Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa na Chenge wameshawajibishwa huko Dodoma au bado? Ni kwa sababu gani aliamua KUTUFICHA mpaka leo hii sisi walipakodi?

na hilo ndo kosa lao!
KAMA ANAIPENDA HII NCHI NA ANGEPENDA KUWA RAISI WA HII NCHI KWANINI AFICHE MAMBO MAKUBWA KAMA HAYO HAWA HAWAKO TAYALI KUFA KWA AJILI YA NCHI HII INAFAA NCHI IWAUWE TUU!
 

Huyu (ENL) alijipanga kujisafisha na bila Mkapa kumnongoneza Mwenyekiti hili swala la Gamba linge leta mwendelezo mkubwa kwenye kikao..kilicho baki kwa EL ni kuhakikisha njia ya kuingia IKULU ni nyeupe ndo maana anarudisha mambo ya 1997 na sasa yanamlenga mwenyekiti.Kwa garama yoyote huyu anaitaka IKULU na mtu wa namna hii mwogope kama ukoma achilia mbali huo ufisadi anaotuhumiwa nao.
 
Mkuu umetaka kunipa BAN bure umeshanihukumu kuwa mimi CCM, natumia masaburi nk ila kwanza umeshindwa kwa jina la aliye hai aka mungu...

Pili nakanusha mimi sio CCM bali ni mtaji tarajiwa wa chama cha mgombea binafsi in future ccm naichukia mpaka najikuta nawachukia na watu wake wote mpaka jirani yangu kisa ni ccm, chadema nakipenda sana kwa sera na utekelezaji wake bali sio msimamo kwani Dr..Slaa ni Mtumishi wa mungu na msomi atachukuwa muda mrefu kuikomboa nchii hii kwani ukombozi wa nchi hii unatakiwa ufanywe na mtu ambaye ni jihad kweli kweli maana hakuna democrasia hivo panahitajika nguvu ya ziada ambayo ni uma na yeye Dr slaa anaogopa lawama na kadhia endapo jaribio likifanikiwa au kutokufanikiwa na kwa sababu ana nia ya dhati ya kurudisha madaraka kwa wananchi kikatiba basi anaogopa asije akahukumiwa na katiba hio hio kwa kusababisha au amasisha maandamano ambayo yatakayo sababisha watu kupoteza maisha..

Mfano mzuri Arusha walikufa watu watatu kama sikosei ndani ya maandamano ya masaa chini ya sita je Tanzania nzima unadhani wakiandamana watakufa watu wangapi ndani ya hayo masaa sita? Ikumbukwe maandamano yenyewe hayatakuwa na kikomo je kwa elimu ndogo ya akina mura afwande nanii wataua wangapi? Je wale watakao kufa kwa sababu nyingine ni wangapi? Dr anapata wakati mgumu anapowaza hayo mambo na alivyojengeka kiimani tena ndio anajikuta akionea huruma roho za watanzania..

Back to Mtu kama Lowassa, Lowassa kama angekuwa ndio dr slaa kishaeleweka siku nyingi maana huyu jamaa ana msimamo sana tena zaidi ya sana jiulize alipata wapi ujasiri wa kujiuzulu uwaziri mkuu? ni mfano wa kuigwa, japokuwa anaiba lakini anapiga kazi sana huyu jamaa, mmelia na akina ngeleja, abasi na wengine mbona ni watu wadogo sana ukilinganisha na waziri mkuu na wamegoma kujiuzulu?? unadhani ni kwa nini aliamua kukaa kimya muda wote huo bila kuliongelea hilo? na kwa sisi tunavoelewa huyu jamaa ndio Tanzania na siku akiamua kufunguka ndio tutajua zaidi ila mimi naona bora huyu kuliko jk..

Kwa hiyo ntake radhi bana mimi sio CCM.
 
kwa mara ya kwanza leo nimeona umeandika zaid ya mistari mitatu...hahahahhaha
Acha kuchakachua mada. Hapa tunaongea mambo ya muhimu yenye mustakabali kwa taifa letu. Leo nataka hii siku tuongelee tu chama chetu tawala. Kile chama kingine hakitakiwi kuzungumziwa kabisa hapa JF. Mpaka 2015 watanzania tutakuwa na option moja tu ya chama cha mababu zetu!
 
"Nguo ya kuazima haisitiri"Masaburi"

Nimekuwa nikifuatilia mara nyingi hoja zako na leo hii nimethibitisha kuwa wewe ni"MNAFIKI"
 
Dah Mwalimu, ufufuke uone wezi na majambazi wanavyotamba ndani ya vikao nyeti vya chama ulichokiasisi. Kwa kuwa wote walioko mle hakuna wa kumnyooshea mwenzake kidole. WATANZANIA nao tunatazama mambo haya kama sinema ya kawaida huku nchi inabaki mifupa. Tunaandamana kwa ajili ya Meya wa Arusha tu.
 
Kweli jk hana ubavu kwa mamvi lakini hilo la mamvi kuwa rais wala haliji.
 

FaizaFoxy; naamini Thread hii haijakaa vizuri masikioni mwacho. Huu ndiyo ukweli wa mambo from a reliable source. Haya ndiyo matunda ya siasa za kibongo zisizo na mashiko; unaweza kutumwa na boss wako uwe puppet-master ktk issue
Fulani, lakini upepo ukibadirika basi usishangae ukawa scape-goat.
Hizo ndo siasa zenu, sasa unashangaa nini !
 
Tatizo lenu CCM wote mnalijua ..tatizo kuu ni kikwete huyu ndiye anakivuruga chama......hizi kashfa za kina Lowassa hizi leo ukimuuliza anaonekana hazijui na anawatetea wezi wenzie....cha maana sijakiona katka vikao vyenu hivyo....
 
Gazeti hilihili liliwahi kutuaminisha kuwa CC ni pro Sitta, ila kikao cha maamuzi NEC ni pro Lowassa.

Sasa kama issue ya gamba imerudishwa CC kwa maamuzi, maana yake ni nini?...

Au kwa vile iko dhahiri sasa kuwa Mwenyekiti mwenyewe ni pro Lowassa, kwa hiyo hoja ndio imekufa?
 
OK, alitaka kuvunja mkataba huo kama walivyokuja kufanya baadaye na matokeo tunadaiwa mabilioni. Lowasa anaweza kuueleza umma wa watanzania ni nani aliyewezesha Richmond kupewa mkataba huo aliotaka kuuvunja?

Ajabu ya wadanganyika hawajiulizi hili swali muhimu sana.

Wao kila siku ni kudandia treni kwa mbele, halafu wakishapondeka ndo wanaanza kulalamika.

Golden question: NI NANI ALIWEZESHA/ALISHINIKIZA RICHMOND IPEWE MKATABA WAKATI HAIKUA NA FEDHA, VIFAA, WALA UZOEFU WA KUFUA UMEME?

Tunaomba LOWASSA amwage kila kitu hadharani kama kweli anataka kujisafisha, la sivyo bado GAMBA limemng'ang'ania machoni kwa watanzania.
 
Kama ni kujiuzulu Lowasa alitakiwa kufanya hivo wakati JK amemkatalia kuvunja mkataba wa Richmond mapema kwa kuwa alishajua ulikuwa wa kitapeli na wizi mtupu. Hakufanya hivo.
 
There are currently 698 users browsing this thread. (140 members and 558 guests)

Bado naendelea kufuatilia filamu ya Magamba naona karibu inamalizika au hamjui mwisho wa picha Steering lazima ashinde !!1.
 
Hizi habari za kujivua gamba zinanichefua mno kwa sababu naona kabisa ni usanii.
 

Muheshimiwa hapo kwenye RED mimi nakukatalia 100% siyo kweli kuwa Mzee ruksa alikuwa chaguo la Mwalimu la hasha...Kulikuwa na zengwe kubwa ndani yake...lakini kulikuwa hakuna jinsi ni lazima ionekane kuwa pendekezo la kwanza ni mzee ruksa....

Chaguo la mwalimu wakati ule alikuwa Waziri mkuu wa wakati ule Salim Ahmed Salimu..Lakini kwa busara zao waliona isingependeza kumpendekeza mgombea wa kwanza awe waziri mkuu badala ya makamo wa raisi na raisi wa Zanzibar kwa wakati ule amabaye alikuwa Mzee ruksa....ndipo alipoitwa mzee ruksa na kuombwa akubaili hilo ombi ...lakini akaambiwa wakati wa mkutano mkuu wa CCM pale Chimwaga atakapo tangazwa kuwa yeye ndio Mgombea uraisi ajaye......baadae yeye ashukuru kwa kumpendekeza lakini atoe udhuru kuwa nafasi hii yeye ahiwezi ni kubwa sana kwake....

Naye mzee Ruksa akapata washauri wakamwambia mzee usiwe mjinga wewe lini tena utakuja kuwa raisi...ndipo yeye alipo simama baada ya kutangazwa kuwa ndio mgombea..badala ya kutoa udhuru yeye alikubali moja kwa moja.....na ndio hapo ilipochipuka uhasama wa chini chini kati ya Mzee ruksa na Mwl...na migongano ya hapa na pale...mwanzoni wa utawala wa mzee ruksa...sasa wewe unatumabia Mzee ruksa alikuwa chaguo la mwalimu hii sio kweli...kama unampigia chapuo Mr Lowasa mpigie tuu lakini sio kwa kisingizio hiki
 

Makatibu (Luhanjo) + JK = Jairo... Ohhh sorry, should be Richmond and Jairo behind,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…