Maajabu: HESLB wamenifutia deni lote lililokuwa limesalia mwezi huu Januari

Maajabu: HESLB wamenifutia deni lote lililokuwa limesalia mwezi huu Januari

Bro wewe na Mimi tuna moyo mmoja Mimi nasema mpk waweke sawa hicho chombo ndio nitajisalimisha kimewaibia maskini Sana..Mara makato yawe juu Mara faini.,,Mara rentetion ,,,

Yaan Mtu anaamka from know where anaingiza makato kihuni..
Ukiajiriwa utakatwa hadi uone dunia chungu,ndo utajua hujui.
 
Mleta mada: Jamani, nimefutiwa deni. Oneni documents zangu. Deni limefutwa ghafla.
Wewe: Kwa hiyo unaona mil 1.2 ni mshahara mkubwa wa kuonyesha JF?
Unachokisema hakina hata chembe ya uhusiano na anachokisema mleta mada. Kama hauoni hapo kuwa akili zako ziko sehemu ya kukalia kwenye kiti basi tena.
Kuweka salary slip na kutoa taarifa ya deni kusitishwa kuna uhusiano gani, mwalimu anza kujitambua....
 
Ukionana naye barabarani utamjua kuwa ndiye mwenye mshahara huo? Ama unafikiri wote wana-share ID zao kama wewe?
Na wewe utakuwa juha vile vile. Kwa kigezo ulichotumia nahisi hutoona tabu kutembea uchi ugenini kwa vile tu watu hawakujui.

Kupitia hizi hizi fake id mtu akiwa na dhamira ya kukujua wsla haishindikani lakini sidhani hilo unalijua pia.

Anyways uwe na jumapili njema
 
Kama hiyo statement uliyoweka ni ya kwako, wewe ndio unatakiwa ukawadai, Deni lilikuwa milioni 7, na wewe umelipa milioni 9, angalia vizuri, nenda kadai chenji
 
MIMI DENI LA KWENYE SALARY SLIP NI TOFAUTI NA DENI LA KWENYE ACCOUNT YANGU YA HELSB
KWENYE SALARY SLIP WAMEWEKA DENI KUBWA
 
Kama hiyo statement uliyoweka ni ya kwako, wewe ndio unatakiwa ukawadai, Deni lilikuwa milioni 7, na wewe umelipa milioni 9, angalia vizuri, nenda kadai chenji
STATEMENT ZA HELSB NA SALARY SLIP ZINASOMA TOFAUTI MFANO MM SALARY SLIP INASOMA 9,000,000 na Statement yao inasoma 7,000,000
 
Mwezi uliopita kuna mtu alinambia kuwa baada ya Rais samia suluhu kuingia madarakani kuna retaining fees iliondolewa, nilienda kuhakiki deni langu ambalo lilikuwa linasoma mil 4.4, ila statement waliyonipa ilionyesha nadaiwa mil 1.4, nikawauliza mbona kunatofauti wakaniambia kabla ya mwezi wa pili watarekebisha zisome sawa za loarnboard na kwenye slip....
 
Kuna uwezekano kweli walikata kupiliza, na kuna watu nilikuta pale wanaidai loanboard, nenda kahakiki, kama walikukata zaidi wanarudisha
 
Mwezi uliopita kuna mtu alinambia kuwa baada ya Rais samia suluhu kuingia madarakani kuna retaining fees iliondolewa, nilienda kuhakiki deni langu ambalo lilikuwa linasoma mil 4.4, ila statement waliyonipa ilionyesha nadaiwa mil 1.4, nikawauliza mbona kunatofauti wakaniambia kabla ya mwezi wa pili watarekebisha zisome sawa za loarnboard na kwenye slip....
dah hapo sawa mama kaupiga mwingi waturekebishiee kwa kweli
 
Hilo ndio deni lako halali ulilosomea kulingana na kozi yako. Mshukuru Mungu kumleta Mama Samia. Mie lilikuwa linasoma zaidi ya milioni kumi na ushee. Baada ya agizo la Mama Samia nimerudi kwenye kiasi ninachostahili kulipa.
 
Hilo ndio deni lako halali ulilosomea kulingana na kozi yako. Mshukuru Mungu kumleta Mama Samia. Mie lilikuwa linasoma zaidi ya milioni kumi na ushee. Baada ya agizo la Mama Samia nimerudi kwenye kiasi ninachostahili kulipa.
kabisa deni langu limebaki about two mil mama samia tumpe mitano tena
 
Nchi hii ina unyonyaji sana. Yaani mtu analipwa gross ya 1.2 M halafu wanakata mpaka anabaki na laki 5!! Laki 5 hapo sasa ule, watoto waende shule, upate nauli, ulipe kodi ya nyumba huku ukinunua mifuko ya sementi ili uanze kujenga yako, ulipe michango ya harusi na vifo... halafu hautakiwi kula rushwa. Hii mishahara inatakiwa kurekebishwa haraka sana.
Bodi ya mikopo hawatoi ruzuku, Ni mikopo ile.

Na hawalazimishi mtu kuchukua. Mambo mengine Ni kujiendekeza.

Sidhani kama Kila mzazi hawezi kulipa Ada ya 1.2M kwa mwaka huko vyuoni.
 
Back
Top Bottom