Maajabu ya mwanamke mjamzito kuomba police wamwambie mume asimpige tena sababu anampenda sana, hii ni baada ya kupewa kipigo kizito!

Marriage imekuwa Suffering....Kuogopa tu kuitwa "Single Mother".
Sasa mbona watu wakileta nyuzi za kukataa ndoa wanawake mnakuwa wa kwanza kukasirika na ku react ?


Mmezidi kuitukuza sana asiye olewa mnamuona kama kapotea hivi ndio maana watu wanavumilia mateso
 
Ila ndo raha ya kuoa wanawake na kuwaweka ndani wakiwa hawana kazi wala kipato unamfumua tu unavyotaka🤣 na wanawake hakuna kukwepa ngumi za macho msije mkaitwa ma feminist sawa?

Akirusha panga egesha kichwa vizuri waonesheni waume zenu utii. Tutazika tu ila kikubwa hatutaki wanawake wenye vielement vya kujitetea tetea wala ubishani. Mumeo akikubutua hivyo nusu kufa usimchukie ni mwanaume huyo sawa? Vumilia mbembeleze arudi nyumbani amalizie kung’oa jicho la pili.
 
SI ongei kitu Kwa maana ukimwangalia wanahali duni halafu mwanaume anampiga mkewe Kisa ya hali Yao

Na anadaiwa pesa nyingi sana .
Za matunzo ya mimbaa na baada ya mwanamke kujifungua .
Nakinaonyesha wote ni walevi na hawajitambui .

So kinachohitajika ni ushauri nasaa Kwa mama na kusaidia ajifungue nakujitambua pia .

Jingine wanaume wengi wa Sasa wanajiona na hawana heshima kuwa Hawa ni wanawake zetu wanatunzwa wao hutukana namuwadhihaki wewe Malaya , unaliwa ovyo kumbe ni yeye anamla so maisha ndio hayoo.
 
Muacheni mwenzenu amependa au hamjui kuwa mapenzi ni kuvumiliana...
 
Ukijua jinsi ya ku control hasira zako jipige pige kifua sema mimi ni one in the million.
Hasira ndio hufanya mtu anaua au kujeruhi mtu vibaya badae akikaa akafikiria alietenda kosa anajilaumu mno, tena unaweza kuta sababu ni ya kijinga kijinga tu.
 
Karne za leo kama mwanaume unaakili timamu kamwe huwezi kumpiga mwanamke, kupiga nankujeruhi ni uonezi na sio funzo kwamba atajifunza
Umewahi kukaa kwenye ndoa..!?

Kama hapana relax kunywa maji kisha vuta subra,
Halafu hiyo comment yako itunze kisha baada ya miaka 10 rudi uisome.
 
Ninauzoefu wa mimba zaidi ya moja.

Kama mwanamke anamimba hapo mwenye kosa ni mwanaume kulingana na mwandiko wako.

kupiga gani huko jamani khee

Kwa hiyo mtu akiwa na mimba ndo apigwe hivyo na aone ni Sawa tu?

Huyu mama anakaa na mtu ambae ameshamiathiri kiakili sasa amehamia rasmi kwenye mwili

Wakienda enda anamnalizia kabisa
 

Ila pombe mnaisingizia tu jamani
 
Yani ye akipigwa atulie akipona vzuri amvizie amelala ashuke kitandani achomeke neti vzuri ikae chini ya godoro kabisa alf atoke nje avunge kama amevamiwa waje shemeji wa mwanaume wawili tu wamshushie kichapo akiwa ndani ya neti.

Akitoka hapo akarudia kumpiga mke wake mwambie aje kwangu nmpe mbinu nyingine ya huyo mwanaume kupigwa hadi kulazwa mwezi mzima
 
Unapigaje mke kama unapiga mandonga?? 😂

Ila kuna nyakati badhi ya wanawake wanajua kukera, uvumilivu na busara vikiwa likizo tu utatembeza mkong'oto
 
Mwanamke atakakuwa kamwambia mwamba mimba c ya kwake na tayar keshaingia migarama kibao
 
Mwanamke atunzwe na ustawi wa jamii.
Mume atunzwe na magereza kwa muda.

Huyo jamaa ni muuaji
 
Mbona hizi nyuzi sioni wahusika🤣🤣🤣🤣wanasubiri wapuuzi wenzao wanapoanzisha nyuzi za kutukana wanawake na kuwaita mafeminist na viumbe wa ajabu yanaenda kujazana kama nzige. Wanawake tafteni kazi za kufanya ona huyu dada anaonekana zamwamwa kwasababu anakomaa na vipigo hana pakwenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…