M23 waliamsha tena DRC, Wauteka mji wa Nyabibwe, Jimbo la Kivu Kusini

M23 waliamsha tena DRC, Wauteka mji wa Nyabibwe, Jimbo la Kivu Kusini

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Siku mbili baada ya waasi wa M23 kutangaza kusitisha mapigano dhidi ya vikosi vya serikali ya DRC kwa sababu za kibinadamu, kundi hilo limeuteka Mji wa Nyabibwe, Jimbo la Kivu Kusini.

1738826793280.png
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, waasi hao wameudhibiti mji huo uliopo kando ya Ziwa Kivu, takriban kilometa 70 kutoka Bukavu—eneo ambalo awali walisema hawana mpango wa kuliteka.

Taarifa kutoka kwa vyanzo mbalimbali, ikiwemo wafanyakazi wa mashirika ya misaada, zimethibitisha kuwa M23 sasa wanashikilia udhibiti wa Nyabibwe.
 
Hawa jamaa walisema wamesitisha mapigano Leo asubuhi wameibuka wametembeza kichapo wakaiteka nyabibwe na Sasa wanaelekea ihusi iliyokaribu na bukavu yaani wakishika hii sehemu ni kama wameikamata bukavu aisee tshekedi kazi anayo na unaambiwa Hawa m23 vijana wao hawana huruma na adui wanapiga kichapo Cha mbwa koko kama wanavyoagizwa na mkuu wao Cornell nangaa
 
Hawa jamaa walisema wamesitisha mapigano Leo asubuhi wameibuka wametembeza kichapo wakaiteka nyabibwe aisee tshekedi kazi anayo na unaambiwa Hawa m23 vijana wao hawana huruma na adui wanapiga kichapo Cha mbwa koko kama wanavyoagizwa na mkuu wao Cornell nangaa
SADC ifanye mambo yanayoeleweka, na kama wamekubali congo igawanywe, basi na iwe hivyo ili watu wasiendelee kufa.
 
Back
Top Bottom