Mabadiliko kutoka Building Better Tomorrow - BBT mpaka kuwa Building Bashe Tomorrow - BBT

Mabadiliko kutoka Building Better Tomorrow - BBT mpaka kuwa Building Bashe Tomorrow - BBT

Ukiangalia hao vijan ni uvccm na ccm waliota hadi mvi. Watu wameshapiga pesa na hakuna maneno tunafanya hapo.

Serikali kuna namna ya kuwezesha kilimo ila kwa ili alilochagua bashe ni baya sana limejaa wizi na ujanja. Fikiri pia wanamilikishwa vitalu kwa miaka zaidi ya 40.

Serikali ingewekeza kutoa mbegu bure, pembejeo za kilimo tukaamua huu mwaka tunakomboa kilimo cha dengu, wao watafute na soko wauziwe kwa malipo ya cash, wao wauze nje wanakoona inafaa. Iyo ndio namna ya kukuomboa nguvu.

Ccm ata wapewe miaka mingine 50 hawawezi kutuvusha. Tuishi tusubiri kufa tuu.
 
Mabadiliko kutoka 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝙀𝙏𝙏𝙀𝙍 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒 - 𝘽𝘽𝙏 mpaka kuwa 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝘼𝙎𝙃𝙀 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒- 𝘽𝘽𝙏. TUMEPIGWA BILIONI 13.

Kwa mujibu wa wizara ya Kilimo chini ya waziri @HusseinBashe ni kwamba serikali inatumia milion 16.4 kufadhili shamba la hekta moja kwenye mradi wa Building a Better Tomorrow kwa kifupi BBT. Gharama hizi hazina uhalisia wowote kwa mtu anayejua kilimo au mkulima yoyote. Na kama zingekuwa na uhalisia kwamba mkulima anaweza kutumia milioni 16 kuandaa shamba la hekta moja ambayo ni sawa na ekari mbili basi nchi hii hakuna ambaye angemudu gharama hizo.

Fikiria unalima nini kwenye shamba la hekta moja ambalo maandalizi yake mpaka kupanda mbegu yanagharimu milioni 16? Unalima dhahabu kwenye hilo shamba? Au unalima almasi? Ama tanzanite? Maana haiwezekani shamba lililoandaliwa kwa milion 16 upande mahindi, Mpunga au ulezi halafu utegemee mtaji wako milioni 16 kurudi achilia mbali kupata faida.

Naomba kujitolea mfano mwenyewe maana ni mkulima. Msimu wa kilimo uliopita nimelima ekari 2 na kidogo ambazo sawa na hekta moja na nilivuna tani 3 au gunia 30 za kg 100. Nilikodi shamba kwa laki moja. Vibarua wakanilimia kwa ng'ombe kwa shilingi laki moja. Gharama za mbegu, madawa ya kuuwa wadudu na kukausha nyasi pamoja na mbolea nikatumia laki tano. Kuvuna na kupukuchua pamoja na mifuko ya kuwekea mahindi nimetumia laki tatu. Jumla ya gharama nilizotumia ni milion 1. Nimeuza mahindi hayo December 2022 kwa milion 2 na nusu baada ya kuuza kwa kg Tsh. 800 hukohuko shambani. Hivyo faida ukawa ni milioni 1.5.

Sasa tukirudi kwa Bwana Bashe na wizara yake ya kilimo kwa hekta 1 au ekari 2 na kidogo bajeti yao ni kama ifutavyo:
  • Kulima shamba Tsh. 4,250,000/
  • Kumwagilia Tsh. 7,500,000/
  • Kupima afya ya udongo Tsh. 2,500,000/
  • Mbolea Tsh. 1,750,000/
  • Viuatilifu Tsh. 375,000/
  • Mbegu Tsh. 112,000/-
JUMLA Tsh. 16, 487, 500/ kwa hekta moja. Sasa hiyo milioni 16 ukizidisha mara hekta 812 za vijana waliochukuliwa tayari awamu ya kwanza na wizara ya kilimo chini ya waziri Bashe unapata bilioni 13.5. Yani dakika ya kwanza kabisa mpira unaanza tunapigwa bilioni 13 na hiyo tu ni awamu ya kwanza maana hatujui mradi huu utahusisha hekta ngapi.

Hapo sijajumlisha gharama za upimaji ardhi na hati miliki ambayo wameweka ni milion 2. Na hapo pia nina mashaka kama hizo ndio bei halisi za kupimia ardhi kwa hekta. Anyway tuachane na mambo ya hati miliki turudi kwenye topic yetu.

Mimi ni miongoni mwa watu ambao naunga mkono wakulima kuinuliwa hasa vijana. Mradi wa Building a Better Tomorrow au BBT lengo kuu lilikuwa ni kuinua kilimo kupitia vijana. Lakini kwa mchanganuo unaonekana ni 𝑩𝒖𝒊𝒍𝒅𝒊𝒏𝒈 𝑩𝒂𝒔𝒉𝒆 𝑻𝒐𝒎𝒐𝒓𝒓𝒐𝒘 - 𝑩𝑩𝑻 na kwamba mradi huu umesukwa kimkakati kuwatumia vijana kufanya ufisadi wa mabilioni. Pengine ndio maana vijana walio wengi kama sio wote waliobebwa au kupewa fursa katika mradi huo hawajui chochote kuhusu kilimo na hawajawahi kulima. Ni wakati sasa wa CAG kwenda kufanya ukaguzi katika mradi huo.

Hawa watu ambao Rais Samia aliwapa ruhusa ya kula kulingana na urefu wa kamba zao imefika mahari sasa wanataka kukata mpaka kamba ili waitafune nchi yote ibaki na mashimo. Kuna wingu zito la ufisadi kuanzia wizarani mpaka nje ya wizara ukiachilia mbali fisadi mmoja mkongwe kupewa tenda ya kusambaza mbolea katika mradi huo.

Imekuwa ngumu sana kumtenga bwana Bashe na ufisadi kwa sababu ya watu waliomlea na kumkuza katika siasa ambao kwa kiasi kikubwa wananuka ufisadi wa nchi hii. Bado nina file zake nazipitia kupata uhakika. Miongoni mwa file hizo zinahusisha baadhi ya viwanda kikiweno kiwanda cha Mbolea ya minjingu somewhere.

Kwa mazingira haya tusitegemee kama kutakuwa na uwajibikaji wowote kwa sababu wazazi wa kisiasa wa Bashe ambao wanazo kashfa nzito nchi hii wameshinda vita dhidi ya mafisadi wa Sukuma Gang ambao nao walitesa kwa miaka mitano.

Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.

𝑴𝒅𝒖𝒅𝒆 𝑵𝒚𝒂𝒈𝒂𝒍𝒊 𝟕 𝒙 𝟕𝟎 𝑺𝒖𝒎𝒖 𝒚𝒂 𝑵𝒚𝒊𝒈𝒖

View attachment 2617458
Pamoja na kuwa hizo gharama za BBT zipo juu
Ila kuna vitu muhimu hujaeleza kuhusu huo mradi. Kwanza kikubwa ni kutayarisha shamba na kuweka miundombinu, ya kulifikia na muhimu zaidi kuweka mfumo wa UMWAGILIAJI. Sina hakika kama wanatumia maji ya mto au wamechimba visima ambapo ni ghali sana kununua miundombinu ya Solar kwa ajili ya kuvuta maji au pengine kupeleka umeme huko mashambani.
Mradi kama huu, hauhitaji kubahatisha Mvua kama wakulima wetu wengi wanavyolima lakini pia; gharama hizo ni kama mtaji; inamaana, wakilima tena gharama nyingi hazitakuwepo
Muhimu pia: kwa kuwa na miundo mbinu sahihi, kuna uwezekano wa kulima mara mbilli kwa mwaka na hata mara tatu kutegemea na aina ya mazao

Mwisho; Kuna wale vijana (Wengi) waliopelekwa huko, ujue kuna gharama za kuwatengenezea mazingira ya kukaa huko shambani (Nyumba/Mahema Chakula, Bima ya Afya nk)
Binafsi najua huu mradi unaweza kuwa na changamoto kadhaa kwa sababu bado tunajifunza ila kutoka rohoni kwangu naamini ni moja ya miradi bora kabisa ya majaribio na inayoweza kutusaidia kama Nchi.
Angalizo: Mimi sihusiki huko kwa mradi, napambana kivyangu huku nje/Private
 
Pamoja na kuwa hizo gharama za BBT zipo juu
Ila kuna kitu muhimu hujakieleza kuhusu huo mradi. Kwanza kikubwa ni kutayarisha shamba na kuweka miundombinu, ya kulifikia na muhimu zaidi kuweka mfumo wa UMWAGILIAJI. Sina hakika kama wanatumia maji ya mto au wamechimba visima ambapo ni ghali sana kununua miundombinu ya Solar kwa ajili ya kuvuta maji au pengine kupeleka umeme huko mashambani.
Mradi kama huu, hauhitaji kubahatisha Mvua kama wakulima wetu wengi wanavyolima lakini pia; gharama hizo ni kama mtaji; inamaana, wakilima tena gharama nyingi hazitakuwepo
Muhimu pia: kwa kuwa na miundo mbinu sahihi, kuna uwezekano wa kulima mara mbilli kwa mwaka na hata mara tatu kutegemea na aina ya mazao

Mwisho; Kuna wale vijana (Wengi) waliopelekwa huko, ujue kuna gharama za kuwatengenezea mazingira ya kukaa huko shambani (Nyumba/Mahema Chakula, Bima ya Afya nk)
Binafsi najua huu mradi unaweza kuwa na changamoto kadhaa kwa sababu bado tunajifunza ila kutoka rohoni kwangu naamini ni moja ya miradi bora kabisa ya majaribio na inayoweza kutusaidia kama Nchi.
Angalizo: Mimi sihusiki huko kwa mradi, napambana kivyangu huku nje/Private
Soma mchanganuo umeandikwa hapo na siyo kujifanya mjuaji wakati kichwa kimejaa kamasi!
 
Mabadiliko kutoka 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝙀𝙏𝙏𝙀𝙍 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒 - 𝘽𝘽𝙏 mpaka kuwa 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝘼𝙎𝙃𝙀 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒- 𝘽𝘽𝙏. TUMEPIGWA BILIONI 13.

Kwa mujibu wa wizara ya Kilimo chini ya waziri @HusseinBashe ni kwamba serikali inatumia milion 16.4 kufadhili shamba la hekta moja kwenye mradi wa Building a Better Tomorrow kwa kifupi BBT. Gharama hizi hazina uhalisia wowote kwa mtu anayejua kilimo au mkulima yoyote. Na kama zingekuwa na uhalisia kwamba mkulima anaweza kutumia milioni 16 kuandaa shamba la hekta moja ambayo ni sawa na ekari mbili basi nchi hii hakuna ambaye angemudu gharama hizo.

Fikiria unalima nini kwenye shamba la hekta moja ambalo maandalizi yake mpaka kupanda mbegu yanagharimu milioni 16? Unalima dhahabu kwenye hilo shamba? Au unalima almasi? Ama tanzanite? Maana haiwezekani shamba lililoandaliwa kwa milion 16 upande mahindi, Mpunga au ulezi halafu utegemee mtaji wako milioni 16 kurudi achilia mbali kupata faida.

Naomba kujitolea mfano mwenyewe maana ni mkulima. Msimu wa kilimo uliopita nimelima ekari 2 na kidogo ambazo sawa na hekta moja na nilivuna tani 3 au gunia 30 za kg 100. Nilikodi shamba kwa laki moja. Vibarua wakanilimia kwa ng'ombe kwa shilingi laki moja. Gharama za mbegu, madawa ya kuuwa wadudu na kukausha nyasi pamoja na mbolea nikatumia laki tano. Kuvuna na kupukuchua pamoja na mifuko ya kuwekea mahindi nimetumia laki tatu. Jumla ya gharama nilizotumia ni milion 1. Nimeuza mahindi hayo December 2022 kwa milion 2 na nusu baada ya kuuza kwa kg Tsh. 800 hukohuko shambani. Hivyo faida ukawa ni milioni 1.5.

Sasa tukirudi kwa Bwana Bashe na wizara yake ya kilimo kwa hekta 1 au ekari 2 na kidogo bajeti yao ni kama ifutavyo:
  • Kulima shamba Tsh. 4,250,000/
  • Kumwagilia Tsh. 7,500,000/
  • Kupima afya ya udongo Tsh. 2,500,000/
  • Mbolea Tsh. 1,750,000/
  • Viuatilifu Tsh. 375,000/
  • Mbegu Tsh. 112,000/-
JUMLA Tsh. 16, 487, 500/ kwa hekta moja. Sasa hiyo milioni 16 ukizidisha mara hekta 812 za vijana waliochukuliwa tayari awamu ya kwanza na wizara ya kilimo chini ya waziri Bashe unapata bilioni 13.5. Yani dakika ya kwanza kabisa mpira unaanza tunapigwa bilioni 13 na hiyo tu ni awamu ya kwanza maana hatujui mradi huu utahusisha hekta ngapi.

Hapo sijajumlisha gharama za upimaji ardhi na hati miliki ambayo wameweka ni milion 2. Na hapo pia nina mashaka kama hizo ndio bei halisi za kupimia ardhi kwa hekta. Anyway tuachane na mambo ya hati miliki turudi kwenye topic yetu.

Mimi ni miongoni mwa watu ambao naunga mkono wakulima kuinuliwa hasa vijana. Mradi wa Building a Better Tomorrow au BBT lengo kuu lilikuwa ni kuinua kilimo kupitia vijana. Lakini kwa mchanganuo unaonekana ni 𝑩𝒖𝒊𝒍𝒅𝒊𝒏𝒈 𝑩𝒂𝒔𝒉𝒆 𝑻𝒐𝒎𝒐𝒓𝒓𝒐𝒘 - 𝑩𝑩𝑻 na kwamba mradi huu umesukwa kimkakati kuwatumia vijana kufanya ufisadi wa mabilioni. Pengine ndio maana vijana walio wengi kama sio wote waliobebwa au kupewa fursa katika mradi huo hawajui chochote kuhusu kilimo na hawajawahi kulima. Ni wakati sasa wa CAG kwenda kufanya ukaguzi katika mradi huo.

Hawa watu ambao Rais Samia aliwapa ruhusa ya kula kulingana na urefu wa kamba zao imefika mahari sasa wanataka kukata mpaka kamba ili waitafune nchi yote ibaki na mashimo. Kuna wingu zito la ufisadi kuanzia wizarani mpaka nje ya wizara ukiachilia mbali fisadi mmoja mkongwe kupewa tenda ya kusambaza mbolea katika mradi huo.

Imekuwa ngumu sana kumtenga bwana Bashe na ufisadi kwa sababu ya watu waliomlea na kumkuza katika siasa ambao kwa kiasi kikubwa wananuka ufisadi wa nchi hii. Bado nina file zake nazipitia kupata uhakika. Miongoni mwa file hizo zinahusisha baadhi ya viwanda kikiweno kiwanda cha Mbolea ya minjingu somewhere.

Kwa mazingira haya tusitegemee kama kutakuwa na uwajibikaji wowote kwa sababu wazazi wa kisiasa wa Bashe ambao wanazo kashfa nzito nchi hii wameshinda vita dhidi ya mafisadi wa Sukuma Gang ambao nao walitesa kwa miaka mitano.

Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.

𝑴𝒅𝒖𝒅𝒆 𝑵𝒚𝒂𝒈𝒂𝒍𝒊 𝟕 𝒙 𝟕𝟎 𝑺𝒖𝒎𝒖 𝒚𝒂 𝑵𝒚𝒊𝒈𝒖

View attachment 2617458
Bashe aondoshwe!
 
Soma mchanganuo umeandikwa hapo na siyo kujifanya mjuaji wakati kichwa kimejaa kamasi!
Kwa mtu mwenye akili akisoma huo mchanganuo uliowekwa hapo anaona kabisa ni wa uongo (Fake!)
Mfano:
1. Hao vijana 800 wanalala wapi (Nyumba & Chakula) kwa gharama zipi
2. Gharama za matibabu ya hao vijana (Bima) zinatoka wapi?
3. Hayo maji ya kunywesha kwa matone yanatoka wapi hadi yafike huko shambani
4. Miundombinu ya kufika huko shambani (barabara) inatengenezwa kwa gharama zipi?
5. Gharama za kununua matractor zinatoka wapi?
Nafikiri tutafute Mchanganuo wa huo mradi badala ya kukaa hapa na kulishwa matango pori.....
 
Hivi ngoja, wizara ya kilimo si ilitengewa Bilioni 210+ hivi za bajeti na ilipitishwa?
 
Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.[emoji848][emoji2827][emoji1545][emoji817][emoji818]
Nakuunga mkono. Watanzania hii laana ya uzembe hebu tuivue. Tujivike ujasiri wa muda tufumue mfumo wa uongozi watu wahovyo waondoke serikalini.
 
Mdude_Nyagali
Hoja zako ni nzuri lakini Mungu alikunyima;
1..Hekima
2...Busara
Uwashilishaji wako siku zote umejaa dharau na kejeli.
Ni vigumu watu wenye akili kukusikiliza na kuheshimu mchango wako.

Jifunze kwa mwenyekiti wako Mbowe na Mnyika.
Kejeli sio unana harakati bali kukosa hekima...badilika muda bado unao
 
Back
Top Bottom