Mabadiliko kutoka Building Better Tomorrow - BBT mpaka kuwa Building Bashe Tomorrow - BBT

Mabadiliko kutoka Building Better Tomorrow - BBT mpaka kuwa Building Bashe Tomorrow - BBT

Kwa mtu mwenye akili akisoma huo mchanganuo uliowekwa hapo anaona kabisa ni wa uongo (Fake!)
Mfano:
1. Hao vijana 800 wanalala wapi (Nyumba & Chakula) kwa gharama zipi
2. Gharama za matibabu ya hao vijana (Bima) zinatoka wapi?
3. Hayo maji ya kunywesha kwa matone yanatoka wapi hadi yafike huko shambani
4. Miundombinu ya kufika huko shambani (barabara) inatengenezwa kwa gharama zipi?
5. Gharama za kununua matractor zinatoka wapi?
Nafikiri tutafute Mchanganuo wa huo mradi badala ya kukaa hapa na kulishwa matango pori.....
Huo ndiyo mchanganuo wa Bashe,na ndiyo hoja iliyopo mezani
 
Wozara ya kilimo nayo sasa ina pesa nyingi sana ndio maana lazima iingie kwenye upigaji!!mbona miaka ya nyuma hukuwahi kusikia!!sasa kuna mipesa mingi imemwagwa huko watu lazima watafute njia za kuzipiga!!
Yule Mwajemi ni genius sana kuchonga line ya kula hela ya serikali hii.
 
Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.[emoji848][emoji2827][emoji1545][emoji817][emoji818]
Sahihi mno Mkuu!

Hiyo ndiyo itakuwa msingi wetu wa kuchagua na kuwawajibisha viongozi na watendaji wakuu wa nchi yetu.
Kwa sasa, technically, hatuna mkataba na hao watawala. Na ndio maana wanafanya yao na wala hawajali wala kutuogopa.

Yatosha! Tunataka Katiba Mpya kufikia 2025
 
Matatizo yalikuwepo siku zote na awamu zote, labda tu awamu hii watu wanaweza kuzungumza zaidi kuliko awamu iliyopita.
Ndio kuna uwazi kiasi kuliko awamu iliyopita. Na ndio maana tunajadili hapa na kwingineko bila woga.
Tunaipenda nchi yetu, tunaumia sana tukiona jinsni mchwa wanavyoitafuna.

Tunataka Katiba Mpya!
 
Hii nchi ngumu kweli kwahyo unataka vijana wakalime na ng'ombe???. tunataka tuachane na kilimo Cha 1960 mkuu
Hata kama atatumia mashine (Tractor 🚜) ila kulima haitazidi shilingi 250,000 kwa Ekari tena hapo imehusisha gharama za awali za kukata miti ili kusafisha hilo shamba.

Lakini ikitokea shamba ni safi i.e halina miti ya kukata gharama inaweza kushuka hadi shilingi 75,000 kwa Ekari Moja
 
Kosa la hao Mawaziri Vijana ni Kuwazia Urais baada ya Mama Samia kuondoka 2030.

Mwangalie Mwigulu, Januari, Bashe hadi Nape wote wanauwinda Urais, hivyo wanafanya Ufisadi kujikusanyia Fedha zitakazowasaidia kuingia Ikulu 2030.
 
Cha muhimu sasa bila kujali tofauti ya vyama vyetu na dini zetu tuungane kudai #KatibaMpya ili angarau tuokoe chenji na maliasili zilizobakia nchi hii. Tofauti na hapo tutapigwa mnada nchi hii pengine tutakosa mpaka sehemu ya kuishi.[emoji848][emoji2827][emoji1545][emoji817][emoji818]
Kweli Lisu tumwelewe
 
we kijana legeza ubongo kidogo pale hazikufyekwa nyasi yalikua mapori tena misitu yenye miti mikubwa imetumika technology kibwa hadi likaitwa shamba
Acha ujinga! Hata kama ungekuwa msitu wa mibuyu huwezi kutumia zaidi ya milioni 4.
 
Kuna Utapeli mkubwa katika hili. Kama mradi upo sehemu moja kawaida udongo hupimi kila hekari. Unachukua sampuli za kuwakilisha eneo zima la mradi. Sasa milioni mbili ya kupimia afya ya ardhi kila Hekari ni utapeli mkubwa. Kwa nini wafunge system ya matone isiyo na uhalisia. Tuna mito mingi, wangetafuta sehemu wafunge burrow irrigation. Mradi mzuri ila hauna uhalisia na umejaa ufisadi.
 
Mabadiliko kutoka 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝙀𝙏𝙏𝙀𝙍 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒 - 𝘽𝘽𝙏 mpaka kuwa 𝘽𝙐𝙄𝙇𝘿𝙄𝙉𝙂 𝘽𝘼𝙎𝙃𝙀 𝙏𝙊𝙈𝙊𝙍𝙍𝙊𝙒- 𝘽𝘽𝙏. TUMEPIGWA BILIONI 13.

Kwa mujibu wa wizara ya Kilimo chini ya waziri @HusseinBashe ni kwamba serikali inatumia milion 16.4 kufadhili shamba la
Kamanda karibu tena Jukwaani
 
Huo mchaganuo haihusiani na malazi au chakula cha hao watu. Huo ni mchanganuo kwa hekta na yeye bashe kupitia wizara ndio walioutoa. Pia sio kwa Dodoma tu huo ndio mchaganuo wataotumia kufanya kwenye mikoa mingine yote

Lengo ni hekta milioni 1 na wamepanga kutumia trillion 17
Kwa mujibu wa maelezo yako
Kuna bajeti nyingine ya kugharamia hao vijna na gharama zote za uendeshaji ambazo baadhi nimeorodhesha hapo juu?. Tuweni basi realistic ili Elimu yetu itusaidie
 
Budget ya kilimo ilikua ndogo.
Ndiyo maana wakulima wakawa maskini .
Acheni sasa iwe zamu yao
Sasa kuna unafuu gani ambao mkulima ameupata?!!hizo pembejeo tu kuzipata kwa wakati bado ni mtihani?!!na fungu kubwa bado liko kwenye matumizi ,kuliko kwenye maendeleo.Kwa mipango hii ya kiza moto usitegemee mkulima atakuja faidika!!
 
Kuna Utapeli mkubwa katika hili. Kama mradi upo sehemu moja kawaida udongo hupimi kila hekari. Unachukua sampuli za kuwakilisha eneo zima la mradi. Sasa milioni mbili ya kupimia afya ya ardhi kila Hekari ni utapeli mkubwa. Kwa nini wafunge system ya matone isiyo na uhalisia. Tuna mito mingi, wangetafuta sehemu wafunge burrow irrigation. Mradi mzuri ila hauna uhalisia na umejaa ufisadi.
Labda anafanya green house. Pia okumbuka mradi wa pampja kama huo kuna gharma z pMoja zinapumgua
 
Sasa kuna unafuu gani ambao mkulima ameupata?!!hizo pembejeo tu kuzipata kwa wakati bado ni mtihani?!!na fungu kubwa bado liko kwenye matumizi ,kuliko kwenye maendeleo.Kwa mipango hii ya kiza moto usitegemee mkulima atakuja faidika!!
Jiepushe na unabii wa kushindwa
 
Pamoja na kuwa hizo gharama za BBT zipo juu
Ila kuna vitu muhimu hujaeleza kuhusu huo mradi. Kwanza kikubwa ni kutayarisha shamba na kuweka miundombinu, ya kulifikia na muhimu zaidi kuweka mfumo wa UMWAGILIAJI. Sina hakika kama wanatumia maji ya mto au wamechimba visima ambapo ni ghali sana kununua miundombinu ya Solar kwa ajili ya kuvuta maji au pengine kupeleka umeme huko mashambani.
Mradi kama huu, hauhitaji kubahatisha Mvua kama wakulima wetu wengi wanavyolima lakini pia; gharama hizo ni kama mtaji; inamaana, wakilima tena gharama nyingi hazitakuwepo
Muhimu pia: kwa kuwa na miundo mbinu sahihi, kuna uwezekano wa kulima mara mbilli kwa mwaka na hata mara tatu kutegemea na aina ya mazao

Mwisho; Kuna wale vijana (Wengi) waliopelekwa huko, ujue kuna gharama za kuwatengenezea mazingira ya kukaa huko shambani (Nyumba/Mahema Chakula, Bima ya Afya nk)
Binafsi najua huu mradi unaweza kuwa na changamoto kadhaa kwa sababu bado tunajifunza ila kutoka rohoni kwangu naamini ni moja ya miradi bora kabisa ya majaribio na inayoweza kutusaidia kama Nchi.
Angalizo: Mimi sihusiki huko kwa mradi, napambana kivyangu huku nje/Private

UNAJIONA UNAJUA KUMBE TAKATAKA TU.

KAA KIMYA TU MAANA UNAJIDHALILISHA
 
Back
Top Bottom