Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Dah..aisee wake zetu hawa wanatupenda sana (sio wote).huyo dada anavyoeleza kampelekea jamaa shuka na chakula na sabun aisee nimehis kulengwa machozi nikakumbuka 2019 nimeugua ghafla nikiwa kwenye mishe zangu town nikaingizwa emergency Temeke hospital wife kaja na na nguo sijui hata alijuaje maana nilizovaa nilichafua chufua kwa kutapika.Mungu wabariki wanawake
 
Mungu wa Mbinguni awwtie nguvu mashahidi, watuhumiwa na awawezeshe Mahakimu watende haki.

Sifa na utukufu viwe kwa Bwana.
 
Nilidhani mimi nina kazi kumbe sio. Mahakimu na majaji wanakazi kubwa sana.

hasa kesi za kutunga hizi.
 
Serikali, polisi, jeshi na nchi zima tuko uchi. Sakata hili limeonyesha ni kwa jinsi makomando wetu ni mdebwedo, ni kwa jinsi gani polisi hawaijui kazi yao na wala hawaijui miongozo yao wenyewe PGO.
Kiufupi Tanzania hatujali haki za msingi za kibinadamu. Tunaishi kama mahayawani.

Unawezaje kumtesa mtubumiwa kiasi hicho na bado watu hawajali kwa sababu tu wana Ukaribu Na Mh Mbowe??

madaraka haya ndio Maana Mungu kamnyanganya Jiwe na kumtowesha kabisa. Mbinu zote hizi zilifanyika kumdhoofisha Mbowe na Chama Chake wakati wa uchaguzi mwaka jana.
 
Shukrani kwa taarifa mkuu
 
Kingai ,Mahita ,Godluck ,jumanne na Sirro wanapaswa kushitakiwa kwa kukiuka haki za mwanadamu.

Kina Adamo walinyimwa haki zao nyingi sana.

Polisi yetu magaidi utadhani KGB au CIA
Unakosa heshima kutaja vyombo makini kama KGB na CIA.

hivi vyombo vinafanya kazi kwa weledi mkubwa mno. Ukiwa mtuhumiwa wao unaishi kama paradiso mpaka uchunguzi wa kina utakapogundua wewe u a hatia.
 
Mie nilishasema hivi niliwahi kufanyiwa uonevu flani na police miaka ya nyuma nikakubali kuwapa hela waliyoitaka ishu ikaisha kimya ila sijawahi kusahau na kwa akili niliyonayo sa hivi ikitokea police akaingia kwenye anga zangu mfano kunifanyia uonevu kama huo ntakachokifanya ni zaidi ya Hamza maana huwa nina hasira sana na hawa watu!
 
Tunafuatilia kama kawaida yetu leo tarehe 29 September 2021. Kesi ndogo ndani ya kesi kubwa .

..mke wa mtuhumiwa anadai polisi walivunja mlango wa nyumba yao.

..na anao utetezi wa madai yake kwa ushuhuda wa jirani yake.

..ushahidi huo utakwenda kuleta shida kwenye vielelezo vilivyokusanywa dhidi ya mtuhumiwa.

..upande wa utetezi unajenga picha kwamba polisi walikuwa hawafuati sheria na taratibu ktk uchunguzi na ukamataji wa watuhumiwa.
 
Ngoja na mimi niiombe mahakama iangalie uwezekano wa kesi hii kurushwa hewani kwenye TV
 
Polisi wamejisahau sana ! Wakubwa wao wanawadanganya kibwege sana kwamba wako juu ya sheria !
 
Ilikuwaje ebu tueleze kidogo
 
Ngoja na mimi niiombe mahakama iangalie uwezekano wa kesi hii kurushwa hewani kwenye TV
Hilo swala ndugu sio la uwezekano, ni haki kufanywa vile na mahakama itaridhia tu;

1) Ni haki ya kikatiba kwa kila raia kufuatilia kesi yoyote mahakamani inayomhusu yeye au maslahi yake au mtu anaemfahamu kama raia. Kesi hio ina Public Interest.

2) Mahakama ni ndogo haina uwezo wa kumudu watu zaidi ya millioni 60 kwenda kufuatilia hio kesi mahakamani. Hivo live coverage inapunguza msongamano na hatari ya raia au watu kufanya fujo.

3) Kupunguza msongamano kwaajili ya afya (Covid 19), live coverage itafanya watu watulie majumbani mwao huku wakifatilia kesi bila kujazana kwenye daladala wala mahakamani.

4) Usalama kwa washtakiwa. Live coverage itapunguza msongamano wa watu nje ya mahakama kwaajili ya usalama wa washtakiwa. Sio kesho tusikie watu wasiojulikana wamemimina risasi kwenye gari ya washtakiwa na kuwaua au kuwajeruhi. Week hii gari ya kina Freeman Mbowe iliharibika mahakamani, hivi kweli unasafirisha makomandoo na mwenyekiti wa upinzani ambao wana kesi kubwa na yenye public interest kidunia kwenye gari bovu??? Usalama wao huoni unakua mashakani??? Watu wasiojulikana (Kama Serikali inavo waita) wakivamia na silaha za moto na kuwamiminia risasi???

Nikiendelea kukuandikia points ntaishia kujaza server za JF. . . . Hizo ni baadhi tu. . . .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…