asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,035
Nioneshe ni wapi niliitetea Serikali mbili? mimi sijali iwe moja, mbili au tatu.
Lakini leo hujamsikia lukuvi? ansema na hofu na Uislaam kuwa Zanzibar ikiwa na mamlaka kamili itakuwa Dola ya Kiislaam.
Tena kakiri kuwa maneno hayo kayasema kanisani na kakiri kuwa alitumwa na Waziri Mkuu.
Tunaposema, Tanzania tunaendeshwa na mfumo kristo , huwa mnabisha, haya bisheni sasa.
Jibu hoja zangu, Jee, Lukuvi unamuweka kundi lipi? au na wewe una Islamophobia kama Lukuvi?
Nani wa kumkanya William Lukuvi? FaizaFoxy
Kanisa gani unazungumzia au unamaanisha CCM? Wale Wazanzibar wote wamepewa maagizo kanisani bwana Ritz, HKigwangalla amepewa maagizo kanisani? Aden Rage na yeye kapewa maagizo kanisani? Samia Suluhu kapewa maagizo kanisani? Ina maana kina Jaji Warioba walipewa maagizo msikitini au wapi? Tundu Lissu alipewa maagizo msikitini au? David Kafulila alipewa na yeye maagizo msikitini au? wewe mwenyewe bwana Ritz umepewa maagizo wapi?
Magaidi bwana hata wewe kibibi unataka kuvaa bomu kweli muhammad kawakamata
Sent from Iphone
Hapana sio mimi mkuu uliposikia wamekudanganya bwana Izz ila ni mteule wa Rais bwana Lukuvi, na ni mnadhimu wa serikali bungeni inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Ndugu Jakaya Mrisho Khalfan Kikwete na makamo wake Dr Gharib Bilal, Lukuvi inawezekana akawa amepata maelekezo kutoka huko...Nasikia wewe ndio unamuandikia speech Lukuvi.
Tumeshawarecord na kesho mkisema tuliwanukuu vibaya tutawaonesha ushahidi mchana kweupe!
Na bado, mtaumbuka sana mwaka huu!
Tatizo ccm hupendwa na wanafiki kama faizafox,watu wakati wakipinga dhuluma za ccm inayoongozwa na kikwete,kinana ambao si wa kanisa anawatetea kwa nguvu zote,ila kwa chuki yake kubwa dhidi ya ukristo inashinda dhamira yake mbaya
Ni aibu kubwa kwa ccm,wanawatisha raia ili wapate nafasi ya kiasiasa bila kujua wanapasua nchi.
Siku waunguja na wapemba wakiungana ccm Znz itakua historia.
Lukuvi alikuwa ana lengo la kutisha na kuchonganisha ili matakwa yao yaweze kutimia ndio maana aliongelea kanisani ili aonekane yupo pamoja na wakristo katika kufanikisha matakwa yao, we si unaona Askofu aliyesimikwa alivyokuja ku bold maneno ya Lukuvi ili record ikae sawa, sasa wewe unataka angeongelea bungeni malengo yangetimiaje!?Lukuvi ni mkiristo na ndio alie sema kwa wakiristo wenzie kanisani kama anawasiwasi na Uislam.
Chakijiuliza kwanini akesemee kanisani wakati yeye ni mjumbe wa bunge la katiba na ktk wajumbe wenye nafasi kubwa ya kuongea mule mjengoni na yeye ni mmoja wapo. Sasa kulikoni ashindwe kuongelea mtazamo na wasiwasi wake dhidi ya uislam mjengoni akaongelee kanisani? Nisinge muona mjinga/masaliti na mchonganishi kama angeongelea ujinga wake mjingoni kama wanavyo ongea ujinga mwengine wenzake.
Mfumo Kristo umetapakaa kila pahala, hakuna chama utachokwenda ambapo hakuna hilo. Mimi ntapiganana huo mfumo nikiwa ndani ya CCM. Uwanja wa mapambano.
Kabla ya kutoka bungeni baadhi ya wabunge wa UKAWA jana, Professor Lipumba aliweka wazi aliyoyaongea kanisani waziri mmoja wa Serikali ya Muungano. Lipumba alisema kuna waziri kaenda kuhutubia kanisani kuwa "ikiwa Zanzibar itapewa mamlaka kamili basi mjuwe itaanzisha dola ya Kiislam".
Jana nikauliza ni waziri gani huyo? sikupata jibu humu JF.
Lakini kwa kuwa Mungu hamfichi mnafik, huyo waziri kajitokeza mwenyewe bungeni leo hii na kwanza kukiri kuwa katumwa na Waziri Mkuu na kusema kuwa hiyo ni hofu, "phobia" yake na akaendelea kusema "hakuna yeyote wa kunizuia hofu yangu hii".
Akazunguka wee na maneno lakini akashindwa kukisema kile alichokieleza Lipumba.
Kwa uchache, Lukuvi ameudhihirishia umma kuwa ana "Islamophobia" au hofu ya Uislaam.
Kiongozi unaefikia kutangaza Kanisani na Bungeni kuwa hutaki kuwapa mamlaka kamili Zanzibar kwa ajili ya dini yao, kweli hiyo si Serikali ya Mfumo Kristo tunayoilalamikia siku zote humu?
Na leo Lukuvi kahitimisha kwa kuniunga mkono yale ninayoyasema humu kila siku kuwa huu Muungano upo kwa ajili ya Kanisa. Na unaongozwa na Kanisa. Huwa mnajifanya hamnielewi lakini leo yamebainika bayana.
Wanaonisikitisha zaidi ni wale Wazanzibari waliobaki kuipigia makofi hoja hii ya Lukuvi, halafu wanajiita wao Waislaam. Waislaam mnaambiwa hampewi nchi yenu kwa kuwa Lukuvi ana hofu mkipewa mtaifanya dola ya Kiislaam na nyinyi mnashangilia? Yaani Lukuvi anawaambia kinaga ubaga kuwa mtabaki ndani ya mfuko Kristo mkitaka msitake na mkikataa basi ni bora nchi hii ishikwe na jeshi na akafikia mpaka kuwapa mfano wa Islamic Brotherhood ya Egypt.
Kinachonishangaza hii hofu yanini kwa Lukuvi? ikiwa nchi anayoiongelea ni Zanzibar na Wazanzibari 99% ni Waislaam ikiwa
wataamuwa nchi yao kuwa ya Kiislaam yeye anapatwa na hofu ya nini?
[video=youtube_share;PIAPAAd3Dck]http://youtu.be/PIAPAAd3Dck[/video]
cc Ritz, gombesugu, kahtaan, THE BIG SHOW, CHAMVIGA
Moderator tafadhali usiiunganishe hii na nyuzi nyingine hii maudhui yake inajitegemea.
Kwa hiyo kikwete na kinana nao ni wa mfumo kristu?Hata cuf inayoongozwa na maalim Seif nayo ni ya mfumo kristo?U r deluded. Nadhani una ugonjwa wa inferiority complex, dawa ni kujipanga na kutafiti kwa nini hawa jamaa wako juu tumia blueprint yao uwapate hata kuwapita si chuki za kiendawazimu,adui mkubwa wa wakristu ni shetan kwa nini unataka kufanya adui mkubwa wa waislam ni ukristu? Huoni kama ni udhaifu
FaizaFoxy
===>Si kila muislamu anataka serikali 3,na sio kila muislamu anataka serikali 2,hii pia iko kwa wakristo,sio kila mkristo anataka serikali 2,na sio kila mkristo anataka serikali 3, maana hapa ni kwamba,kuna vyama vimezoea kutumia dini kuwatishia watu na kupata ushindi wa bure kwenye chaguzi mbalimbali,siku utakayotembea uchi ndio ambayo utakutana na mama mkwe,au za mwizi ni arobaini,naamini watanzania wamegundua nini kinaendelea kuhusu siasa za vyama hasa CCM,Kumekuwa na malalamiko kila wakati wa kuwashutumu CDM kuwa wanatumia mgongo wa kanisa kujikita kisiasa,wamekuwa wakituhumu CUF kutumia misikiti kujikita kisiasa sasa nani anatumia dini imeonekana na imedhihirika wazi.
===>Pamoja na yoote hayo wapo wakristo wengi tu ambao wanataka serikali tatu na wapo waislamu wengi tu wanataka serikali tatu,hawa CCM wanalazimisha serikali mbili ili waendelee kukaa madarakani,waendeleze kurithi mema ya nchi hiii,na kama alivyosema mwenyewe Mh Lukuvi CCM wana hofu kuwa Chadema watatawala Tanganyika,na pia wana hofu kuwa CUF watatawala Zanzibar iwapo tu kutakuwa na serikali tatu,na hilo linaonekana wazi,hivyo hofu yao hawa ni Muungano wa CUF VS CDM kuelekea 2015 na kuelekea serikali tatu
===>Mchawi ameshaonekana,Adui wa nchi hii kajidhihirisha wazi kabisa,akataliwe kwa nguvu zote,ipatikane katiba ya wananchi ambayo itajenga Umoja,Undugu na mshikamano wa nchi hii,hizi janja za CCM kwenda kwenye nyumba za ibada ziwe mwanzo na mwisho wao,Watanzania tushirikiane kwa pamoja kuweka historia ya kuwa na katiba nzuri na kuwaondoa wakoloni weusi kwenye nchi hii
===>Serikali tatu zenye nguvu inawezekana kwa kila mtu kutimiza wajibu wako,AMKA TANZANIA!