Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!


Redbold


Katika hotuba yake ya mwisho kama waziri mkuu Bungeni Mh. Lowassa alisema hivi na mnukuu " mwisho wa kunukuu.

1. Mh.Lowassa naye alilidanganya bunge kwa kusema kuwa alifikiria tuhuma dhidi yake ni uwaziri mkuu wakati anajua kabisa hilo haikuwa sababu ya kutuhumiwa hivyo.

2. Kama alijiuzulu kwa kulinda heshima ya chama(Mwenyekiti wake) na serikali yake(Rais); huku akijua kitendo hicho kilikuwa kinatoa fursa ya kuficha uovu(ufisadi), haoni kuwa hakututendea haki watanzania tupendao utawala bora na wala hatupendi kabisa utawala balaa?
 

SOURCE: TANZANIA DAIMA 25/11/11.

WanaJF, sasa nitawahoji:
1. Je, baada ya kupasua jipu huko Dodoma, CCM sasa ni wamoja na wamepona kabisa au jipu limegeuka kuwa kidonda ndugu?
2. Kitendo cha Mkapa kumpa mwongozo Kikwete wa jinsi ya kuipotezea hii issue ya ufisadi kinaleta taswira gani juu ya uwezo wa Kikwete kama kiongozi mkuu?
3. CCM waendelee na mfumo wa sasa wa mwenyekiti kuwa ndiye mtendaji mkuu, mkufunzi mkuu, mnadhimu mkuu, judge mkuu na msimamizi mkuu wa mambo yote ya chama?
 
Masikini Nape mmemponza mwenzenu (kwa ujinga wake ofcourse) kwa kumvimbisha kichwa na posts zenu zisizo na miguu wala kichwa, kama Nape atawajibishwa wewe Rejao, ritz, mzee, faizafoxy, Topical mnahusika kwa njia moja au nyingine na yatakayompata hamuwezi kujitetea.
 
Nape ni mtu niliyemwaminia sana CCM kuwa ni asset kubwa yenye very bright futute, alipoanza kupuliza vuvuzela la kujivua gamba, kuna kitu nilimweleza humu humu jf, sasa kimetimia!.

Masikini Nape sio asset tena, ni liability!.

Mkuu hebu tuweke hisia zetu pembeni for once. Hebu nieleze makosa ya Nape kwa kuzingatia

1. Nini Kazi za Katibu Mwenezi Taifa wa CCM
2. Kikao cha NEC cha April 2011 kilitoka na maazimio 26, lipi lilipewa uzito zaidi.
3. Hilo Azimio Lilisemaje?

Binafsi bado nafkiri Nape ni kiongozi imara na ameprove kuwa na guts ambazo ni nadra sana kuzikuta kwa wanasiasa za Tanzania.

Lakini Bosi wake mwenyewe ndio haeleweki ana nia gani au ni KIGEUGEU.
 
Licha ya hii ya Richmond ambayo tunajua urafiki, unafiki na kubebana kunakoiua CCM ndio kulimbebesha Lowasa hili zigo (offcouse alipata chochote) kuna ufisadi/ wizi, kutokuwajibika kwingine anakohusishwa nako?

Kujilimbikizia Ranch za Taifa alipokua Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo na hata namba za vitalu zipo. Kuingia mkataba wa kifisadi wa jengo la Umoja wa Vijana CCM, Nape akamchana live kwa kuonesha sahihi yake kwenye huo mkataba bomu. Kwa taarifa tu, huo mkataba umeshafanyiwa marekebisho makubwa sana na kuondoa vipengele vya kifisadi. Jiulize wakati anasign hakuviona hivyo vipengele au kitu alicholishwa kilimpofua?

Na mengine mengi yamejaa kwenye thread nyingine nyingi juu ya huyu mtu...
 
Ndio maana baadhi yetu tunahoji kwa nini Lowasa hakujiuzulu wakati ule JK alipomkatalia kuuvunja mkataba wa Richmond baada ya kumpigia simu akiwa nje ya nchi? Kwa nini suala hili liliendelea kuzimwazimwa na Lowasa mwenyewe kwa kuwatumia akina Hosea hadi Bunge lilipounda kamati ile ya akina Mwakyembe?
 

Mkuu huyu jamaa anamatatizo sana.

Badala ya kujitazama alipojikwaa, yeye yuko busy kushift the blame.

Kazi kusema TATIZO NI UWAZIRI MKUU, mara TATIZO NI URAIS,... Hakuna hata siku amejiuliza pengine TATIZO NI TAMAA YANGU NA TABIA YA WIZI.
 
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), alinukuliwa akisema: “Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?”.

“Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,”alinukuliwa akihoji Lowassa.

Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: “Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo”.

Lowassa alisema kama alivyozungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa walipokutana jijini Dar es Salaam, tatizo kubwa analolifahamu la vita ya sasa ni urais wa 2015.

“Mwenyekiti nikukumbushe jambo jingine, kule Zanzibar mwaka 1997 walipoleta tuhuma za mtizamo wa umma dhidi yako, ulisema kwamba kuwa Rais ni mipango ya Mungu,”alinukuliwa Lowassa katika maelezo yake ndani ya NEC

Alisema kwa kuzingatia mazingira hayo, hii leo si sahihi hata yeye (Lowassa) kuhukumiwa kwa kuzingatia kile kinachodaiwa kuwa ni mtizamo wa umma dhidi yake unaompa sura ya ufisadi, jambo ambalo alidai kwamba siyo la kweli.



"LOWASSA UKIGOMBEA MIMI KURA YANGU UNAYO NA KAMPENI NITAPIGA. ACHA WALE WENYE CHUKI BINAFSI KWA SABABU YA NAFSI ZAO BINAFSI. TUNAHITAJI KIONGOZI WA KUIVUSHA NCHI KUTOKA HAPA ILIPO KWENDA KWENYE HALI NZURI ZAIDI" WEWE NI CANDIDATE NAMBA MOJA AMBAYE MIMI NAMWONA HASA KUTOKA KATIKA CCM NA HATA UPINZANI!
 
Lowassa, acha waseme tu lakini wewe unafaa najua wale watz wasiopenda kuwajibika hawataki kukuona uko bado kwenye system!
 
wadau niwaambie ukweli lowasa wamemchafua tu.kama ccm itakuwa madarakani basi raisi wao awe lowasa hawa wngn wanafiki tu
 

Damn... I hope and pray this is not the case. Outright udini na MoU kabisa!

Mkuu ninavyofahamu mimi, wakatoliki na waprotestanti wanavyama mabalimbali miongoni mwao. Sasa hapa unataka kusema hata wapenzi na wanachama wa CHADEMA, chama chao hakitasimamisha mgombea wa URAIS iwapo Lowassa atapitishwa na CCM pamoja na zigo la mikashfa ya kuliangamiza taifa kwa ufisadi au watamuweka mgombea "boya" ili Lowassa ashinde kirahisi na kusiwe na mgogoro ya uchakachuaji?

If that is the case then naililia nchi yangu. UKOMBOZI wa kweli kumbe bado sana... Akina Slaa, Mbowe, Lissu wote watakua wanatuchezea akili zetu kama watoto wadogo. Huku hawana chembe ya uzalendo wa kweli. It has to be Slaa or LISSU for CHADEMA
ticket.

Lets wait and see 2015 kama CHADEMA wasiposimamisha a "really strong" candidate then the WRITING WILL BE ON THE WALL!
 
Hakuna mkweli kati yao. Kwa nguvu na mamlaka aliyonayo jk ndani ya chama na serikali kwa ujumla. It was a deal between lowassa aje aseme ivyo. Since wanachama wa ccm wanasurvive kwa kujipendekeza kwa rais ,ivyo walijua hakuna wa kumuandama jk kama wanavyofanya kwa lowasa
 

Hapa anatumia tu vitisho wasimshughulikie. Tatizo lipo kwenye kuingia huo mkataba, angetueleza aliyeshinikiza kutuingiza kwenye mkataba huo wa kitapeli, anatumia hoja dhaifu kutisha magamba wenzake na kwa sababu sehemu kubwa ni wezi basi wanahofu.

Atueleze mchako tangu mwanzo, unaingia mkataba mbovu na kampuni hewa, kisha unajijengea mwanya wa kuja jitetea eti nilimshauri rais tuvunje, utetezi wa kitoto kabisa.
 
Niceeeeee............!!!!! veriiiiiiiii gudiiiiiii, let me add this ujue Lowassa is free from magamba,...

JK kasemaaaaaaa....MWENYE USHAHIDI KUHUSU TUHUMA ZA LOWASSA AZILETE, LA SIVYO WAPAYUKAJI WAKINA NAPE & CHILLI. WATACHUKULIWA HATUA ZA KINIDHAMU, eeeehh bana JK kamaliza kazi, SUMAYE KAPIGILIA MSUMARI WA MOTO, yaani NGUVU YA SUMAYE + LOWASSA ni nomaaaa,

EL FOR PRESIDENT 2015, u hve ma vote, sisikii, sielewiii, sioniii, tunataka Kiongozi mchapa kazi, hata YESU ALICHUKIWA NA KUUAWA, sembuse Lowassa, go buddy....i am done, period..!!!
 
CCM wanamwaya EL and of course he has bigger brains than the rest Ikulu aspirant. CCM mtaji wao uliobaki ni EL JK anamalizia last chapters za riwaya yake ya Maendeleo kwa Kila Mtanzania.
 
Safari hii akina Makongoro kimyaaaa! Au wamepata ukweli mwingine kutoka "site"?
 
Reactions: 911
Mfumo wa Vyama vingi ulianza kipindi cha 92/93.

Uchaguzi Mkuu wa Urais ni kila baada ya miaka mitano, yaani 1995, 2000, 2010 n.k

Hiyo ripoti ya Mwakawago ya 1997 naamini ilikua ni huko CCM.

Jakaya Kikwete alishateuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa tangu 1995.

Rais Mkapa kwa utamaduni wa CCM ilikua akae vipindi viwili mpaka 2005.

Sasa hili la wananchi kutomkubali Jakaya Kikwete, tena mwaka 1997 mbona haliingii kichwani? au waandishi wamekosea kumnukuu?

Hii haijakaa sawasawa...
 
Mamvi ni rais wa JF tu na si vinginevyo... na ni raisi wa wale tu walio na mtindio wa Ubongo
 
Hiyo ni sehemu tu ya yale mengi ambayo Lowassa atayaweka wazi kadri siku zinavyozidi kwenda kimaandishi na kisauti pia kuna na hapo ndipo utakapogundua kuwa hakurupuki na ana sababu za kukaa kimya. Walimtoa Sokoine sasa tunae lowassa kumbuka mmsai hakisoma hafanyi ajizi.
 
Na bado, mengi yaja maana watu walimchafua sana EL bila kutafakari huku wakijua kuwa mzee huyu bado hajavunja ukimya wake! Kikubwa tumsisitize EL avunje ukimya aseme ukweli na aache huruma ya kuulinda maslahi ya serikali na chama kinachomchafua kila kukicha!! Huo ndio mwanza bado traller yaja.....pasua jipu hata kama itakugharimu maana ni aheri uhukumiwe na serikali na chama chako kuliko kuadhibiwa na umma. Maana yake ni nini; kwamba umma wataujua ukweli kwamba EL kahukumiwa kwa kuvunja ukimya na kueleza ukweli juu ya Richmond kwa umma!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…