Mughonile.
Niliapa sitaharibu ambacho hakijaharibika au kuharibiwa. Sitaondoa Bikra kama sitamuoa huyo Mwanamke. Kama una bikra basi nisingekuchezea lakini kama umejiharibu au kuharibiwa nilijipa uhalali wa kuendelea kufanya uharibifu.
Niliapa sitokuja kuoa Mwanamke asiye na Bikra hata nichomwe moto. Hata angesema nani. Labda ulikuwa ni utoto. Lakini kwa sasa nimekua na nipo ndoani kwa miaka kumi sasa tangu nilipooa 2013. Miaka kumi ya ndoa imekuwa ya furaha kwangu. Ndoa ya Mwanamke wa ndoto yangu, Bikra safi.
Najivunia kuwa miongoni mwao wanaume bora wenye bahati kwa kuoa na kuanzisha familia Safi. Najivunia watoto wangu kuwa na mama ambaye ni msafi ambaye usafi wake niliuthibitisha mimi mwenyewe siku nilipokata utepe.
Msimamo wangu wa kizamani unaninufaisha, umeniletea familia yenye furaha yenye uaminifu. Mama mwaminifu, msafi, mama mzuri, Watoto waliotoka katika mama mwenye kujitunza na kujizuia.
Kama hujaoa na unataka familia yenye furaha. Basi OA Mwanamke mwenye Bikra. Usiharibu ambavyo havijaharibika wala kuharibiwa. Utaishi maisha matamu Sana.
Bikra Matters
Usioe asiye na Bikra
Kalaghabaho