Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Rais Mstaafu BM akiwa na mkewe wakielekea kupiga kura huko Sea View:
 
Mgambo watishia kuzuia masanduku endapo hawatapewa ela yao, coz toka jana wamelala na njaa, sijui ni jimbo gani , mwenye taharifa zaidi atupe, nimeikuta kati habari hii chanel ten
 
Need we say more?

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00047.jpg
    DSC00047.jpg
    24.1 KB · Views: 138
Haya sasa, mie nataka nipumzike kidogo, updates muhimu, sijasikia toka Mbeya, kuna endelea nini huko jamani??? tafadhali tujulisheni basi, DAR kwema sana na leo magari ni machache sana mtaani!!! haya baadae ili tujiandae kwa safari ya kukuhabarisheni usiku kucha!!! vipi tutashinda jamani? Nisalimieni malaria sugu
 
Star TV wanareport kuwa Rukwa hali ni Shwari na zoezi linaendelea vizuri.
 
Lakini huyu bwana mdogo RIZ1 ni nani katika nchi mpaka anapewa nafasi ya kuulizwa masuala ya kitaifa? Haifurahishi kabisa jinsi nchi inavyoendelea!

Hao waandishi kama wanafikiri kuwa wanamjenga huyo dogo, ndo wanammaliza kabisa. Yaani baada ya JK kuhama Magogoni huyu kijana ataishi maisha ya taabu sana. Asipoangalia atakuwa anarushiwa mayai viza kila siku.
 
naelekea kupiga kura, sijafika bado ila sina shaka nitawahi. Ambye bado hajapiga namsihi akapige. Kigogo, katavi, baba enock, na wadau kama burn, MS sijakusikieni kabisa rafiki. Mpo?
 
PayGod, nadhani itakua ni Dar kwani si ndio walitangaza kuwatumia mgambo? haya sasa, wameshikwa pabaya!!!
 
Pwani.....mawakala wako nje wanapunga upepo wakati masanduku yako ndani!!!Ngoja kura zichakachuliwe:A S angry:
 
JK:

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00049.jpg
    DSC00049.jpg
    29.1 KB · Views: 122
kazi nimeimaliza kwa sasa... Narudi home kupata lunch kwa amaaaani. Kazi niliyobakiza ni kuomba ili haki itendeke.. Jamani ambao bado pleeeease wahini dk chache hizi!
 
Kwa Mathias: mgombea wa ccm abeba wapiga kura kwenda kwenye kituo, naskia kuna vurugu tandika
 
CUF NA CCM wanazipiga saa hizi hukooo AZIMIO- TANDIKA kisa CCM wanalazimisha kua karibu na kituo tofauti na sheria ya kua mita mia moja, POLISI wamefika
 
Kituo nilichopigia kura mimi wale makarani waongozaji bure kabisa, wamenilekeza milango zaidi ya minne na huko kote hakukuwa na jina langu. Nikawaambia, acheni ubabaishaji, nitajihudumia mwenyewe.

Nikapitia milango yote 15; pale kituoni nikisoma kila jina kwa kutrack kialphabet, baada ya milango tisa nikaona jina Mama mdogo, moyo ukatulia, nikapiga kura kuchagua rais, mbunge na diwani wangu! Ajabu yule msimamizi hata hakuniuliza kamna najua kusoma na kuandika, wala kunielekeza tick niweke chumba gani.

Niliamua kukaa pale kuwasaidia wazee na wasiofahamu kusoma na kuandika wapatao kumi na watano, I repeat 15, kutambuwa wamepangwa kuingia chumba gani. Nimechukia sana kufanya kazi za hawa makarani waongozaji wakati wao wamekaa tu wanatumbua macho na kunywa soda! Ila nimefurahi nimetimiza wajibu wangu wa kiraia, na niliowasaidia, nilishia kuwaonyesha milango husika, sijaifluence kura zao.

Rai yangu, tume ya uchaguzi naona hawajifunzi kutokana na makosa, kwani errors za 1995, 200 na 2005 zinajirudia leo 2010, hawakuwa wamejitayarisha kikamilifu!!
 
Muda wa kupiga kura umeshaisha lakini kulingana na habari kutoka kwenye vituo vingi hakuna watu wameshaisha. Kuna habari kwamba vituo vingi wamejitokeza watu KATI YA 100-200 TU. Wengine wameshindwa kuona majina yao kwenye Orodha ya wapiga kura au wamekuta namba zao zimekosewa.

Kwa maana hiyo kama wastani wa watu waliojitokeza ni kati ya 100-200 kwa vituo vyote 53,000 tunategemea IDADI KAMILI ITAKUWA KATI YA 150(wastani kwa kituo) x 53,000=7,950,000 ondoa majimbo au vituo ambavyo Uchaguzi umesimamishwa wastani wa vituo 150 x 3 majimbox 500 =225,000. Ukitoa idadi hii toka 7,950,000 unabaki na kitu kama 7,725,000.

SWALI NI:
  1. JE, NEC WALITOA HESABU ZA UONGO ZA WAPIGA KURA MILIONI 19.6????
  2. MILIONI 12 WAKO WAPI????JE WAMESHINDWA KUJITOKEZA, KWANINI?
  3. JE,CCM WATATUAMBIA WAMEPATA KURA NGAPI ZA KISHINDO KWA 80%?????
80% YA 19.6M NI KURA 15.6M.
80% YA 7.7M NI KURA 6.16M JE,CCM WATATUPA FIGURE IPI KATI YA HIZI MBILI NA HAPA HUJAONDOA KURA ZA CHADEMA,CUF,UDP n.k.

MIMI NASEMA HAPA NDIPO PA KUWAKAMATA CCM NA KURA ZAO ZA KUCHAKACHUA! ANY FIGURE RELATED TO THE 2 FIGRES ABOVE WILL BE QUESTIONABLE!!!!!

TUSUBIRINI MATOKEO BILA SHAKA YATASHTUA WENGI.
 
ngoja tuwasikilize akina kiravu sijui watatokaje .....wajue kabisa hii sio 2005 wala 1995
 
makoye

kwenye vituo vya watu 300 ndo wamejitoeza hao 200 labda

vituo vyengine wamesema watu 95% wamefika na kupiga kura
 
muda wa mwisho kupiga kura ni saa kumi na mbili jioni, kwa hiyo kama kuna eneo ambalo lina foleni na saa kumi iliwakuta kwenye foleni hao wataendelea na foleni na zoezi la kupiga kura mpaka saa kumi na mbili jioni
 
Back
Top Bottom