwa basi nitarejea,” alisema.

Lissu alimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa anaweza kumsaidia katika mambo hayo sita kwa sababu kiongozi huyo alipokuwa makamu wa Rais alikwenda kumjulia hali wakati amelazwa hospitali jijini Nairobi.

Baada ya kushambuliwa Dodoma, Lissu alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu kuanzia Septemba 8 mwaka 2017 hadi Januari 2018 na kati ya waliomtembelea ni Rais Samia wakati huo akiwa makamu wa rais, na kwenye mahojiano na gazeti hili makamu mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kwa kitendo hicho ni wazi kuwa Samia anaweza kumsaidia.

“Nataka nielezwe waliotaka kuniua ni kina nani na nikirudi Tanzania nitakuwa salama kiasi gani.

“Je, nikirudi nitaendelea na kesi na nitakuwa huru kufanya siasa? Vipi kuhusu haki zangu walizokalia, hivi unajua sijalipwa na Bunge, hawakunilipa gratuity (kiinua mgongo),” alisema Lissu.

Akifafanua zaidi kuhusu haki zake bungeni, Lissu alisema alikuwa mbunge kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015 kabla ya kuelezwa kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi Juni mwaka 2019, akisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka hiyo minne hakupata kiinua mgongo.

“Pia wakati naugua sikulipwa gharama za matibabu na katika hili Rais Samia anajua nilikuwa wapi na alikuja kunijulia hali. Kimsingi hili nalo napaswa kupewa majibu ni kwa nini sikulipwa,” alisisitiza.

Mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki mkoani Singida alihoji kuhusu lilipo gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi.

“Kwa nini wameshikilia gari langu wakati hakuna kesi wala uchunguzi wowote uliofanyika tangu niliposhambuliwa.

“Pia kama watawafungulia wafungwa wa kisiasa na kufuta kesi za kisiasa zinazowakabili wengi, nikiwemo mimi, kwa kweli nikipewa majibu ya haya ninarudi nyumbani,” alisema.
Kauli ya polisi

Akieleza zaidi kuhusu suala hilo, Misime alisema: “Kazi ya Jeshi la Polisi Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi ni kulinda maisha ya watu na mali zao. Kubaini, kuzuia kusimamia sheria na kudumisha amani na utengamano. Kulingana na mikakati iliyowekwa hali ya ulinzi na usalama ni amani na utulivu kwa wananchi, wakiwepo na wageni kutoka nchi mbalimbali.

“Hivyo kama kuna mtu anataka kuja

Tanzania, awe raia halali au mgeni anakaribishwa kwa sababu hali ya ulinzi na usalama ni shwari na ya amani kubwa,” alisema.

Misime alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Jeshi la Polisi hutoa ulinzi kwa wananchi wote bila ubaguzi na kama kuna mwenye changamoto za kiusalama ni jukumu lake kutoa taarifa kwa njia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Msimamo wa Ndugai

Aprili mwaka jana, Spika Ndugai alisema Lissu amelipwa mishahara yake yote, ukiwamo wa Juni 2019 ambao anadai hajalipwa.

Alisisitiza kuwa amelipwa zaidi ya Sh200 milioni, posho mbalimbali zaidi ya Sh360 milioni na kwamba amelipwa zaidi ya Sh500 milioni kwa kipindi alichokuwa Ubelgiji. Alieleza hayo mara baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2020/2021.

Mbali na madai hayo, Spika alilitangazia Bunge kuwa Lissu alikuwa na madeni ya Sh70 milioni aliyokopa maeneo mbalimbali kupitia Bunge na kumtaka arejeshe fedha hizo.

Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.


CHANZO: MWANANCHI
Urudi kuijenga nchi yetu, ndugu yetu Lissu, Mama Samia hataki dhuruma na matendo yeyote ya kukanyaga demokrasia, zaidi anawahitaji sana great thinkers of your nature. Nilitamani uwepo ktk kikao na wapinzani ambacho amekisema ktk hotuba yake.
 
Kuhusu malipo ya Tundu Lissu kama posho na stahiki zake mbalimbali kwa mujibu wa Spika Ndugai, kuna maswali yanahitaji majibu;

1. Ndugai anasema Tundu keshalipwa

- Tshs. 200,000,000 (za nini?Haijulikani...!!)

  • Tshs. 360,000,000 (za mini? Haijulikani...!!)
  • Tshs. 500,000,000 (za mini? Haijulikani...!!
...............................................................
JUMLA Tshs. 1,060,000,000 (billion moja na sitini milioni..!!!)
................................................................

2. Je, Spika Ndugai anaweza kutoa uthibitisho Wa malipo haya kutoka Bunge kwenda kwa Tundu Lissu ili kukata mzizi Wa fitina..??

3. Kama Tundu Lissu amelipwa pesa zote hizi na serikali kupitia Bunge, iweje bado analalamika kudhulumiwa mafao na haki yake ya kulipiwa gharama za matibabu..??

4. Je Spika Ndugai anaweza kutoa mchanganuo wa pesa zote alizolipwa Tundu Lissu ni kwa ajili ya nini?

NB:
Mimi naamini mambo mawili juu ya sakata hili;

MOSI: fedha za mafao, gharama za matibabu, posho na mishahara ya Tundu Lissu kuanzia Septemba, 2017 hadi ukomo wa bunge la 11 zimelipwa lakini hazijaenda kwa muhusika..!

PILI; Spika Ndugai anaweza kuwa sahihi kwa sababu yeye (inawezekana) anapokea taarifa tu za utekelezaji na kisha kuzitetea tu bila kujiridhisha kuwa zina ukweli. Hapa tunaweza kusema (labda) anacheza ngoma ya watu wengine...!

TATU; Tundu Lissu, binafsi, naamini hawezi kudai pesa mara mbili huku akitambua kuwa ameshalipwa..!

NNE; Kama Spika anadai Lissu alishalipwa Tshs. bilini 1.06 halafu wakati huohuo muhusika anasema hajapokea hata senti, hapa inakuwa na maana gani hasa..?

Je, kuna uwezekano kuna ufisadi wa fedha bungeni kwa kutumia kivuli cha ugonjwa na kuvuliwa kwa ubunge wa Tundu Lissu...?

Uchunguzi ufanyike tu...
Aweke risiti tuzione.
 
Lisu ni nani mpaka anaweka masharti ya namna hiyo,anaumuhimu upi kwenye taifa letu mpaka atuwekee masharti?
Akae huko atumtaki hana jipya.
Kamuulize dereva aliyetumbukia mtaroni na roli, anaujua mchakamchaka aliomkimbiza kikamanda nyakati za kampeni.
 
Hata shujaa alikua kwenye dozi ya Lithium au umesahau alikua na bipolar ?
 
Ukomavu n kusimamia haki za wengine akiwemo na yeye,kwa nilivyoelewa,kesi za wafungwa kwa makosa ya kisiasa(kipindi cha kampeni & uchaguzi mkuu),watu wamebambikiwa.
Tatizo Lissu anaamrisha kuwa yafanywe hayo yasipofanywa yeye haludi ndio tunapojiuliza yeye ni nani mpaka atoe amri kama hiyo?

Rais Samia mpaka sasa ameshaonyesha kutaka maridhiano na ndio maana yupo tayari kukaa na viongozi wa vyama vya upinzani na kutatua baadhi ya kero ili Nchi ifanye siasa za kistaarabu tofauti na utawala uliopita

Sasa yeye anapoibuka huko alipo na kutoa masharti yake kwa Rais maana yake nini? Amwache Mheshimiwa kwanza afanye mambo yake pale tutakapomuona Mheshimiwa anakosea ndio aanze kubwabwaja ila kwa sasa ni kama anatupigia kelele na kutaka kumtoa Mama kwenye njia
 
Back
Top Bottom