Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Status
Not open for further replies.
Lipumba aliufahamisha Umma kuwa kila wakati waislamu wanapoomba dua (kwa kiarabu mara zote), wanaomba kuwa Mwenyezi Mungu awanusuru na Makafir, awaepushe na mbinu za Makafir. Akajibiwa Takbir.

Makafir ndio wakina nani?

Amandla.......
Mkuu............wala usipate tabu.

A confused mind is a lost mind.
Mnaipenda CCM ya LUKUVI, na Kuipenda Serikali ya Kikwete, ambayo ni ya Mfumo Kristo...
.....wtf !!is that?
 
FaizaFoxy kila siku nakwambia CCM hawafai siku zote unakana na kuwatetea. Wakati CUF ina nguvu walisema ni ya Kiislamu na CUF wamekuja na majambia kuua watu kumbe ilikuwa ni propaganda ya kutaka ushindi. Ikaja Chadema mliona walivyoeneza propaganda eti cahama cha Wakristo na Kikanda na nia yao ilikuwa ni ushindi, inakuja Muungano wanasema tukiruhusu nchi tatu Zanzibar watakuwa nchi ya Kiislamu na Jeshi litatawala. Leo hii wamesahau wananchi kwa maoni yao kupitia Tume ya Rais (Ingawa wao wanaita tume ya Warioba) ikiongozwa na Mheshimiwa Judge Warioba Former makamu wa pili wa Rais, Waziri Mkuu, Waziri wa sheria, mwanasheria mkuu wa serikali, judge wa kimataifa wa mambo ya bahari, judge wa jumuia ya Africa Mashariki, Ahmed Salum, Former Waziri mkuu, waziri wa Ulinzi, Katibu mkuu wa Africa, katibu wa Kudumu katika umoja wa Maifa,; Mh. Judge Ramadhan, Former Jaji Mkuu, Brigedia general wa jeshi, Mwenyeki wa Tume ya Uchaguzi na wengine watu wengi mashuhuri lakini CCM wanasema hawa watu ni wapuuzi

Ndio ujue kwamba hawa watu CCM hawaitakii nchi mema na wapo tayari kutumia hata jeshi ili kufanikisha mambo yao

Lukuvi leo kadhihirisha kinaga ubaga kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo. Haya tuliyajadili sana kwenye nyuzi ya Mohamed Said, watu wakapinga sana na kutubeza sana Waislaam. Lakini leo Lukuvi kadhihirisha na kasema ana "hofu" na hiyo hofu (phobia) yake kwa Uislaam hakuna wa kumzuwia.

Kikwete, ndio waziri wako huyo, ana hofu na Uislaam, jee hana hofu na wewe?
 
Huyu ajuza FaizaFoxy ni mnafiki sana..

Kwa hili halilolisema ni la ukweli asilimia zote! Unafiki huko wapi hapo? Kama kuzungumza lukuvi kazungumza kila mtu amesikia.

Na hapa amewapa majibu waislam yaliyo wazi kuwa hii serikali ni ya inaendeshwa kivatican.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli katoa kanisani..........So what?

Mtafanya nini?........Labda kuja kumbwelambwela hapa JF. Nothing More, nothing less.

A confused mind is a lost mind.
Mnaipenda CCM ya LUKUVI, na Kuipenda Serikali ya Kikwete, ambayo ni ya Mfumo Kristo...
.....wtf !!is that?

Mkuu,

Nakhis watumia mno lugha za tashtit na kebehi, ambazo haijengi asilan!...bali zazidi kuhatarisha hii hali tete inayolikabili Taifa letu changa kwa sasa!

Kama labda unajikhis una ghadhab nyingi!?... basi, kwanini usiketi kando na kuwaachia Wanajamvi wanzio wenye kumudu stahamala na staha ili kuendeleza mjadala huu!? Daah!

Ahsanta.
 
Wewe Kenge shosti, AK47 unqijuwa peke yako? Kwani mliikuta Zanzibar iko Africa Kusini? Ivyo unadhani huu Muungano feki ulikuja kuondoa Uislamu, umesikia wapi imani ikaondolewa na mtutu wa bunduki? Wameshindwa bwana zenu wazungu kule Afghanistan, mtaweza nyinyi? Watu wenyewe hata kuogelea hamjui.
Dogo kajifunze Afaghanstan ishakwisha habari yake.Halafu wewe sio gaidi ni mtoto wa mama flani hivi.Kaa pembeni ngoja nikuitie wenye vielement vya ugaidi uone povu lao.Haya @Bhoko Haram njoo kuja huku umfundishe ugaidi huyu kijana mpenda dunia.
 
Lukuvi leo kadhihirisha kinaga ubaga kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo. Haya tuliyajadili sana kwenye nyuzi ya Mohamed Said, watu wakapinga sana na kutubeza sana Waislaam. Lakini leo Lukuvi kadhihirisha na kasema ana "hofu" na hiyo hofu (phobia) yake kwa Uislaam hakuna wa kumzuwia.

Kikwete, ndio waziri wako huyo, ana hofu na Uislaam, jee hana hofu na wewe?

Serikali ya CCM haina maslahi kwa Watanzania, wewe pia unalijua hilo ingawa kila kukicha unaipigania hapa lakini zikija issues ndiyo unanza kuja na haya ya serikali Kristo blah blah blah. With CCM Tanzania haitafika popote ........... ni siasa tu hakuna maendeleo zaidi ya propaganda. Juzi juzi tu watu walikuwa wanauponda walaka wa Lema wakati una ukweli ndani yake. Udini unanuka Bongo noma na chanzo ni CCM!!
 
Leo nimeshuhudia wale wanaotugawa kwa kutumia Dini na hata ukabila,Lukuvi na chama chake hakika hawakwepi yatokanayo na kauli zenye kupandikiza chuki za Kidini.
Kwa kauli aliyoitoa Lukuvi na hakika madhara yake yanaweza kuigharimu Muungano hata kuliko hiyo serikali Tatu wanayoisingizia
 
wakati lukuvi anatamka (kujipaka mavi kanisani kama ulivyo sema) huo uharo alikuwa kajivua uanachama wa CCM?.

Mkuu,

Mbona watuletea hizo "siasa za uwanja wa fisi"!? Daah!

Tatizo lenu nyinyi "wataalamu" wa Bavicha/Ufipa...yaani takriban kila jambo basi mnahusisha ile vita ya walevi...yaani Chadema Vs CCM,sio!? Daah!

Ahsanta.
 
Hivi kwa nini Mheshimiwa Lipumba ametumia neno Interahamwe na sio Janjaweed? Wote hawa si vinara wa ethnic cleansing? Au ndio yale yale ya Umma?

Amandla.....
 
Wewe mwanamke always umekuwa na udini sana kila jukwaa upo. Huwa nafuatilia hoja zako zisizo na miguu wala kichwa naomba upunguze udini na kuwachukia wakristo maana wewe kila siku roho yako mbaya ni kwenye ukristo tu why. Jaribu kustaarabika
 
Lukuvi leo kadhihirisha kinaga ubaga kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo. Haya tuliyajadili sana kwenye nyuzi ya Mohamed Said, watu wakapinga sana na kutubeza sana Waislaam. Lakini leo Lukuvi kadhihirisha na kasema ana "hofu" na hiyo hofu (phobia) yake kwa Uislaam hakuna wa kumzuwia.

Kikwete, ndio waziri wako huyo, ana hofu na Uislaam, jee hana hofu na wewe?

Angalia nawe usije ingia mtegoni kuuchukia ukristo kwa sababu ya Lukuvi. Lukuvi hakutumwa na wakristo. Kumbuka kampeni za Makamba Arusha wakati akimnadi Batilda,alipoingia msikitini na kutaka waislamu wampe kura. Wanasiasa wetu wanadhani hayo yanaishia ktk siasa tu. Wamevuka mipaka!

Somo kubwa kabisa ktk maelezo ya mtu kama Lukuvi, ni imani yangu kwamba nchi hii inaongozwa na watu hovyo kabisa! wote tunahisia binafsi na watu mbalimbali ktk maisha yetu na hata ktk familia zetu. mengine yanastahili kuwa ni siri ya moyo wako na hasa unapokuwa huna ushahidi. Huyu kiumbe naamini kwa viwango vyote vya ngazi zote, tangu kijijini hadi taifa, hakuna anapostahili kushika madaraka. Lakini jiulize Rais wetu ambaye ni muislamu, naye ana hisia hiyo? Kama ni hapana kwa nini mtu huyu aendelee kuwa ni public figure?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

Mbona watuletea hizo "siasa za uwanja wa fisi"!? Daah!

Tatizo lenu nyinyi "wataalamu" wa Bavicha/Ufipa...yaani takriban kila jambo basi mnahusisha ile vita ya walevi...yaani Chadema Vs CCM,sio!? Daah!

Ahsanta.

ndivyo anavyopaswa kujibiwa yule mwanamama mwana CCM.hutakiwi kutumia upeo mkubwa kumjibu FF.saa zingine ni bora kucheza na akili yake ndogo.
BTW wewe unadhani muungano wa tz bara na znz una ukatoliki?!.kama sio akili ndogo nini hicho.
 
Serikali ya CCM haina maslahi kwa Watanzania, wewe pia unalijua hilo ingawa kila kukicha unaipigania hapa lakini zikija issues ndiyo unanza kuja na haya ya serikali Kristo blah blah blah. With CCM Tanzania haitafika popote ........... ni siasa tu hakuna maendeleo zaidi ya propaganda. Juzi juzi tu watu walikuwa wanauponda walaka wa Lema wakati una ukweli ndani yake. Udini unanuka Bongo noma na chanzo ni CCM!!

Yes! Huyu FaizaFoxy nimesoma mara nyingi maandiko yake, hudhani CCM ni mtetezi wake, ni kinga yake, ni mkombozi wake, n.k. Lakini anashindwa kabisa kuelewa kwamba huwezi kumutegemea CCM wakati unajua ni kundi lisilo na ethics. Watakufanyia lolote!

Leo sasa wamemuning'iniza na badala ya kuona ni kasoro ya CCM bado anapinda na kusema ukristo sijui ni nini!.... hai hoi hai hoi! Next time unapowasifia CCM ujue ni kazi ya kusafisha paka. Hakuna faida na sana sana tegemea makucha.
 
!
!
iyena iyena iyena iyeeena iyena iyeena sisiem nambari wani...
!
!
nadiriki kusema kwamba mbali nu kumpond lukuvi humu ndani ya jf hakuna lolote ambalo aidha waislamu au wakristo wanaweza kufanya.
!
!
selikali mbili ni lazima......tutake tusitake ila la maana tu kama wanavyohubiri kuwa hii ni ndoa,ni muda muafaka kutuambia katika ndoa hii nani mwanamke na ni nani mwanaume,baasi!...ili sasa baba mwenye nyumba aongoze familia yake.
 
Kabla ya kutoka bungeni baadhi ya wabunge wa UKAWA jana, Professor Lipumba aliweka wazi aliyoyaongea kanisani waziri mmoja wa Serikali ya Muungano. Lipumba alisema kuna waziri kaenda kuhutubia kanisani kuwa "ikiwa Zanzibar itapewa mamlaka kamili basi mjuwe itaanzisha dola ya Kiislam".

Jana nikauliza ni waziri gani huyo? sikupata jibu humu JF.

Lakini kwa kuwa Mungu hamfichi mnafik, huyo waziri kajitokeza mwenyewe bungeni leo hii na kwanza kukiri kuwa katumwa na Waziri Mkuu na kusema kuwa hiyo ni hofu, "phobia" yake na akaendelea kusema "hakuna yeyote wa kunizuia hofu yangu hii".

Akazunguka wee na maneno lakini akashindwa kukisema kile alichokieleza Lipumba.

Kwa uchache, Lukuvi ameudhihirishia umma kuwa ana "Islamophobia" au hofu ya Uislaam.

Kiongozi unaefikia kutangaza Kanisani na Bungeni kuwa hutaki kuwapa mamlaka kamili Zanzibar kwa ajili ya dini yao, kweli hiyo si Serikali ya Mfumo Kristo tunayoilalamikia siku zote humu?

Na leo Lukuvi kahitimisha kwa kuniunga mkono yale ninayoyasema humu kila siku kuwa huu Muungano upo kwa ajili ya Kanisa. Na unaongozwa na Kanisa. Huwa mnajifanya hamnielewi lakini leo yamebainika bayana.

Wanaonisikitisha zaidi ni wale Wazanzibari waliobaki kuipigia makofi hoja hii ya Lukuvi, halafu wanajiita wao Waislaam. Waislaam mnaambiwa hampewi nchi yenu kwa kuwa Lukuvi ana hofu mkipewa mtaifanya dola ya Kiislaam na nyinyi mnashangilia? Yaani Lukuvi anawaambia kinaga ubaga kuwa mtabaki ndani ya mfuko Kristo mkitaka msitake na mkikataa basi ni bora nchi hii ishikwe na jeshi na akafikia mpaka kuwapa mfano wa Islamic Brotherhood ya Egypt.

Kinachonishangaza hii hofu yanini kwa Lukuvi? ikiwa nchi anayoiongelea ni Zanzibar na Wazanzibari 99% ni Waislaam ikiwa
wataamuwa nchi yao kuwa ya Kiislaam yeye anapatwa na hofu ya nini?

[video=youtube_share;PIAPAAd3Dck]http://youtu.be/PIAPAAd3Dck[/video]

cc Ritz, gombesugu, kahtaan, THE BIG SHOW, CHAMVIGA
Moderator tafadhali usiiunganishe hii na nyuzi nyingine hii maudhui yake inajitegemea.

FaizaFoxy na Ritz mbona mnakinzana na CCM chama adhimu ?? Kwanini safari hii mnajitenga na kuweka dini mbele?
Nimekuwa nikiwauliza swali rahisi sana, kama katiba mpya ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, kwanini CCM wanataka kuidominate?
 
Last edited by a moderator:
Usikwepe hoja Mkuu,M/Kiti wa chama chako anataka serikali mbili za huo "Muungano wa kanisa" kwani kashikiwa bunduki na kulazimishwa? Wewe ni CCM damu na M/kiti wako katoa msimamo wa chama chenu ni Serikali mbili,swali Je unataka wapambane vipi kuuondoa huo muungano wa kanisa wakati wewe Mwislam na M/kiti wako mwislam pia mnautetea kwa mapovu na kuwakejeli kina Mzee Warioba (Mkristo) ambae alishauri kuwe na serikali 3?
Nadhani haumfahamu Ritz vizuri mimi sishikiwi akili na viongozi wa siasa kama nyie mnavyoshukiwa akili na Mbowe na Dr.Slaa, mimi naangalia dini yangu kwanza, wewe mbona hautaki kufuata tamko la Pengo anataka serikali mbili. mimi ni Mtanganyika nataka huu muungano uvunjike tuwakabidhi Zanzabar nchi yao halafu tupambane sisi kwa sisi huku Tanganyika, nyie wakirsto si mnafundishwa makinisani kwenu kuwa mchague serikali mbili, tusubiri tuone.
 
Huu nao ni Mfumo Gani FOX? Usipepese macho wala Kumung'unya maneno!! LIPUMBA AIBUA JAMBO ZITO - AKIRI KUMNUSURU KIKWETE UCHAGUZI MKUU MWAKA 2010

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na “kumnusuru” Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.

Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa.

Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.

Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.

“Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi,” alisema.

Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.

Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema “wenzetu wameanza kujipanga” kuelekea 2015.

“Kwahiyo kama Waislamu tunataka kupata haki zetu, kama tunataka kuishi kama raia wa daraja la kwanza katika nchi yetu, lazima tujipange kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; na sisi tuanze kujipanga kwa sababu wenzetu wameanza kujipanga, vinginevyo tutaendelea kubaki maskini na raia wa daraja la nne katika nchi yetu wenyewe.

“Mwaka 2010 wakati mshindi wa uchaguzi wa rais alipotangazwa, mimi nilikwenda kwenye hafla ya kutangazwa matokeo, na nilikwenda makusudi tu, siyo kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, ila nilikwenda makusudi kwa kujua hali ya kisiasa ilivyokuwa wakati huo.

“Huku nilikutana na Sheikh Basaleh. Nilipokutana naye, alinipongeza; sijui kama yeye anakumbuka, akaniambia ‘umeweka mbele imani yako na umekuwa mwelewa wa mambo.’”

Hata hivyo, licha ya Profesa Lipumba kuwaambia Waislamu wajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu, hakusema wajipange kupitia chama kipi.

Lakini alisisitiza kwamba uchaguzi ujao ni zaidi ya siasa au rais yupi anafaa, bali maslahi, hasa ya rasilimali nyeti zinazopatikana katika ukanda wa Pwani ya Mashariki, eneo ambalo alisema linakaliwa zaidi na watu wenye imani ya Kiislamu.

Katika moja ya kauli zake, Profesa Lipumba alisema kwamba kuna chama kimoja kinataka kuchukua madaraka ya nchi, lakini kinasaidiwa na mataifa ya magharibi, yasiyoenzi wala kuthamini imani ya Kiislamu.

Kwa muda sasa, zimekuwapo tetesi kwamba CCM imekuwa inafanya siasa za udini dhidi ya vyama vya upinzani, hasa inapoona maslahi yake yapo hatarini.

Mwaka 2010 makada kadhaa wa CCM walitumia mitandao ya simu kuchonga (spoofing) ujumbe wa simu ulioshambulia mgombea mmoja wa upinzani, ukimhusisha na imani yake.

Kauli ya Lipumba imethibitisha pia minong’ono iliyokuwapo muda mrefu kuwa baadhi ya kura za Profesa Lipumba zilipotelea kwa Rais Kikwete.

Katika uchaguzi huo, Lipumba alitangazwa kushika namba ya tatu, nyuma ya Rais Kikwete na Dk. Willibrod Slaa wa CHADEMA.

Alipoulizwa kuhusu ziara yake msikitini na kauli aliyotoa, Profesa Lipumba alikiri kwamba alikwenda kuzungumzia hali ya kisiasa nchini.
CHANZO: Tanzania Daima - Mei 26, 2013


Mkuu mimi ni Mkristo Mkatoliki. Tumtofautishe Prof. Lipumba,Mwenyekiti wa CUF Taifa na Waziri ktk Serikali yetu ya JMT. Lukuvi amefanya makosa makubwa,kama ingekua nchi nyingine ameisha jiuzulu!
 
Lipumba aliufahamisha Umma kuwa kila wakati waislamu wanapoomba dua (kwa kiarabu mara zote), wanaomba kuwa Mwenyezi Mungu awanusuru na Makafir, awaepushe na mbinu za Makafir. Akajibiwa Takbir.

Makafir ndio wakina nani?


Amandla.......

Wote wenye hofu na Uislaam "Islamophobia" kama vile Lukuvi, eti hiyo ni khofu yake binafsi!

Wewe vipi? huna hofu?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom