Mabadiliko Baraza la Mawaziri: Doto Biteko ateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Makamba Mambo ya Nje, Pindi Chana Katiba na Sheria

Majaliwa ajitafakari... aachie ngazi kwa busara na heshima yake iendelee kuwepo kwa wananchi... hii movie inavyoenda anaweza tolewa... kwa cheo cha waziri mkuu, rais akitumia utashi wake kukupa msaidizi ni wazi 'umeshindwa' kazi..
 
Rais Samia Suluhu amefanya mabadiliko na teuzi za sura mpya kwenye baraza la mawaziri. Uapisho utafanyika September 1, Ikulu ndogo Zanzibar saa tano kamili asubuhi...
1. Kuna ulazima gani wa kuwa na naibu waziri mkuu?
Zaidi ya miaka 20 hiki cheo hakipo kinaletwa tena, kwa miaka yote hii ambayo hakikuwepo kuna madhara yaliyojitokeza?

Wizara ya nishati ni wizara pasua kichwa je waziri wake kuwa na ofisi zaidi ya moja ataweza kusimamia kote kwa umakini?

2. Tanzania inaonekana ina fedha za kuchezea viongozi, majuzi kati kuna wizara mpya iliazishwa akawekwa Mkumbo je wanaongeza ufanisi, utendaji, ubunifu au wanaongeza mzigo wa bajeti ya nchi na kuwaelemea raia kwa kodi?

3. Je Mh Dotto Biteko yupo kwenye timing au ameaminiwa au kuna kundi linapunguzwa makali?

Dotto atakuwa na performance zuri kiasi kwamba kero ya umeme inyosumbua tangu JM awe nayo wizara au atakuwa kawekwa mtu kati?
 
Kwenye nishati ni waziri kamaili.
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje. Akawa mwanadiplomasia mahiri sana. Pia kuwepo kwake kwenye wizara hiyo kulimuepusha na vurugu za siasa za ndani. Akaja kuwa Rais baadae...
Wacha apate uzoefu...tutamuangalia mbeleni...
 
Katika biblia takatifu kuna hadithi moja ya Washami. Hawa nchi yao ilikuwa imetekwa na chakula chote kilifungiwa kwenye lango la mji wao wakawa nje ya lango hawana chakula. Na ilikuwa ukisogea kwenye lile lango chakula kinauzwa bei mbaya na askari walikuua kama ulitaka kufanya ujanja ujanja. Hawa Washami Mungu alikuwa upande wao na walikuwa wamemlilia Mungu kwa muda mrefu.

Njaa ilipowazidi Washami wakajiambia moyoni mwao kuwa TUKIBAKI HAPA TUTAKUFA NA NJAA NA TUKIENDA KULE KWENYE LANGO ASKARI WATATUUA LAKINI PIA BWANA ANAWEZA KUTUFANYIA MUUJIZA. Wakaamua kwenda kule kwenye lango na Mungu akaleta kishindo cha farasi wengi wale askari kule kwenye lango lenye chakula wakakimbia wakijua kuwa kuna jeshi kubwa linakuja kuwapiga.

Kwako Kassim Majaliwa hadithi hii ikusaidie japo sio ya kitabu cha dini yako. Kwa ulipofikishwa leo ni kuwa unapaswa kumalizwa kisiasa kabisa. UKINYAMAZA WATAKUMALIZA NA UKIZUNGUMZA WATAKUMALIZA ila ukizungumza unaweza kupata kishindo cha jeshi la wananchi kikakusaidia. Uchaguzi ni wako.

Mimi nakushauri PAMBANA utakuwa umeisaidia nchi yako kidemokrasia. Otherwise utabaki kuwa Waziri Mkuu wa kusaini na kutia mihuri na mpaka Dec. Bunge lijalo atateuliwa Waziri Mkuu mwingine na utakuwa umejeruhiwa sana kisiasa au kuuawa kisiasa kabisa.
 
Anachapa kazi anaposukumwa, mama style yake ni mtu ajisukume mwenyewe.

Majaliwa ana "typical mindset" ya utumwa.
Kuna watu huwa wanasema humu kuwa wewe ndiye "mama wa Taifa"! Kwa post yako hii naanza kushawishika na hilo!! wewe unasemaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…