Maandamano Kenya: Mwanaume mmoja aandamana kwa kujifunga mnyororo kwenye nguzo na kutoa kero zake

Maandamano Kenya: Mwanaume mmoja aandamana kwa kujifunga mnyororo kwenye nguzo na kutoa kero zake

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Mwanaume mmoja huko Kenya aandamana kwa aina yake leo kwa kujifunga kwenye nguzo na mnyororo na kuanza kuongea kero zake.

Polisi walifika eneo la tukio na kujaribu kumfungua ili wamkamte huku watu wengine wakiwa wanarekodi tukio hilo. Polisi walipomuomba ufunguo, akasema mimi sina funguo. Kwa jinsi jamaa alivyokuwa amejifunga ilichukua muda polisi kuweza kumfungua.

Kwenye video mwanaume huyo anasema amekuja kuiambia serikari isiwanyanyase, kuwapiga, kuwaua, na kufanya waishi kwa vitisho, badala yake serikali inatakiwa kuwahudumia wananchi. Ahoji nani ameturoga Afrika, akisema uoga na ukabila ndio unafanya Afrika kuwa watumwa. Akisema kwamba muda umefika kwa Afrika kupata ukombozi wake na haogopi kitu chochote kumtokea yeye. Na hata walipoweza kumfungua na kumkamata huku wakimkokota kwenye gari, aliwaambia polisi mnachofanya ni unyanyasaji na kuendelea kusema haogopi kitu na yuko tayari kufa kwaajili ya wengine.


 
Mwanaume mmoja huko Kenya aandamana kwa aina yake leo kwa kujifunga kwenye nguzo na mnyororo na kuanza kuongea kero zake.

Polisi walifika eneo la tukio na kujaribu kumfungua ili wamkamte huku watu wengine wakiwa wanarekodi tukio hilo. Kwa jinsi jamaa alivyokuwa amejifunga ilichukua muda polisi kuweza kumfungua.

Hata baada ya polisi kumfungua jamaa alitia ugumu kupakiwa kwenye gari la polisi, na hata baada ya kukamatwa alisema haogopi kitu chochote!
Kwahiyo picha tutajitungia kichwani..??
 
Labda kama tumerogwa:



Ila nchi zetu hizi zenye changamoto zile zile zitakombolewa kwa umoja na ujasiri wetu dhidi ya hofu.

ShIme waungwana:

"Mola atujalie."
 
Mwanaume mmoja huko Kenya aandamana kwa aina yake leo kwa kujifunga kwenye nguzo na mnyororo na kuanza kuongea kero zake.

Polisi walifika eneo la tukio na kujaribu kumfungua ili wamkamte huku watu wengine wakiwa wanarekodi tukio hilo. Polisi walipomuomba ufunguo, akasema mimi sina funguo. Kwa jinsi jamaa alivyokuwa amejifunga ilichukua muda polisi kuweza kumfungua.

Kwenye video mwanaume huyo anasema amekuja kuiambia serikari isiwanyanyase, kuwapiga, kuwaua, na kufanya waishi kwa vitisho, badala yake serikali inatakiwa kuwahudumia wananchi. Ahoji nani ameturoga Afrika, akisema uoga na ukabila ndio unafanya Afrika kuwa watumwa. Akisema kwamba muda umefika kwa Afrika kupata ukombozi wake na haogopi kitu chochote kumtokea yeye. Na hata walipoweza kumfungua na kumkamata huku wakimkokota kwenye gari, aliwaambia polisi mnachofanya ni unyanyasaji na kuendelea kusema haogopi kitu na yuko tayari kufa kwaajili ya wengine.


Watanzania tuendelee kupinga ushenzi wa CCM.
 
Kuna njia nyingi bora za kuwaondoa au kuwawajibisha hawa hapa kwetu, siyo lazima tukaige hayo ya huko Kenya.
Ipo tofauti ya kuiga na ku copy kisha ku paste. Kiswahili kifunyu.
 
Back
Top Bottom