Sio unafiki ni kwamba Watanzania wengi wamewasoma. Wapo pale kwa matumbo yao. Hakuna anayekubaliana na kuteka, angalia misimamo ya Chadema, walimchukua Lowassa, fisadi kuu, waliungana na Makamba, nape, Samia kumtukana JPM, huku wakimsifia Samia, anaupiga mwingi, kwamba tatizo ni wasukuma.
JPM aliamua kuwakabili Chadema baada ya kuona hawako kwa maslahi ya taifa, Acacia na mikataba mingine mibovu walikuwa upande wa mabeberu. Walitoa dhihaka wakimwita dikteta uchwara akaamua kuwa dicketa kamili.
JPM akaleta nidhamu serikalini, kupunguza rushwa, umeme, maji, barabara, SGR, wanasema hawataki hayo wanataka maendeleo ya watu. Hawajui wanachotaka wako tayari kuungana na wahuni wowote kwa kupata madaraka.