Ukituliza kichwa huu uzi utakufungua macho (hasa sie ambao hatujaoa). Kuchukulia mambo haya ya bikra na ndoa kiurahisi ndio janja ya ibilisi kupotosha hiki kizazi na kile kijacho.
Ibilisi anataka tuamini kua bikra hazipo tena,hata zikiwepo upatikanaji wake ni mgumu sana hivyo hazina umuhimu kiviile!
Tunasahau kua mambo mazuri yapo ila si rahisi kuyapata, na ni wachache wenye uvumilivu wa kuyafikia mfano ni pepo na hizo ndoa takatifu(mwanamke akiwa bikra).
Mtoa mada kaelezea vizuri maana ya bikra kimwili na kiroho pamoja na faida zake, lakini vijana tunajitoa ufahamu na kujifanya hayawani kisa tu mwanamke kakuvutia!
Mwenyezi Mungu sio kigeugeu km sie binadamu tusioelezeka,neno lake halijawahi kubadilika.
Mtoa hoja kaweka na vifungu mbalimbali kuthibitisha umuhimu wa hiyo bikra, na akaweka na fungu ktk biblia linalosema kua hata Yesu alizaliwa na mwanamke bikra!(huu ni muujiza mkubwa na ushahidi kua Mungu anasimamia neno lake).
ibilisi anataka tuwe watumwa wa tamaa za mwili, siku zote ibilisi yuko kinyume na neno la Mwenyezi Mungu, ibilisi anatutoa ufahamu ili tuchukulie mambo kiurahisi na kwa mazoea!
Chanzo cha dhambi ulimwenguni ni ibilisi kupitia mwanamke, na leo hii wanawake wanajitahidi ku'justify uzinzi wao kisa kila mtu ni mdhambi eti hata wasio na bikra huolewa na kuzaa pia, ndio watazaa lakini uzao mchafu!
Mwanamke unashindwa kujitunza, halafu unajitetea eti Mungu husamehe.. ushaambiwa Mungu hachukii mtenda dhambi bali huchukia dhambi (iwe ya aina yoyote ile), na binadamu anayefanya dhambi kusudi kwakua Mungu atamsamehe anajidanganya..hilo liko wazi( yaani leo uzini uombe msamaha,kesho urudie tena uombe msamaha and so on..huo ni upumbavu! Na Mungu anakuona km mbwa anayerudia kula matapishi yake)
Vijana (wa kiume) tujifunze kutopelekeshwa na hawa wanawake, tuwe na msimamo..ndoa na mwanamke utakayemfungua mwenyewe itakuepusha na majanga mengi (kimwili na kiroho).
Mwanamke aliyejitunza hata fikra zake ni kama mtoto mdogo na anakua na imani haswa pia akiwa mkeo obviously atakusikiliza maana weww ndio kiongozi wake.
Binafsi nimemuelewa sana mtoa hoja na nia yake njema ya kukemea huu uovu unaoendelea kuhalalishwa hasa na wanawake waovu (wakisaidiwa na shosti yao mkuu ibilisi bin kigalula).
Hakuna mtakatifu chini ya jua ila haituzuii kukemea dhambi kwa faida ya kizazi kijacho (maana hiki cha sasa nahisi ndio basi tena).
Tusiogope, km torati ya Musa ilitoa adhabu ya kifo kwa mwanamke asiyejitunza utu wake kabla ya kuolewa basi hii kitu ni siriasi sana zaidi ya tunavyodhani!
Narudia tena, mambo mazuri yapo kwa wavumilivu pekee (awe me au ke)..usitegemee kuzurura mitaani kutafuta bikra km majani ya chai.
Ushaambiwa mke mwema hutoka kwa Bwana, unadhani hiyo sentensi ina maana gani?? Kijana wa kiume jitunze kimaadili uwe na heshima, eventually utapata mwenza mnayeendana (amini kwamba lazima tu atakua bikra maana Mungu mwenyewe ndio kakukonektia). Mfano Isaka alivyotunukiwa Rebeka..
Mtoa hoja usihofu, endelea hivyo hivyo..binafsi umenifungua macho na panapo majaaliwa nitaoa bikra safiii kutoka kwa incharge mwenyewe Allah Yehova Bwana wa majeshi..ameen!