List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

Thats is JF we dare to offend openly.... teh teh teh....
 
Kuna habari za ndani kabisa zisizo rasmi zinasema muungwana anakula sahani moja na wote waliohusika na rushwa wakati wa Mkapa. Inasemekana hata Mkapa mwenyewe yuko matatani. Nasikia wanatakiwa kurudisha walichochota na kuficha nje ya nchi. Hata Balali nasikia kaambiwa asiguse faili lolote Benki Kuu hadi uchunguzi ukamilike. Actually amefukuzwa kazi kimya kimya.
 

Another spinning? Lolote litakalofanyika litawavunjavunja CCM katika makundi mengi zaidi. Ndo maana tunawapongeza kina Dk. Slaa kwa utumishi mwema.
 
MKONO AJIBU MAPIGO KWA KUZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI.
-Slaa muongo
-Adai ushahidi alioutoa ni feki
-Afichua mawakili wanaoidai BOT kesi ya mdai mfu
-Asema shughuli zake BOT sio kwa kesi moja tu

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono amejibu mapigo ya Dk. Willbrod Slaa kuhusu tuhuma dhidi yake na kusema kiongozi huyo wa CHADEMA ni muongo.

"Slaa hana silaha...huyu alikuwa kanisani enzi zake inashangaza anasema uongo. Huyo (Slaa) ni muongo, kama mimi amenitungia yote hayo, naamini na wengine kafanya hivyo," alisema jana Mkono alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake.

Mkono ambaye pia ni mwanasheria kitaaluma alisema tuhuma zote zilizotolewa na Dk. Slaa dhidi yake hazina ukweli na kuwa lengo la kiongozi huyo wa upinzani lilikuwa kuwadanganya wananchi.

Akifafanua kuhusu tuhuma hizo, Mkono alisema madai ya Dk. Slaa kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imekuwa ikilipa malipo makubwa kwa Mkono & Co. Advocates hasa yale yanayohusu kesi ya Valambhia, siyo sahihi.

Alisema katika kesi hiyo ambayo aliipokea mwaka 2003, amefanikisha mambo mengi ikiwemo kuokoa fedha za serikali zilizokuwa zichukuliwe na wadai na ambazo zina walakini ndani yake na kuwa hatua hiyo imemzushia chuki miongoni mwa mawakili.

Mkono alisema kuna kampuni ya mawakili (majina tunayahifadhi) ambayo katika madai yake ya awali ya Aprili 3, 2003 iliomba kulipwa dola 9,917,850 (sawa na sh. bilioni 11) kama gharama za kuendesha kesi hiyo.

Aliongeza kuwa: "Kampuni hiyo hiyo ilipofika Juni 6, mwaka huu, iliomba kulipwa dola 19,835,701 (sawa na sh. bilioni 25.4) kuhusiana na kesi hiyo ambayo muhusika alifariki dunia muda mrefu uliopita."

"Sasa hapo nani ni mfisadi. Waandaishi mtapima wenyewe, mimi naendelea kutetea BOT ili fedha za walipa kodi ambao ni wananchi isiende bure," alisema Mkono na kuwa anafanya shughuli nyingi mbalimbaliza BOT mbali ya kesi hiyo.

Kuhusu kuhusika kwake na kampuni kama vile Azania Agricultural Enterprises, Liberty Leather Shoe Ltd, Azania Eximco na mengineyo, Mkono alisema hausiki nayo kwa maana ya kuwa na hisa au kuwa mkurugenzi wake.

Katika kuthibitisha hilo, alitoa taarifa kuhusu ukaguzi wa kampuni hizo kwa maana ya wana hisa na wakurugenzi wake kama ilivyotolewa na BRELA wiki hii.

Kuhusu kampuni za Oxford Services Ltd na Marcus Ltd, mbunge huyo alikanusha kuwa mkurugenzi au mwenye hisa na kufafanua kuwa alikuwa wakili wa kampuni hizo.

"Haya ni mambo ya ajabu sana. Hivi mtu kuwa wakili wa kampuni au wa mtu ni dhambi au ndiyo unakuwa mfisadi," alihoji Mkono na kuwa katika biashara za kampuni hiyo miongoni mwa waliochukua fedha na kupata matatizo ni Chavda.

Alisema kutokana na matatizo aliyopata Chavda, alitakiwa kufukuzwa nchini mara moja, lakini kutokana na taaluma yake alimtetea kwa mujibu wa sheria na kuhoji iweje wakili ahusishwe na dhambi ya mtuhumiwa.

"Kila mtu ana haki ya kutetewa. Wapo wauaji wamefanya makosa, lakini wana haki ya kutetewa...hata hivyo wakili anayemtetea mtu wa aina hiyo hawezi naye kuitwa muuaji," alisema Mkono na kuwa baadhi ya mambo hawezi kuyazungumza hadharani kwa undani kwa kuwa kama wakili kuna miiko ya kazi.

Mkono alitumia fursa hiyo kueleza ukweli kuhusu suala la kampuni ya City Water na kuwa katika kesi kwenye Mahakama ya Kimataifa nchini Uholanzi ambayo inashughulikia usuluhishi wa migogoro, kamwe hakupata kumuona.

"Huyu mwingine anayeitwa Tundu Lissu, sikumuona na wala simfahamu kwa kuwa kule mimi nilikuwa naongoza jopo la mawakili wa serikali," alisema Mkono.

Katika tuhuma mbalimbali walizozitoa kwenye mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Mwembeyanga, Dar es Salaam ambapo Dk. Slaa na Lissu walikuwa wasemaji wakuu, Lissu alitajwa kama mmoja wa mawakili wa serikali katika shauri la City Water.

Akihitimisha kwa ujumla tuhuma dhidi yake, Mkono alisema waliotoa madai hayo anahisi wanamuonea wivu kutoka na mafanikio katika kazi yake na jinsi anavyojitahidi kupeleka maendeleo jimboni mwake Musoma Vijijini.

"Nimemuita Slaa, lakini amegwaya na kwa jinsi anavyosema uongo huenda ningemchapa makonde,"alisema huku akionyesha kusikitishwa na tuhuma hizo.


Imetolewa kwenye Gazeti la Uhuru 21/10/07.
 
Aende MAHAKAMANI asilete ngonjera hapa.

Kukimbilia kwenye vyombo vya habari wakati umetukanwa si kawaida ya Mafisadi wa Tanzania.

Soo hili lingekuwa na pa kukwepea Mkono angefungua Kesi mara moja.

Tuhuma za ufisadi zimewakolea ipasavyo hapakaliki. Safari hii mtasema yote bila kujitambua.
 
Huyo mzee kibaragashia chekundu anamdanganya nani?

Mbona this day walimuandika vyema anavochota mabilioni BOT kiasi kwamba malipo ya wakili yanazidi pesa zinazo tetewa?? Tena nadhani hiyo thread ilikuwepo pia hapa JF!

Asitufanye sie ni wasahaulifu namna hiyo!

Mbinafsi mkubwa anatanguliza maslahi yake mbele bila kujali maslahi ya taifa, kutetea wawekezaji na kutuingiza mikataba mibovu kama ile ya NBC!
 
1.
Kila mtu ana haki ya kimsingi ya kutathmini ushahidi na kutoa conclusion Field Marshall ES,
Nashukuru kwamba bado tunaendelea kukata ishu huku tukielimishana/kueleweshana na kuipa jamii ya JF mitazamo mbali mbali ya jambo husika.

Tathmini ya ushahidi inatolewa na wataalamu wa sheria, au mahakama na sio mimi na wewe, unless wewe na mimi ni watuhumiwa au mawakili wa watuhumiwa, kama Wakili mtuhumiwa Mkono, alivyofanya leo, ni muhimu sana kuipa JF mitizamo mbali mbali ya ishus, lakini isiwe ni njia ya ku-abuse the luxury, just because JF wananchi wengi wanaikosoa serikali basi kwa mwananchi mmoja kutoa tathmini isiyoendana na ishu ili tu iwe tofauti na the usual maana forum inahitaji mitizamo mbali mbali ni hoja hafifu sana mkuu wangu!



2.
That said, hoja yako ya msingi kwamba mimi na wewe ni watazamaji tu na kwamba hatuwezi kutoa tathmini zetu isipokuwa mahakama ni hoja hafifu mno. Kama unavyosema ndivyo basi nakushauri uondoe neno DEBATE kwenye kamusi.

Hoja yangu ni ya msingi sana na ndio maana hata Spika wa bunge wa CCM, anakubaliana nayo, baada ya kuipitia hii orodha kama mimi na wewe tulivyofanya, ameamua kuwa kuna ushahidi unaohitajika kuchambuliwa na wataalam kama Mwanasheria mkuu wa serikali, ndipo ataamua kama kuna ishu kweli, na ndio msimamo wangu kuwa mimi na wewe hatujui ukweli wa kilichofanyika na ambacho hakikufanyika katika maelezo ya DR. Slaa, kwa hiyo wanaohusika kwanza waipitie na kutoa maoni yao, na inaweza kuwa mahakamani ndio tunapoweza kutoa conclusion, kama kuna ushaidi au hakuna, lakini sio at this stage, tunachoweza kutoa ni political analysis kutokana na orodha hii ya Dr. Slaa, lakini sio hukumu za kisheria kama ulivyofanya mkuu, siasa na sheria ni vitu viwili tofauti na hilo limethibitishwa na msimamo wa Spika wa CCM on this ishu!

Kuhusu neno debate, huwezi kulilazimisha kutumika pasipotakiwa, so far hii ishu ya Dr. Slaa bado ni ishu ya siasa, ushahidi ni ishu ya sheria ambayo ni mapema sana kuizungumzia, mpaka watuhumiwa watakapo jitokeza kama alivyojitokeza mtuhumiwa mmoja tayari ambaye ni mwanasheria, ukisoma maneno ya Mkono on this ishu, ukasema hakuna ushahidi then tutakuwa na a true debate kama bado ninaamini upo, kwa hiyo hoja ya kufuta neno debate, labda uichukue mwenyewe back!


3.
Hivi ulipobandika list ya Dr Slaa ulitegemea kwamba wasomaji wasome tu kama bibilia bila kutoa uchambuzi wao?

Nilitegemea wananchi watoe mishangao yao na analysis zao kisiasa, au kama binadamu na wananchi wa Tanzania, lakini sikutegemea kuwa watatoa hukumu za kisheria based on one side story, kama ulivyofanya mkuu wangu!

Hata Biblia huwa inatolewa uchambuzi, ndio maana kuna makanisa yenye viongozi mashoga na mengine hayana kabisaa!


4.
Hoja hujibiwa kwa hoja, kama MMKJJ anavyosema....ila naona mzee mwenzangu concept hii ndo kwanza unai-abuse. Badala ya kujibu hoja zangu kwa kueleza strength za ushahidi wa Dr Slaa,

Strength za ushaidi wa Dr. Slaa, so far hauwezi kuwepo maana the whole thing inahitaji kuchambuliwa na wataalamu kwanza ili kujua wapi zipo criminal charges na wapi kuna maoni tu ya kisiasa, na huwezi fanya hivyo bila kwanza kuwahoji watuhumiwa unless wewe ni mmoja wa watuhumiwa wenyewe, au wakili wa hao watuhumiwa. Strength za charges za Dr. Slaa zinaweza kuonekana pale tu tutakapokuwa na rebuttal toka kwa watuhumiwa, ndio maana hoja yangu kwako nimeilekeza kwenye general ishu yako ya ushaidi, na sio hoja ambazo kwangu ninaziona kuwa ni imaginations tu, kwa hiyo hakuna abuse yoyote as of your claim!


5.
Hiyo mkuu, ilikuwa kujibu hoja yako kuwa kuna wananchi wanachekesha hapa wanapodai kuwa watuhumiwa wajibu tuhuma za DR. Slaaa, je wananchi hapa forum kuchekesha unaiona ni kujenga character za wananchi hapa forum? The rst ni mazungumzo baada ya habari au ni kelele za mlango huwa hazinizuii kulala, na hazinizuiii kumkoma nyani giladi hapa, tena kiroho mbaya!


6.
Nimesema hoja za Mugongo, huwa ana hoja nzito za kuwakosoa Zitto na Freeman, na zinakubalika hapa, hiii ya kwako ya ushahidi wengi hapa tunaikataa kwa sababu haijitoshelezi, na sio mahali pake mkuu maana wakati wake bado ila unakuja!

7.
Hiii ndio ile kitu ninaiita kulia mbweha! mbweha! mbweha! ili usaidiwe na watu hapa, Mugongo ametajwa kukufahamisha tu for your future refference kuwa wananchi hapa hawakupingi tu kwa sababu una hoja ya kuitetea serikali, hapana maana kuna kina Mugongo ambao huitetea serikali na hoja zao zinaheshimika hapa forum!

8.
Mimi nitautoa wapi ushahidi ambao bado haujatolewa na waliotuhumiwa? Spika emshindwa kufanya uchambuzi amepeleka ishu kwa mtaalamu mwanasheria mkuu, sasa sembuse mimi mwananchi wa kawaida? Sasa wewe kuwa na ushahidi kwenye hii stage basi na wewe ni mtuhumiwa au wakili wa watuhumiwa, na ndio maana ninapingana na uchambuzi wako kuwa unless ukinithibitishia kuwa wewe ni mtuhumiwa sitakuwa na pingamizi kuwa una ukweli,

otherwise ni mpaka kesi hii itakapokwenda mhakamani, au watuhumiwa watakapotoa rebuttal, ndio nitakujibu kuhusiana na hoja ya ushahidi kama upo au haupo, maana os far nimesoma maneno ya Dr. Slaa peke yake, ninahitaji pia kusoma maneno ya upande wa pili ili niamue kama ushahidi upo au haupo, na sasa hivi nitasoma maneno ya Wakili/Mtuhumiwa Mkono, na nitaamua kma akweli ushaidi upo au hakuna na nitasema, hapa hapa!

Otherwise mkuu ahsante kwa hii useful debate, na tuendelee kukata ishus, ila for now ninatafuta rebuttal toka kwa watuhumiwa kwanza, ndipo nitaendelea na hii debate kwenye upande wa sheria, for now nitaendelea na kuikata ishu hii on siasa side yake!
 
1. DR. Slaa anasema:-

6. NIMROD ELIREHEMA MKONO

Hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu ni kuwa kesi hii haina muda maalumu wa kumalizika na hivyo inawezekana kabisa malipo ya wanasheria yakazidi kiasi cha fedha inachodaiwa Benki Kuu.

Kampuni ya mawakili ya Mkono & Co. Advocates imekuwa ikitajwa kuhusiana na kashfa kubwa za ufujaji na/au ubadhirifu wa fedha za umma kwa muda mrefu.




Baada ya kuelezea uhusiano huo ulivyokuwa Mheshimiwa Ayila alimalizia kwa kusema yafuatayo: "Mheshimiwa Spika, ni vigumu kabisa katika hali ya kawaida kwa mtu yeyote kuamini kwamba makubaliano haya na uhusiano uliojitokeza hapa haukuwa wa hila.


Majibu Ya Mtuhumiwa Wakili Mkono:-


MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono amejibu mapigo ya Dk. Willbrod Slaa kuhusu tuhuma dhidi yake na kusema kiongozi huyo wa CHADEMA ni muongo.



Wakuuu huu ni mfano mdogo wa utata wa hii ishu, DR. Slaa anamtuhumu Wakili/Mbunge Mkono, akitumia madai ya msingi yaliyotolewa na mwenyekiti wa kamati ya bunge iliyomchunguza Mkono na BOT, sasa tazama majibu ya Mkono, je ni kweli yanafanana na the charges?
 


Naona akisisitiza jambo, jeee ni kweli anaweza mapambano au just anazuga tu, maana keshapima nyakati na kugundua sasa sooo?
 
Nimrod Mkono kama mwanasheria uliyebobea nenda mahakamani kajisafishe.

Ukweli unauma, ni kweli umeshiriki kutuibia, unachokifanya sasa jimboni mwako ni kuwapatia wananchi makombo.

kama kweli wewe sio mwizi, wewe kama mwanasheria wa kimataifa kama unavyojiita unaonashida gani kumburuza Slaa mahakamani. kumbuka Slaa katoa ushahidi ndani ya serikali na kachambua kazi zako BOT. Wewe ni mwizi, mhujumu, na mfisadi wa fedha za wananchi. Pipi unazo zitoa sasa hivi jimboni mwako ni baada ya kuvimbiwa na wajinga ndio waliwao.

Mkono sidhani kama kuna kuoneana wivu kwenye swala la kuiba fedha za umma, kumbuka Slaa ni mmoja kati yetu sisi waliahoi ambaye amepata nafasi ya kusema hadharani tupo wengi wenye uchungu kuliko unavyofikiria.

Heko Slaa sisi walia hoi tupo nyuma yako.
Ninaomba yeyote mwenye simu ya Mkono anipatie tafadhali ilinifanye mahojiano naye.
 
Ukitupa jiwe kwenye mbwa wengi anaye bweka ndiyo aliyepigwa na jiwe. Hapa inaelekea kibabu kimepigwa na jiwe. Guess what? kinaiona milango ya gereza. Uwiii, uwii, uwiiiiii!
 
Kweli mambo yanakwenda kombo. Huyu jamaa hana sababu yoyote ya kubwata bwata, alitakiwa amburuze Slaa mahakamani na hata kama Slaa hana hiyo fedha ya kumlipa, atakua amejisafisha jina lake. Anaogopa na hata serikali inaogopa kumpeleka Slaa mahakamani kwa sababu hawajui ni mabomu gani mengine atayalipua akipandishwa kizimbani. BAHARI IMECHAFUKA!
 
Mkono: Ninalipwa dola 500 kwa saa

* Ashangaa Dk. Slaa kutokamatwa


Na Irene Mark
 
Absolutely stupid hata top barristers wanaolipwa $500.00 huku majuu wanahesabika itakuwa yeye. Hii serikali imeoza na hivi viwango ni extortion. Shame on him!

Nategemea TRA analipa kodi ya hizo pesa anazochaji.
 
This was probably the worst thing to say among the millions of hungry and impoverished Tanzanians. Unajua, ingawa huyu jamaa amesoma na kubobea katika sheria, inaonekana ame-panic na ameshindwa kujua aseme nini ili kujitetea. You can't just blubber kwa watanzania kwamba benki yenu ya BoT inanilipa mamilioni ya saa moja wakati mtanzania wa kawaida kiasi hicho hakipati mpaka afanye kazi miaka 10. What an old fart this asshole has become.I feel sooooooooooo sorry for him.
 
Kwani anatetea kiasi gani cha pesa hadi alipwe kiasi hicho? maana tuseme hiyo kesi ikiendeshwa kwa miaka mitano atalipwa kiasi ghani? Duh kweli jamaa anavuna pesa ya wananchi. Hata huruma hana? Any way hata wewe ukipata dili kama hili utakula tuu na watu wanaendelea kufa njaa na maradhi. Kweli hii dunia haiko fair.
 
Unaweza kucheka kwa ajili ya hasira!

Hivi kweli Mkono anaona ni sawa kabisa kukuri kwamba analipwa dola 500 yaani zaidi ya shilingi laki sita kwa saa moja? tena analipwa masaa nane??

Nashindwa hata andika! nina hasira sana!!!
 
sasa inabidi aweke mahesabu yake wazi kwa ummah tujue hiyo kampuni yake inavyopata fedha na inavyotumia pesa hizo au iunde tume maalumu kuchunguza pesa zake hapo ndio haki itatendeka au mnasemaje jamani ?

hata hii benki yake , ni vizuri iwekwe wazi pesa zimetoka wapi mpaka wamefungua
 
Hivi kuna mtu anaweza kupata english translation ya hizi tuhuma za Dr. Slaa? Kama itapatikana, watu waliopo Marekani tunaweza kuji mobilise ili kuomba marafiki na ndugu zetu wapiga kura wa kimarekani ili wawashawishi masenator na representatives wao ili wazuie misaada kwa Tanzania. Muungwana amekua akipewa sifa nyingi za bure tu na Wamarekani ambao hawajui ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya serikali yake ya Mafisadi.

KAMA ENGLISH VERSION INAWEZA KUPATIKANA, TUNAOMBA IBANDIKWE HAPA ILI WATU TUANZE KAMPENI.
 
Unaweza kucheka kwa ajili ya hasira!

Hivi kweli Mkono anaona ni sawa kabisa kukuri kwamba analipwa dola 500 yaani zaidi ya shilingi laki sita kwa saa moja? tena analipwa masaa nane??

Nashindwa hata andika! nina hasira sana!!!

Muhimu ni masaa mangapi alicharge kwenye hiyo kesi? Uthibiti wa hayo masaa ukichunguza ni mdogo sana na alifanya nini kwenye hayo masaa? Kila mahali WIZI WIZI WIZI ama kweli ipo siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…