Lissu sio mtu wa mchezo mchezo, ndani ya miezi miwili kafanikisha kumpatia Sativa vibali vya kuishi Ubelgiji.

Mimi nacho jua Lissu anapendwa na watanzania ambao hawapendi mambo ya unafiki au ndumila kuwili sie mambo ya ulaya hayatuhusu tunahitaji chama pizani dhabiti sio cha kupiga deal za maridhiano
Maridhiano= vibuyu vya asali.
 
kuwa na nidhamu ndugu
 
Hii michezo ya kutekana na kuuana madhara yake yanakwenda kuwa makubwa sana Kwa Taifa kuliko tunavyofikiri.
Kama kweli wanaondamwa ni wanaharakati na wakosoaji wa serikali basi tutambue tutavunja daraja na madhara yake ni makubwa kuliko tunavyofikiria.

Itafika mahala vijana na watu wengi watakuwa ughahibuni na hati za ukimbizi na Taifa litakuwa limechafuka pakubwa sana kuliko tunavyofikiria, Wazungu ni wajanja sana, wakishaona tayari tumetengeneza wakimbizi wengi basi nao huwatumia kama bargaining chip Kwa maslahi yao binafsi.
Hao hao wakimbizi wanaweza kuwa financed na kuja kudestabilize nchi maana hawana cha kupoteza huko waliko zaidi ya kupambana kuuondoa utawala nao warudi nyumbani.

Tutambue pia hakuna mnyonge miaka yoote, hawa wanyonge watachoka na kuamua kurevange au kukataa uonevu, hali hii ikifika madhara yake ni makubwa kuliko utekaji wenyewe.

Binafsi sioni athari zozote za hao wanaharakati au wakosoaji kiasi cha kutumia nguvu kiasi hicho, ninachoona inahitajika akili ndogo kudeal nao kuliko kuwateka na kuwaua, akili ndogo itakayotumika haihitaji kuumiza wala kutumia nguvu.

TUJITAFAKARI, TUNAELEKEA GIZANI.
 
Na ndio aina hii ya Machiavellian politics watu wakamuita shujaa kumbe ni ujinga na kutotumia akili zaidi ya ubabe mahali ambapo alitakiwa kuacha wataalamu wafanye kazi zao .
 
Picha kama hii nilikuwa naisaka sana
Good.
Tahira anajengewa choo huku nchi yake imejaa rasilimali.
Tuna viongozi matahira
 
Na ndio aina hii ya Machiavellian politics watu wakamuita shujaa kumbe ni ujinga na kutotumia akili zaidi ya ubabe mahali ambapo alitakiwa kuacha wataalamu wafanye kazi zao .
Naam,

Na bado mpaka leo watu wanashangilia ujinga, mpaka leo.
 
Hiyo ni rahisi ukisema wewe ni kitako cha mshare yaani upinde na umekimbia wanataka kukuua wanakupatia paper ndani ya wiki tu!
 
kwenu nyote msiojua ,LISu ni mwajiliwa rasmi na umoja wa ulaya ...mwandishi pekee wa vitabu vinavyohusu siasa ya afrika mashariki ,yeye Yuko pekeake ulaya haishi kama mkimbizi anavibali vya kufanya kazi na analipwa mshahara

Mnavyoona ccm na serikali wameajili akina yericko NYERERE kumtukana LISu wasamehewe ...LISu amekuwa mshawishi hasa kwa washirika wa marekani na marekani wenyewe

Trump amewahi sema kama angekuwa mzaliwa amerika basi angemteua kuwa waziri wa Sheria
 
Mungu amembariki sana Lissu
 
waarabu kila kukicha wanajaribu kuingia ulaya bila mafanikio pamoja na kuwa na sifa sahihi za kuwa wakimbizi.
Ndani ya muda mchache na kupitia connection zake umoja wa Ulaya, Lissu amefanikiwa kumpatia karatasi

WaTanzania tunakosa utu, Sativa Edgar Edson Mwakalebela kutekwa, kuteswa, kuumizwa, kutupwa porini awe chakula cha mamba wa mbuga ya Katavi bado mnaona ni kitu kidogo alichofanyiwa Sativa kiasi mnaona hastahili kupata hadhi ya ukimbizi ili aishi uhamishoni?


Toka Maktaba :
June 2024
Katavi, Tanzania.

Ya Edgar Edson Mwakalebela Sativa aliyeokotwa porini Katavi msitu wa Mlela walisema hivi, taarifa rasmi ya Polisi mkoa wa Katavi ...


View: https://m.youtube.com/watch?v=UBmnNL2qxJUKamanda wa polisi mkoa wa Katavi RPC Kaster Ngonyani alisema kuwa Mwakalebela kajeruhiwa kidogo tu, na kuwa Sativa majeraha yake siyo ya kutisha ....lakini tumemuona yupo hospitali

Kamanda RPC Kaster Ngonyani alipozungumza kwa njia ya simu kutoka Mpanda mkoa wa Katavi nchini Tanzania kuzungumzia kutekwa kwa Sativa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…