Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Lissu: Nitarejea Tanzania endapo yafuatayo yatafanyika

Mimi nilikuwa shabiki mkubwa wa Tundu Lissu lakini lazima niseme ukweli ulio moyoni mwangu huyu jamaa amefeli kisiasa kabisa hakuwa na mipango mizuri wala mshauri mzuri., Kwa sababu kama haya anayodai sasa kuhakikishiwa usalama wake ndio aje swali ni mbona uchaguzi alikuja hivyo hivyo kugombea hakujali kuhakikishiwa usalama wala chochote alikuja tu,

Ulipomaliza uchaguzi akadai anataka kuuliwa na mtu aliyemtumia sms akakimbilia ubalozi lakini mbona hakukua na na chochote ule mpango kama ulipita na upepo tu wala hakuna anayezungumza tena sio nje huko aliko wala Tz ni kama vile alijaribu kutaka kutengeneza issue lakini haikuwa na vidhibiti angalau vimuweke katika mazingira mazuri zaidi, alifeli

Umemaliza uchaguzi hakuvumilia ata wiki moja kuonyesha wapiga kura wake kote alikotembelea angalau kuwambia chochote, alienda ubalozi na kutimkia belgium na hata alipofika kule belgum hakuwambia chochote wanachadema ni kama vile alikuja kwa shida ya kusaka urais tu bas ndio iliyokuwa shida yake hakujali wananchi wake., sijuwi alifeli wapi angalau angemsoma maalim seif na vitisho alivyofanyiwa lakini hakuwa mbali na wazanzibari.

Ile kupigwa risasi ilitokea lakini je kwa dunia ilivyoliona lile kweli angepigwa tena marisasi kiongozi aliyetoka kugombea urais?

Huko youtube na twitter anaona ndio jukwaa lake la kisiasa anadhan inatosha? Watanzania wangap hawaelewi twitter wala youtube, jana tumeambiwa watu milioni 8 tu tanzania ndio wanaotumia internet hawa watu wengi waliobaki atawafikia vipi kwa twitter na youtube?

Ndio mana nimesema amefeli sana

..Lissu ni mwanasheria, na maamuzi yake mengi huyafanya kwa jicho la kisheria. wakati wa uchaguzi sheria zetu zinalaelekeza kwamba wagombea wote wa Uraisi ni lazima wapewe ulinzi wa jeshi la Polisi. Lissu alirejea kwasababu alijua hakuna namna serikali ingeweza kukwepa jukumu la kumlinda wakati akiwa mgombea Uraisi.

..kuhusu tishio la kutaka kuuwawa baada ya uchaguzi mkuu, sidhani kama ni sahihi kumlaumu kwamba halina ushahidi. kwa upande mwingine tunapaswa kuilaumu serikali kwa kutokuchunguza tukio la mauaji dhidi ya Tundu Lissu ambalo lina ushahidi wa wazi kabisa. Labda tungejiuliza, ni nchi gani nyingine ambayo kiongozi mwandamizi wa kisiasa anashambuliwa halafu serikali inapuuzia kufanya uchunguzi?

..kuhusu kufanya siasa ktk mtandao nakuomba ufanye utafiti mpya. kama madai yako kuwa watumiaji wa mitandao Tz ni watu milioni 8 ni ya kweli, basi bila shaka mitandao ni uwanja muhimu wa kufanya siasa. ripoti za tume ya uchaguzi zinasema waTz takriban million 15+ walipiga kura ktk uchaguzi wa 2020, hivyo basi zaidi ya nusu ya Watz hao huenda wanatumia mitandao. Kwa msingi huo mwanasiasa yeyote makini hapa Tz lazima ajishughulishe ktk mitandao ya kijamii.
 
Dar es Salaam. Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameomba kuhakikishiwa mambo sita ili aweze kuanza safari ya kurejea nchini akitokea Ubelgiji anakoishi tangu Januari mwaka 2018.

Lissu, aliyepelekwa kwa matibabu nchini Ubelgiji Januari 2018 baada ya kushambuliwa kwa risasi akitokea bungeni Dodoma Septemba 7, 2017, amelieleza Mwananchi kuwa mambo hayo yakifanyika, akirejea nchini ataishi kwa amani na hatakuwa na wasiwasi.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake, kusamehewa kwa wafungwa wote wa kisiasa, kupewa gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi, kulipwa gharama za matibabu, kupewa mafao yake ya ubunge na kesi zinazomkabili kuangaliwa kwa jicho la pili, akisema amebambikiwa.

Wakati Lissu akieleza hayo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema, “mara ya mwisho ilitolewa taarifa anasubiriwa Lissu aje achukuliwe maelezo yake ila alikataa, kwa maana hiyo uchunguzi haujakamilika. Mtu aliyetendewa kosa akikataa kuja polisi kuandika maelezo hawezi kukamatwa..., anatakiwa aje atoe maelezo yake.”

Mwananchi lilimtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai kuzungumzia suala hilo jana bila mafanikio, lakini mara kadhaa gazeti hili limewahi kumnukuu akisema Lissu alilipwa stahiki zake zote.

Lissu, aliyegombea urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka jana alisema aliporejea nchini na kushiriki uchaguzi huo alikuwa na walinzi, lakini baada ya uchaguzi waliondolewa, hali aliyodai ilitishia usalama wake.

“Nadhani mnakumbuka nilikamatwa nikapelekwa polisi baadaye nikaachiwa na jinsi nilivyoondoka huko, hili jambo na mengine nikihakikishiwa basi nitarejea,” alisema.

Lissu alimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa anaweza kumsaidia katika mambo hayo sita kwa sababu kiongozi huyo alipokuwa makamu wa Rais alikwenda kumjulia hali wakati amelazwa hospitali jijini Nairobi.

Baada ya kushambuliwa Dodoma, Lissu alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu kuanzia Septemba 8 mwaka 2017 hadi Januari 2018 na kati ya waliomtembelea ni Rais Samia wakati huo akiwa makamu wa rais, na kwenye mahojiano na gazeti hili makamu mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kwa kitendo hicho ni wazi kuwa Samia anaweza kumsaidia.

“Nataka nielezwe waliotaka kuniua ni kina nani na nikirudi Tanzania nitakuwa salama kiasi gani.

“Je, nikirudi nitaendelea na kesi na nitakuwa huru kufanya siasa? Vipi kuhusu haki zangu walizokalia, hivi unajua sijalipwa na Bunge, hawakunilipa gratuity (kiinua mgongo),” alisema Lissu.

Akifafanua zaidi kuhusu haki zake bungeni, Lissu alisema alikuwa mbunge kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015 kabla ya kuelezwa kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi Juni mwaka 2019, akisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka hiyo minne hakupata kiinua mgongo.

“Pia wakati naugua sikulipwa gharama za matibabu na katika hili Rais Samia anajua nilikuwa wapi na alikuja kunijulia hali. Kimsingi hili nalo napaswa kupewa majibu ni kwa nini sikulipwa,” alisisitiza.

Mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki mkoani Singida alihoji kuhusu lilipo gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi.

“Kwa nini wameshikilia gari langu wakati hakuna kesi wala uchunguzi wowote uliofanyika tangu niliposhambuliwa.

“Pia kama watawafungulia wafungwa wa kisiasa na kufuta kesi za kisiasa zinazowakabili wengi, nikiwemo mimi, kwa kweli nikipewa majibu ya haya ninarudi nyumbani,” alisema.
Kauli ya polisi

Akieleza zaidi kuhusu suala hilo, Misime alisema: “Kazi ya Jeshi la Polisi Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi ni kulinda maisha ya watu na mali zao. Kubaini, kuzuia kusimamia sheria na kudumisha amani na utengamano. Kulingana na mikakati iliyowekwa hali ya ulinzi na usalama ni amani na utulivu kwa wananchi, wakiwepo na wageni kutoka nchi mbalimbali.

“Hivyo kama kuna mtu anataka kuja

Tanzania, awe raia halali au mgeni anakaribishwa kwa sababu hali ya ulinzi na usalama ni shwari na ya amani kubwa,” alisema.

Misime alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Jeshi la Polisi hutoa ulinzi kwa wananchi wote bila ubaguzi na kama kuna mwenye changamoto za kiusalama ni jukumu lake kutoa taarifa kwa njia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Msimamo wa Ndugai

Aprili mwaka jana, Spika Ndugai alisema Lissu amelipwa mishahara yake yote, ukiwamo wa Juni 2019 ambao anadai hajalipwa.

Alisisitiza kuwa amelipwa zaidi ya Sh200 milioni, posho mbalimbali zaidi ya Sh360 milioni na kwamba amelipwa zaidi ya Sh500 milioni kwa kipindi alichokuwa Ubelgiji. Alieleza hayo mara baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2020/2021.

Mbali na madai hayo, Spika alilitangazia Bunge kuwa Lissu alikuwa na madeni ya Sh70 milioni aliyokopa maeneo mbalimbali kupitia Bunge na kumtaka arejeshe fedha hizo.

Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.


CHANZO: MWANANCHI
Kwani ye Lissu ndio nani mpaka apangie nchi masharti ya kurudi unyankindi kwao, kama hataki kurudi aendelee na mumewe huko
 
mkuu nashukuru kwa maelezo mazuri pia

Ila nimesema maada hii ni outdated now

CDM wanajua kila kitu na waweke wazi sasa kila kitu ...kuna demokrasia sasa sio? issue ya mwaka juzi tu

Ninaposema wanajua, sitanii waanike
1. Let me believe that, unaposema CDM una maana ya CHADEMA, right...?

2. Kama una maana ya CHADEMA, basi, hebu na wewe tusaidie kidogo.

Una maana gani unaposema CHADEMA "wanajua" na "hutanii..?"
å Na wanajua nini..?

å Je, una maana ya kuwa wanawajua waliompiga Tundu Lissu risasi 38 na 16 kuingia mwilini mwake?

√• Je, una maàna ya kuwa, CHADEMA wanawajua waliotoa CCTV camera na walinzi kwenye makazi ya viongozi wakubwa serikalini Area "D" akiwemo Naibu Spika Tulia, Waziri wa Nishati Kalemani nk nk? Wanawajua? Really? Kwa hiyo unawaambia CHADEMA wafanye kazi ya uPolisi..?

NA WEWE WABEROYA HEBU JIBU MASWALI HAYA:

1. Wewe unadhani ni kwanini polisi hawafanyii kazi jinai hii ya jaribio la kuuwawa kwa TL..?

2. Kama unadhani CHADEMA wanaweza kuwa na taarifa muhimu sana juu ya sakata zima la jaribio la kuuwawa kwa TL mwaka 2017, kwanini polisi wasifanye kazi yao? Hata kama wanazo "hizo taarifa na hutanii" wampe nani sasa maana polisi wamezuiwa au hawataki kabisa kuchunguza..?

3. Kwa scenario hii, hivi unategemea mimi na wewe tuielewe vipi serikali kupitia Jeshi la polisi..? There is no other way zaidi ya kusema kuwa, kumbe ni halali kabisa kwa serikali kupitia Jeshi la polisi kushutumiwa kuwa inalinda wahalifu waliohusika ktk unyama huu...!

Na hapa naomba unielewe kuwa, ninaposema, inalinda wahalifu basi nina maanisha wahalifu kweli bila kujali ni kina nani aidha wawe ni CHADEMA, CCM au wewe mwenyewe Waberoya. Polisi wafanye kazi yao. That's all...!!

4. Na Je, wewe nawe Waberoya unaamini kuwa serikali kupitia Jeshi la polisi linashindwa kufanya upelelezi wa tukio/kesi hii kwa sababu ya assumption ya kuwa eti "CHADEMA wamemficha Ubelgiji" aliyekuwa dereva wa Tundu Lissu..??

Kama unaamini ujinga huu, basi wewe hufai kuitwa GT...!!
 
Hayo mambo yanatekelezeka maccm yanaona shida gani kurudisha gari ,stahiki za kibunge na kufuta kesi za kubambikizwa za kisiasa
 
Dar es Salaam. Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu ameomba kuhakikishiwa mambo sita ili aweze kuanza safari ya kurejea nchini akitokea Ubelgiji anakoishi tangu Januari mwaka 2018.

Lissu, aliyepelekwa kwa matibabu nchini Ubelgiji Januari 2018 baada ya kushambuliwa kwa risasi akitokea bungeni Dodoma Septemba 7, 2017, amelieleza Mwananchi kuwa mambo hayo yakifanyika, akirejea nchini ataishi kwa amani na hatakuwa na wasiwasi.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake, kusamehewa kwa wafungwa wote wa kisiasa, kupewa gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi, kulipwa gharama za matibabu, kupewa mafao yake ya ubunge na kesi zinazomkabili kuangaliwa kwa jicho la pili, akisema amebambikiwa.

Wakati Lissu akieleza hayo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime amesema, “mara ya mwisho ilitolewa taarifa anasubiriwa Lissu aje achukuliwe maelezo yake ila alikataa, kwa maana hiyo uchunguzi haujakamilika. Mtu aliyetendewa kosa akikataa kuja polisi kuandika maelezo hawezi kukamatwa..., anatakiwa aje atoe maelezo yake.”

Mwananchi lilimtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai kuzungumzia suala hilo jana bila mafanikio, lakini mara kadhaa gazeti hili limewahi kumnukuu akisema Lissu alilipwa stahiki zake zote.

Lissu, aliyegombea urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka jana alisema aliporejea nchini na kushiriki uchaguzi huo alikuwa na walinzi, lakini baada ya uchaguzi waliondolewa, hali aliyodai ilitishia usalama wake.

“Nadhani mnakumbuka nilikamatwa nikapelekwa polisi baadaye nikaachiwa na jinsi nilivyoondoka huko, hili jambo na mengine nikihakikishiwa basi nitarejea,” alisema.

Lissu alimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kuwa anaweza kumsaidia katika mambo hayo sita kwa sababu kiongozi huyo alipokuwa makamu wa Rais alikwenda kumjulia hali wakati amelazwa hospitali jijini Nairobi.

Baada ya kushambuliwa Dodoma, Lissu alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu kuanzia Septemba 8 mwaka 2017 hadi Januari 2018 na kati ya waliomtembelea ni Rais Samia wakati huo akiwa makamu wa rais, na kwenye mahojiano na gazeti hili makamu mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kwa kitendo hicho ni wazi kuwa Samia anaweza kumsaidia.

“Nataka nielezwe waliotaka kuniua ni kina nani na nikirudi Tanzania nitakuwa salama kiasi gani.

“Je, nikirudi nitaendelea na kesi na nitakuwa huru kufanya siasa? Vipi kuhusu haki zangu walizokalia, hivi unajua sijalipwa na Bunge, hawakunilipa gratuity (kiinua mgongo),” alisema Lissu.

Akifafanua zaidi kuhusu haki zake bungeni, Lissu alisema alikuwa mbunge kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015 kabla ya kuelezwa kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi Juni mwaka 2019, akisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka hiyo minne hakupata kiinua mgongo.

“Pia wakati naugua sikulipwa gharama za matibabu na katika hili Rais Samia anajua nilikuwa wapi na alikuja kunijulia hali. Kimsingi hili nalo napaswa kupewa majibu ni kwa nini sikulipwa,” alisisitiza.

Mbunge huyo wa zamani wa Singida Mashariki mkoani Singida alihoji kuhusu lilipo gari lake alilokuwa amepanda siku anashambuliwa kwa risasi.

“Kwa nini wameshikilia gari langu wakati hakuna kesi wala uchunguzi wowote uliofanyika tangu niliposhambuliwa.

“Pia kama watawafungulia wafungwa wa kisiasa na kufuta kesi za kisiasa zinazowakabili wengi, nikiwemo mimi, kwa kweli nikipewa majibu ya haya ninarudi nyumbani,” alisema.
Kauli ya polisi

Akieleza zaidi kuhusu suala hilo, Misime alisema: “Kazi ya Jeshi la Polisi Tanzania kwa mujibu wa sheria za nchi ni kulinda maisha ya watu na mali zao. Kubaini, kuzuia kusimamia sheria na kudumisha amani na utengamano. Kulingana na mikakati iliyowekwa hali ya ulinzi na usalama ni amani na utulivu kwa wananchi, wakiwepo na wageni kutoka nchi mbalimbali.

“Hivyo kama kuna mtu anataka kuja

Tanzania, awe raia halali au mgeni anakaribishwa kwa sababu hali ya ulinzi na usalama ni shwari na ya amani kubwa,” alisema.

Misime alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Jeshi la Polisi hutoa ulinzi kwa wananchi wote bila ubaguzi na kama kuna mwenye changamoto za kiusalama ni jukumu lake kutoa taarifa kwa njia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Msimamo wa Ndugai

Aprili mwaka jana, Spika Ndugai alisema Lissu amelipwa mishahara yake yote, ukiwamo wa Juni 2019 ambao anadai hajalipwa.

Alisisitiza kuwa amelipwa zaidi ya Sh200 milioni, posho mbalimbali zaidi ya Sh360 milioni na kwamba amelipwa zaidi ya Sh500 milioni kwa kipindi alichokuwa Ubelgiji. Alieleza hayo mara baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2020/2021.

Mbali na madai hayo, Spika alilitangazia Bunge kuwa Lissu alikuwa na madeni ya Sh70 milioni aliyokopa maeneo mbalimbali kupitia Bunge na kumtaka arejeshe fedha hizo.

Hata hivyo, alisema kama angeendelea, wangekwenda mbali zaidi na kuhoji jinsi alivyotumia fedha za wananchi, mishahara ya dereva wake na mafuta ya kumpeleka jimboni wakati akijua anazitumia isivyo halali kwa sababu yupo nje ya nchi, jambo ambalo lingemletea shida kwa kutakiwa kuzirudisha.


CHANZO: MWANANCHI
🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hayo mambo yanatekelezeka maccm yanaona shida gani kurudisha gari ,stahiki za kibunge na kufuta kesi za kubambikizwa za kisiasa
Abaki huko huko huku hatumtaki, kwanza aliowatapeli na kumfanyizia bado wako mtaani, akae huko huko kwa usalama wake...
 
Bana abaki huko huko, mbona kuna raha kule za kufa mtu, vipi anafuata makorona, mbu, uchafu, miundo mbinu hovyo, huduma za afya hovyo na nini na nini?
Kumbe nyumbani kutamu eeehhhh?!
 
Anataka tumsamehe na ile aliyomwambia Shaka Ssali wa VOA kuwa mlinzi wa Rais alifariki kwa Corona akijua anasema uongo?
 
Tundu Lisu, pamoja na mengine yote, usilotakiwa kulisahau kunena wakati wote, ni ukuu na uweza wa Mungu:

Mtu anaamua kukuua, unashambuliwa kwa risasi 16, yaani kuhakikisha kwa vyovyote iwavyo ufe, halafu hufi. Anaamua kukunyima matibabu ili ufe, hufi. Anaamua kukunyima pesa stahiki yako ili ushindwe kuishi, lakini unaishi.

Mwishowe, yule aliyeamua kukua, aliyeamua wewe usiishi, anakufa yeye, nawe unashuhudia na kutangaza kifo chake kabla hata ya watu wake wa karibu, wewe unaendelea kuishi. Fumbo hili ni kubwa sana katika maisha ya kiimani.
 
Nini lengo la Tundu Lissu hasa? Tujaalie Serikali imepuuza kabisa kuhusu suala lake la kwamba lazima ahakikishiwe ulinzi ndio arejee nchini au mpaka stahiki zake apewe za matibabu na maposho yake pamoja na kiinua mgongo cha ubunge aliokuwa nao, Je nini atafanya Tundu Lissu atasalia belgium maisha yake?

Tija ya Tundu Lissu kufanya siasa kwa twitter na youtube itasaidia nini mpaka lini ilhali hawezi kuja kwa kugombea wala chochote, au unafikiri Tundu Lissu mara hii atachukua form za kugombea urais online na kurejesha online akiwa kule kule na kampeni zake atafanyia online? pia akichaguliwa ataongoza Tanzania kwa online?

Ndio mana nasema Lissu amefeli kisiasa.

Kwanini Lissu baada ya mwendazake kufariki hakushauriwa kukaa kimya kidogo ili kuleta ulaini fulani na kupata muda kufanya mazungumzo na Rais mama Samia akarudi nchini na baada ya kufika kwanza akaangalia hali halisi ya mazingira ya kurudi kwenye siasa tena? Unajua siasa ni kila kitu kinahitaji siasa., maalim seif ni kiongozi wa kuigwa siku zote, maalim alikuwa mvumilivu sana ni kiongozi ambaye hakuwahi kushindwa kufanya siasa kwa njia zozote zile
 
..mama samia amesema tufungue ukurasa mpya.

..siasa za kupigana risasi, kubambikiana kesi , na kudhulumiana,zikome.
 
Sijui kama kuna anayemhitaji. Muache akichoka atarudi. Kwani kuna aliyemtuma huko? Mbona alipokuja kufanya kampeni aliishi vizuri hadi akatengeneza mazingira ya kurejea kwa mabwana zake bila kupigwa hata kofi?
 
Kwani wakati amerudi wakati wa kampeni alihakikishiwa ulinzi na nani?
 
Back
Top Bottom