Luteni Ian Kagame

Luteni Ian Kagame

Pale kulikua na beef kati ya kagame na fred gisa rwegyema, kama ulivosema kagame alipoenda mafunzoni the issue ilikua Museveni alimpenda sana fred so ilikua zuga kwa kagame, ili jamaa akapindue kule ashike nchi, kagame ilimuuma na ukumbuke ni mwanzilishi wa RPF ndio maana wale founder wote wa RPF kagame aliwala vichwa maana walikua wanaona jamaa kadakia mchongo juu kwa juu, na Rwigyema ni mzaliwa wa Rwanda lakini akachanja mbuga kwenda Uganda ndio alikua moja ya makamanda hatari wa museveni, basi umafia wa PK kwa wenzake haujaanza leo kwenye vilima vya matimba akiwa na miaka 33 akauliwa na kuzikwa Remera, hadi hapo kagame akawa hana mpinzani wa maana tena, kwa ufupi ilikua hivo
Mbona huyu jamaa ana matukio mengi ya kutisha[emoji848][emoji848][emoji848]

Karma haifanyi kazi kwake kabisa
 
Hivi ilikuwaje watusi wa kutokea burundi na uganda wakatoboa huku waliotokea tz wakikwama?

Halafu ukumbuke watutsi wao walitokea tu Rwanda na Burundi huku majority ya waha wakitembea kutoka Bunyoro na nyankole uganda ndio wakawapitia wengine rwanda na burundi na wengine wakabaki ngara yaani wale wahangaza ni koo kwa waha na wanaongea lugha moja pia na kuelewana pamoja na wanyankole nao wakiongea wanaelewana na watu karibu wa Rwanda, Burundi, Ngara, Kigoma hasa Kibondo na kule kasulu, hivo number na uchache wao viliwazuia kuanzisha nchi nyingine kule kigoma wakamezwa wakawa wapole
 
Huyo bana alikua anampenda sana demu mmoja alikua anaitwa Alexia mupende ambae aliuawa 2019 kwa kupigwa risasi, maana huyo mwamba alikua anapiga alexia na ange sasa ange akatafuta means sana hadi abaki peke yake na pk anavopenda furaha ya mwanae inasemekana alexia akauliwa ilikua kama movie hivi, huyo mwamba ndio akawa analewa chakarii kwa kumpoteza kipenzi chake maana ange na mwamba walikutana USA wakiwa wote wanasoma na jamaa sio kwamba familia yao ya kinyonge hapana, sema wazazi wake walihamia Rwanda wakitokea Burundi ni watutsi wa Burundi japo ana uraia wa Rwanda,
Duuuh

Naonaga kama Ange anaishi marekani

So wazazi wa Alexia hawakutafuta justice?
 
Halafu ukumbuke watutsi wao walitokea tu Rwanda na Burundi huku majority ya waha wakitembea kutoka Bunyoro na nyankole uganda ndio wakawapitia wengine rwanda na burundi na wengine wakabaki ngara yaani wale wahangaza ni koo kwa waha na wanaongea lugha moja pia na kuelewana pamoja na wanyankole nao wakiongea wanaelewana na watu karibu wa Rwanda, Burundi, Ngara, Kigoma hasa Kibondo na kule kasulu, hivo number na uchache wao viliwazuia kuanzisha nchi nyingine kule kigoma wakamezwa wakawa wapole
Katika orodha makabila ya bongo watusi hamna ila wahutu wapo hii huwa nashindwa kuielewa kabisa
 
Katika orodha makabila ya bongo watusi hamna ila wahutu wapo hii huwa nashindwa kuielewa kabisa

Sema orodha ya makabila Tanzania imechanganywa ngoja nibase huko kigoma utakuta watu wanaitwa Wajiji wazirankende, hiyo ni koo ambayo inapatikana rwanda, Burundi, Uganda, Muleba kwa wahaya yaani koo moja ilikua inasafiri wnawaacha wenzao wale wanaobaki wanaitwa jina la kabila la pale wakafika hadi ujiji wakatulia, halafu kuna koo inaitwa abayango iko nchi zote hizo lakini kuna kitu hua nawaza kwamba bila wakoloni kugawa watu kwa mipaka jamii za afrika zinaingiliana sawa na mila na desturi za wameru wa kenya na tanzania, wajaluo wa kenya na tanzania, wamasai vilevile, wamakonde wapo msumbiji na mtwara huko, yaani mambo yalivurugika miaka ile ya 1884/1885 kwenye berlin conference
 
Kwanza wale katika nchi zao race hazizidi tatu yaani kuna wahutu ambao ni wengi Rwanda na burundi, kuna Watusti kabila linalofuata kwa idadi ya watu kwenye nchi zote sasa kuna watwa hii ni jamii dhalili na maskini sasa kwa Burundi na Rwanda wakoloni walichagua kufanya kazi za kiofisi na watutsi huku wahutu ambao ni wengi wakiachwa wafanye kazi za nguvu na kuwatumikia watusti ambao walikua wanamiliki mifugo mingi, na ikawa hivo uongozi ukaanza kua vita hadi leo sema watutsi shule iliwasaidia na kumiliki uchumi, na wanaushirikiano kupita maelezo yaani mtutsi wa Tanzania, Rwanda na Burundi kukuta wanaconnection sio ajabu, halafu walivoingia Tanzania walikuta wenzao waha wametangulia muda mrefu, ambapo kwa hao waha wakawameza watutsi sasa waha wanakua na viukoo vyao wanaita milyango kama wakimbili, wanyongozi , wajiji na kadhalika lakini walikua na tawala zenye nguvu na zinazomiliki uchumi tayari wakawa na akina mwami ntare na watangulizi wao hivo wakakosa nguvu na wakishia kule manyovu tu hawakusambaa zaidi, halafu, warundi, wanyarwanda na watu wa kigoma hasa waha wanaongea lugha moja na wanaelewana tofauti ni utamshi wa maneno wengine huvuta, wengine huongea haraka, halafu mfumo wa kiuongozi kwa Tanzania yenye makabila 120 , mila desturi za mtanzania wale wasingefurukuta kwanza wachache sana

Halafu ukumbuke watutsi wao walitokea tu Rwanda na Burundi huku majority ya waha wakitembea kutoka Bunyoro na nyankole uganda ndio wakawapitia wengine rwanda na burundi na wengine wakabaki ngara yaani wale wahangaza ni koo kwa waha na wanaongea lugha moja pia na kuelewana pamoja na wanyankole nao wakiongea wanaelewana na watu karibu wa Rwanda, Burundi, Ngara, Kigoma hasa Kibondo na kule kasulu, hivo number na uchache wao viliwazuia kuanzisha nchi nyingine kule kigoma wakamezwa wakawa wapole
Vita ya 1994 walikusanyika watutsi kutoka tz, ud na burundi sasa ilikuwaje wa kutokea tz hawakupata vyeo (kutoboa) baada ya ushindi wa 94?
 
Vita ya 1994 walikusanyika watutsi kutoka tz, ud na burundi sasa ilikuwaje wa kutokea tz hawakupata vyeo (kutoboa) baada ya ushindi wa 94?
Kwani wale wakina Prof Silas Rwakabamba,David Kaberuka etc wao walitokea nchi gani?
 
Pichani ni Ian Kagame (jina lake kamili ni lan Kagame Deogratius Rutagambwa) ambaye alijiunga na jeshi la nchi hiyo wiki iliyopita.

Ian alikuwa ni miongoni mwa Maofisa cadets 568 waliopewa kamisheni katika Chuo cha Kijeshi cha Rwanda ambao waliweza kufaulu mafunzo ya kijeshi nchini Rwanda, kemisheni hizo zilitolewa na Rais Paul Kagame mwenyewe.

Ian Kagame Deogratius Rutagambwa ambae ni moja ya askali wapya katika jeshi la Rwanda alijiunga na Chuo cha kijeshi cha Royal Military Academy huko Sandhurst nchini Uingereza mnamo Agosti 8, 2021 na kuhitimu mafunzo yake Agosti 12, mwaka huu ambapo alitunukiwa cheo cha Luteni wa Pili (Second Lieutenant).

Chuo hiki cha Royal Military Academy cha huko Sandhurst ni miongoni mwa vyuo bora vya Kijeshi nchini Uingereza, vinavyo wafunza watoto wa viongozi wakubwa duniani, hasa kutoka Afrika, Mtoto wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Muhoozi Kainerugaba pia alipata mafunzo yake chuo hiki na kuhitimu mwaka 2000.

Hiyo Tisa, Kumi ni Kwamba...

Ian alikuwa ni miongoni mwa askali 24 maalumu waliopelekwa nje ya nchi kupata mafunzo muhimu, Ian Kagame Deogratius Rutagambwa ni mtoto wa 3 kuzaliwa kati ya watoto wa Kagame na mtoto wa pili wa kiume.

Huyu ndio mtoto pekee wa Kagame aliweza kufaulu mafunzo ya juu ya kijeshi na kujiunga na jeshi la nchi hiyo, mtoto mkubwa wa Kagame aitwae Ivan aliachilia masomo katikati katika Chuo cha Kijeshi cha West Point huko Marekani mwaka 2010 miezi miwili tu baada ya kujiunga, Alisema hakupendezwa na Jeshi.

Huyu Ivan alimkatisha tamaa baba yake sana, Paul Kagame alikili hilo hadharani.

Kuna tetesi kwamba Rais Kagame anapanga Ian (Ian Kagame Deogratius Rutagambwa) achukue nafasi yake mwaka 2034, awe ndio mrithi wake wa kiti cha uraisi.

MUHIMU: Itambulike ni tetesi..[emoji1]

Ndimi Comred Mbwana Allyamtu CMCAView attachment 2414354View attachment 2414358View attachment 2414355View attachment 2414356View attachment 2414357View attachment 2414359
Jamaa anatoka mwaka 2034?🤬🤬
 
Kwani wale wakina Prof Silas Rwakabamba,David Kaberuka etc wao walitokea nchi gani?
Ukweli ni kwamba namba ya wabongo waliotoboa ni ndogo mno ukilinganisha na wa ug ama burundi pengine labda waliotokea bongo hawakuwa na elimu au exposure kama hao waliotokea mataifa jirani au pia labda mchango wa wabongo ulikuwa mdogo sana na wanastahili walichopata
 
Vita ya 1994 walikusanyika watutsi kutoka tz, ud na burundi sasa ilikuwaje wa kutokea tz hawakupata vyeo (kutoboa) baada ya ushindi wa 94?

Aaahhh wengi walirudi kwao kutoka makambini ukumbuke hao wakimbizi baadhi walipelekwa mishamo tabora wale wa kutoka burundi na watutsi hasa wa Rwanda na Burundi walipelekwa Mwese katavi huko ili kuzuia wasipigane, hao ni walioingia Tanzania miaka ya 1970, nadhani baadae walipata uraia kabisa wa Tanzania lakini wengi walirudi kwao na wengine wakabaki Tanzania lakini hata wakirudi kwao ajabu wanapata haki zote kama Raia wa nchi zao yaani tunakataa uraia pacha lakini hizo jamii zikirudi kwao wakajiandikisha wanapata full citizenship japo kuitwa watanzania wako proud kuliko kuitwa warundi au wanyarwanda, hasa wale wakimbizi wengine wa mwaka 1994 ndio hao baadhi wako makambini sasa kigoma, nadhani na katavi kama hawakufunga kambi sina hakika, hata Rais wa sasa wa Burundi aliishi sana mishamo tabora na ana ndugu pale hadi leo,
 
Ukweli ni kwamba namba ya wabongo waliotoboa ni ndogo mno ukilinganisha na wa ug ama burundi pengine labda waliotokea bongo hawakuwa na elimu au exposure kama hao waliotokea mataifa jirani au pia labda mchango wa wabongo ulikuwa mdogo sana na wanastahili walichopata

Waliopigana vita kutokea Tanzania wengi ni warundi na walidaka vyeo kwao, kwa Rwanda wengi ni crew ya kutoka pori la uganda waliokua na museveni,
 
Wakimbizi wengi kutoka Congo, Burundi walikua Tanzania huku wakimbizi wa Rwanda wengi aalienda Uganda, na wote walinufaika na mpango wa nchi ya pili ya ukimbizi wengi wako ulaya na marekani ndio maana warundi ni wengi marekani kuliko watanzania,
 
Back
Top Bottom