Maamuzi mengi katika Mihimili ya Uongozi Tanzania yanatolewa kufuata hisia za mtu na sio ushahidi (facts) au Sheria

Maamuzi mengi katika Mihimili ya Uongozi Tanzania yanatolewa kufuata hisia za mtu na sio ushahidi (facts) au Sheria

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Hili ni tatizo kubwa sana Tanzania, na huwa naliona katika mihimili mitatu ya usimamizi wa nchi, kuanzia Raisi, Spika, Mwanasheria Mkuu na hata mahakimu katika mahakama zetu!

Viongoi wetu wamefika mahali wanavunja Katiba, Sheria au Taratibu zinazokubalika kwa ulevi tu wa hisia zao binafsi.

Na ni tatizo limekubuhu sana katika siasa, lakini labda huko tunaweza kuwapuuza, kwa kuwa wanasiasa kutumia hisia kufanya maamuzi ni bora kuliko kile ambacho husemwa kuwa tabia yao, uongo!

Lakini sasa, tunapukuwa na Taasisi ya uraisi nchini, ikifanya maamuzi kwa hisia, Bunge likitoa matamko na maamuzi kwa hisia, mahakimu katika maamuzi ya kesi, wakitoa hukumu kwa hisia, tunakuwa tunaenda wapi?

Baada ya wanasiasa, kundi la pili linaloambukizwa kirahisi sana na kirusi cha kufanya mambo na maamuzi kwa hisia ni Polisi. Na hakika nawaambieni, Polisi wetu hapa nchini kirusi cha hisia kilishawakumba siku nyingi sana.

Ni lini Tanzania tutaondokana na kuamua mambo, kutoa matamko au kutenda mambo kwa kuongozwa na hisia? Tmeingiliwa na ugonjwa mbaya sana!
 
Hilo ndugu ni GIZA KUU limeshaingia Tanzania.

Lakini, unapoona giza linazidi kuwa giza kuu, tunapaswa kutambua kuwa kumekaribia kupambazuka na kuiona NURU au MWANGA wa jua...!!
 
Hawa jamaa wananikumbusha usemi wa Nyerere - kama unampenda peleka posa!

Sasa unakuta mfano mtu anang'ang'ania huyu lazima awe mbunge, hata akifukuzwa uanachama wa chama chake nk. Kama unampenda peleka posa!
 
Hilo ndugu ni GIZA KUU limeshaingia Tanzania...

Lakini, unapoona giza linazidi kuwa giza kuu, tunapaswa kutambua kuwa kumekaribia kupambazuka na kuiona NURU au MWANGA wa jua...!!

When dua la kuku.watu waovu uishi miaka mingi
 
When dua la kuku.watu waovu uishi miaka mingi

Huwa unahariri kweli kabla ya kupost jambo?

Sentensi yako ni fupi lakini umeiandika katika SARUFI mbovu kupindukia...

Ukipenda unaweza kurekebisha ili watu wakusome na kukuelewa vizuri...

Na ukiweza andika kwa Kiingereza ama Kiswahili tu. Usiandike kwa kuchanganya lugha mbili kwa wakati mmoja, yaani Kiswa - English..

Obviously, kuna lugha moja inakushinda. Likely ni Kiingereza...
 
Hahaha hatuna viongozi, edit andiko lako, tunao watawala.
 
Huwa unahariri kweli kabla ya kupost jambo?

Sentensi yako ni fupi lakini umeiandika katika SARUFI mbovu kupindukia...

Ukipenda unaweza kurekebisha ili watu wakusome na kukuelewa vizuri...

Na ukiweza andika kwa Kiingereza ama Kiswahili tu. Usiandike kwa kuchanganya lugha mbili kwa wakati mmoja, yaani Kiswa - English..

Obviously, kuna lugha moja inakushinda. Likely ni Kiingereza...
Si lzm uelewe wwe
 
Si lzm uelewe wwe
Umekasirika ndugu? Nimekukosoa kwa nia njema. I didn't mean to offend you...

Na ofcoz siyo lazima nielewe Mimi. Wengine wanaweza kuelewa tu maana "labda" mnafanana nao kiakili/kiufahamu...!!
 
Hili ni tatizo kubwa sana Tanzania, na huwa naliona katika mihimili mitatu ya usimamizi wa nchi, kuanzia Raisi, Spika, Mwanasheria Mkuu na hata mahakimu katika mahakama zetu!

Viongoi wetu wamefika mahali wanavunja Katiba, Sheria au Taratibu zinazokubalika kwa ulevi tu wa hisia zao binafsi.

Na ni tatizo limekubuhu sana katika siasa, lakini labda huko tunaweza kuwapuuza, kwa kuwa wanasiasa kutumia hisia kufanya maamuzi ni bora kuliko kile ambacho husemwa kuwa tabia yao, uongo!

Lakini sasa, tunapukuwa na Taasisi ya uraisi nchini, ikifanya maamuzi kwa hisia, Bunge likitoa matamko na maamuzi kwa hisia, mahakimu katika maamuzi ya kesi, wakitoa hukumu kwa hisia, tunakuwa tunaenda wapi?

Baada ya wanasiasa, kundi la pili linaloambukizwa kirahisi sana na kirusi cha kufanya mambo na maamuzi kwa hisia ni Polisi. Na hakika nawaambieni, Polisi wetu hapa nchini kirusi cha hisia kilishawakumba siku nyingi sana.

Ni lini Tanzania tutaondokana na kuamua mambo, kutoa matamko au kutenda mambo kwa kuongozwa na hisia? Tmeingiliwa na ugonjwa mbaya sana!
Ndiyo maana CCM haitaki watu wengi waelimike
 
Ushabiki kitu mbaya sana. Yaani ule usemi akipenda chongo huita kengeza ni muafaka kabisa!
 
Back
Top Bottom