1.
Kila mtu ana haki ya kimsingi ya kutathmini ushahidi na kutoa conclusion Field Marshall ES,
Nashukuru kwamba bado tunaendelea kukata ishu huku tukielimishana/kueleweshana na kuipa jamii ya JF mitazamo mbali mbali ya jambo husika.
Tathmini ya ushahidi inatolewa na wataalamu wa sheria, au mahakama na sio mimi na wewe, unless wewe na mimi ni watuhumiwa au mawakili wa watuhumiwa, kama Wakili mtuhumiwa Mkono, alivyofanya leo, ni muhimu sana kuipa JF mitizamo mbali mbali ya ishus, lakini isiwe ni njia ya ku-abuse the luxury, just because JF wananchi wengi wanaikosoa serikali basi kwa mwananchi mmoja kutoa tathmini isiyoendana na ishu ili tu iwe tofauti na the usual maana forum inahitaji mitizamo mbali mbali ni hoja hafifu sana mkuu wangu!
2.
That said, hoja yako ya msingi kwamba mimi na wewe ni watazamaji tu na kwamba hatuwezi kutoa tathmini zetu isipokuwa mahakama ni hoja hafifu mno. Kama unavyosema ndivyo basi nakushauri uondoe neno DEBATE kwenye kamusi.
Hoja yangu ni ya msingi sana na ndio maana hata Spika wa bunge wa CCM, anakubaliana nayo, baada ya kuipitia hii orodha kama mimi na wewe tulivyofanya, ameamua kuwa kuna ushahidi unaohitajika kuchambuliwa na wataalam kama Mwanasheria mkuu wa serikali, ndipo ataamua kama kuna ishu kweli, na ndio msimamo wangu kuwa mimi na wewe hatujui ukweli wa kilichofanyika na ambacho hakikufanyika katika maelezo ya DR. Slaa, kwa hiyo wanaohusika kwanza waipitie na kutoa maoni yao, na inaweza kuwa mahakamani ndio tunapoweza kutoa conclusion, kama kuna ushaidi au hakuna, lakini sio at this stage, tunachoweza kutoa ni political analysis kutokana na orodha hii ya Dr. Slaa, lakini sio hukumu za kisheria kama ulivyofanya mkuu, siasa na sheria ni vitu viwili tofauti na hilo limethibitishwa na msimamo wa Spika wa CCM on this ishu!
Kuhusu neno debate, huwezi kulilazimisha kutumika pasipotakiwa, so far hii ishu ya Dr. Slaa bado ni ishu ya siasa, ushahidi ni ishu ya sheria ambayo ni mapema sana kuizungumzia, mpaka watuhumiwa watakapo jitokeza kama alivyojitokeza mtuhumiwa mmoja tayari ambaye ni mwanasheria, ukisoma maneno ya Mkono on this ishu, ukasema hakuna ushahidi then tutakuwa na a true debate kama bado ninaamini upo, kwa hiyo hoja ya kufuta neno debate, labda uichukue mwenyewe back!
3.
Hivi ulipobandika list ya Dr Slaa ulitegemea kwamba wasomaji wasome tu kama bibilia bila kutoa uchambuzi wao?
Nilitegemea wananchi watoe mishangao yao na analysis zao kisiasa, au kama binadamu na wananchi wa Tanzania, lakini sikutegemea kuwa watatoa hukumu za kisheria based on one side story, kama ulivyofanya mkuu wangu!
Hata Biblia huwa inatolewa uchambuzi, ndio maana kuna makanisa yenye viongozi mashoga na mengine hayana kabisaa!
4.
Hoja hujibiwa kwa hoja, kama MMKJJ anavyosema....ila naona mzee mwenzangu concept hii ndo kwanza unai-abuse. Badala ya kujibu hoja zangu kwa kueleza strength za ushahidi wa Dr Slaa,
Strength za ushaidi wa Dr. Slaa, so far hauwezi kuwepo maana the whole thing inahitaji kuchambuliwa na wataalamu kwanza ili kujua wapi zipo criminal charges na wapi kuna maoni tu ya kisiasa, na huwezi fanya hivyo bila kwanza kuwahoji watuhumiwa unless wewe ni mmoja wa watuhumiwa wenyewe, au wakili wa hao watuhumiwa. Strength za charges za Dr. Slaa zinaweza kuonekana pale tu tutakapokuwa na rebuttal toka kwa watuhumiwa, ndio maana hoja yangu kwako nimeilekeza kwenye general ishu yako ya ushaidi, na sio hoja ambazo kwangu ninaziona kuwa ni imaginations tu, kwa hiyo hakuna abuse yoyote as of your claim!
5.
naona unarukia character assassination kwa kudai kwamba nimetoa uchambuzi kwa lengo la kuonyesha education credential zangu....I think Field Marshall ES you have more to offer to JF than this. You have my trust in your wisdom when it comes to JF but sometimes your lowest points reduce your JF wisdom to nothing.
Hiyo mkuu, ilikuwa kujibu hoja yako kuwa kuna wananchi wanachekesha hapa wanapodai kuwa watuhumiwa wajibu tuhuma za DR. Slaaa, je wananchi hapa forum kuchekesha unaiona ni kujenga character za wananchi hapa forum? The rst ni mazungumzo baada ya habari au ni kelele za mlango huwa hazinizuii kulala, na hazinizuiii kumkoma nyani giladi hapa, tena kiroho mbaya!
6.
Then katika posting yako unamwingiza Mugongo-Mugongo katika kujaribu kunifanya niamini kwamba Mugongo-Mugongo akikubali jambo basi na mimi nikubali. Naamini kwamba una utashi wa kujuwa kwamba Mugongo-mugongo ni mtu mwenye mawazo na msimamo wake unaojitegemea, kadhalika na mimi.
Nimesema hoja za Mugongo, huwa ana hoja nzito za kuwakosoa Zitto na Freeman, na zinakubalika hapa, hiii ya kwako ya ushahidi wengi hapa tunaikataa kwa sababu haijitoshelezi, na sio mahali pake mkuu maana wakati wake bado ila unakuja!
7.
JF hatushawishi watu kwa kutoa reference ya watu tuliofanikiwa kuwashawishi katika jambo fulani. Kesho naweza kukubaliana na wewe, keshokutwa nikapingana na wewe na kukubaliana na MMKJJ, wala sitasema kwamba kwakuwa MMKJJ alikubaliana nami basi ni budi wewe nawe pia ukubaliane nami.
Hiii ndio ile kitu ninaiita kulia mbweha! mbweha! mbweha! ili usaidiwe na watu hapa, Mugongo ametajwa kukufahamisha tu for your future refference kuwa wananchi hapa hawakupingi tu kwa sababu una hoja ya kuitetea serikali, hapana maana kuna kina Mugongo ambao huitetea serikali na hoja zao zinaheshimika hapa forum!
8.
All in all mzee mwenzangu, sikubaliani nawe kwamba niwe mtazamaji bila kutoa uchambuzi wa ushahidi wa Dr Slaa. Kama unapingana na uchambuzi wangu, it is very simple; leta wakwako. Na hilo tu ndilo litanishawishi vinginevyo. Kweli uchambuzi wangu ni wamitaani, kama ulivyodai, ila ni bora ukasema hivyo baada ya kutoa uchambuzi wa ofisini....nisaidie kwa kunipa uchambuzi unaouna ni wamaana. Sio kunitaka nizibe kinywa na nisubiri mahakama. Mahakama itatoa uamuzi wa mwisho, na it is possible ikaamua kwamba Dr Slaa ana ushahidi mzito, bado nitakuwa na uchambuzi wangu, na conclusion yangu, na wala haitakuwa mwisho wa debate.
Mimi nitautoa wapi ushahidi ambao bado haujatolewa na waliotuhumiwa? Spika emshindwa kufanya uchambuzi amepeleka ishu kwa mtaalamu mwanasheria mkuu, sasa sembuse mimi mwananchi wa kawaida? Sasa wewe kuwa na ushahidi kwenye hii stage basi na wewe ni mtuhumiwa au wakili wa watuhumiwa, na ndio maana ninapingana na uchambuzi wako kuwa unless ukinithibitishia kuwa wewe ni mtuhumiwa sitakuwa na pingamizi kuwa una ukweli,
otherwise ni mpaka kesi hii itakapokwenda mhakamani, au watuhumiwa watakapotoa rebuttal, ndio nitakujibu kuhusiana na hoja ya ushahidi kama upo au haupo, maana os far nimesoma maneno ya Dr. Slaa peke yake, ninahitaji pia kusoma maneno ya upande wa pili ili niamue kama ushahidi upo au haupo, na sasa hivi nitasoma maneno ya Wakili/Mtuhumiwa Mkono, na nitaamua kma akweli ushaidi upo au hakuna na nitasema, hapa hapa!
Otherwise mkuu ahsante kwa hii useful debate, na tuendelee kukata ishus, ila for now ninatafuta rebuttal toka kwa watuhumiwa kwanza, ndipo nitaendelea na hii debate kwenye upande wa sheria, for now nitaendelea na kuikata ishu hii on siasa side yake!