List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania


Unatakiwa kujua hukumu ni nini kabla ya kuuliza swali!

Kama unadhani hukumu ni kwenda jela, au faini ya hela... nadhani umeliwa,,,!!!
 
sasa hii ni kesi ya kuku na yai kipi kilianza,Dua,mwenyekiti wa hiyo kamati dk mwakyembe alisema hawawezi kuchunguza hizo tuhuma kwa sababu serikali inazishughulikia kwa hiyo itakuwa kuingilia kazi ambayo tayari serikali inazifanya.
 
kilitime,
hebu nipe mfano mmoja tu ambao serikali ilishindwa mahakamani na hukumu yake ikatekelezwa
 
Still ni tuhuma, mamlaka yenye uwezo wa kuhakikisha vielelezo vyako au ushahidi wako ni sahihi sio Jasusi, Kilitime, MKJJ, Kichwa Maji... ni Mahakama!!!

Killtime mahakama ipi unayo iongelea na sheria ipi unayo iongelea?

-0Unaongea sheria ya mahakama iliyo funikwa na CCM ya kumuachia muuaji Ditto mtaani ili atukane wakazi wa Tabora??

-Unaongea sheria ile inayo mpa mamlka JK amwambie Hosea kwamba usimchunguze fisadi ANBEM mwache apumzike??

-Unaongea sheria inayo wakataza watu wasimshitaki mbunge aliye foji vyeti na polisi wakachunguza na kuthibitisha hilo.. ???

--Unaongea sheria ya mahakama iliyo ruhusu mgombea binafsi CCM wakatunga sheria ya kumkataza mgombea binafsi??

Ndugu yangu unaongelea sheria ya wapi hiyo isiyo chini ya mkono wa CCM ambayo itaiacha mahakama itende haki??
 
 
 
Maneno ya Rais Kikwete ni sawa na maneno ya mwenda wazimu ambaye kauri zake hubadirika badirika bila kufuata trend yeyote ya maana. Si mara nyingi maneno ya Mwendawazimu huweza wekwa pamoja na kuleta maana inayo kusudiwa.

Katika hotuba zake kama Rais wa nchi na kwa msimamo wa chama chake SISIEMU, kumekuwa na kauri za ujumla majukwaani ambazo zimekuwa zikirudiwa mara nyingi kuhusu kuwahimiza wananchi kuwafichua Wahujumu wa mali ya wananchi na Taifa kwa ujumla kwa kumpelekea majina na nyendo zao zote yeye mwenyewe binafsi, kna kwamba POLISI CID Usalama wa Taifa na serikali nzima imeshindwa kufanya kazi.

Maneno yaliyoandikwa katika taarifa ya mwandishi Maura Mwingira ni ya kugeuka na kukana kama si kurunga kimanga maneno yote yaliyo wahi semwa na Rais JMK, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Rais wa awamu ya pili Ali Hasana Mwinyi na viongozi wengi wengi wa SISIEMU akiwemo mshika Hirizi wao SISIEMU Mzee Kingunge.

Sisi watanzania siyo hamnazo kama kundi hili la Mamruki wa KISISIEMU wapendavyo Dunia nzima kuamnini.Tumetambua fika kwamba Viongozi wa SISIEMU ni mabingwa wa kubwabwaja na wepesi wa kusahau walicho bwabwaja.Mara zote SISIEMU wamekuwa wakitoa kauri nyingi za kujichanganya kwa madhumuni ya kufanikisha malengo ya muda mfupi au kujitoa kimaso maso mbele ya halaiki.

SISI wanananchi tunaijua fika Tabia Kinyonga ya Viongozi wa SISIEMU ukiwemo wewe Rais.Siku zote Viongozi wa SISIEMU wakiona jambo walilo lianzisha linaungwa mkono kwa dhati na linageuka moto wa kuwaunguza Makalio yao wenyewe, huanza kutoa taarifa zinazo pingana kwa nia ya kuwachanganya na kuwakoroga Watanzania wote ili kuficha uovu wao.

Tamko la Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuomba kupelekewa taarifa na wananchi juu ya Wezi Majambazi na Mafisadi ndani ya serikali ambao ni wakwamisha Juhudi za kuiendeleza Tanzania huru kwenye maendeleo ya kweli, lilikuwa na maana ya Kuruhusu wananchi kuchukua kazi ya Polisi na Usalama wa Taifa ya KUPELELEZA kupata vithibitisho na kumshawishi yeye kama Rais wa nchi kuchukua hatua sahihi dhidi ya watuhumiwa.

Kwa sababu Wananchi tuliitikia wito wake tukampelekea List ndefu sana ya Wananchi wenzetu walio na dhamana serikalini na walio amua kuwa Mamruki kwa faida zao Binafsi, kumweleza kirefu namna wafanikishavyo nyendo zao chafu na yeye kama Rais wa nchi kupokea Taarifa hiyo na KULA JIWE alitaka sisi tufanye nini ili yeye achukue hatua?


TAMKO.
Kwa sababu wewe MH rais Umekula jiwe usitegemee sisi wananchi kukuletea list ya Mafisadi ndani ya Bahasha na kujaza shelfu za Ikulu tena.
List na taarifa za wezi wote wa mali ya umma utaziona on Line kama hapa JF na YOU TUBE.
Kama mwenyewe ulivyo bashiri kwa uhakika kabisa, watoa Hukumu watakuwa ni Wananchi wa Tanzania na siyo Mahakama zilizo jaa wala Rushwa na Zipewazo Mashinikizo kutoka ndani ya Serikali yako ambayo ni Agent Mkubwa wa UKOLONI MAMBOLEO nchini Tanzania .

Kuhusu mtumishi yeyote wa serikali au mwanachama mwaminifu wa SISIEMU kutotendewa haki kwa Wananchi ambao wametoa hukumu bila wao watuhumiwa kuwepo, natoa ushauri kwako Rais na wenzio kwenye List ya Best 11 MAFISADI Players kwenda Mahakamani na kufungua Kesi za nguvu.

Mahakama zote za Tanzania ziko ndani ya uwezo wenu na zinapokea shinikizo toka serikalini na mnaamini zinatoa hukumu ya haki mnasubiri nini kwenda kuitafuta haki mnayoendelea kuipoteza kwa kuhukumiwa mitaani na wananchi na muwaitao wachochezi?

Kuhusu Utawala wa Sheria.

MH Rais miaka michache iliyopita ulikuwa ni kiongozi katika kada ya kawaida na umepata kujionea mwenyewe jinsi Sheria na taratibu nyingi zipindishwavyo kwa manufaa ya WaTanzania wachache wenye sura za binadamu lakini wana akili na roho za hayawani.

Viongozi wa serikali wakiiba mali ya umma, wakibaka vibinti vyetu, wakiwapa mimba wanafunzi, wakipiga watu mitaani, wakiiba wake za watu mchana kweupe kama MH Ditto alivyowahi kamatwa akila uloda mke wa mtu kule Peninsula au wakiua mbele ya halaiki ya watu kwa silaha kali hawafungwi Jela.
Badala yake wanashiriki kikamilifu katika KAmpeni za serikali zza Kuwabeza wananchi huku wakitoa Lugha za matusi ya Nguoni kwa kujiamnini kwamba wana Kinga madhubuti toka ndani ya serikali yako ya SISIEMU.

MH RAis JMK, huo utawala wa sheria unao uongelea ni upi?
Wa mtuhumiwa wa mauaji kusimama na kuongea matusi kwa niaba ya serikali yako Tukufu ya SISIEMU?

MH Rais Kikwete naona wewe na wenzi wako mnapenda sana tabia yetu wananchi ya kukaa kimya kama Msukule huku ninyi nkiiba na kijineemesha na kugawia wezi wa kimataifa rasilimali za nchi yetu.
Watanzania tumekuwa tukipata maamivu kwa muda mrefu sasa tumesema Basi.

MH Rais na wenzi wako mnafurihia sana Umasikini wa kutupwa na hali Duni za wananchi wanaoshindwa kuwabana kwa vile wanatumia muda wao wote kuhangaika kutafuta mlo mmoja tu katika siku. Mahanagaiko yao ni neema yenu. Kadri ya Utashi wenu SISIEMU Juhudi zozote za kuwaamsha au kuwazindua Watanzaniawalioko mijini na vijijini ni Uchochezi na ni kwenda kinyume cha Kanuni, Taratibu na Sheria za Nchi.

MH Rais na wenzi wako wa SISIEMU mnafurahia na kusherehekea hali hii mbaya ya Chakula Makazi na Mavazi ya wananchi inayowafanya muonekane Miungu watu mbele za wananchi wa Tanzania.
Wananchi tumegundua kwambaViongozi wa SISIEMU mnatumia UNYONGE WETU kama mtaji madhubuti wa kuendeleza utawala wenu haramu na wa kienda wazimu( Kuuza nchi hali ninyi na vizazi vyenu bado mnaiihitaji)

Kwa sababu sisi wananchi si wajinga kama wewe Rais upendavyo tuwe tumeamua kugeukiana wananchi wenyewe kwa wenyewe na kubadirishana taarifa na maelezo ya kina juu ya uchafu uoza na juu ya yote Ufisadi wenu ndani ya dhamana mliyopewa nasi wananchi.

MH Rais naomba ujue kwamba hakuna tabia yeyote inayojengeka miongoni mwa wananchi na hasa wanasiasa ya kuwa WAPELELEZI.
Sisi wananchi tunatekereza kauri yako mwenyewe ya kuchukua kazi ya Polisi na Usalama wa Taifa ya kupeleleza ili kupata taarifa za Wezi wa mali yetu.

Kuna Ubaya Gani wananchi kupeleleza juu ya wezi wa Kuku mbuzi na ng'ombe wao vijijini mwao na kujadiri janja zao hadharani na mafichoni hasa ukizingatia kwamba Usungusungu ni Ruksa Tanzania?

MH rais unachekesha sana ukiongelea kuhusu Uhasama na Chuki.

Hivi kauri za Viongozi wa SISIEMU za Kuupuza tuhuma za Dr Slaa Zitto na Lissu zinazoenezwa na Viongozi wa ngazi ya juu kabisa ya SISIEMU hazina lengo la kujenga Uhasama miongozni mwa wananchi?

Kauri za viongozi wa SISIEMU zisemazo Mtanzania yeyote anaye taka amendeleoa aachane na vyama vya upinzani na kujiunga na SISIEMU zina maana gani kama si kuvuruga na kujenga chuki kati ya mtu na mtu?
Je kauri hizo si kinyume na Kanuni Taratibu na Sheria za nchi hasa Sheria ya vyama vingi na sheria ya haki za binadamu?

Endapo Dr Slaa Zitto na Tundu Lissu wametoa kauri zisizo za kweli na kwa maneno yako umesema wafuate taratibu na sheria. Je SISIEMU kuwaambia wananchi wawapuuze maneno ya Dr Slaa na Tuhuma zake kwa kutumia majukwaa yale yale waliyotumia Dr Slaa Zitto na Lissu kuna maanisha nini?

Kwanini Viongozi wa SISIEMU waliokashifiwa hawaendi mahakamani kudai haki yao ya msingi kama ilivyo ada ya viongozi wa SISIEMU?

Je si kweli kwamba Viongozi waliotuhumiwa katika Ufisadi wameamua Kuvaa mashati ya KIJANI na kujifanya WANYONGE waliioonewa na kudhurumiwa ili wananchi wawahurumie na kusahau Ufisadi wao??

Kwako Mchungaji wa Kondoo wa Bwana.

Kauri ya Askofu Laizer ya kumsifia Rais Kikwete kwa kupambana na vitendo vya Rushwa ni Taarifa ya Askofu Mnafiki ambaye pengine huko mafichoni hula kondoo walio nona kisirisiri.
Askofu Laizer alitakiwa kutumia Busara nyingine za Kichungaji kumsifia Rais. Zaidi alitakiwa kuwa mkweli juu ya hali halisi ya Watanzania ambao ni sehemu ya kondooo wa Bwana alio pewa kuwachunga.
Kondoo wanaangamia kwa sabu ya Ufukara wa kutisha na kukosa maarifa na hekima yeye mchungaji wa kondoo wa Bwana hata Roho haimuumi.

Kwako Aksofu Laizer ni Ujasiri upi na juhudi zipi ambazo Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameonyesha kiasi cha wewe Askofu mzima ndani ya KKKT umeamua kumwagia Sifa kwa niaba ya kondoo wa Bwana na kanisa??

Ni hiyo kesi ya Vidagaa wa Rushwa hapo Arusha??

Askofu Laizer tunakuheshimu sana, usianze kuipindisha heshima.

MH Rais Moto uliouanzisha kwa kauri yako utazima tu endapo Mafisadi watateketea wote na kuacha jivu.
 

..so,what is your take?

..kwamba yote yanayosemwa ni upuuzi au hayapo au hayana ukweli?

..unajua,anyways....wewe unafaidika na nini katika kutetea haya!

..kama ungekuwa mwizi,wakakumata na kuanza kukupiga mawe,nami niko mtaa mmoja na hao jamaa[maana yake nimeathirika kwa namna moja au nyingine na wizi wako],nisingerusha jiwe hata moja!ningeangalia halafu nikaondoka mara moja...nisije takwa ushahidi!

...hayo ndo maneno yangu!
 
..so,what is your take?

Yote yaliyosemwa ni TUHUMA kutoka upande mmoja!


..kwamba yote yanayosemwa ni upuuzi au hayapo au hayana ukweli?
Mambo yaliyosemwa ni ya maana sana kwa taifa hili, lakini TUSISITIZE UCHUNGUZI ZAIDI kuliko HUKUMU kabla ya UCHUNGUZI wa namna YOYOTE

..unajua,anyways....wewe unafaidika na nini katika kutetea haya!
Nafaidika kwa namna ile ile unayofaidika wewe,,, tofauti na wengine ni kwamba mimi napenda haki itendeke MAHALI kote hata KWA waziri amepewe haki yake ya KIKATIBA kujitetea kwenye mamlaka husika...


..kama ungekuwa mwizi,wakakumata na kuanza kukupiga mawe,nami niko mtaa mmoja na hao jamaa[maana yake nimeathirika kwa namna moja au nyingine na wizi wako],nisingerusha jiwe hata moja!ningeangalia halafu nikaondoka mara moja...nisije takwa ushahidi!
Yesi nisingepiga mawe, kumbukeni KWAMBA si vyema kuua waporaji wa simu,,, KUMBUKA HUKUMU YA KUA KWENYE VITABU VYA DINI, Havikusema UUE ukiibiwa

...hayo ndo maneno yangu!

Ahsante kwa maswali mazuri yenye kuhitaji kuchanganua mambo
 
Yesi nisingepiga mawe, kumbukeni KWAMBA si vyema kuua waporaji wa simu,,, KUMBUKA HUKUMU YA KUA KWENYE VITABU VYA DINI, Havikusema UUE ukiibiwa

..haswaa!usingepiga...ungekuwa unapigwa!.kama umenifahamu hapo!

..sikufahamu kama we ni mcha mungu!hongera!ila kumbuka kuwa vitabu vinasema dhuluma ni dhambi!na uongo ni dhambi pia!na kutochukua hatua ni dhambi pia!

..asaalam aleykhum!
 
..haswaa!usingepiga...ungekuwa unapigwa!.kama umenifahamu hapo!

..sikufahamu kama we ni mcha mungu!hongera!ila kumbuka kuwa vitabu vinasema dhuluma ni dhambi!na uongo ni dhambi pia!na kutochukua hatua ni dhambi pia!

..asaalam aleykhum!

--Waleykhum Salaam!!!

Lakini dhambi ya KUDHANIA ni Mbaya sana, Na DAMBI ya KUA sisemi...

Dar si Lamu,

Mrudie/Mche Mola wako Ukweli ule wa Kumcha, haswa hizi siku chache za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani!!! Acha Kumdhania Mwenzako Uongo!!! Inshallah Ukatubu especially kwenye mwezi huu wa toba!!!

Yote tunayosema ni HEARSAY,
 
Dar si Lamu,

Mrudie/Mche Mola wako Ukweli ule wa Kumcha, haswa hizi siku chache za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani!!! Acha Kumdhania Mwenzako Uongo!!! Inshallah Ukatubu especially kwenye mwezi huu wa toba!!!

Yote tunayosema ni HEARSAY,

..uko dunia gani weye?

..ngoja nijinyamazie miye!

..aliyegizani usimwekee mwanga,akiona njia atakutelekeza!
 
Kilitime yuko sawa, mpaka sasa hizi ni TUHUMA. Aliyetoa hizi TUHUMA mwenyewe hajakwenda MAHAKAMANI.

Itakuwa vyema kama Dr Slaa atafungua kesi dhidi ya anaowatuhumu ili haki itendeke badala ya kutumia dhana kuwachafua.
 
Kilitime yuko sawa, mpaka sasa hizi ni TUHUMA. Aliyetoa hizi TUHUMA mwenyewe hajakwenda MAHAKAMANI.

Itakuwa vyema kama Dr Slaa atafungua kesi dhidi ya anaowatuhumu ili haki itendeke badala ya kutumia dhana kuwachafua.

..nshakufamu ustaadh!

..natafakari maana ya jina lako!

..ila,si vyote au yote yanayofunguliwa kesi...ndo maana hata baadhi ya walio-supposedly chafuliwa hawajafungua kesi!
 
kuna kesi nyingine anayetakiwa kufungua ni Jamhuri!! makosa ya Kuhujumu uchumi na vitu kama hivyo Jamhuri ndiyo inapaswa kuyaleta.
 
huyu kikwete anadhania tanzania bado iko enzi za ujima. siki hizi hata wanakijiji hawadanganyiki. ni aibu kwa rais wa nchi kulichukulia taifa zima kama mazezeta. serikali ya ccm ni serikali ya wezi. period.hakuna hata fisadi mmoja ambaye anaweza kuwajibishwa na vyombo/taasisi zetu kama zilivyo sasa. wote wananuka rushwa. uvundo mtupu.

ni aibu kumuona mtu mzima kama ngombale mwiru akitishia kuwakama ta watu wanaohoji ufisadi. hii ni sawa kweli? eti mshauri wa siasa..well kama yeye ni political guru ushahidi uko wapi? vitabu gani kaandika? hakuna. kazi ni kusinzia tu na kuiba.

sasa huyu mwaura kweli mnategemea aseme nini wakati ni mtoto wa system? nchi yetu imetekwa nyara na mafisadi, lakini tutaikomboa tu. na watalipa!
 
Inashangaza sana JK anapodai kuwa wapinzani wamekuwa washtaki na mahakimu (watoa hukumu) hali ni yeye aliyeombwa kuunda kamati maalum na muda wote amekataa akidai anataka Ushahidi!.. Huu ushahidi yeye anautakia nini ikiwa swala hili litamalizwa mahakamani?..Hawa jamaa ni suspect tumeomba kikao maalum kuchunguza report zote za pande mbili ili kuweza kutoa hukumu yenye haki kwa pande zote.

Ni ushahidi gani JK anautaka ikiwa kweli Karamagi alikwenda London na kuweka mkataba! Huu ndio ushahidi wa wananchi ambao Karamagi hajakana kuwa maneno haya ni ya Uongo ila alichokataa ni maelezo yaliyodaiwa kuwepo ndani ya mkataba huo..Kati yetu wanaounga mkono na wale wasiounga mkono hatuwezi kujua ni yapi maelezo ya ukweli unless kuna kikao maalum kitakachotazama ushahidi wa pande zote mbili. Rais wetu kumtetea Karamagi hii ndiyo HUKUMU!

Ni hukumu kwa sababu kauli yake ndiyo pekee yenye uwezo wa kusimamisha uchunguzi ama kutokuwepo! Dr. Slaa hana uwezo wa kutoa hukumu wala hakuna hatua hata moja iliyokwisha tekelezwa kutokana na hukumu inayodaiwa na rais!... Ni hukumu gani imetolewa na wapinzani?

Ajabu rais wa nchi kutetea mkataba ulowekwa sahihi ktk chumba hotelini kisha bado anawadai wananchi ushahidi!..Kwa nini asimwombe Karamagi ushahidi unaopinga maelezo ya wananchi?.. he know kuwa Karamagi kaweka mkataba kwa nini asiutupie jicho kuona - Je yanayosemwa ni uongo, atueleze yeye huo mkataba unasema nini.
 
Halafu kama kawaida hakuana aliye tayari kujibu hoja za msingi isipokuwa kutoa siasa za vitisho!
 

Baaada ya kuisoma hii article, ni kwamba ukweli au betweeen the lines wa ishu nzima uko kwenye hivi vifungu viwili, Mkuu Killtime, heshima sana kwa maneno yako ambayo ni clear kuwa ni ya mwananchi mstaarabu, na asiyekuwa na unazi,

Muungwana is right, kuwa so far ni tuhuma tu, ila tunataka kumkumbusha kuwa effort zake hazitoshi kwenye rushwa, asiwe na wasi wasi sana, lakini pia aheshimu changes za ki-maisha, ambazo ndizo haswa zilizompa urais against all the odds, ni hizo hizo changes zinazoendelea kisiasa katika wananchi wetu sasa hivi, na zilitakiwa zi-sart somewhere, na in some fashion, sasa kilichobaki ni pamoja na yeye sasa kuanza kubadilika ili awe on the top of the game za hizi changes za kisiasa, hakuna anyetaka kumpindua au kumfanyia matatizo, au kupunguza heshima yake, ila tu ni a wake up call,

Huko Nigeria, wao huwa wanapindua nchi, sisi ni makelele ya kuwazomea mawaziri na kuunywea chai mktaba wa Buzwagi, we are doing better than Nigeria na Psakistan kwenye hilo, kwa hiyo aongeze kazi na seriousness kazini, kwenye ishu ya Zitto na bunge, tumelikoroga wenyewe CCM sio siri tena, sasa tulinywe likiwa la moto, hakuna wa kumlaumu maana tunahitaji tu kuangalia kwenye kiooo kumpata aliyetuponza!

Isipokuwa next time asidanganywe tena na hawa mapadiri wanaotaka kumtumia tu kuchanga pesa za kanisa!

Heshima Mbele!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…